Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Status
Not open for further replies.
"Anapaswa kujifunza kuwa na subira waliyonayo vijana wengi ndani ya CCM na serikalini, ambao pamoja na kuwa na fursa nyingi za harakaharaka, wameamua kuwa watulivu na wenye subira, wakiwa na uhakika kuwa, wakati wao utafika".

Kwanza namuomba huyu mheshimiwa Kibanda ajue kuwa hakuna cha kujifunza CCM. Pili sijui anaishia kwenye kifupisho cha "CHADEMA" haendi zaidi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo.

Kifupi kinachoendelea ni mkondo mzima wa Demokrasia ni vyema tuufagilie na kujivunia.

Naomba Kibanda ajiulize Chama Cha Mapinduzi kinapindua nini? Labda kinapindua Democrasia na maendeleo ya watanzania hakifai kuigwa.

Nina miaka 60 nimeona CCM ikijipidua hata yenyewe licha ya kupindua mema mengi ya nchi hii.

Mungu bariki vijana wanaojitosa. Mungu awatangualie waonyeshe democrasia mbadala wa domocrasia
 
Nafikiri huu ni mpango mzuri kwa CHADEMA. Wamepanga hili kwa lengo lao mahususi. Sidhani kama Zitto ameamka na kuamuu kuchukua form. Ni kujipanga vema kwa mambo yajayo!!! this is possibility no.1

Inawezekana pia ni mipango kabambe ya wale waichukiao Chadema hasa kupambana na mafisadi. Hivyo Chadema be careully!! possibility no. 2

Hukumu ipo miongoni mwa Chadema eligibles for voting!!!

Anyway, hizo ndizo siasa na uhuruu au tuseme demokrasia!!! Kwani ni nani ambaye ametakiwa kuwa kiongozi maisha isipokuwa baba na mama ndani ya nyumba yao!!! Ni Mugabe tu na Museven wanataka eti wawe life time viongozi, bila kumsahau comrade mzee wa Kiraracha na TLP yake!!
 
kanda2

Nimeisoma makala yangu yote mara mbili mbili na kuihakiki akili yangu na kubaini kwamba pengine kuna aya moja tu ambayo pengine imepotosha dhana nzima iliyokusudiwa.

Hata hivyo ni jambo la kusikitisha kwamba 'The Home of Great Thinkers' inataka kuchafuliwa na Watanzania ambao ni wavivu wa kufikiri na ambao kwao wao furaha ni kuona kukithiri kwa mitikisiko isiyo ya lazima ndani ya vyama vya siasa hususan hivi vichanga vya upinzani.

Ninayo imani kubwa kwa Zitto na pengine ninaujali sana mustakabali wake kuliko ilivyo kwa wengi ambao leo hii wanajifanya wakimtetea na kumpigania kinafiki ili mbele ya safari wapate maneno ya kuinyoshea kidole Chadema, au Mbowe au Zitto.

Sijakatishwa tamaa.
 
Last edited by a moderator:
Nimeisoma makala yangu yote mara mbili mbili na kuihakiki akili yangu na kubaini kwamba pengine kuna aya moja tu ambayo pengine imepotosha dhana nzima iliyokusudiwa.

Hata hivyo ni jambo la kusikitisha kwamba 'The Home of Great Thinkers' inataka kuchafuliwa na Watanzania ambao ni wavivu wa kufikiri na ambao kwao wao furaha ni kuona kukithiri kwa mitikisiko isiyo ya lazima ndani ya vyama vya siasa hususan hivi vichanga vya upinzani.

Ninayo imani kubwa kwa Zitto na pengine ninaujali sana mustakabali wake kuliko ilivyo kwa wengi ambao leo hii wanajifanya wakimtetea na kumpigania kinafiki ili mbele ya safari wapate maneno ya kuinyoshea kidole Chadema, au Mbowe au Zitto.

Sijakatishwa tamaa.
Kibanda,

Great Thinking inakuja pale tunapokubali "Kutofautiana mitizamo".

Kisha, hii ndiyo Jamii, tunapopeleka mawazo tutarajie kuwa na pande mbili: Inayounga mkono yale tunayoipelekea na ile inayoyapuuza kabisa. Upande wa tatu siufikirii kwa sana (usiofungamana na upande wowote) kwani huenda ukawa hauna athari kwako.

Hata hivyo, napenda kukukaribisha JamiiForums | Where we Dare to Talk Openly!
 
Kwa kipindi kirefu hapa Tanzania na pengine kwa baadhi ya nchi za kiafrika uendeshaji wa vyama vya siasa imekuwa sawa na mtu anavyoendesha familia yake.

Hapa nina maana kuwa anaweza kuamua kuoa mke leo na akamfukuza kesho,anaweza kuajiri house girl leo akikataa kutembea na baba mwenye nyumba anamfukuza yaana alimradi tu anayekiongoza chama anafanya analotaka bila watu kumuuliza na inapofika kipindi cha uchaguzi anataka kupita bila kupingwa, hili si sawa kidemokrasia.

Mfano wa hivi karibuni ni wa Mheshimiwa wa Injii hii alipoona naakaribiwa kutolewa kwenye kiti akavua watu uanachama ili aendelee kutetea kiti chake bila kupingwa.

Kwa mtazamo wangu nimekuwa nikiona kama chadema kuwa ni chama cha kutolewa mfano na nimekuwa nikishawishika hata kutafuta ofisi zao ili nijiunge nacho lakini kumbe yaleyale ya mtu kuendesha chama kama familia. Binafsi sioni kama kuna tatizo la Zitto kuchukua form za kugombea maana ni haki yake kikatiba na hakuhitajika kupiga hodi maana mwandishi hapa anasema ''tena kwa staili ya kushitukiza'' haijalishi zito amechukua form kwa staili gani cha muhimu hapa ni je kuna kipengele kinachomzuia kugombea huo uenyekiti kwa kutotimiza vigezo fulani? Kama hakuna basi anapaswa kuchukua form kama ambavyo hata mimi ningeweza kuchukua.

Ifike wakati watanzania tusiweke maslahi binafsi mbele bali tuweke maslahi ya nchi mbele, chama si mali ya mtu ni mali ya wanachama kama kina muheshimiwa Mtei na Bob Makani walivyoachia madaraka kwa hiari vivyo hivyo na hawa wanaofuata wanapaswa kuachia madaraka kwa hiari eidha kwa kujiuzuru au kwa kushindwa katika chaguzi halali na sio kwa mtutu.

Naomba mwandishi wa makala hii aache busara ya wanachama wa CHADEMA ichukue mkondo wake kama anahisi kuwa zito anatumiwa na mafisadi hizo ni hisia zake na hakuna wa kupinga na wengine tuna hisia zetu kuwa hatua ya Zitto kuchukua form ni katika kuimarisha demokrasia ndani ya chama.

Mabadiliko ya uongozi mara nyingine huleta tija mahala fulani, Zitto namfahamu vizuri nimekuwa nae katika bunge la wanafunzi pale mlimani nafahamu uanaharakati wake na maamuzi yake si ya kukurupuka ngoja tuone demokrasia itakavyochukua nafasi juu ya hili na hapo chadema kitakuea kimejijengea heshima kubwa ndani ya nchii hii.
 
Nimeisoma makala yangu yote mara mbili mbili na kuihakiki akili yangu na kubaini kwamba pengine kuna aya moja tu ambayo pengine imepotosha dhana nzima iliyokusudiwa.

Hata hivyo ni jambo la kusikitisha kwamba 'The Home of Great Thinkers' inataka kuchafuliwa na Watanzania ambao ni wavivu wa kufikiri na ambao kwao wao furaha ni kuona kukithiri kwa mitikisiko isiyo ya lazima ndani ya vyama vya siasa hususan hivi vichanga vya upinzani.

Ninayo imani kubwa kwa Zitto na pengine ninaujali sana mustakabali wake kuliko ilivyo kwa wengi ambao leo hii wanajifanya wakimtetea na kumpigania kinafiki ili mbele ya safari wapate maneno ya kuinyoshea kidole Chadema, au Mbowe au Zitto.

Sijakatishwa tamaa.

Kwanza umegonga panapostahili na kwa wakati mwafaka. Nadhani kwa sasa hiki ni kipindi muhimu na nyeti kwa Chadema kuliko kipindi kingine chochote kile katika siasa za Tanzania. Ni jambo la msingi kwetu sote kuhakikisha kwamba Zitto anafanikisha malengo yake mema. Kwanza kutokana na hali ilivyo amejibu karibu maswali yote ya msingi yaliyoulizwa.

Pengine kwa kuongezea hapa ni kwamba Chadema sasa inahitaji mshikamano zaidi kuliko wakati wowote ule na kwamba Zitto na Mbowe wanataka demokrasia iwe kwa mfano na wazee wa Chadema wanalifahamu hilo na kwa upande mwingine ndani ya CCM kutakuwa na kishindo na hadi sasa wameanza kushituka kuwa wameingia mtegoni.

Kwa hali halisi ilivyo ni kwamba kwa sasa Mbowe na Zitto ni wamoja kwa dhati na hakuna tatizo kati yao. Kitachotokea naamini kitawashangaza wengi kwa kuwa hakuna atakayechukia kati yao baada ya matokeo na Chadema itakuwa imara kuliko wakati wowote ule.

Mambo ni shwari kabisa na ndio maana Mtei na Makani wamekuwa makini
 
Jk kazaliwa oktoba 1955.kapata unaibu waziri wa madini mwaka 1988,kamaliza chuo kikuu 1975 akiwa na miaka 20 akapangiwa kazi za chama Singida ndio kituo chake cha kwanza kama katibu wa chama. akaenda Tabora na mwaka 1977 akapelekwa makao makuu ya chama Zanzibar ofisi ya Kisiwandui kama Naibu Katibu mkuu wa CCM ofisi ya Zanzibar.mara tu baada ya kuzaliwa CCM.

Huu ni uongo wa hali ya juu, JK kazaliwa Oktoba 7 1950, hizi ndio records zilizopo kila mahali unless umeamua kutunga za kwako! It's very simple to note that during that time it was not easy/possible for someone to graduate at the age of 20 years! Kuanza shule tu mpaka mkono ushike sikio la upande wa pili kupitia juu ya kichwa (talking of seven to nine year old), plus JKT mwaka mmoja!
 
Nimepitia kwa kituo maoni mbalimbali ya wachangiaji wa makala yangu ambayo thread yake imetumwa jana. Kimsingi nayaheshimu mawazo mbalimbali yaliyotolewa na Watanzania ambao wameonyesha namna wanavyoguswa na masuala mazito ya kitaifa.

Hata hivyo ni jambo la bahati mbaya sana kwamba baadhi ya maoni yaliyotolewa na wachangiaji yamechukua mwelekeo wa kebehi, kashfa, uzushi, matusi na mambo yanayofanana na hayo. Hayo yamenisikitisha.

Siku zote naamini hoja hujibiwa na hoja na ndiyo maana nimekuwa tayari kuanzisha mijadala mbalimbali katika magazeti lengo likiwa ni kujua mitazamo ya Watanzania wenzangu katika mambo mbalimbali yanayohusu hatima ya taifa letu.

Nimeona nifanye juhudi za makusudi kuweka sawa baada ya mambo ambayo yameibuliwa katika mawazo ya Watanzania ambao naamini yametolewa kwa nia mbaya.

Kwanza si kweli kwamba makala ile imeandikwa kwa malengo ya kumfurahisa, kujipendekeza au kujikomba kwa Mbowe kama ambavyo imetakwa iaminiwe na baadhi ya wachangiaji wa JF.

Naamini Zitto mwenyewe angekuwa mkweli na muwazi angeweza kuwathibitishia wana JF wengine kuhusu maoni yangu katika masuala mbalimbali ya kisiasa likiwamo hili ambalo linamgusa yeye moja kwa moja.

Niseme wazi kwamba siku zote nimekuwa nikimtakia mema Zitto na wanasiasa wengine mbalimbali vijana ambao wamesambaa katika vyama mbalimbali kwa sababu nina imani kuwa, Vijana ni Taifa la Leo. Kwa sababu hiyo basi hoja yangu kuhusu Zitto haikugusia umri wa Zitto bali uchanga wake katika masuala mbalimbali ya siasa. (Huo ni mtazamo wangu).

Uamuzi wangu wa kuandika makala hii na kueleza 'maono yangu ya kisiasa' kuhusu anguko la Zitto ninaloliona, halimaanishi hata kidogo kuwa ninamuombea mwanasiasa huyo kijana baya lolote, zaidi ya tu ya kumtaka atambue uzito wa wajibu ambao anaelekea kuuchukua.

Napenda kusema bayana kwamba anguko naloliona likimkabili Zitto si la kushinda au kushindwa katika kinyang'anyiro cha uenyekiti wa taifa wa Chadema. Anguko ninaloliona kwa Zitto litakuja akishindwa na hata akishinda wadhifa huo anaogombea.

Ni kwa sababu hiyo katika makala hiyo nilimtaja James Mbatia ambaye alipoamua kugombea uenyekiti wa NCCR akiwa na lengo la kupambana na Marando kwa sababu tu ya makosa kadha wa kadha ya kimaamuzi ambayo Marando aliyasimamia na kukiletea matatizo chama hicho, aliishia kukiingiza shimoni kabisa chama hicho na hata baada ya kushinda wadhifa huo.

Nilitegemea wachangiaji wangempima Zitto wa Chadema kwa kumlinganisha na Mbatia na Marando wa NCCR Mageuzi kwanza, kabla ya kukimbilia na kumlinganisha Nyerere aliyeshika madaraka akiwa mdogo wa miaka 32 ndani ya Tanu na miaka 39 akiwa rais wa Tanzania.

Kwa mantiki hiyo hiyo, nilitarajia kusikia wachangiaji wakijenga hoja yao ya anguko la Zitto kwa kuangalia mahitaji ya vyama vya siasa vya upinzani wakati huu, ukiwa ni mwaka mmoja kabla ya Uchaguzi Mkuu.

Aidha matarajio yangu yalikuwa ni kuona watu wakimpima Zitto kwa kuangalia vigezo vya namna anavyoweza kuwaongoza watu na si kujiongoza mwenyewe kwa namna ya kuonyesha njia chini ya msingi imara wa uwajibikaji wa pamoja na si wa kila mtu kujitafutia umaarufu wake binafsi.

Kwa kusema hivi sina maana hata kidogo kwamba, Zitto hana uwezo wa kiuongozi bali kwa namna ninavyomfahamu nimetumia neno 'mwanasiasa mchanga' nikimaanisha kuwa ni mtu anayepaswa kujifunza masuala mengi katika kuongoza.

Katika hili ni makosa kulinganisha umri wa Zitto na wa Nyerere na kuishia katika kigezo hicho na kusahau ukomavu, nidhamu na namna viongozi hao wawili wanavyotofautiana katika medani ya kiuongozi.

Pengine ni wale tu tunaomfahamu Zitto vizuri ndiyo tunaojua namna alivyo tayari kujenga hoja zake binafsi pasipo kujali msingi wa msimamo wa chama chake katika jambo hilo hilo tena hadharani, Je mtu wa namna hiyo anafaa kuwa Mwenyekiti wa Chama.

Zitto ni shahidi kwamba siku zote amekuwa akihimizwa kutambua dhana ya uwajibikaji wa pamoja ndani ya chama chake akiwa mbunge jambo ambalo hadi leo hii kijana huyu anaonekana kulipuuza (huo ni mtazamo wangu).

Ni kwa sababu hiyo nilimuita mchanga na kuona anao muda wa kujifunza zaidi masuala kadhaa ya kiuongozi kabla hajapewa dhamana kubwa ya kuwa mwenyekiti na hivyo kuishia akianguka.

Ukiacha hayo, nimesikitishwa na wachangiaji ambao wamefikia hatua ya kunihusisha na ufisadi hata kutunga uongo kwamba eti mimi na Muhingo Rweyemamu tumenunuliwa magari yanayofanana na ambayo yanafuatana namba. Hakika huu ni upuuzi na uongo.

Ni kweli mimi na Muhingo tuna magari yanayofanana. Mbali ya kuwa kaka yangu, Muhingo ni rafiki yangu mkubwa. Nilinunua gari kwa fedha zangu na nyingine nikapewa kwa nyakati tofauti na mwajiri wangu.

Nikiwa nimeshalitumia gari langu kwa miezi mitatu, Muhingo alilipenda na nikampeleka kwa watu ambao waliniuzia kwa kuliagiza kutoka Japan. Alipofika pale akasema anahitaji gari kama langu na wakati huo namba za usajili zilikuwa zimesogea sana. Ni kwa nini Watanzania tumejenga tabia ya kusema hata kabla hatutafanya uchunguzi wa kutosha? Haya ni maradhi ambayo mara nyingi nimekutana nayo JF. Hata hivyo siku zote ukweli utasimama.

Ni jambo la kusikitisha sana kwamba, hivi sasa mtu anapotoa maoni yake ambayo huonekana kuwa tofauti na mawazo ya wengi basi mtu huyo hupewa majina mengi machafu; ametumwa, amehongwa au anajipendekeza.

Huku tukijua umuhimu wa watu kuheshimu maoni tofauti ya watu kwani ndiyo msingi wa maendeleo, wengi wetu tumekuwa tukikimbilia kuwahukumu wenzao. Nimefikwa na hali hiyo mara nyingi tu na hata Zitto mwenyewe amekuwa majeruhi wa tuhuma hizo hizo.

Kwa kusema hivyo simaanishi hata kidogo kwamba watu hawatumiwi au hawatumwi au hawajipendekezi, la hasha ninachotaka kusema hapa ni kutokuwa wepesi kuhukumu watu kwa sababu tu ya hisia. Haya ni maradhi ya hatari na ambayo kwa kiwango kikubwa yamekuwa yakiwakatisha tamaa wachambuzi wengi wenye mioyo dhaifu.
 
Huu ni wakati wa CHEDEMA kutumia opportunity ya mgogoro wa ndani kwa ndani ndani ya CCM na nuamko uliojitokeza miongoni mwa wananchi kwa sasa, watanzania wako0 tayari tatizo kubwa ni imani yao kwa CHAMA mbadala bado haijawa kubwa vya kutosha kuweza kuitoa CCM madarakani,CHADEMA haipaswi kulizika na mafanikio iliyonayo mpaka sasa,tukumbuke kuwa NCCR walishafikia zaidi ya umaarufu wa sasa wa CHADEMA na CUF walifikia umaarufu huu lakini leo hii imani ya watanzania(kwa CUF bara) kwa vyama hivi imekufa kwa kiasi kikubwa na uwezekano wao kuchukua dola umekwisha kabisa.

CHADEMA lazima ifanye zaidi ya walivyofanya NCCR,zaidi ya walivyofanya CUF kwa kujenga imani ya watanzania na kujenga safu ya chama inayoonekana na yenye kuaminika kuweza kubeba uongozi wa taifa na kuliendesha taifa kwa mafanikio,na haitawezekana kufikia huko kwa kauli za vitisho,na kulalamikalalamika na kuwa driven na matukio(ufisadi n.k),ni lazima CHAEMA ipeleke kwa watanzania ajenda mbadala za kulikwamua taifa kutosha kwenye hali ya mkwamo ya kiuchumi.

Kuwa na akili ni pamoja na kujua unachokiweza na usichokiweza,nakubaliana na ZITO kuwa ili CHADEMA iwe tayari kuchukua dola inahitaji kufanya zaidi ya ilivyo sasa,lakini hilo litawezekana tu kama Chama kiutakuwa kimoja na kisicho na migogoro na kitawaingiza watanzania wengi zaidi wenye uwezo na kuhakikiwa vya kutosha kwa kuanzia atleast kwenye majimbo yote ndani ya nchi hii,ni process na inahitaji muda na resources(pesa) za kutosha,pamoja tutaweza kuikomboa nchi hii.

iliyopo kwa
 
Mkuu Bora umeamua kujitokeza ukajibu walau hoja chache. Si unaona faida ya kuwa Mwana-JF japo sidhani kama kweli umejiunga leo. Au ndo akina guests or multiple IDs!

.....Ni kwa nini Watanzania tumejenga tabia ya kusema hata kabla hatutafanya uchunguzi wa kutosha? Haya ni maradhi ambayo mara nyingi nimekutana nayo JF.

Kumbe tuko nawe kila siku humu. Ulikuwa kama Guest nini kaka maana naona:
Join Date: Thu Aug 2009
Posts: 3
Thanks: 0
Thanked 4 Times in 2 Posts

Karibu sana tukate nyanga humu. Tena inaelekea uko fiti sana.

Thanks Though
 
.

Naamini Zitto mwenyewe angekuwa mkweli na muwazi angeweza kuwathibitishia wana JF wengine kuhusu maoni yangu katika masuala mbalimbali ya kisiasa likiwamo hili ambalo linamgusa yeye moja kwa moja

.....

Pengine ni wale tu tunaomfahamu Zitto vizuri ndiyo tunaojua namna alivyo tayari kujenga hoja zake binafsi pasipo kujali msingi wa msimamo wa chama chake katika jambo hilo hilo tena hadharani, Je mtu wa namna hiyo anafaa kuwa Mwenyekiti wa Chama.

Zitto ni shahidi kwamba siku zote amekuwa akihimizwa kutambua dhana ya uwajibikaji wa pamoja ndani ya chama chake akiwa mbunge jambo ambalo hadi leo hii kijana huyu anaonekana kulipuuza (huo ni mtazamo wangu).
Kaka unazidi kulikoroga. Sasa haya ya kukubali dhana ya uwajibikaji wa pamoja ndani ya chama hata kama yeye anaona ni makosa si ndio yaleyale ya wiki iliyopita ya sakata la NEC-CCM Vs Sitta na wenziwe?

Ujana ni uthubutu, isingekuwa uthubutu wa Mwalimu hata Tanzania tusingepata uhuru kwa style na wakati ule kwani wapo waliokuwa wakiamini kuwa muda bado, yeye ni mchanga, mvaa makaputura hawezi kuongoza n.k..

omarilyas
 
..Mbowe awaachie wengine wajaribu.

..nadhani akiondoka Mbowe basi hoja za kuiandama Chadema kwa Udini na Ukabila zitakwisha.
 
Katika hili ni makosa kulinganisha umri wa Zitto na wa Nyerere na kuishia katika kigezo hicho na kusahau ukomavu, nidhamu na namna viongozi hao wawili wanavyotofautiana katika medani ya kiuongozi.

.
Kimsingi mimi tatizo langu na wengi ni pale wanapotaka tuamini kwamba watu maarufu ni watu exptional. zito ni maarufu lakini si Exptional kama nyerere.

Tyson ni Tyson lakini ni ujinga kuamini kwamba hata Matumla naye anaweza kuwa kama Tyson. majaaliwa kwa binadamu hayawezi kuwa sawa, na ndiyo maana ingawa kumeshatokea wachezaji mahirikuliko Pele, lakini Pele atabakia kuwa Pele.

Mimi naamini kwamba Zito ana safari ndefu ili awe na sifa ya kuwa kiongozi. kasoro yake kubwa ninayoijua mimi ni kwamba Zito anaamini ana "akili" nyingi sana na hili linasababisha awe ni mwanasiasa anayedharau ushauri wa wenzake hata wale waliomzunguka.

Tuwe tunayasema mambo tunayoyajua kiundani. Obama ana miaka 47 na siyo 32 kama ya Zitto, na pia Kabila hakuingia madarakani kidemokrasia na wala hatawali kidemokrasia bali kwa mtutu wa bunduki.

Nakumbuka mwaka 1995 Mwalimu alipomwambia Kikwete muda wake wa kuwa Rais bado, watu tulitafsiri kwamba labda anazungumzia Umri. tumempa nchi akiwa na miaka 55 kituko chake ndiyo hiki, jee angepewa akiwa na miaka 45 ingekuwaje. Mwl. alimaanisha akili ya Muungwana ilikuwa haijakomaa kuwa Rais wa Nchi, kama na mimi (bila ya kushawishiwa na Kibanda) ninavyoaamini kuwa muda wa Zitto kuwa Mwenyekiti wa CHADEMA haujafika bado!
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom