Udini, ukabila, ukanda, na sasa ugaidi ni propaganda ambazo zimetawala kwenye vichwa vya wanaccm dhidi ya chadema na zimekuwa zikitukera sana wanachama, wafuasi na wapenzi wa chadema huku ikiwa ni shangwe na furaha kwa ccm wakiamini kuwa chama hichi kitakufa hivi karibu kutokana na propaganda hizo
Nianze kwa kusema tu kwamba mchimba kaburi huingia mwenyewe kabla ya marehemu kuzikwa.Hivyo basi mchimba kaburi hulijua vizuri joto, mazingira na dhahama japo kidogo ya kaburi.Nianze kuzifafanua hizi propaganda za udini, ukabila, ukanda na ugaidi na ni jinsi gani zitaipeleka ccm kuzimu katika uchaguzi ujao wa mwaka 2015
udini
Moja. Kama chadema ni chama cha udini yaani chama cha wakristo basi tunaomba wakristo wote warudi kwenye chama chao na wakipigie kura chama chao kwa misingi ya dini zao. Na kwa maana hiyo mwaka 2015 wakristo wote wakipigie kura chadema.watu hao kama wakina Pinda, Job ndugai, Mkapa, Malecela,Membe,anna makinda na wakristo wengineo
Pili. Kwasababu ndani ya chadema kuna waislamu safi kama Zitto kabwe, Prof. Safari, Mh Arfi, Mh Halima na wengine basi tunaomba waislamu wote wanaowasupport hawa makamanda wawapigie kura na kuuaminisha umma kuwa chadema siyo chama cha udini ndiyo maana kuna waislamu safi ndani ya chama. Hivyo basi mwaka 2015 kuna kundi kubwa la waislamu wanaokisupport chadema na hawaamini hii propaganda za udini watakipigia kura chadema
ukabila
Moja. Kama chadema ni chama cha kikabila basi tunaomba wachaga wote warudi kwenye chama chao na kukipigia kura chadema mwaka 2015 kwa misingi ya kabila lao. Watu hao kama Sumaye,Mama anna mkapa, Mrema na wachaga wengineo
Pili. Kwasababu kuna makabila kama wasukuma ambao wana wabunge wengi kuliko hata hao wachaga. Basi wasukuma, waha, wahehe, wafipa, wanyiramba na makabila mengine yenye wabunge wa chadema yaikomoe ccm kwa kuichagua chadema mwaka 2015 na kuionesha ccm kuwa chadema siyo chama cha kikabila ndiyo maana makabila mengine yana wabunge wengi kuliko hao wachaga
ukanda
Moja. Kama chadema ni chama cha kikanda basi tunaomba kanda ya kaskazini yote yaani Arusha, kilimanjaro mi mikoa mingine ya kanda ya kaskazini warudi kwenye chama chao na kukipigia kura chadema mwaka 2015 kwa kufuata misingi ya kanda zao
Pili. Kwasababu kuna kanda ambazo ni ngome ya chadema na haziamini kuwa chadema ni chama cha kikanda hivyo basi kanda ya ziwa yaani mwanza na shinyanga zenye wabunge wengi wa chadema, kanda ya kusini na kanda nyingine ziikomoe ccm kwa kuionesha kuwa kanda zao ndiyo zenye wabunge wengi kuliko hata hiyo kanda ya kaskazini hivyo basi chadema siyo chama cha kikanda
ugaidi
Moja. Kama chadema ni chama cha magaidi basi tunawaomba magaidi wote wakiwemo wale wa usal.... na watekaji wote warudi kwenye chama chao na kukipigia kura chadema mwaka 2015 kwa misingi ya kuwa ni chama cha ugaidi
Pili. Kwasababu kuna watanzania wengi wasioamini kuwa chadema ni chama cha kigaidi. Hivyo basi watanzania wote tusioamini kuwa chadema ni chama cha magaidi wapige kura kuichagua chadema mwaka 2015 na kutuma salamu kuwa wanaokiita chadema ni chama cha magaidi wao ndiyo magaidi ndiyo maana wanawateka wapenzi wa haki na wanaharakati wanaopinga uonevu na dhuluma ndani ya taifa hili
hitimisho
Kwa idadi hii ya wapiga kura wa chadema. Chadema itashinda kwa zaidi ya asilimia 70. Lakini hoja ya msingi hapa ni kwa propaganda hizi za udini, ukabila, ukanda na ugaidi je zinaingia akilini. Je kama tuliyempa madaraka anakuwa muongo wa kuzushia watu mambo ya mabaya je yeye atakuwa salama. Je ni kwanini anazusha mambo hayo ukizingatia kuwa yeye amekaa madarakani miaka mingi?
Basi hizo ndiyo sababu zitakazoiua ccm kutokana na propaganda za udini,ukabila,ukanda na ugaidi inayozushiwa wa chadema
Mohamed ally aliwahi kusema ukiona watu wanakusemasema sana ujue wanakuogopa na ni changamoto zinazoashilia upo karibu kufanikiwa
baada ya miaka kupita Mohamed ally alifanikiwa na kuwa the greatest boxer in the world
NAOMBA NIWASILISHE WADAU