Kifo cha CCM kimetimia

Kifo cha CCM kimetimia

quote_icon.png
By notradamme
hizi ndoto za chagaboyz hizi! hivi ulimsikia kwa masikio yako NAPE NAUYE akitoa msimamo wa chama! au unashikiliwa akili yako na magazeti(ambayo yote yamegeuka udaku??)
nyie malengo yenu kama chama hayavuki2015

Hivi humu kuna watu wengine huwa wanafikiria kwa masaburi au ni nini??? Mbona jana tumemwona live nape akitoa msimamo wa chama. Moja ya mambo aliotangaza kuwa wao ccm hawakubaliani ni serikali 3, na kwamba wanaipeleka Rasimu ya katiba kwa wanachama wao hadi ngazi ya kijiji na wanaunda mabaraza ya katiba ya chma chao ili waipitia rasimu ya katiba. Sasa wewe unapinga nini??

Ukweli ni kwamba kwa ccm wanachama wao ni muhimu kuliko tanzania na wananchi walio wengi waliokubali kutoa maoni haya na kupendekeza katika katiba mpya. Wanaona sasa upuuzi wao umeshtukiwa na hakutakuwa na vijiwe vya Lumumba tena kwa ajili ya kutengeneza video fake. ccm imekula kwenu
 
Ujinga mkubwa wa ccm ni kudhani kuwa bado iko kwenye damu za wajinga walewale kumbe sivyo, watu wamejanjaruka na hawadanganyiki tena.Ukweli tu ndio unaohitajika nyakati hizi.
 
Lumumba project acheni porojo, CCM ilisha jinyonga yenyewe, tena kitambo.
Tutaizika rasmi ifikapo 2015.
 
Katika awamu ya nne ya urais,tumeshuhudia mengi matendo ambayo kiuhalisia ni kinyume na haki za binadamu,pia ni kinyume na utawala bora.Lakini ni nani anajali?
1.Mauaji ya raia wasio na hatia
kifo cha mwangosi mkoani Iringa nidhahiri kuwa hakuna anayejali,matokeo yake ni kupandishana vyeo n.k.Mauaji ya padri Mushi huko Zanzibar ni dhahiri kuwa hakuna anayejali na kuona utu wa binadamu si lolote si chochote katka utawala.
2.Utesaji na uonevu
Hapa tunaona,jins Dr.Ulimboka na kibanda wanafanyiwa kitendo cha kinyama km kung'olewa meno na kucha,kutobolewa macho na matendo mengine ya kinyama.
Lakini hakuna anayejali,na matokeo ya waziri anasimama na kusema kibanda yeye ni nani? Hii ni dharau tosha dhidi ya utu wa binadamu na kinyume na haki za binadamu.
Kwa hiyo kuteswa kwa kibanda,hakumpi shida mzee wassira.Pia tulisikia kauli za kwamba tukio la Ulimboka ni siri ya taifa.Sasa najiuliza taifa ni nini?.Pia kauli ya Mzee Pinda ya liwalo na liwe na likawa kweli inatia mashaka.Pamoja na haya yote hakuna anayejali,wakati serikali ndiyo jukumu la kulinda raia wake.Na mengine mengi huko mtwara,morogoro,songea,Arusha nk.Yote haya ni yametokana na matumizi ya dola iliyochini ya serikali ya CCM.
3.Rushwa na ufisadi.
Matumizi mabaya ya mali ya umma,rushwa n.k pamoja na kuwa na majina ya wahusika wa rushwa na ufisadi lakin hakuna hatua zozote zilizochukuliwa juu yao.mfano The list of shame,sakata la David Jairo na ufisadi mwingi tu katika mashirika ya umma na migodi ya madini.
n.k:Lakuna anayejali.
4.Biashara ya madawa ya kulevya.Pamoja na kuwa na madai mengi juu watu wanauza madawa ya kulevya,hakuna hatua yoyote iliyochukuliwa hii ni kutufanya kuwa na mashaka na wahusika,inawezekana kuna usiri mkubwa unaondelea juu ya suala hili.Matokeo yake ni kuharibu kizazi cha taifa la kesho,mali waibe wao,ufisad wafanye wao,hata kizazi wakiharibu wao kwa madawa ya kulevya hii haiwezekani hata kidogo.
6.Maisha magumu.Hii inajulikana kwa kila mtanzania mwenye kujua maana ya maisha na mwenye akili timamu.Kama una akili zisizo timamu utasema tuna maisha bora,kumbe ni bora maisha n.k
 
Katika hali isiyo ya kawaida,chama tawala yaani CCM kimekuwa katika wakati mgumu kuliko siku zote toka kuanzishwa kwake.
Chama hiki kimejaribu kutumia kila mbinu chafu dhidi ya CHADEMA,lakini kimeshindwa.Na matokeo yake imekuwa ikikipa umaarufu chama cha demokrasia na maendeleo,kwa kushinda kila hujuma.
Zaidi ya yote,kinazidi kuungwa mkono na wananchi kila kukicha,huku CCM ikizidi kuhamwa na kuonwa kama chama cha kinachokandamiza haki,demokrasia na chenye kutugawa watanzania kwa misingi ya dini na kabila.Hili ni dhahiri!
Ccm mwisho wenu umefika, jehanamu inawasubiri kwa hamu baada kutesa watu,kung'oa kucha na meno bila ganzi,kifo cha mwangosi.Damu za hawa watu hazikumwagika bure na huu mzimu wa mwangosi wanawafuatilia na ni laana kwenu na serikali ya chama chenu.
Badala ya kuwajibishana mnapandishana vyeo as if mmeua fisi au mnyama fulani,damu ya mwangosi inaongea.
"Jiandaeni kukabidhi madaraka kwa upinzani,nchi imewashinda"
 
Ni kweli mkuu, kifo cha daudi mwangosi kinasikitisha mno tena sana.damu yake itawagharimu sana ccm na policcm.
 
Kabla ya kukata roho,ng'ombe hurusha miguu huku na kule,hatimaye hutulia na roho yake huenda kusikojulikana, wala sio peponi...ccm itabaki historia na watu watakuwa huru
 
Ni kweli mkuu, kifo cha daudi mwangosi kinasikitisha mno tena sana.damu yake itawagharimu sana ccm na policcm.

mkuu Lupe,picha ya mauaji ya Mwangosi inasikitisha sana tena sana,nilpoiona ile picha machozi yalinitoka.Hii damu ya Mwangosi ni chanzo cha anguko la CCM.
 
Kabla ya kukata roho,ng'ombe hurusha miguu huku na kule,hatimaye hutulia na roho yake huenda kusikojulikana, wala sio peponi...ccm itabaki historia na watu watakuwa huru

Well said mkuu,tuko maskini,wanyonge kwa sababu ya CCM
 
Kamuhanda hajapona na wala asijidanganye ! Labda afe kabla ya 2015 , kila damu iliyomwagika italipwa !
 
Hivi kulikuwa na ulazima wa kumpandisha cheo kamuhanda? Tena so soon!
 
Penye ukweli daima,uongo hujitenga.Pamoja kuwadanganya watanzania juu ya nini serikali imekifanya.Bado ukweli umejulikana kuwa CCM inawadanganya watanzania.
CCM wamakuwa wepesi sana kusema wameleta maendeleo,lakini hawajatueleza ni kwa kiwango gani,wapi hawajafikia malengo na sababu gani zimesababisha kutofikia malengo.Kusema kuwa mmeleta maendeleo kwa kutamka majukwaani haina maana kwani wananchi hawajui ni % ngapi ya malengo imefikiwa.
Hivyo tunataka data na siyo maneno matupua.Sasa ni dhahiri kuwa,maendeleo yaliyopo si kile ambacho watanzania wanatarajiwa kwa kuwa nchi imetawaliwa na Raslimali nyingi kama madini,maji,mistu nk.
Tunataka uwazi katika utekeklezaji wamajukumu
 
Kwa kweli mkuu hakuna atakaekushangaa endapo ukiipa ccm jina lolote baya! Maana hata sasa kuna wanaolitumia hili jina kama tusi

sasa hivi zaidi ya ugaidi tuwaite nani.
 
Labda nifanye ku declare interest.Naichukia CCM(CHAMA ANALOGIA) kwa moyo wangu wote, kwa nguvu zangu, kwa fikra zangu zote,akili yangu yote bila kusahau na chuki zangu zote.

Kwa hiyo fikra analogia zozote zijue hilo.Mazungumzo yote yaende kweny epoint na si kuulizia hilo.
Mkuu Nicholas ubarikiwe sana

Wewe ni mtu mwenye uzalendo na nchi yako.yungekuwa na vijana 100 kama wewe hawa magamba tungewang'oa.
 
Kufuatia matokeo ya udiwan yanayoendelea kutoa sasa hivi inaonesha wazi kuwa CCM sasa inakufa kwa kasi. Hii inadhihishwa na jinsi gap kubwa la kura linavyojioneshapale CHADEMA iliposhinda. Sijajua kama tukio la mabomu Arusha kuna mkono wa CCM lakini kama ndiyo hivyo basi hata CCM yenyewe itakuwa imejitambua kabisa kuwa iko kwenye maandalizi ya chama cha upinzani. Kazeni buti makamanda ushindi umekaribia kufika.
 
CCM ndio nini? hiyo ilishakufaga zamaniiiii. Sasa wamebaki mafisadi tu.
 
Kufuatia matokeo ya udiwan yanayoendelea kutoa sasa hivi inaonesha wazi kuwa CCM sasa inakufa kwa kasi. Hii inadhihishwa na jinsi gap kubwa la kura linavyojioneshapale CHADEMA iliposhinda. Sijajua kama tukio la mabomu Arusha kuna mkono wa CCM lakini kama ndiyo hivyo basi hata CCM yenyewe itakuwa imejitambua kabisa kuwa iko kwenye maandalizi ya chama cha upinzani. Kazeni buti makamanda ushindi umekaribia kufika.

Ni ukweli ulio wazi sasa kwamba CCM iko ICU inapumulia kw mashine yiitwayo TISS, Polisi, Tume ya uchaguzi, JWTZ Rushwa, Ufisadi na propoganda CCM haipo tena mioyoni mwa wananchi Nape, Mwigulu, JK wote wanajua ni siri iko wazi na dhahiri sasa
 
Back
Top Bottom