palalisote
JF-Expert Member
- Aug 4, 2010
- 8,335
- 1,462
"jiwe walilolikataa waashi sasa limekuwa jiwe la msingi"
Mm sina chama, lakini kila ninayekutana naye hataki
sikia kuhusu CCM, kila mtu CHADEMA CHADEMA CHADEMA; mpaka sasa hivi
nikikutana na mtu hata kama simjui na assume ana sura ya
ki-CHADEMA, kudadeeeeeeeeeeki mamangi ni noma
Mimi ni mpiga kura wa kata moja wapo inaitwa kata ya Themi,WAPIGANAJI WETU A-TAUNI TUPENI RAHA KATIKA UCHAGUZI MDOGO WA MADIWANI HAPO JIJINI KWA KUUNGA MKONO KWA DHATI NA VITENDO ZOEZI LA 'OPARESHENI WOTE CHADEMA' HIVI KARIBUNI
Siku zote pale pote palipo na MWANGA, hakuna shaka, GIZA hukimbia tena kwa kasi isielezeka. Ukandamizaji dhidi ya CHADEMA Mungu wetu mwema na aliyehai azidi kuwaumbua watesi wetu na VIHUNZI vyote vya kisasi kisiasa huturukisha salama bila kutuacha tuadhirike na mitego ya maadui zetu.
Enyi wana wa A-Tauni, sasa ni muda wa kufanya KWELI kikweli kweli vile; sote kwa pamoja tena bila ajizi hebu tujitokeze 'TO THE LAST MAN' tukakipigie CCM 'kura za chuki' kwenye uchaguzi wa madiwani hivi karibuni na tupate kumpa Mhe Lema ZAWADI STAHIKI kwa kumchagulia Madiwani wooote toka CHADEMA peke yake ili tupate kuandika historia mpya hapa jijini.
Chini ya mapendekezo haya vile vile tuchukue nafasi hii kuomba viongozi wetu CHADEMA Makao Makuu kutulete mapema ile timu mahiri ya Dogo Nyerere iliopata 'kumuumbua' Mzee Wassira kule jimbo la Meru na hatimaye kutuletea mbunge Nassari sebuleni kule Dodoma.
Katu wasibaki nyuma hata kidogo wabunge vijana kama vile Zitto, Mch Msigwa, Sugu aka Rais wa Taifa la Jamhuri ya Watu wa Mbeya, Kamanda Heche, Kamanda Mawazo wa kule BK, Kamanda Halima Mdee wote chini ya Gwiji Mabere Nyaucho Marando na Mzee wa Anga katika kumkaribisha Dokta wa ukweli kuja kuongoza safu ya 'OPARESHENI WOTE CHADEMA' ili kuliweka sawa jiji la Arusha kisiasa katika ramni ya kuwa NGOME KUU ya mabadiliko ya kweli nchini.
Wakuu 'Crashwise', 'Mungi', Kamanda Ole Millya na Kamanda Ephata, Kamanda Gologwa na uongozi mzima wa CHADEMA Mkoa; hebu tuandalieni jiji na ukaribisho shwari kwa kazi moja kubwa ya kumpa Mhe Lema ZAWADI STAHIKI kwa kumchagulia timu ya Madiwani wenye nembo ya 'WOTECHADEMA' hapo Jijini.
kuna kila dalili kuwa CCM itakufa kabla ya 2014.
Mojawapo ni:=
- makundi ya urais,
-kukosa viongozi wenye sifa. CCM bado watabadili sana frames ila picture ni ileile. Nafasi wanayoweza itoa ni ya Mwenyekiti ila zote watabadili hadi warudie.
-tenacity ya CHADEMA na ufanisi wa mamluki wa CHADEMA ndani ya CCM ni tishio kubwa kwa CCM ambao hawawezi tena jitokeza kwa raia.
-CCM imeoza kutoka ndani, na kinachoonekana ni zile sehemu uozo umeanza tokeza.
Ha ha..ndio nilikuwa najiuliza km "mwamba wa mtandao toka kaskazini" anaweza vumilia ten yrs ya rais mwingine alimweka kwa mtandao wake?miaka 7+ hii tunaona afya yake.ccm wakichagua mwingine ni km death sentence na usaliti mkuu.There you are!..makundi ndani ya CCM hawatayakwepa, na kila kundi lina interests against the upposite. Pili, kuna suala la zanzibar, hili ni hatari,zanzibar hawataruhusu bara itoe rais wa Jamhuri ya muungano mfululizo zaidi ya miaka 20 ikiwa CCM itatoa mgombea wa urais kutoka bara ktk uchaguzi 2015. Tatu, CDM wamepandikiza watu wa ukweli,wenye nguvu na weledi kwa mission waliotumwa kufanya,CCM haiponi, acha wafanye maigizo yao ya kitoto
Chama Cha Mapinduzi hakitaweza tena kuinuka na kuongoza nchi baada ya kipindi cha rais Kikwete kuisha. Chama hakiaminiwi tena kwa mambo yafuatayo:
1. Rais alijipa mamlaka ya kuisamehe orodha ya wezi wa fedha EPA na orodha ya wafanyabiashara madawa ya kulevya yaani "list of shame" (viongozi wa CCM wenye vyeo serikalini) na kuiweka kapuni.
2 Serikali ya Chama Cha Mapindunduzi, kwa dhamira haram, kukubali kusaini mikataba na makampuni hewa kama Richmond na mengine amabayo kimsingi ni makampuni hewa ya viongozi wa chama cha mapinduzi..huu ni uhujumu uchumi wa kukusudia na unaolindwa na kiongozi wa juu zaidi katika nchi.
3 CCM inaumri wa miaka 34 kwa sasa, huduma za afya bado ni duni, elimu hovyo,uchumi hovyo na huduma zingine bado...hii ni total failure, haihitaji excuse any more.
4 CCM imeshindwa ku-practise political torelance kwa vyama pinzani na wtu wowote wale wenye mlengo huo. Kupitia vyombo vya usalama vimekuwa vikikibeba chama, polisi kumuuwa mwangosi inatosha kuuona utawala unaoamini "liwalo na liwe".
Sasa ni utawala wa imla...ni ishara ya chama na serikali yake kuanguka. Haitaweza kuinuka tena!...Madhambi ya chama yako wazi na dhahili. Change is is an irreversible process, CCM haitaweza kubadili hali hii ambayo imo mioyoni mwa wananchi.