Mutakyamirwa
JF-Expert Member
- Jan 24, 2011
- 4,942
- 1,360
CCM wameamua kuachana na siasa za Analogia kwasababu zimekuwa zikiwachelewesha katika kufikia malengo yao ya kukimaliza na kukifutilia mbali chama cha HADEMA.Sasa wameamua kuja na siasa za kidigitali zaidi hii ni kuwabambikizia wapinzani wao kesi zisizokuwa na Kichwa wala miguu.
Uhalifu wowote unaotokea sasa iwe ujambazi,uvamizi wa aina yeyote iwe utekaji nyara na utesaji,Mafuriko watu wa mabondeni ,machafuko kama yaliyotokea kule Lindi na Mtwara n.k CCM hawaumizi kichwa tena zaidi ya kusema ni CHADEMA ndiyo wahsika wa kuu.
Kwahiyo napenda kuwashauri CCM kuwa wayaongezee yafuatayo katika hayo ili wakifutilie mbali chama hiki kibaki historia tu:
1. Kesi ya EPA -wahusika CHADEMA
2.Utoroshwaji wa wanyama hai- CHADEMA
3.Kiwango cha Elimu kushuka, wanafunzi kufeli -CHADEMA
4.Rushwa na Mafisadi-CHADEMA
5.Tuhuma za Kagoda,Meremeta, ufisadi UDA-CHADEMA
6Ufisadi TRL -CHADEMA NK
Mkuu umenichekesha, Hawa jamaa umewa-note vizuri. Hawana aibu hata kidogo. Kama wanasema kifo cha Mwangosi ni CDM watashindwaje kusema hayo uliyoyataja? Kilichobakia hata mafuriko ya dar mwaka juzi watasema cdm. Utaniambia tu, kuna vijana wao kutoka Lumumba kwa kazi hiyo.
Kinacho shangaza ni kuwa wao wanafikiri tzn ni ile ya '47. Zaidi wanafikiri kuficha huso wakati kiwiliwili kingine kinaoneka.