Salaam makamanda!
Wingi wa maneno sio ukweli wa mambo. Kwa kifupi CCM ina hali mbali sana kwenye siasa za hapa Tanzania, huo ni ukweli ulio wazi. Wenye upeo wa kutosha wameshang'amua hilo muda mrefu sana, wanasema its just a matter of time. Mabadiliko wananchi wanayataka iwe kupitia chadema ama kupitia njia yeyote ile lakini ccm bye bye hawataki kuisikia tena. HIKI NI KIZAZI KIPYA WANATAKA KUSIMIKA UTAWALA WAO IWE KUPITIA CHADEMA AMA CHAMA CHOCHOTE KILE, LAKINI LAZIMA WASIMIKE UTAWALA WAO. Fuatilia historia ya vyama vingine kwenye mataifa mengine vyenye hadhi ya CCM utanielewa kwa urahisi zaidi. Tazama haya machache:-
1.Viongozi njaa wa chadema wanatangaza kujiuzulu lakini hawatangazi wapi wanahamia, tofauti na miaka ya zamani kiongozi akihama anatangaza amehamia wapi asap
2.Zitto, Mkumbo, Samson wamesimamishwa nyadhifa zao lakini hawataki kuondoka, wanapambana wabaki mle!
3.Mtela, Habib, Juliana, Kisandu wamefukuzwa lakini bado wanang'ang'ania chadema; bado wana mapenzi ya moyoni na chadema; japo baadhi wapo ccm lakini ni kwa sababu ya dhiki tu si kwa kupenda. Mioyo yao ipo chadema
4.Beneficiaries wakubwa wa mfumo wa ccm (wenye upeo mkubwa wa kuona jinsi upepo wa mabadiliko unavyovuma nchini) hawajitokezi waziwazi kuiponda chadema badala yake wanawatumia akina
Mwigulu Nchemba (aka aibu katibu mkuu wa ccm na sio naibu katibu mkuu wa ccm) na akina
Nape Nnauye, wao wanafanya mambo yao kimya kimya kwa kuelewa kuwa ccm days are just numbered!
Lumumba FC B7 project wanatumika tu na wenye upeo kujaribu kuchelewesha siku za CCM kuondoka lakini mwisho wa siku ccm wanapoteza huu mchezo, huu sio utabiri ni hali halisi wenye upeo wa kutosha wananielewa! Lumumba FC b7 project hawapendi kutumika lakini dhiki iliyoletwa na ccm ndio inayowafanya kukubali kutumika na si vinginevyo! Unajua dhiki ikizidi unakuwa nusu msukule akili inastak kufikiri, nadhani naeleweka! Usidhani
Simiyu Yetu na wenzake mfano
chamvida wanafanya wanachojua la hasha tatizo ni dhiki kuu iliyoletwa na ccm, wamepumbazika ila soon watarejewa na ufahamu wao halisi!
5.Kwa ujumla chuki ni kubwa sana kwa ccm toka kwa watu wa kawaida na wasio wa kawaida
NB:Wingi wa maneno sio ukweli wa mambo, kwa kifupi ccm hours are numbered! Naomba tuishie hapo!
Wenu katika ukombozi!
TeamChadema