Kibanda, heshima mbele!
Kwanza siamini kuwa Kibanda amenunuliwa na Mbowe bali one thing for sure, Kibanda anajikomba kwa Mbowe, what for ndio sijui ni kutetea kibarua chake, ama kujikomba komba tuu ili mradi kujikomba.
Namuheshimu sana tuu Kibanda kama mwandishi, mhariri na mchambuzi, na Tanzania Daima la Jumatato, ni miongoni mwa magazeti ambayo sio tuu can't afford to miss, bali pia ends up in my achive, hivyo halifungii samaki.ila kwa makala hii, Kibanda amechemsha big time.Hoja ya umri haina mashiko, hapa tunaangalia uwezo wa uongozi kati yao. Kibanda angepaswa kuogopa kama Zitto hana uwezo alionao Mbowe na sio umri.
Kitendo cha Zitto kuwania kugombea uenyekiti wa Chadema, ni kitendo cha kuungwa mkono na waona mbali wengi na kitalaaniwa na myopic wote wenye myopia ambapo Kibanda nae sasa anaingia kwenye kundi hili.Japo mimi sio mwanachama wa chama chochote, ila ni mshabiki wa demokrasia ya kweli, nawaambieni kuingia kwa Zitto kwenye kinyanganyiro hicho ni uthibitisho wa demokrasia ya kweli ndani ya Chadema.
Chadema kama chama cha upinzani kinakubalika sana bara, lakini pia kinashutuma za chini kwa chini za ukabila, Mbowe amepewa chama na Bamkwe, ili kuliondoa hilo, chama kishikwe na mtu baki asiyetokana na Uchagga au uKaskazini ili kuwathibitishia Watanzania kuwa Chadema hakina ukabila.
Kama kilivyo CUF kuandamwa na udini wa kichinichini kuwa ni chama cha Kiislamu, ndivyo Waislamu wenye msimamo mkali wanakiona Chadema kama chama cha Kikristo, tangu kimeanzishwa, wenyeviti wake wote na makatibu wakuu ni Wakristo tuu, kuingia kwa Zitto kutaliondoa hili na kukifanya Chadema chama cha kitaifa zaidi tayari kuchukua nchi, 2015.
Zitto ni reformist na strategist leader, Mbowe ni kiongozi mzuri ila kwa vile politics zake ni spoon fed na bamkwe, hapo alipokifikisha Chadema ndio mwisho wa uwezo wa Freeman kama Lipumba alivyogota na CUF bara. Kuendelea na uenyekiti ni kuididimiza Chadema. Zitto ni damu mpya, damu changa inayoweza kuibua tumaini jipya kwa Chadema, kitendo cha kuamua kugombea uenyekiti, lazima kuna mambo ameyaona ambayo Mbowe hayawezi hivyo anataka kushika usukani aokoe jahazi.
Hongera Zitto for just daring.