Kheri James, achana na sisi kabisa

Kheri James, achana na sisi kabisa

Tumeshakuwa sugu wa kutekwa,kufungwa,kupigwa,kubambikwa kesi na kuuawa,hayo ndo maisha yetu wapinzani wa Tanzania.

Kheri James wakati Magufuli akiwa hai ulisimama hadharani kwa ujasiri mkubwa ukasema huku Taifa na Dunia wakishuhudia,ulisema kwamba,sasa hivi Tundu Lissu mtamchoma sindano ya sumu ndo kilichobakia.

Baada ya Mungu kumchukua Magufuli, hofu imekujaa,unajiona wazi huna kinga hasa baada ya Mama yetu kugoma kukujibu sms mbili ulizomwandikia kumpongeza baada ya kuapishwa.

Mama anakujua nje ndani, hakupenda kabisa Tabia zenu za kikatili vijana wa UVCCM jinsi mlivyokuwa mnawa treat wapinzani kama wanyama.

Tuliwaonya sana kuwa kuna kesho lakini hamkusikia,eti leo unataka maridhiano, na nani?

Endelea ulipoishia na wenzako,sisi mtuache na maisha yetu.
huyu kijana ni hayawani mwenye asie na macho
 
Binafsi mimi naona haina haja ya Kheri James KUOMBA RADHI,
bora hii kauli angesema hata WAKATI WA KAMPENI....
 
Kipindi hiki watanena kila lugha. Hakika Mungu wetu ametuheshimisha sana. Miaka 5 iliyopita ilikuwa kama miaka 500. Sasa ni muda wa wapuliza zumari kukipata cha moto.
Hadi walio mpiga Lissu risasi wata jisema.
Nani alijua Magu ni mpigaji. Si haya tana fumuka sasa?
 
sasa si amesema wameshakua sugu ama? tatizo la wapinzani wanajikutaga wajuaji sana ingawa sio wote, hawa wanawake wa uku wanajikutaga kama wanajikuataga wajuaji sana, sasa yeye anatuambia amekua sugu ili iweje? kwamba aendelee kupata kichapo si ndo maana yake? badala ya kuraise concerns ya kutoshirikiana nae ama kushirkiana nae ama kuchukua hatua wanatuambia wamekua sugu,
-
si bora ccm iendelee kwa miaka ingine 60
Ni kweli ni kipindi kigumu cha maombolezo na wasiwasi mkubwa wa yaliyo mbele yenu mliokuwa mwamtumaini Goliath.
Lakini waonaje ukisoma upya ulichoandika ili ukisahihishe.
 
wakipewa kichapo mtandaoni oooh sjui uonevu unaofanywa na ccm, mara sjui ICC haya mtu ameamua kukiri makosa wanasema wamekua sugu what do you expect
Wewe nae walewale, ungewashauri wenzio wakiri makosa kipindi baba yao yupo tungejua wana nia ya dhati, hizi ni hadaa.
 
Hivi wewe mtoa mada na wenzio ni mna matatizo ya akili au ni uyatima wa siasa unawasumbua.

Kila mtu akiandika nyuzi ni kulopoka lopoka tu mamaaa mamaa....sasa kati ya wewe na henry james nani ni mtoto halisi wa huyo mnaemwita mama.Mwenzio anayo namba yake na anamtext sasa wewe mwenzangu na mie hata mtandao anaoutumia huujui na bado unajivimbisha mashavu.

Embu tutoleeni ujinga wenu wa kukuita Rais wetu mamaaa mamaa utafikili mpo mayatima wa siasa.
Mmh?rais wenu tena wakwenu alikua jiwe tu alisemaa msinichanganyie ??? Huyo aliopo Sasa niwawote kwamujibu wakatiba
 
Back
Top Bottom