Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Kibanda: Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Status
Not open for further replies.
pia tuelewe chama cha siasa lazima kiwe na vuguvugu la uchaguzi ...haya ni maendeleo ukiona chama kinafanya uchaguzi wa kumpigia mwenyekiti kura ya ndio au hapana ujuwe hakuna demokrasia ......au kuna demokrasia ya woga...
 
Kwanza napenda kuwafahamisha wachangiaji wa JF kwamba niliandika makala ya uchambuzi (analysis) iliyochapishwa katika ukurasa wa 11 wa maoni na mawazo ya watu binafsi. Baadhi ya watu wamenihukumu kwa kuwa bias wakati yale ni maoni na si habari kama inavyodaiwa na kuelezwa na wachangiaji mbalimbali.

Pili haikuwa lengo langu kuanika udhaifu wa mtu yeyote katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti. Mimi binafsi naamini katika demokrasia lakini pia natambua kwamba demokrasia ikitumika vibaya inaweza kutumika vibaya.

Pengine nilichokisahau ni kuandika pia kwamba, Zitto, Mbowe na wana Chadema walipaswa kutambua kuwa wanakwenda katika uchaguzi wa ndani katika chama chao wakati wakiwa tishio kubwa kwa CCM na katika kipindi kifupi sana kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.

Kwa sababu hiyo basi, wote wanapaswa kuwa makini kuepuka kuzalisha vidonda ambavyo vinaweza kusababisha chama hicho kikawa dhaifu sana badala ya kuwa imara wakati huu. Ni kwa mantiki hiyo nilitumia neno 'anguko' nikionyesha hofu ya kupwaya kwa chama hicho.

Hata hivyo nikiwa mwanahabari, natambua baadhi ya maoni ya wachangiaji wanaojifanya wakimtetea Zitto ni vijana wa CCM ambao tumewasikia mitaani wakisema 'acha Zitto apewe tuwaonyesha jeuri ya CCM'.

Niseme wazi nimekuwa nikiamini siku zote kwamba Zitto ni 'visionary leader' na ambaye kwake yeye hutanguliza maslahi ya chama chake kabla ya yake binafsi. Naamini anaweza akatimiza malengo yake yote mengine ya kisiasa pasipo kuwa mwenyekiti.

Tunaweza kusema lolote tunalolipenda lakini wako watu ambao wanao uwezo wa kujisifu kwamba wameifikisha Chadema na Zitto hapo walipo leo, miongoni mwa watu hao ni sisi 'Wahariri wa Tanzania Daima' ambao siku zote tume-shape ajenda za huyu kijana shupavu.

Nautambua ujasiri wake, nauenzi uwezo wake lakini pia nautambua udhaifu wake kama kiongozi. Anao uhuru wa kukataa au kuukubali ushauri. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.


Kibanda nisaidie kuelewa hapa .Wanasema Zitto achukue waonyeshe jeuri ya Chama in what way ? Jeuri hiyo ambayo wataionyesha baada ya Mbowe na si muda wote ambao Mbowe yupo madarakani ? Wanataka kuonyesha nini hasa labda utusaidie kuweke sawa kila jambo litusidie kujua pa kusimamia .Tupe maana ya wao kuonyesha jeuri ya Chama baada ya Zitto kutwaa madaraka Chadema if at all atapewa uongozi tafadhali .
 
katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti.

- Ndugu Kibanda, kwanza karibu sana JF Kumkoma Nyani na Where We Dare, ninajaribu kutafakari kwa makini sana maneno yako na hii post, sasa wakati bado ninajaribu ku-catch the spirit na motivation behind your post, naomba kukuuliza hivi nini maana hayo maneno juu?

- Halafu what CCM has to do na Zitto kutaka kugombea uongozi wa juu wa Chadema, hapo I am lost nisaidie kidogo mkuu!

- And then nitakupa my peace of mind na post yako, otherwise karibu sana mkuu.

Respect.


Field Marshall Es!
 
Mbowe ana udhaifu wake tena wa hali ya juu sana, lakini siyo kwenye kila kitu. lakini dhamira yake ya kuijenga CHADEMA ni kubwa zaidi kuliko ya Zitto.

Zitto anajifikiria yeye na "akili" zake nyingi na umaarufu alionao kwa sasa. yeye ni Naibu Katibu mkuu wa Chama inakuwaje kwa miezi mitatu mfululizo ashindwe kufika makao Makuu ya chama chake tena kikiwa kwenye mchakato wa kuelekea kwenye uchaguzi wake wa ndani ya Chama?

Kama Katibu, mikakati yake ya kuhakikisha Chama kinaongeza idadi ya viongozi wa ngazi ya serikali za mitaa ikoje?

Sena kingine,

Naibu katibu mkuu anaweza kuwa ziarani vijijini au nje ya nchi kwa muda huo.
 
Tatizo moja la waandishi wetu wengi (wachache wanafanya) ni kuandika bila kuongozwa na falsafa yeyote ya kimantiki. Ukiandika bila falsafa lazima utajichanganya kwa kukosa consistency. Ndio maana sio vigumu kuelewa maandishi ya Jenerali Ulimwengu kwa sababu yeye ana mtazamo na falsafa fulani kwenye uandishi wake kiasi kwamba ukisoma kichwa cha habari na aya mbili za mwanzo unaweza kupata picha anapoelekea. Sasa bahati mbaya waandishi wa namna hii kwa nchi zetu hizi sio wengi, ni kiduchu.

Ukisoma article hii ya juzi ya Kibanda na ukasoma na zingine kadhaa za nyuma huwezi kuamini kama ni mtu huyuhuyu anayeandika au namna gani. Huyu ni Kibanda ambaye siku zote amekuwa akimwandika Zitto kwamba ni hero na sifa kemukemu. Mimi siku zote nilidhani kwamba anaunga mkono mawazo fulani ambayo Zitto anasimamia. Sasa leo ghafla anamtabiria Zitto anguko kisa kagombea uenyekiti, tena utabiri wenyewe ambao hauna msingi wa kimantiki.

Hata hivyo kuna vitu kadhaa vya angalizo na vya kielimu ambavyo ni vizuri mwenzetu Kibanda akatambua

i) Kibanda anashangaa leo Zitto kusema kwamba wanatofautiana na Mbowe katika msimamo wa kiitikadi. yaani Kibanda ulikuwa hujui hili? Siku zote msimamo wa Zitto kiitikadi umekuwa tofauti kabisa na mwasisi wa chama hicho mzee Mtei, achilia mbali Mbowe. Msimamo wa Zitto kiitikadi na baadhi yetu katika chama hicho ni mlengo wa kushoto wakati msimamo rasmi wa chama uliopo katika vitabu ni mlengo wa kati. Na hapa tumejitahidi katika makongamano mbalimbali kusogea kidogo kushoto mwa mzee Mtei maana yeye alikuwa kulia kabisa. Sasa wewe kama hili nalo ulikuwa hujui sijui ushabiki wako kwa Zitto ulikuwa based kwenye nini hasa?

ii) Hakuna cha ajabu viongozi katika chama kuwa na misimamo tofauti ya kiitikadi, na wala hakuna cha ajabu kiongozi kwenda tofauti kimsimamo na chama chake, madamu anazingatia zile zinaitwa core principles za chama. Ndio maana ukienda Uingereza Conservatives ya leo ni tofauti kabisa na Conservatives ya akina Margareth Thatcher. Mwaka 2005 walipokuwa wanapambana kuwania uongozi wa chama kati ya Davis Davis na David Cameron walikuwa na misimamo tofauti kabisa. Actually, David Cameron alikuwa labelled kwamba anakwenda kuharibu misingi ya Conservatives na hii ndiyo ilikuwa kete ya Davis Davis, lakini hatimaye David Cameron alishinda na ameibadilisha kabisa Conservatives hadi sasa inakubalika kwa jamii ya Uingereza. Vivyo hivyo Barack Obama alionekana wakati wa kampeni na ndiyo alivyo anavyoonekana sasa kwamba yupo too left to the left of the Democracts; he is almost seen as a socialist. Kibanda soma haya mambo yatakusaidia sana kujenga hoja zako, vinginevyo utaonekana unashambulia watu bila msingi wowote, na hakuna kitu kibaya kwa mwandishi kuandika uandishi ambao unaonekana umetumwa!!

iii) Uandishi ulioibuka nao ni wa ajabu kidogo maana ni conclusive, judgemental, sadistic and cynical, and all these are basic and fundamental qualities of poor and unprofessional writing, which are completely unexpected of Mhariri Mkuu!! Kwa mtu anayejua uandishi hana sababu ya kusoma article yako baada ya kusoma heading.

iv) Unafanya makosa makubwa ya kimantika kulinganisha aftermath ya NCCR baada ya mchuano wa Mbatia na Marando. Kimsingi NCCR ilikufa kabla ya uchaguzi uliomuweka Mbatia madarakani. Iliuugua Tanga na ilikuja kufa kufuatia kuondoka kwa Mrema. Walichokuwa wanagombania Mbatia na Marando ni mtu wa kuizika na kuwa msimamizi wa mirathi ya NCCR, mazingira ambayo ni tofauti kabisa na yaliyopo CHADEMA ya leo. Wakati NCCR wanaenda kufanya uchaguzi mkuu wajumbe zaidi ya 3/4 wa mkutano mkuu walikuwa fake maana walikuwa hawajafanya uongozi katika ngazi za chini. Leo hii tunapoenda kwenye uchaguzi wiki ijayo ndani ya CHADEMA tunatoka kwenye uchaguzi mkali kabisa katika ngazi za majimbo, wilaya na mikoa. Two different contexts. Ni ajabu kwamba mwandishi mwenye kiwango cha Mhariri Mkuu anafanya ulinganifu ambao hauna mantiki.

v) Labda Kibanda na wengine wanaopinga Zitto kugombea watueleze kidogo-tatizo ni nini hasa kwa Zitto kugombea? Ni kwamba hafai? Ni vibaya kumpinga Mbowe kwa sababu kaitendea CHADEMA makubwa? Kwa nini jana Zitto alikuwa 'hero' wa Kibanda na wengine, ghafla anageuka msaliti kwa sababu tu anagombea uenyekiti kwa taratibu sahihi kabisa ambazo zimewekwa na chama chake? What is exactly the problem.

vi) Mwisho nitoe maoni yangu kuhusu huu mchakato. Kuna watu wengi wana wasiwasi sana na hatima ya CHADEMA kwa kuwa watu wawili wazito wanagombea uenyekiti. Pengine wana haki ya kuwa na wasiwasi kwa sababu ya utamaduni wetu tuliokuzwa nao katika nchi hii na katika bara la Afrika kwa ujumla. Tumekuzwa kwamba mkubwa huwa hapingwi, na ukimpinga mkubwa wewe ni msaliti. Tumekuzwa na kukulia katika mfumo wa CCM ambao tumezoea mwenyekiti wa chama akipita bila kupingwa. Huu ni utamaduni uliodumu kwa zaidi ya miaka 50, na watu wamezeeka nao. Kwa hiyo ni lazima watu washtushwe na Zitto kugombea, tena akimpinga rafiki yake wa karibu kabisa aliyemlea katika siasa. Watu wamenuna. Wamevimba uso. Wengine wameacha na kutusalimia kisa wengine tumeweka waziwazi msimamo wetu wa kumuunga mkono Zitto. Understandable given our history and our political traditional realities. Lakini CHADEMA haipaswi kuyumba kwa sababu ya kuwa na ushindani mkali. Kinyume chaka CHADEMA inapaswa kuibuka even stronger baada ya uchaguzi huu na kutoa somo la maana ya demokrasia kwa watanzania. CHADEMA itasambaratika tu endapo wagombea na wapambe wao watakubali ushabiki wa waandishi kama akina Kibanda wa kuendesha kampeni kwa msingi wa kuchafuana majina na kuibulia kashfa za kubuni na kufikirika, kama hizo za kusema mgombea fulani ametumwa. Kwa hiyo ushauri wangu ni kwamba wagombea wote wawili na wapambe wao waendesha kampeni zilizojengwa katika msingi wa issues, kwamba:

a) Zitto atueleze kwa nini anagombea na kwa nini tumpe yeye uenyekiti badala ya mwenyekiti tuliyemzoea na ambaye amemlea kisiasa

b) mbowe atueleze kwa nini tumchague tena; anataka kufanya nini ambacho ameshindwa kufanya katika kipindi cha miaka mitano tangu awe mwenyekiti wa CHADEMA, na pengine kwa nini yeye awe mwenyekiti kwa awamu mbili wakati wenzake wote waliopita walikaa kwa wamu moja moja?

Kama tukiendesha kampeni za namna hii sioni sababu chama kisambaratike. Tatizo ni hapo upande mmoja unapoanza kampeni kwa kutabiria wengine maanguko na kuwaona wengine wanagombea kwa sababu wametumwa kukimaliza chama. Huo utakuwa uchuro na ndio maana ni muhimu sana kwa wana chadema kuyapuuza maandishi ya akina Kibanda na mwenzake Restuta James.
 
Kwanza napenda kuwafahamisha wachangiaji wa JF kwamba niliandika makala ya uchambuzi (analysis) iliyochapishwa katika ukurasa wa 11 wa maoni na mawazo ya watu binafsi. Baadhi ya watu wamenihukumu kwa kuwa bias wakati yale ni maoni na si habari kama inavyodaiwa na kuelezwa na wachangiaji mbalimbali.

Pili haikuwa lengo langu kuanika udhaifu wa mtu yeyote katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti. Mimi binafsi naamini katika demokrasia lakini pia natambua kwamba demokrasia ikitumika vibaya inaweza kutumika vibaya.

Pengine nilichokisahau ni kuandika pia kwamba, Zitto, Mbowe na wana Chadema walipaswa kutambua kuwa wanakwenda katika uchaguzi wa ndani katika chama chao wakati wakiwa tishio kubwa kwa CCM na katika kipindi kifupi sana kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.

Kwa sababu hiyo basi, wote wanapaswa kuwa makini kuepuka kuzalisha vidonda ambavyo vinaweza kusababisha chama hicho kikawa dhaifu sana badala ya kuwa imara wakati huu. Ni kwa mantiki hiyo nilitumia neno 'anguko' nikionyesha hofu ya kupwaya kwa chama hicho.

Hata hivyo nikiwa mwanahabari, natambua baadhi ya maoni ya wachangiaji wanaojifanya wakimtetea Zitto ni vijana wa CCM ambao tumewasikia mitaani wakisema 'acha Zitto apewe tuwaonyesha jeuri ya CCM'.

Niseme wazi nimekuwa nikiamini siku zote kwamba Zitto ni 'visionary leader' na ambaye kwake yeye hutanguliza maslahi ya chama chake kabla ya yake binafsi. Naamini anaweza akatimiza malengo yake yote mengine ya kisiasa pasipo kuwa mwenyekiti.

Tunaweza kusema lolote tunalolipenda lakini wako watu ambao wanao uwezo wa kujisifu kwamba wameifikisha Chadema na Zitto hapo walipo leo, miongoni mwa watu hao ni sisi 'Wahariri wa Tanzania Daima' ambao siku zote tume-shape ajenda za huyu kijana shupavu.

Nautambua ujasiri wake, nauenzi uwezo wake lakini pia nautambua udhaifu wake kama kiongozi. Anao uhuru wa kukataa au kuukubali ushauri. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.

Mara useme anaungwa mkono na vijana wa CCM mara vijana wajinga wa Chadema. mara ume SHAPE AGENDA YA KIJANA HUYU.

habari kuu kwenye gazeti lako ukurasa wa kwanza uliandika kuwa ZITTO AZUA MJADALA. kwanini usiandike Zitto na Mbwe wazua mjadala?

Mbona wamarekani hawakuwa na Hofu kumpa kura OBAMA kama hofu uliyonayo wewe? pia hujatuambia nini cheo chako Chadema hadi ujue kuwa kuna vijana wajinga ndio wanamuunga mkono Zitto?nilitegemea maneno hayo aseme Katibu mkuu wa Chadema. pia kama Zitto anaungwa mkono na vijana wajinga kwa tafsiri ya haraka nae ni Mjinga. kwani mwelevu anaungwa mkono na welevu wenziwake.

mkuu Mwache Zitto akibadili chama kutoka kwenye NGO na kuwa Chama chenye sifa ya kitaifa?

Zitto kwa nia yake anataka awe mwenyekiti.Mbowe umeandika kuwa alikuwa hataki ila wazee wamemlazimisha.mtu hatakiwi kufanya kazi kwa kulazimishwa afanye kwa hiyari yake bila kulazimishwa na wazee.

KIBANDA umembomoa Zitto.

kama ulishape agenda yake kwanini wewe usiwe mbunge wa Chadema? wewe si mwanafunzi wa Muhingo Rweyemamu jee anakusimanga kuwa alishape agenda yako ya kumfagilia Mbowe?
 
Kwanza napenda kuwafahamisha wachangiaji wa JF kwamba niliandika makala ya uchambuzi (analysis) iliyochapishwa katika ukurasa wa 11 wa maoni na mawazo ya watu binafsi. Baadhi ya watu wamenihukumu kwa kuwa bias wakati yale ni maoni na si habari kama inavyodaiwa na kuelezwa na wachangiaji mbalimbali.

Pili haikuwa lengo langu kuanika udhaifu wa mtu yeyote katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti. Mimi binafsi naamini katika demokrasia lakini pia natambua kwamba demokrasia ikitumika vibaya inaweza kutumika vibaya.

Pengine nilichokisahau ni kuandika pia kwamba, Zitto, Mbowe na wana Chadema walipaswa kutambua kuwa wanakwenda katika uchaguzi wa ndani katika chama chao wakati wakiwa tishio kubwa kwa CCM na katika kipindi kifupi sana kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.

Kwa sababu hiyo basi, wote wanapaswa kuwa makini kuepuka kuzalisha vidonda ambavyo vinaweza kusababisha chama hicho kikawa dhaifu sana badala ya kuwa imara wakati huu. Ni kwa mantiki hiyo nilitumia neno 'anguko' nikionyesha hofu ya kupwaya kwa chama hicho.

Hata hivyo nikiwa mwanahabari, natambua baadhi ya maoni ya wachangiaji wanaojifanya wakimtetea Zitto ni vijana wa CCM ambao tumewasikia mitaani wakisema 'acha Zitto apewe tuwaonyesha jeuri ya CCM'.

Niseme wazi nimekuwa nikiamini siku zote kwamba Zitto ni 'visionary leader' na ambaye kwake yeye hutanguliza maslahi ya chama chake kabla ya yake binafsi. Naamini anaweza akatimiza malengo yake yote mengine ya kisiasa pasipo kuwa mwenyekiti.

Tunaweza kusema lolote tunalolipenda lakini wako watu ambao wanao uwezo wa kujisifu kwamba wameifikisha Chadema na Zitto hapo walipo leo, miongoni mwa watu hao ni sisi 'Wahariri wa Tanzania Daima' ambao siku zote tume-shape ajenda za huyu kijana shupavu.

Nautambua ujasiri wake, nauenzi uwezo wake lakini pia nautambua udhaifu wake kama kiongozi. Anao uhuru wa kukataa au kuukubali ushauri. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.

Duh! Kweli huyu Kibanda!
 
Wanajamvi,
Mimi binafsi simuamini sana Zitto kutokana na matukio mengine siku za nyuma. Nimeandika mara nyingi sana humu ndani kuhusu mwenendo na ushirika wa karibu wa Zitto na wale wanaotajwa kuwa mafisadi na chama chake cha CHADEMA. Mimi nina uhakika kabisa ZItto ni mtu wa karibu sana na RA hilo wala hawezi kulikanusha na pia ni mtu wa karibu sana na Bashe ambaye yupo karibu sana na RA.
Hebu tufanye litmus paper test:

Kwa kuwa moja ya contemporary agenda ya CHADEMA ni kupinga ufisadi, na kwa kuwa Slaa kwa niaba ya CHADEMA alisoma listi ya mafisadi na RA akiwemo pamoja na JK, na kwa kuwa Zitto akishinda uenyekiti atalazimika kuendeleza agenda ya chama chake kutaka waliotajwa katika orodha ya mafisadi wanachukuliwa hatua. Mimi binafsi siamini kama Zitto ataendeleza hiyo ajenda kwa vile haamini waliotajwa na Slaa kuwa ni mafisadi , ndio maana juzi kawasifia sana Zakia Meghji, Chenge Andrew na Mrema wa TANROADS kuwa walimsaidia kujengwa barabara jimboni kwake Kigoma as if watu hao walitoa fedha mifukoni mwao. Hao wote aliowasifia wanatajwa sana humu JF kama mafisadi. Kwanini asimsifie hata meneja wa mkoa wa TANROADS au naibu waziri?

Kwa maana nyingine ina maana watu hao walimfanyia favour, maana hakustahili. Swali, kwanini wamfanyie upendeleo yeye wakati wabunge wengine wa upinzania hata wale wapinga ufisadi ndani ya CCM majimbo yao yametelekezwa hakuna kupeleka fedha wala miradi yoyote ya maendeleo (rejea mjadala wa Mwakyembe Vs Mwakalinga).

Ni Zitto huyo huyo aliyeunga mkono kampuni ya Dowans ituuzie mitambo kitapeli, hali akijua hali halisi ya mambo, ni huyo huyo aliyeteuliwa kinamna kwenye kamati ya rais ya madini hata ripoti yake ilipotua kwanza mikono mwa yule mzungu Sinclair? Zitto hakushtuka kabisa- labda vile alishajua.

Sasa namtaka Zitto aje hapa, asema je Rostam ni fisadi kama Slaa alivyosema? huu ndio mtihani naompa. Wengine mnaweza kuona ni upuuzi ila mimi naeelewa uhusiano wa Zitto na RA najua nafanya nini.

Kuhusu Kibanda ameshundwa kujebga hoja na kwa vile TD linajulikana kuwa ni la ''CHADEMA'' ilikuwa ni makosa yeye kuwa na upande katika uchaguzi ht kama anampenda Mbowe au Zitto hakupaswa kusema hvyo maana anajenga uhasama- kwa njia rahisi naweza kusema ''ametumika'' maana siku hizi naye haaminiki sana.

Nawasilisha
 
Last edited:
Kwanza napenda kuwafahamisha wachangiaji wa JF kwamba niliandika makala ya uchambuzi (analysis) iliyochapishwa katika ukurasa wa 11 wa maoni na mawazo ya watu binafsi. Baadhi ya watu wamenihukumu kwa kuwa bias wakati yale ni maoni na si habari kama inavyodaiwa na kuelezwa na wachangiaji mbalimbali.

Pili haikuwa lengo langu kuanika udhaifu wa mtu yeyote katika ile makala bali lengo langu lilikuwa ni kumuonyesha Zitto athari za kuitumia ndivyo sivyo haki yake ya kikatiba ya kugombea uenyekiti. Mimi binafsi naamini katika demokrasia lakini pia natambua kwamba demokrasia ikitumika vibaya inaweza kutumika vibaya.

Pengine nilichokisahau ni kuandika pia kwamba, Zitto, Mbowe na wana Chadema walipaswa kutambua kuwa wanakwenda katika uchaguzi wa ndani katika chama chao wakati wakiwa tishio kubwa kwa CCM na katika kipindi kifupi sana kabla ya kufanyika kwa Uchaguzi Mkuu.

Kwa sababu hiyo basi, wote wanapaswa kuwa makini kuepuka kuzalisha vidonda ambavyo vinaweza kusababisha chama hicho kikawa dhaifu sana badala ya kuwa imara wakati huu. Ni kwa mantiki hiyo nilitumia neno 'anguko' nikionyesha hofu ya kupwaya kwa chama hicho.

Hata hivyo nikiwa mwanahabari, natambua baadhi ya maoni ya wachangiaji wanaojifanya wakimtetea Zitto ni vijana wa CCM ambao tumewasikia mitaani wakisema 'acha Zitto apewe tuwaonyesha jeuri ya CCM'.

Niseme wazi nimekuwa nikiamini siku zote kwamba Zitto ni 'visionary leader' na ambaye kwake yeye hutanguliza maslahi ya chama chake kabla ya yake binafsi. Naamini anaweza akatimiza malengo yake yote mengine ya kisiasa pasipo kuwa mwenyekiti.

Tunaweza kusema lolote tunalolipenda lakini wako watu ambao wanao uwezo wa kujisifu kwamba wameifikisha Chadema na Zitto hapo walipo leo, miongoni mwa watu hao ni sisi 'Wahariri wa Tanzania Daima' ambao siku zote tume-shape ajenda za huyu kijana shupavu.

Nautambua ujasiri wake, nauenzi uwezo wake lakini pia nautambua udhaifu wake kama kiongozi. Anao uhuru wa kukataa au kuukubali ushauri. Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.

Kibanda,

Yaani hii mistari yako imetengeneza kumbukumbu ya history ambayo inaweza kukusafishia madhambi yako ya kula nyama chungu kimoja na Zitto; yaani kuwa ndani ya Payroll ya RA.

Si unakumbuka tukiwa Business Times 2005 wakati JK anarudi Dar baada ya kupitishwa na NEC Dodoma, Kina Ngurumo, Madata na wenye kutaza mbele waliwaambia nini waandishi waliokuwa wanashangilia JK kushinda?!! Na leo anayofanya JK ni sawa kabisa na yale ambayo waliohuzunika kupita kwake waliyatarajia.

Sasa katika suala hili la Uongozi wa CHADEMA, Zitto anakwenda kujitengenezea laana yake na upinzani Tanzania kwa ujumla. Nasema hivi kwa sababu hekima ya Zitto inakosa baadhi ya bolts muhimu katika vipaumbele vya kitaifa na halaiki anayoiongoza. Na hivi karibuni hata zile chache alizokuwanazo zimelegea sana. Angalia mifano miwili ya hivi karibuni suala la Dowans na malipo ya fidia kwa waathirika wa Barabara Jimboni kwake. Naamini Karamaghi akiwa Nishati na Madini angekubali ombi la zitto kumpelekea umeme jimboni, kama walivyofanya Chenge na Meghji kwa barabara, Zitto asingekuwa maarufu katika siasa za kitaifa kama alivyo sasa.

Lakini Kibanda kwa nini nawe unakuwa mpiganaji pale mkate unapoelekea kukosa siagi au kumwagikiwa disel?
 
- Ndugu Kibanda, kwanza karibu sana JF Kumkoma Nyani na Where We Dare, ninajaribu kutafakari kwa makini sana maneno yako na hii post, sasa wakati bado ninajaribu ku-catch the spirit na motivation behind your post, naomba kukuuliza hivi nini maana hayo maneno juu?

- Halafu what CCM has to do na Zitto kutaka kugombea uongozi wa juu wa Chadema, hapo I am lost nisaidie kidogo mkuu!

Ujumbe wangu katika hoja hii ni rahisi kabisa. Uamuzi wa Zitto kugombea uwe ni uamuzi binafsi au wa kusukumwa na watu walio ndani au nje ya Chadema unaungwa mkono sana na baadhi ya viongozi wa juu wa CCM.

Unajua kwa hulka yake (kama nilivyo mimi pia) Zitto ni mtu wa kujichanganya sana. Amekuwa akikutana na kubadilishana mawazo na makada mbalimbali maarufu wa CCM ukianzia na vijana.

Tabia yake hii imekuwa ikimkutanisha na watu mbalimbali maarufu ndani ya chama hicho ambao mara nyingi wamekuwa wakimpa changamoto nyingi.

Ni jambo jema na baya kwamba vigogo hao wa CCM anaokutana nao mara nyingi wamekuwa wakimueleza kuwa yeye ni moja ya viongozi dhabiti ndani ya Chadema ambao kwa kiwango kikubwa wanayo dhamana nzito ya kukiongoza chama.

Mbali ya hilo vigogo hao wa CCM wamekuwa hawasiti kueleza pia wasifu wa Mbowe na wa Chadema kwa ujumla. vigogo hao ambao hata sisi wana habari tumekuwa tukikutana nao wamekuwa wakimuelezea Mbowe kuwa ni mkabila (akiwapendelea wachaga), mbinafsi (anayekerwa na umaarufu na uwezo wa Zitto) na mtu mwenye elimu ndogo (wakizungumzia elimu ya darasani.

Maneno ya namna hii yanaonekana kumuingia Zitto sana akilini (uamuzi wake wa kugombea) na kuna hatari kuwa anayaamini (kwani yana sehemu ya ukweli na uongo pia).

Nimefanya kazi na viongozi wote hao wawili wa Chadema; Mbowe na Zitto na katika kipindi cha miaka mitatu wamekuwa ni watu wangu wa karibu sana.

Kwa kiwango kikubwa makala niliyoandika inasema sehemu tu ya ukweli ambao wakati mwingine ni mgumu kuuweka katika maandishi.

Naweza kukuhakikishia kuwa Mbowe si mtu mjinga wala mpumbavu (Zitto analitambua hilo), ni mtu mwenye ufahamu wa masuala makubwa na mazito ya kitaifa na kimataifa.

Mbowe ni aina ya wanasiasa ambao japo hawakupata elimu kubwa ya darasani, ametumia muda mrefu kujisomea na kujielimisha kwa njia mbalimbali.

Ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja japo kuwa wakati mwingine huelemewa na jazba za kisiasa awapo jukwaani. Si mbinafsi, japo kuwa ni 'mtoto wa mjini' kutokana na mazingira aliyoishi na kukulia.

Tabia yake ya kujiamini kutokana na uwezo wake wa kifedha na kutokuwa tayari kujichanganya katika makundi tofauti ya kijamii hususan na wana siasa wa CCM imekuwa ikimfanya wakati mwingine aonekane dhaifu, japo ukweli ni tofauti.

Hata hivyo naweza kukuhakikishia kwamba, huyu jamaa, pamoja na mapungufu yake mengi ni mpiganaji na mpambanaji ambaye CCM ina muogopa na kila njia ya kujaribu kumfitini na kumchafua inaonekana kugonga mwamba.

Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba amekuwa mzito kuchukua hatua za kukabiliana na tuhuma na shutuma nyingi za uongo zinazoelekezwa kwake.

Hata katika masuala ambayo ukimsikiliza anayo majibu mazuri na mazito kukabiliana nayo kwa hoja, yeye huamua kukaa kimya na wakati mwingine kuhamaki akitamani kuchukua hatua za kibabe kukabiliana na wazushi dhidi yake na chama chake.

Hata hivyo anabakia kuwa mtu wa vitendo na upendo mkubwa kwa Chadema pengine kuliko kiongozi mwingine yeyote ndani ya chama hicho, ukiwaacha John Mnyika na John Mrema ambao uchapakazi wao si wa kutiliwa shaka.

Zitto Kabwe si mtu wa kutulia, ni mtu mwenye mambo mengi na mara zote amekuwa ni mwanasiasa anayeishi kwa mawasiliano ya simu ya mara kwa mara na vikao vingi kila siku. Japo kuwa ni msomaji mzuri wa vitabu na magazeti, bado ni kijana ambaye hadi sasa amekosa utulivu anaopaswa kuwa nao mwanasiasa aliyekomaa.

Ni wazi kwamba akili ya Zitto inafanya kazi haraka haraka kuliko vijana wengi ndani ya chama hicho. hata hivyo kutochangamana kwake na wana Chadema wenzake katika masuala mbalimbali ya kitaifa kumempotezea ukaribu na watu wengi katika ofisi za Makao Makuu ya Chadema.

Hayo ni sehemu ya mambo ambayo Zitto anapaswa kujifunza kabla hajakabidhiwa dhamana nzito. Sidhani kwamba wapinzani kwa wakati huu, wanao muda wa kumpata Mwenyekiti wa kujifunza ustaarabu wa siasa ndani ya vyama vingi. Huo ni mtazamo wangu.
 
Tatizo moja la waandishi wetu wengi (wachache wanafanya) ni kuandika bila kuongozwa na falsafa yeyote ya kimantiki. Ukiandika bila falsafa lazima utajichanganya kwa kukosa consistency. Ndio maana sio vigumu kuelewa maandishi ya Jenerali Ulimwengu kwa sababu yeye ana mtazamo na falsafa fulani kwenye uandishi wake kiasi kwamba ukisoma kichwa cha habari na aya mbili za mwanzo unaweza kupata picha anapoelekea. Sasa bahati mbaya waandishi wa namna hii kwa nchi zetu hizi sio wengi, ni kiduchu.

Ukisoma article hii ya juzi ya Kibanda na ukasoma na zingine kadhaa za nyuma huwezi kuamini kama ni mtu huyuhuyu anayeandika au namna gani. Huyu ni Kibanda ambaye siku zote amekuwa akimwandika Zitto kwamba ni hero na sifa kemukemu. Mimi siku zote nilidhani kwamba anaunga mkono mawazo fulani ambayo Zitto anasimamia. Sasa leo ghafla anamtabiria Zitto anguko kisa kagombea uenyekiti, tena utabiri wenyewe ambao hauna msingi wa kimantiki.

Hata hivyo kuna vitu kadhaa vya angalizo na vya kielimu ambavyo ni vizuri mwenzetu Kibanda akatambua

i) Kibanda anashangaa leo Zitto kusema kwamba wanatofautiana na Mbowe katika msimamo wa kiitikadi. yaani Kibanda ulikuwa hujui hili? Siku zote msimamo wa Zitto kiitikadi umekuwa tofauti kabisa na mwasisi wa chama hicho mzee Mtei, achilia mbali Mbowe. Msimamo wa Zitto kiitikadi na baadhi yetu katika chama hicho ni mlengo wa kushoto wakati msimamo rasmi wa chama uliopo katika vitabu ni mlengo wa kati. Na hapa tumejitahidi katika makongamano mbalimbali kusogea kidogo kushoto mwa mzee Mtei maana yeye alikuwa kulia kabisa. Sasa wewe kama hili nalo ulikuwa hujui sijui ushabiki wako kwa Zitto ulikuwa based kwenye nini hasa?

ii) Hakuna cha ajabu viongozi katika chama kuwa na misimamo tofauti ya kiitikadi, na wala hakuna cha ajabu kiongozi kwenda tofauti kimsimamo na chama chake, madamu anazingatia zile zinaitwa core principles za chama. Ndio maana ukienda Uingereza Conservatives ya leo ni tofauti kabisa na Conservatives ya akina Margareth Thatcher. Mwaka 2005 walipokuwa wanapambana kuwania uongozi wa chama kati ya Davis Davis na David Cameron walikuwa na misimamo tofauti kabisa. Actually, David Cameron alikuwa labelled kwamba anakwenda kuharibu misingi ya Conservatives na hii ndiyo ilikuwa kete ya Davis Davis, lakini hatimaye David Cameron alishinda na ameibadilisha kabisa Conservatives hadi sasa inakubalika kwa jamii ya Uingereza. Vivyo hivyo Barack Obama alionekana wakati wa kampeni na ndiyo alivyo anavyoonekana sasa kwamba yupo too left to the left of the Democracts; he is almost seen as a socialist. Kibanda soma haya mambo yatakusaidia sana kujenga hoja zako, vinginevyo utaonekana unashambulia watu bila msingi wowote, na hakuna kitu kibaya kwa mwandishi kuandika uandishi ambao unaonekana umetumwa!!

iii) Uandishi ulioibuka nao ni wa ajabu kidogo maana ni conclusive, judgemental, sadistic and cynical, and all these are basic and fundamental qualities of poor and unprofessional writing, which are completely unexpected of Mhariri Mkuu!! Kwa mtu anayejua uandishi hana sababu ya kusoma article yako baada ya kusoma heading.

iv) Unafanya makosa makubwa ya kimantika kulinganisha aftermath ya NCCR baada ya mchuano wa Mbatia na Marando. Kimsingi NCCR ilikufa kabla ya uchaguzi uliomuweka Mbatia madarakani. Iliuugua Tanga na ilikuja kufa kufuatia kuondoka kwa Mrema. Walichokuwa wanagombania Mbatia na Marando ni mtu wa kuizika na kuwa msimamizi wa mirathi ya NCCR, mazingira ambayo ni tofauti kabisa na yaliyopo CHADEMA ya leo. Wakati NCCR wanaenda kufanya uchaguzi mkuu wajumbe zaidi ya 3/4 wa mkutano mkuu walikuwa fake maana walikuwa hawajafanya uongozi katika ngazi za chini. Leo hii tunapoenda kwenye uchaguzi wiki ijayo ndani ya CHADEMA tunatoka kwenye uchaguzi mkali kabisa katika ngazi za majimbo, wilaya na mikoa. Two different contexts. Ni ajabu kwamba mwandishi mwenye kiwango cha Mhariri Mkuu anafanya ulinganifu ambao hauna mantiki.

v) Labda Kibanda na wengine wanaopinga Zitto kugombea watueleze kidogo-tatizo ni nini hasa kwa Zitto kugombea? Ni kwamba hafai? Ni vibaya kumpinga Mbowe kwa sababu kaitendea CHADEMA makubwa? Kwa nini jana Zitto alikuwa 'hero' wa Kibanda na wengine, ghafla anageuka msaliti kwa sababu tu anagombea uenyekiti kwa taratibu sahihi kabisa ambazo zimewekwa na chama chake? What is exactly the problem.

vi) Mwisho nitoe maoni yangu kuhusu huu mchakato. Kuna watu wengi wana wasiwasi sana na hatima ya CHADEMA kwa kuwa watu wawili wazito wanagombea uenyekiti. Pengine wana haki ya kuwa na wasiwasi kwa sababu ya utamaduni wetu tuliokuzwa nao katika nchi hii na katika bara la Afrika kwa ujumla. Tumekuzwa kwamba mkubwa huwa hapingwi, na ukimpinga mkubwa wewe ni msaliti. Tumekuzwa na kukulia katika mfumo wa CCM ambao tumezoea mwenyekiti wa chama akipita bila kupingwa. Huu ni utamaduni uliodumu kwa zaidi ya miaka 50, na watu wamezeeka nao. Kwa hiyo ni lazima watu washtushwe na Zitto kugombea, tena akimpinga rafiki yake wa karibu kabisa aliyemlea katika siasa. Watu wamenuna. Wamevimba uso. Wengine wameacha na kutusalimia kisa wengine tumeweka waziwazi msimamo wetu wa kumuunga mkono Zitto. Understandable given our history and our political traditional realities. Lakini CHADEMA haipaswi kuyumba kwa sababu ya kuwa na ushindani mkali. Kinyume chaka CHADEMA inapaswa kuibuka even stronger baada ya uchaguzi huu na kutoa somo la maana ya demokrasia kwa watanzania. CHADEMA itasambaratika tu endapo wagombea na wapambe wao watakubali ushabiki wa waandishi kama akina Kibanda wa kuendesha kampeni kwa msingi wa kuchafuana majina na kuibulia kashfa za kubuni na kufikirika, kama hizo za kusema mgombea fulani ametumwa. Kwa hiyo ushauri wangu ni kwamba wagombea wote wawili na wapambe wao waendesha kampeni zilizojengwa katika msingi wa issues, kwamba:

a) Zitto atueleze kwa nini anagombea na kwa nini tumpe yeye uenyekiti badala ya mwenyekiti tuliyemzoea na ambaye amemlea kisiasa

b) mbowe atueleze kwa nini tumchague tena; anataka kufanya nini ambacho ameshindwa kufanya katika kipindi cha miaka mitano tangu awe mwenyekiti wa CHADEMA, na pengine kwa nini yeye awe mwenyekiti kwa awamu mbili wakati wenzake wote waliopita walikaa kwa wamu moja moja?

Kama tukiendesha kampeni za namna hii sioni sababu chama kisambaratike. Tatizo ni hapo upande mmoja unapoanza kampeni kwa kutabiria wengine maanguko na kuwaona wengine wanagombea kwa sababu wametumwa kukimaliza chama. Huo utakuwa uchuro na ndio maana ni muhimu sana kwa wana chadema kuyapuuza maandishi ya akina Kibanda na mwenzake Restuta James.

KWANINI HUKUGOMBEA ?kwa mujibu wa KIBANDA WANAOMUUNGA MKONO ZITTO NI VIJANA WA CHADEMA AMBAO NI WAJINGA, na wewe umsema unaunga mkono Zitto kugombea jee wewe uko kundi la wajinga wa Chadema?
 
Tatizo moja la waandishi wetu wengi (wachache wanafanya) ni kuandika bila kuongozwa na falsafa yeyote ya kimantiki. Ukiandika bila falsafa lazima utajichanganya kwa kukosa consistency. Ndio maana sio vigumu kuelewa maandishi ya Jenerali Ulimwengu kwa sababu yeye ana mtazamo na falsafa fulani kwenye uandishi wake kiasi kwamba ukisoma kichwa cha habari na aya mbili za mwanzo unaweza kupata picha anapoelekea. Sasa bahati mbaya waandishi wa namna hii kwa nchi zetu hizi sio wengi, ni kiduchu.

Ukisoma article hii ya juzi ya Kibanda na ukasoma na zingine kadhaa za nyuma huwezi kuamini kama ni mtu huyuhuyu anayeandika au namna gani. Huyu ni Kibanda ambaye siku zote amekuwa akimwandika Zitto kwamba ni hero na sifa kemukemu. Mimi siku zote nilidhani kwamba anaunga mkono mawazo fulani ambayo Zitto anasimamia. Sasa leo ghafla anamtabiria Zitto anguko kisa kagombea uenyekiti, tena utabiri wenyewe ambao hauna msingi wa kimantiki.

Hata hivyo kuna vitu kadhaa vya angalizo na vya kielimu ambavyo ni vizuri mwenzetu Kibanda akatambua

i) Kibanda anashangaa leo Zitto kusema kwamba wanatofautiana na Mbowe katika msimamo wa kiitikadi. yaani Kibanda ulikuwa hujui hili? Siku zote msimamo wa Zitto kiitikadi umekuwa tofauti kabisa na mwasisi wa chama hicho mzee Mtei, achilia mbali Mbowe. Msimamo wa Zitto kiitikadi na baadhi yetu katika chama hicho ni mlengo wa kushoto wakati msimamo rasmi wa chama uliopo katika vitabu ni mlengo wa kati. Na hapa tumejitahidi katika makongamano mbalimbali kusogea kidogo kushoto mwa mzee Mtei maana yeye alikuwa kulia kabisa. Sasa wewe kama hili nalo ulikuwa hujui sijui ushabiki wako kwa Zitto ulikuwa based kwenye nini hasa?

ii) Hakuna cha ajabu viongozi katika chama kuwa na misimamo tofauti ya kiitikadi, na wala hakuna cha ajabu kiongozi kwenda tofauti kimsimamo na chama chake, madamu anazingatia zile zinaitwa core principles za chama. Ndio maana ukienda Uingereza Conservatives ya leo ni tofauti kabisa na Conservatives ya akina Margareth Thatcher. Mwaka 2005 walipokuwa wanapambana kuwania uongozi wa chama kati ya Davis Davis na David Cameron walikuwa na misimamo tofauti kabisa. Actually, David Cameron alikuwa labelled kwamba anakwenda kuharibu misingi ya Conservatives na hii ndiyo ilikuwa kete ya Davis Davis, lakini hatimaye David Cameron alishinda na ameibadilisha kabisa Conservatives hadi sasa inakubalika kwa jamii ya Uingereza. Vivyo hivyo Barack Obama alionekana wakati wa kampeni na ndiyo alivyo anavyoonekana sasa kwamba yupo too left to the left of the Democracts; he is almost seen as a socialist. Kibanda soma haya mambo yatakusaidia sana kujenga hoja zako, vinginevyo utaonekana unashambulia watu bila msingi wowote, na hakuna kitu kibaya kwa mwandishi kuandika uandishi ambao unaonekana umetumwa!!

iii) Uandishi ulioibuka nao ni wa ajabu kidogo maana ni conclusive, judgemental, sadistic and cynical, and all these are basic and fundamental qualities of poor and unprofessional writing, which are completely unexpected of Mhariri Mkuu!! Kwa mtu anayejua uandishi hana sababu ya kusoma article yako baada ya kusoma heading.

iv) Unafanya makosa makubwa ya kimantika kulinganisha aftermath ya NCCR baada ya mchuano wa Mbatia na Marando. Kimsingi NCCR ilikufa kabla ya uchaguzi uliomuweka Mbatia madarakani. Iliuugua Tanga na ilikuja kufa kufuatia kuondoka kwa Mrema. Walichokuwa wanagombania Mbatia na Marando ni mtu wa kuizika na kuwa msimamizi wa mirathi ya NCCR, mazingira ambayo ni tofauti kabisa na yaliyopo CHADEMA ya leo. Wakati NCCR wanaenda kufanya uchaguzi mkuu wajumbe zaidi ya 3/4 wa mkutano mkuu walikuwa fake maana walikuwa hawajafanya uongozi katika ngazi za chini. Leo hii tunapoenda kwenye uchaguzi wiki ijayo ndani ya CHADEMA tunatoka kwenye uchaguzi mkali kabisa katika ngazi za majimbo, wilaya na mikoa. Two different contexts. Ni ajabu kwamba mwandishi mwenye kiwango cha Mhariri Mkuu anafanya ulinganifu ambao hauna mantiki.

v) Labda Kibanda na wengine wanaopinga Zitto kugombea watueleze kidogo-tatizo ni nini hasa kwa Zitto kugombea? Ni kwamba hafai? Ni vibaya kumpinga Mbowe kwa sababu kaitendea CHADEMA makubwa? Kwa nini jana Zitto alikuwa 'hero' wa Kibanda na wengine, ghafla anageuka msaliti kwa sababu tu anagombea uenyekiti kwa taratibu sahihi kabisa ambazo zimewekwa na chama chake? What is exactly the problem.

vi) Mwisho nitoe maoni yangu kuhusu huu mchakato. Kuna watu wengi wana wasiwasi sana na hatima ya CHADEMA kwa kuwa watu wawili wazito wanagombea uenyekiti. Pengine wana haki ya kuwa na wasiwasi kwa sababu ya utamaduni wetu tuliokuzwa nao katika nchi hii na katika bara la Afrika kwa ujumla. Tumekuzwa kwamba mkubwa huwa hapingwi, na ukimpinga mkubwa wewe ni msaliti. Tumekuzwa na kukulia katika mfumo wa CCM ambao tumezoea mwenyekiti wa chama akipita bila kupingwa. Huu ni utamaduni uliodumu kwa zaidi ya miaka 50, na watu wamezeeka nao. Kwa hiyo ni lazima watu washtushwe na Zitto kugombea, tena akimpinga rafiki yake wa karibu kabisa aliyemlea katika siasa. Watu wamenuna. Wamevimba uso. Wengine wameacha na kutusalimia kisa wengine tumeweka waziwazi msimamo wetu wa kumuunga mkono Zitto. Understandable given our history and our political traditional realities. Lakini CHADEMA haipaswi kuyumba kwa sababu ya kuwa na ushindani mkali. Kinyume chaka CHADEMA inapaswa kuibuka even stronger baada ya uchaguzi huu na kutoa somo la maana ya demokrasia kwa watanzania. CHADEMA itasambaratika tu endapo wagombea na wapambe wao watakubali ushabiki wa waandishi kama akina Kibanda wa kuendesha kampeni kwa msingi wa kuchafuana majina na kuibulia kashfa za kubuni na kufikirika, kama hizo za kusema mgombea fulani ametumwa. Kwa hiyo ushauri wangu ni kwamba wagombea wote wawili na wapambe wao waendesha kampeni zilizojengwa katika msingi wa issues, kwamba:

a) Zitto atueleze kwa nini anagombea na kwa nini tumpe yeye uenyekiti badala ya mwenyekiti tuliyemzoea na ambaye amemlea kisiasa

b) mbowe atueleze kwa nini tumchague tena; anataka kufanya nini ambacho ameshindwa kufanya katika kipindi cha miaka mitano tangu awe mwenyekiti wa CHADEMA, na pengine kwa nini yeye awe mwenyekiti kwa awamu mbili wakati wenzake wote waliopita walikaa kwa wamu moja moja?

Kama tukiendesha kampeni za namna hii sioni sababu chama kisambaratike. Tatizo ni hapo upande mmoja unapoanza kampeni kwa kutabiria wengine maanguko na kuwaona wengine wanagombea kwa sababu wametumwa kukimaliza chama. Huo utakuwa uchuro na ndio maana ni muhimu sana kwa wana chadema kuyapuuza maandishi ya akina Kibanda na mwenzake Restuta James.

I ain't sure anybody can put it better than this! Take five Kitila.
 
Kibanda said:
Ni jambo jema na baya kwamba vigogo hao wa CCM anaokutana nao mara nyingi wamekuwa wakimueleza kuwa yeye ni moja ya viongozi dhabiti ndani ya Chadema ambao kwa kiwango kikubwa wanayo dhamana nzito ya kukiongoza chama.

Aghaghaghaghagha!,
Umenikumbusha mbali sana. Muasisi mmoja wa TANU aliwahi kunieleza kuwa hata Mwalimu JK Nyerere alikuwa na package yake stahili ya kuhongwa, na hivyo kila mmoja anahongeka tofauti ni bei tu. (ila ya Mwanakijiji haijapatikana).

Wazungu kwa kujua mapenzi makubwa na ndoto ya Mwl kuiona Afrika inakuwa moja, mara kwa mara Rais Ford na wazungu wengi walikuwa wakimsifia Mwl kuwa hakustahili kuiongoza Tanganyika tu bali Afrika na dunia nzima. Lakini wakati Mwl. anafurahia kejeli hizo na kujenga kichwa anaowatawala hawakuwa hata na chumvi. Na kwa jinsi hii walikuwa wanaweza kumtumia kufikia agenda zao.
 
Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba, ndani ya Chadema anaungwa mkono na vijana wajinga.

Kibanda,

Unayamaanisha haya uliyoyaandika, au vidole vimekuteleza? Kama unamaanisha, unaweza kutupa orodha fupi za wajinga na welevu wa Chadema?
 
- Ndugu Kibanda, kwanza karibu sana JF Kumkoma Nyani na Where We Dare, ninajaribu kutafakari kwa makini sana maneno yako na hii post, sasa wakati bado ninajaribu ku-catch the spirit na motivation behind your post, naomba kukuuliza hivi nini maana hayo maneno juu?

- Halafu what CCM has to do na Zitto kutaka kugombea uongozi wa juu wa Chadema, hapo I am lost nisaidie kidogo mkuu!


Ujumbe wangu katika hoja hii ni rahisi kabisa. Uamuzi wa Zitto kugombea uwe ni uamuzi binafsi au wa kusukumwa na watu walio ndani au nje ya Chadema unaungwa mkono sana na baadhi ya viongozi wa juu wa CCM.

Unajua kwa hulka yake (kama nilivyo mimi pia) Zitto ni mtu wa kujichanganya sana. Amekuwa akikutana na kubadilishana mawazo na makada mbalimbali maarufu wa CCM ukianzia na vijana.

Tabia yake hii imekuwa ikimkutanisha na watu mbalimbali maarufu ndani ya chama hicho ambao mara nyingi wamekuwa wakimpa changamoto nyingi.

Ni jambo jema na baya kwamba vigogo hao wa CCM anaokutana nao mara nyingi wamekuwa wakimueleza kuwa yeye ni moja ya viongozi dhabiti ndani ya Chadema ambao kwa kiwango kikubwa wanayo dhamana nzito ya kukiongoza chama.

Mbali ya hilo vigogo hao wa CCM wamekuwa hawasiti kueleza pia wasifu wa Mbowe na wa Chadema kwa ujumla. vigogo hao ambao hata sisi wana habari tumekuwa tukikutana nao wamekuwa wakimuelezea Mbowe kuwa ni mkabila (akiwapendelea wachaga), mbinafsi (anayekerwa na umaarufu na uwezo wa Zitto) na mtu mwenye elimu ndogo (wakizungumzia elimu ya darasani.

Maneno ya namna hii yanaonekana kumuingia Zitto sana akilini (uamuzi wake wa kugombea) na kuna hatari kuwa anayaamini (kwani yana sehemu ya ukweli na uongo pia).

Nimefanya kazi na viongozi wote hao wawili wa Chadema; Mbowe na Zitto na katika kipindi cha miaka mitatu wamekuwa ni watu wangu wa karibu sana.

Kwa kiwango kikubwa makala niliyoandika inasema sehemu tu ya ukweli ambao wakati mwingine ni mgumu kuuweka katika maandishi.

Naweza kukuhakikishia kuwa Mbowe si mtu mjinga wala mpumbavu (Zitto analitambua hilo), ni mtu mwenye ufahamu wa masuala makubwa na mazito ya kitaifa na kimataifa.

Mbowe ni aina ya wanasiasa ambao japo hawakupata elimu kubwa ya darasani, ametumia muda mrefu kujisomea na kujielimisha kwa njia mbalimbali.

Ana uwezo mkubwa wa kujenga hoja japo kuwa wakati mwingine huelemewa na jazba za kisiasa awapo jukwaani. Si mbinafsi, japo kuwa ni 'mtoto wa mjini' kutokana na mazingira aliyoishi na kukulia.

Tabia yake ya kujiamini kutokana na uwezo wake wa kifedha na kutokuwa tayari kujichanganya katika makundi tofauti ya kijamii hususan na wana siasa wa CCM imekuwa ikimfanya wakati mwingine aonekane dhaifu, japo ukweli ni tofauti.

Hata hivyo naweza kukuhakikishia kwamba, huyu jamaa, pamoja na mapungufu yake mengi ni mpiganaji na mpambanaji ambaye CCM ina muogopa na kila njia ya kujaribu kumfitini na kumchafua inaonekana kugonga mwamba.

Ni jambo la bahati mbaya sana kwamba amekuwa mzito kuchukua hatua za kukabiliana na tuhuma na shutuma nyingi za uongo zinazoelekezwa kwake.

Hata katika masuala ambayo ukimsikiliza anayo majibu mazuri na mazito kukabiliana nayo kwa hoja, yeye huamua kukaa kimya na wakati mwingine kuhamaki akitamani kuchukua hatua za kibabe kukabiliana na wazushi dhidi yake na chama chake.

Hata hivyo anabakia kuwa mtu wa vitendo na upendo mkubwa kwa Chadema pengine kuliko kiongozi mwingine yeyote ndani ya chama hicho, ukiwaacha John Mnyika na John Mrema ambao uchapakazi wao si wa kutiliwa shaka.

Zitto Kabwe si mtu wa kutulia, ni mtu mwenye mambo mengi na mara zote amekuwa ni mwanasiasa anayeishi kwa mawasiliano ya simu ya mara kwa mara na vikao vingi kila siku. Japo kuwa ni msomaji mzuri wa vitabu na magazeti, bado ni kijana ambaye hadi sasa amekosa utulivu anaopaswa kuwa nao mwanasiasa aliyekomaa.

Ni wazi kwamba akili ya Zitto inafanya kazi haraka haraka kuliko vijana wengi ndani ya chama hicho. hata hivyo kutochangamana kwake na wana Chadema wenzake katika masuala mbalimbali ya kitaifa kumempotezea ukaribu na watu wengi katika ofisi za Makao Makuu ya Chadema.

Hayo ni sehemu ya mambo ambayo Zitto anapaswa kujifunza kabla hajakabidhiwa dhamana nzito. Sidhani kwamba wapinzani kwa wakati huu, wanao muda wa kumpata Mwenyekiti wa kujifunza ustaarabu wa siasa ndani ya vyama vingi. Huo ni mtazamo wangu.

- Mkuu Kibanda unasema haya maneno mengi hivi yanayohusu tabia na elimu za Mwenyekiti wa sasa wa Chadema ndiyo majibu ya vijiswali vyangu viwili nilivyokuuliza kule juu?

- Are you serious or what? Maana toka post yako ya kwanza you were off the line, na sasa ndio kabisaa unazidi kuharibu unaleta mpaka ya elimu ya Mwenyekiti, nani aliyekuuliza mkuu?

- Halafu unasema uko karibu nao sana hawa viongozi wawili? Is that a joke au ni April Fool?

Respect.


Field Marshall Es!
 
.

1. Ni jambo la kusikitisha sana kwamba, leo inapofikia hatua ya mwanasiasa kijana aliyekuwa akionekana kuwa moja ya mazao ya kuigwa ndani ya kambi ya upinzani tangu kukwama kwa akina James Mbatia, Mabere Marando, Augustine Mrema na wenzao wengine wengi, akifuata mkondo ule ule, basi ni wazi Watanzania wanaweza wakajikuta wakilazimika kukata tamaa zaidi na zaidi.

2. Ingawa ni kweli kwamba pengine nyuma ya Zitto wako watu wengi ndani ya CHADEMA na nje, waliojitoa mhanga kumuunga mkono katika mapambano haya, mwanasiasa huyo anapaswa kutambua wazi kwamba, uamuzi wake huu wa sasa, unamuandalia anguko ambalo si mimi wala mwingine yeyote atamwepusha nalo.


3. Anapaswa kujifunza kuwa na subira waliyonayo vijana wengi ndani ya CCM na serikalini, ambao pamoja na kuwa na fursa nyingi za harakaharaka, wameamua kuwa watulivu na wenye subira, wakiwa na uhakika kuwa, wakati wao utafika.

4. Naliona anguko la kihistoria la Zitto.


- Mkuu Kibanda, again naomba kukuelewa hebu niweke sawa kwa haya maneno hapo juu ulikuwa na maana gani hasa? Je ni maneno yako kweli au?

- Unasema Zitto ajifunze tabia za ki-CCM, halafu tena unakuja na maneno mapya na kuwalaumu CCM kumshinikza Zitto kugombea? Mbona unajichanganya sana mkuu?

Respect


Field Marshall Es!
 
- Mkuu Kibanda, again naomba kukuelewa hebu niweke sawa kwa haya maneno hapo juu ulikuwa na maana gani hasa? Je ni maneno yako kweli au?

- Unasema Zitto ajifunze tabia za ki-CCM, halafu tena unakuja na maneno mapya na kuwalaumu CCM kumshinikza Zitto kugombea? Mbona unajichanganya sana mkuu?

Respect


Field Marshall Es!
Du mkuu FMS kweli JF is the HOME OF GREAT THINKERS,chukua five
 
"Anapaswa kujifunza kuwa na subira waliyonayo vijana wengi ndani ya CCM na serikalini, ambao pamoja na kuwa na fursa nyingi za harakaharaka, wameamua kuwa watulivu na wenye subira, wakiwa na uhakika kuwa, wakati wao utafika."

Nukuu hii kutoka kwa Kibanda iliwahi kutolewa kwa MH Baraka Oboma na Clinton Machine, matokeo yake wote tunayajua.

Ni vipi Mfano bora wa subra utoke CCM na ndani ya serikali ya CCM, wakati Mizee ilokwisha haribu mambo mengi na kudhoofisha nguvu za taifa nakufikia umri wa kustaafu bado ina renew mikataba kuendelea kufanya kazi!!??
HAo vijana wa CCM wana subra au wamefisadiwa?

Eti asubiri wakati wake utafika! Maneno yako yamejaa wazimu.

Mbowe ni kiongozi shupavu lakini haimaanishi kwamba hawezi kuwa challenged.

Utamaduni wa kumwachia mtu mmoja aendelee na uongozi ni mila ya CCM isiyotakiwa kurithiwa na kundi lolote. Ni heshima dume, heshima isiyozaa wala kujua kesho. Ni heshima isiyo na hekima. Ni heshima ilojaa woga,kibri dharau na unyanyapaa.

Hata Musa yule kiongozi wa taifa la Israel alifanya kazi kubwa na ya kutisha kuwaondoa Israel utumwani Misri lakini kuwafikisha Kanaani alipewa mtu mwingine kabisa, tena bwana mdogo wa mbali kwa umri.

Nukuu hii ya kibanbda inanikumbusha jambo moja" Unaweza kuihama CCM lakini si rahisi kuihamisha CCM kutoka mawazoni na katika vitendo vyako".

Endapo kibanda umetumwa uandike maneno haya basi aliyekutuma ni muflisi wa kisiasa na kiuchumi na hafai kuwa kiongozi wa kundi lolote la kisiasa.
Kama uliyoandika ni maneno yako umepumua hewa ya ukaa na kutunyima fursa ya kufaidi hewa ya Mwenyezi Mungu.

Rekebisha haijakaa vizuri hata kidogo.
 
Last edited:
Naliona anguko la Zitto Kabwe!

Absalom Kibanda


1. Kikubwa kinachoonekana kuzusha maswali vichwani mwa watu wengi, nikiwamo mimi mwenyewe, ni uamuzi wa kijana huyo kuamua kugombea nafasi hiyo pasipo kujali iwapoMwenyekiti wa Taifa wa chama hicho, Freeman Mbowe anayemaliza muda wake atachukua fomu au la.

2. Watu wanaojua masuala ya CHADEMA ni mashahidi wazuri kwamba, uamuzi huu wa Zitto kuchukua fomu kupambana na Mbowe ambaye yeye mwenyewe (Zitto), mara zote amekuwa akimtambulisha kuwa ni ‘mentor’ wake wa kisiasa ndani ya chama hicho cha upinzani, tena kwa staili ya kumshtukiza, umesababisha mtafaruku mkubwa wa mawazo.

3. Ni wazi kwamba, uamuzi huu wa Zitto kuchukua fomu, kwa kiwango kikubwa umekuwa ni wa faraja kubwa kwa wana CCM, ambao siku zote wamekuwa wakitaka kuiona CHADEMA ikisambaratika na kukipa fursa chama hicho tawala kupumua.


4. Anapaswa kujifunza kuwa na subira waliyonayo vijana wengi ndani ya CCM na serikalini, ambao pamoja na kuwa na fursa nyingi za harakaharaka, wameamua kuwa watulivu na wenye subira, wakiwa na uhakika kuwa, wakati wao utafika.

5. Naliona anguko la kihistoria la Zitto.

- Wakuu kwakweli I am lost, hebu angalia hizi hoja hapo juu eti mmesema huyu Mkuu Kibanda ni Mhariri mkuu wa a serious paper Tanzania Daima, au?

- Ohhh my Gosh! hivi Tanzania tumemkosea nini Mungu jamani?

Respect.


FMEs!
 
Hebu tuachane na Kibanda hana mantiki,

Turudi katika maswali aliyouliza Mkumbo na nilililouliza mimi. Kwanini Zitto uchaguliwe kuwa Mwenyekiti?

Je Rostam ni fisadi?

Zitto tupatie hayo majibu hata kwa mistari miwili tu
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom