Curriculum Specialist
JF-Expert Member
- Oct 8, 2007
- 2,732
- 750
Sikweli kwamba CCM wanapenda Amani na Utulivu wa nchi hii kuliko vyama vingine, CCM watapenda Amani na Utulivu wa nchi hii kama utawasaidia kubaki madarakani, isipokuwa hivyo watatumia dhana ya kutoweka kwa Amani na Utulivu kama silaha ya wao kubaki madarakani! Na hiki ndo wanachofanya kwasasa kujifanya wanapenda Amani na Utulivu kuliko vyama vingine, wakitumia kila fursa wanayopata mbele ya watanzania kuwaaminisha hivyo, huku wakisahau kuwa wao ndo waanzilishi wa siasa za udini hapa nchini! Mtu huwezi kudanganywa mara mbili....