Khatima ya Zanzibar na Mustakbali wa Muungano

Mkuu Mkandara.
Uache kukurupuka...soma kwa makini hiyo taarifa niliyoibandika.
Unaona umeleta suala la OIC, jumuiya ya kiislamu...makala inazungumzia OIC hii;the Indian Ocean Commission (IOC), a regional cooperation body whose current members are Comoros, Mauritius, Seychelles, Madagascar and Reunion......
Mkuu vipi leo.. ama hizi ndio hatari za ku copy na kupaste?.. Ni wapi wewe umezungumzia IMF au Saudia na Afghanstan mbona hatuelewani?..
Nimeisoma habari vizuri sana na nimepingana nayo na kukueleza sababu zake halafu paraghraph iliyofuata nimesema nachoweza kubaliana na wewe ni Zanzibar kujiunga na OIC (Organisation of Islamic coopreration) japokuwa pia nimeeleza hofu yangu.

Na hii sii mara yangu ya kwanza mimi kuzungumzia kuafiki swala hili kwa sababu Zanzibar ilitawaliwa na Oman (Sultan) na nimeshatoa mifano ya Quebec kuwa wanachama wa umoja wa nchi za Kifaransa wakati the rest of canada ni mwanachama wa Commonwealth..Halfu pia lengo kubwa la OIC ni kufundisha watu kuvua samaki na sio kupewa kipande cha samaki..

Hiyo OIC (Indian Ocean Commission) inahusiana na mazingira na nimekwambia vizuri kwa nini nyie msipeleke vijana wenu wakajifunze taaluma ya mabadiliko ya hali ya hewa (climate changes) badala ya kutegemea wageni ambao kwanza inakula kwenu, sasa unataka nieleze nini zaidi. Na bila shaka umewahi kunisoma, mimi huunganisha habari nyingi kwa wakati mmoja kuwataarifu ubaya wa jambo na yanayowezekana..Hakuna mahala umeniuliza kuhusu IMF, Saudia wala OIC na nimeyaweka baada ya kuchambua yako kuonyesha wapi napakubali. Siku zote hujibu swali halafu nakupa alternative solution, huu ndio uandishi wangu siku zote.

Kuhusu wafadhili na mikopo tunaihitaji sana tu ikiwa tutalenga ujenzi wa miundombinu na kuwafundisha vijana wetu elimu dunia kulingana na mazingira yetu. Leo hii kweli kinachofanyika ni usanii mtupu maana JK majuzi ati ndio anatangaza kuanzisha chuo cha madini nchini.

Jambo zuri lakini tulikuwa wapi siku zote hadi tumegawa karibu 3/4 ya miradi yote mikubwa ya madini wakati Nyerere alituachia usia ambalo kila Mtanzania anaujua wakati akiwaambiwa mabeberu (Imperialist) kwamba anaacha madini huko chini hadi sisi wenyewe tutakapo kuwa na ujuzi wa kuyachimba.

Kwa nini hatukuendelea kuwafunza vijana wetu? Kwa hiyo usanii upo kila sehemu na ndio maana sikubaliani na mawazo ya wageni kuwekeza ktk madini, Uranium na sijui gesi matokeo yake tunanyimwa hata share ya maana kutokana na kwamba hatuna cha ku offer..
 
Shukrani zangu za zati kwako mkuu. Maneno uliyoyasema hapo ni ukweli mtupu na kama kila mtu angelikuwa na busara kama zako basi hii leo tungekuwa niwatu wa kuheshimiana na kuelewana hata pale tunapokuwa na tafauti. mimi kwa kweli ni mtu wa haya na upole kabisa lakini mimi naishi na watu wa kutoka Tanganyika na kila tunapoka tukizungumza basi wao mazungumzo yao ni kashfa na mazarau tupu ju ya Zanzibar na Wazanzibari. Imefika kipindi nikawambia jama mimi ni Mzanzibari kwanza kabla ya Utanzania nikimanisha hayo mnayo sema yananiuma lakini wapi nisawa na kumpigia mbuzi gita tuu. Na fikiri kwa hili limenifanya nione Watanganyika wote msimamo wao ni sawa ju ya Wazanzibari lakini wewe umenionesha kuwa sikwali na kwa hili nakiri kwamba nilifikiria makosa. Kwa hivyo mkuu at last nimeona mtuu ambaye tunaweza tukazungu kwa kutumia hoja.
 
Kumekuwa na mijadala mingi juu ya suala la huu muungano, kwa upande wa zanzibar wananchi wamechoshwa na muungano mpaka pale walipofikia kuchukua hatua za kufungua case katika mahakama ya East Africa community.

Pia tukiangalia viongozi wanzibar hasa wale waliopo madarakani wakisema muungano wataulinda kwa nguvu yoyote, hata viongozi wa Tanganyika pia ni hivyo hivyo kauli za kibabe muungano tutaulinda na upo imara, hizo ndo kauli zao viongozi.

Tukija hapa jf kauli ndo hizo hizo muungano upo imara, suala langu ni hili, muungano upo imara au mkoloni yupo imara kuitawala zanzibar ?

Mbona wananchi wa zanzibar hawataki huu muungano? Kipimo cha ukusanyaji wa maoni ya katiba mpya wazanzibari walitaka muungano wa mkataba, na Kipimo cha pili wananchi kufungua case East Africa court kudai uhalali wa muungano, na Kipimo cha tatu wananchi wa zanzibar kwa mujibu wa uchaguzi 25 Oct wameichagua cuf kwa asilia 52 kwa sababu cuf ilani yake ni kudai mamlaka kamili ya zanzibar.

Je muungano upo imara kivipi ?
 
Kumekuwa na mijadala mingi juu ya suala la huu muungano, kwa upande wa zanzibar wananchi wamechoshwa na muungano mpaka pale walipofikia kuchukua hatua za kufungua case katika mahakama ya East Africa community.

Pia tukiangalia viongozi wanzibar hasa wale waliopo madarakani wakisema muungano wataulinda kwa nguvu yoyote, hata viongozi wa Tanganyika pia ni hivyo hivyo kauli za kibabe muungano tutaulinda na upo imara, hizo ndo kauli zao viongozi.

Tukija hapa jf kauli ndo hizo hizo muungano upo imara, suala langu ni hili, muungano upo imara au mkoloni yupo imara kuitawala zanzibar ?

Mbona wananchi wa zanzibar hawataki huu muungano? Kipimo cha ukusanyaji wa maoni ya katiba mpya wazanzibari walitaka muungano wa mkataba, na Kipimo cha pili wananchi kufungua case East Africa court kudai uhalali wa muungano, na Kipimo cha tatu wananchi wa zanzibar kwa mujibu wa uchaguzi 25 Oct wameichagua cuf kwa asilia 52 kwa sababu cuf ilani yake ni kudai mamlaka kamili ya zanzibar.

Je muungano upo imara kivipi ?
Uchochezi
 
wenzio wanasema upo imara wewe unasema haupo imara
wewe na amiri jeshi tumuamini nani
Unaposema upo imara wewe na bwana yule, upo imara kivipi?
Wakati wananchi hawautaki huu muungano au mfumo wa muungano.

Ni sawa kusema mwanao anaenda shule, wakati shule wenyewe hafiki, jee huku kwa wananchi hali ipo vipi ?
 
Unaposema upo imara wewe na bwana yule, upo imara kivipi?
Wakati wananchi hawautaki huu muungano au mfumo wa muungano.

Ni sawa kusema mwanao anaenda shule, wakati shule wenyewe hafiki, jee huku kwa wananchi hali ipo vipi ?
wananchi mvimbe mpasuke mtajijua wenyewe, huu muungano lazima ulindwe kwa nguvu zote na ndio sababu Maalim hawezi kupewa nchi kwa makaratasi.
 
Kumekuwa na mijadala mingi juu ya suala la huu muungano,
Je muungano upo imara kivipi ?
Muungano uko imara sana just by uwepo wake tuu, ile hali ya being present, ni uthibitisho tosha Muungano huu ni imara sana na haukabiliwi na kitisho chochote hata cha kuutingisha hata unywele mmoja wa Muungano.

Mungu ibariki Tanzania.

Paskali.
 
Muungano uko imara sana just by uwepo wake tuu, ile hali ya being present, ni uthibitisho tosha Muungano huu ni imara sana na haukabiliwi na kitisho chochote hata cha kuutingisha hata unywele mmoja wa Muungano.

Mungu ibariki Tanzania.

Paskali.
Mungu akubariki wewe, kwa maana huu muungano bado unaendelea kuwanyima usingiz, musha foji hadi mkataba wa muungano. Bwana yule asinge kuja huku zanzibar kuubisha na kuwatisha wazanzibari eti hakuna fyoko fyoko atajibu mapigo.

Nadhani wananchi wako imara juu ya huu muungano wa mabavu na hawako tayari kutawaliwa
 
Mungu akubariki wewe, kwa maana huu muungano bado unaendelea kuwanyima usingiz, musha foji hadi mkataba wa muungano. Bwana yule asinge kuja huku zanzibar kuubisha na kuwatisha wazanzibari eti hakuna fyoko fyoko atajibu mapigo.

Nadhani wananchi wako imara juu ya huu muungano wa mabavu na hawako tayari kutawaliwa
Mkuu Ghibuu, muungano wetu ni kama ndoa, ndoana, aliyetaka kuolewa tangia mwanzo ni binti, na aliyeichoka ndoa na kutaka kuachana pia ni binti, hivyo anafanya visa ili apewe talaka, bahati mbaya sana, bwana kampenda kiukweli kweli, hata afanye visa kiasi gani, bwana hatoi talaka, sana sana visa vya fyoko fyoko vikizidi, atamfungia tuu ndani huyo mkewe ili kumtuliza kama ilivyokuwa mwaka 1984, lakini talaka kamwe hatoi sababu kapenda.

https://www.jamiiforums.com/threads...kaomba-uhuru-ili-kutoka-nje-ya-ndoa-aruhusiwe.

Paskal
 
Muungano wa Serikali tatu utaongeza gharama?


Baada ya kuangalia nafasi ya Tanganyika na ya Zanzibar katika Muungano na madaraka yao, na kuonyesha kwamba njia pekee ya kushughulikia matatizo ya msingi ya Muungano ni kwa kurejea katika Mkataba wa Muungano na hivyo kuanzisha mfumo wa Serikali tatu, ni vyema tutafakari kidogo suala la gharama za uendeshaji wa mfumo huo.


Wapinzani wa Muungano imara chini ya msingi madhubuti wa Shirikisho la Serikali tatu wamekuwa wakiibua mara kwa mara hoja ya kuongezeka kwa gharama za utawala na uendeshaji kama kikwazo cha kukwamisha juhudi za kuuimarisha Muungano.


Hoja hii imeonekana ni dhaifu na isiyo na msingi kabisa kufuatia kuundwa kwa Tume ya Pamoja ya Fedha (Joint Finance Commission) ambayo ripoti zake za awali zimekaliwa na Serikali ya Muungano hadi leo baada ya kutoa picha halisi ya jinsi mchango wa Muungano unavyopaswa uwe. Tume hiyo imeipa kazi kampuni ya PriceWaterhouseCoopers kufanya uchambuzi halisi wa mambo yepi ni ya Muungano halisi na yepi ni ya Tanganyika na yepi ni ya Zanzibar. Baada ya orodha kupatikana, watafiti wakatafuta matumizi halisi ya bajeti ya vifungu hivyo kwa muda wa kiasi cha miaka 10 iliyopita. Watafiti hao walikwenda mbali zaidi ya hapo na kukusanya mapato yote kwa kila kifungu cha mambo ya Muungano halisi. Mwishowe, wakalinganisha iwapo mapato yanakidhi matumizi au yana nakisi (upungufu)?


Kilichojitokeza ni kwamba kwa mwaka wa fedha 2003/2004 pekee, matumizi halisi kwa vifungu vya Muungano yalikuwa Shs. 537,258.4 bilioni na mapato halisi kwa mwaka huo yalikuwa ni Shs. 1,030,826.1 bilioni. Tofauti ya vifungu hivyo vimetoa ziada ya ya Shs. 493,567.7 bilioni kwa mwaka huo. Ziada hii haiingizi mapato yanayotokana na misaada kutoka nje au mikopo. Ziada hii hutumika kwa shughuli za Tanganyika zisizo za Muungano.


Ukweli huu unaonyesha hata kama kungekuwa na Serikali tatu kusingekuwa na haja yoyote kwa Serikali ya Zanzibar na ile ya Tanganyika kulipia fedha za ziada kama wahusika watatunza na kuweka kumbukumbu sahihi za mapato na matumizi ya mambo ya Muungano halisi badala ya yale ya Tanganyika kuchanganywa na ya Muungano. Mambo yasiyokuwa ya Muungano yaTanganyika yalipotengwa nje ya yale ya Muungano, gharama za mambo ya Muungano zimejidhihirisha wazi bila ya kujificha na kuonesha kwamba zinaweza kulipiwa kupitia mapato ya mambo ya Muungano pekee na ziada kubaki. Lakini hili limekuwa rahisi kwa kukubali ukweli kwamba kuna mafungu matatu ya mapato na matumizi katika Serikali zetu mbili. Mafungu hayo ni la SMZ kwa mambo yake yasiyo mambo ya Muungano, la Serikali ya Muungano kwa mambo ya Muungano, na la Serikali ya Muungano inayofanya kazi za Tanganyika kwa mambo yasiyokuwa ya Muungano. Kinachohitajika sasa ni hili kuliweka wazi kwa viongozi kuweka nia njema na kuuweka sawa muundo wa Muungano wetu ili uzionyeshe waziwazi mamlaka zote tatu.










Vipi tutoke hapa tulipo?


Inakaribia miaka 45 sasa tangu uundwe Muungano wa Tanganyika na Zanzibar. Kulikuwa na wakati wa kutosha kurekebisha kasoro zilizopo. Hilo halikuwezekana kutokana na ubabe wa Mwalimu Nyerere ambaye aliamua kuwatia shemere Wazanzibari na kuhakikisha Muungano unakwenda kama alivyotaka yeye hata baada ya &[HASHTAG]#8216[/HASHTAG];kuondoka madarakani'.


Si jambo la kuficha kwamba wananchi wa pande zote mbili za Muungano wamechoshwa na unafiki uliopo na wanadai Katiba ya kweli kweli itakayoweka misingi mipya ya ushirikiano.


Kama nilivyoeleza mwanzoni, kiini cha matatizo ya Muungano ni kutokuheshimiwa kwa Mkataba wa Muungano (Articles of Union) ambao kisheria ni Mkataba wa Kimataifa unaopaswa kuheshimiwa kwa kuzingatia masharti yote yanayohusu mikataba ya kimataifa.


Haidhuru sasa ni takriban miaka 45 tokea kuanza kwa hatua za kuukanyaga kanyaga Mkataba wa Muungano mara tu baada ya kutiwa saini na Rais wa Jamhuri ya Watu wa Zanzibar, Marehemu Mzee Abeid Amani Karume, na Rais wa Jamhuri ya Tanganyika, Marehemu Mwalimu Julius Kambarage Nyerere, lakini ukweli utabaki kuwa huo ulikuwa ndiyo msingi pekee, nasisitiza tena, pekee, uliokubaliwa na viongozi hao wawili kuongoza mahusiano ya nchi zetu mbili kupitia Muungano.


Wakati sasa umefika tukubali kwamba suluhisho la matatizo haya siyo kuendelea kuunda Tume au Kamati au kuandaa warsha, semina, makongamano na mikutano. Suluhisho ni kutekeleza kwa dhati Mkataba wa Muungano (Articles of Union) ambao ni mkataba wa kimataifa wa nchi mbili huru.


Kujaribu kulazimisha kutumia Katiba inayoitwa ya Jamhuri ya Muungano kama ilivyo sasa ambayo inakosa uhalali wa kisheria kuzima madai ya wananchi wa Zanzibar hakuwezi kukubalika tena katika zama hizi.


Kwa msingi huo, hakuna njia ya mkato ya kuyashughulikia matatizo ya Muungano bila ya kwenda kwenye kiini cha matatizo hayo ambacho ni kutokuheshimiwa kwa Mkataba wa Muungano. Wahenga wamesema, Mwiba uchomeapo ndipo utokeapo. Ili kuyaheshimu Makubaliano ya Muungano, yafuatayo ni lazima yafanyike:



  1. Kwa kuwa Baraza la Kutunga Sheria la Zanzibar la mwaka 1964 ambalo lilikuwa ni Baraza la Mapinduzi halikupewa nafasi ya kuuridhia (ratify) Mkataba wa Muungano, hivyo basi kwanza kabisa, na kabla ya kuchukua hatua nyengine yoyote, ni lazima Baraza la Kutunga Sheria la Zanzibar kwa sasa ambalo ni Baraza la Wawakilishi lipewe nafasi ya kuuridhia Mkataba huo ili kuupa uhalali wa kisheria kwa upande wa Zanzibar na hivyo kuupa uhalali wa kisheria Muungano wenyewe kama yalivyo masharti ya kifungu cha (viii) cha Mkataba huo wa Muungano.



  1. Kwa ujumla tuupitie tena Mkataba wa Muungano na kurekebisha vifungu vyenye utatanishi. Kama Muungano huu haukuwa na mtego, ulikuja kwa ridhaa za Serikali zetu mbili, vipi tunashindwa kukaa tena tukaupitia baada ya miaka 45 na kuuweka kwenye hali ya kuvutia hata majirani zetu wakajiunga?



  1. Katiba ya Zanzibar itumike Zanzibar kwa mambo yote yasiyo mambo ya Muungano kama yalivyo masharti ya kifungu cha (v) cha Mkataba wa Muungano.



  1. Katiba ya Tanganyika (ile iliyokuwepo kabla ya kurekebishwa kuingiza mambo ya Muungano) nayo irejee kutumika Tanganyika kwa mambo yote yasiyo mambo ya Muungano kama yalivyo masharti ya kifungu cha (v) cha Mkataba wa Muungano.



  1. Kwa kutumia Katiba ya Tanganyika, iundwe Serikali ya Tanganyika inayoshughulika na mambo yasiyo ya Muungano, kama Serikali ya Zanzibar inavyoshughulika na mambo yake ambayo si ya Muungano.



  1. Serikali ya Muungano ishughulike na yale mambo 11 tu ya asili yaliyokubaliwa kuwa ndiyo mambo ya Muungano kwa mujibu wa kifungu cha (iv) cha Mkataba wa Muungano.



  1. Mambo mengine yote 12 yaliyoongezwa katika orodha ya mambo ya Muungano kinyume na Mkataba wa Muungano yaondolewe katika orodha hiyo na yarudi katika mamlaka za Zanzibar na Tanganyika.



  1. Wafanyakazi wa Tanganyika wasihusike na mambo ya Muungano, wawe katika "civil service" (mfumo wa wafanyakazi Serikalini) wa Tanganyika, kama walivyo wa Zanzibar kwa Zanzibar (wasio wa taasisi za Muungano).



  1. Urejee utaratibu wa kuwepo kwa Makamu wawili wa Rais wa Muungano kama yalivyo masharti ya kifungu cha (iii) (b) cha Mkataba wa Muungano ambapo Rais wa Zanzibar na Rais wa Tanganyika wawe Makamu wa Rais wa Muungano kwa mujibu wa nyadhifa zao.



  1. Iundwe Tume ya kutayarisha rasimu ya Katiba ya Kudumu ya Muungano ambayo itakuwa na idadi sawa ya wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika kama yalivyo matakwa ya kifungu cha (vii) (a) cha Mkataba wa Muungano.



  1. Liundwe Bunge la Katiba (Constituent Assembly) litakalokuwa na idadi sawa ya wajumbe kutoka Zanzibar na Tanganyika ambalo litakuwa na majukumu ya kupokea rasimu iliyotayarishwa na Tume ya Katiba na baada ya hapo kupitisha rasmi Katiba ya Kudumu ya Muungano kama yalivyo matakwa ya kifungu cha (vii) (b) cha Mkataba wa Muungano.


Itaonekana kwamba msingi wa hatua zote zilizoorodheshwa hapa ni kuheshimu mapatano ya nchi zetu mbili yaliyomo katika Mkataba wa Muungano. Haya yalibidi yafanyike ndani ya mwaka mmoja tokea kusainiwa kwa Makubaliano ya Muungano. Hata hivyo, Waingereza wanasema,"Better late than never" (Bora kuchelewa kuliko kutofanya kabisa). Wakati ndio huu ikiwa tunataka Muungano wa kweli, Muungano wa haki kwa pande zote mbili.


Wasioitakia mema CUF wanaweza kudai kwamba hatua hizi zinazopendekezwa haziashirii nia njema ya kuendeleza na kuimarisha Muungano. Sisi katika CUF hatuamini hivyo. Tunaamini katika kuwa wakweli na wawazi, kwamba hivyo ndivyo yalivyo makubaliano katika Mkataba unaoanzisha Muungano.


Ulimwengu unabadilika kwa kasi. Zama za kuendesha mambo kwa ubabe na ukichwa ngumu zimepitwa na wakati. Tuache ile tabia ya kuyaona mapendekezo ya kubadili mfumo wa Muungano kuwa yana nia ya kuuvunja Muungano huo. Muungano ili udumu unahitaji ridhaa ya walioungana. Muasisi wa Muungano huu, Mwalimu Nyerere mwenyewe, aliwahi kueleza umuhimu wa ridhaa katika masuala haya na kuonyesha kwamba ridhaa ya mshirika mmojawapo ikiondoka, Muungano hauwezi kusimama. Alisema mwaka 1968:


"If the mass of the people of Zanzibar should, without external manipulation, and for some reason of their own, decide that the Union was prejudicial to their existence, I could not bomb them into submission &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG]; The Union would have ceased to exist when the consent of its constituent members was withdrawn." [12]


"Iwapo wananchi walio wengi wa Zanzibar wataamua, bila ya msukumo wa kutoka nje, na kwa sababu zao wenyewe, kwamba Muungano unaathiri kuendelea kuwepo kwao, siwezi kuwalazimisha kwa kuwapiga mabomu &[HASHTAG]#8230[/HASHTAG]; Muungano utasita kuendelea pale ridhaa ya washirika wake itakapoondolewa."


Wazanzibari ni watu wenye historia ya maingiliano ya jamii za watu mbali mbali na hivyo hawawezi kukataa umoja, alimradi tu umoja huo uwe na maslahi na faida kwao. Mfumo uliopo sasa hauinufaishi Zanzibar na hivyo haukubaliki kwa Wazanzibari. Koti la Muungano kama lilivyo sasa linabana sana. Wakati umefika tushone koti jipya kwa mujibu wa mahitaji ya zama hizi.


Hitimisho: Mazungumzo ya dhati yenye nia njema ndiyo njia


CUF, kama ulivyo Muungano tunaoujadili, imekumbana na dhoruba nyingi katika kipindi kifupi cha kuwepo kwake. Miongoni mwa dhoruba hizo ni kupakaziwa kila ubaya ili kuwazuia wananchi wasikiunge mkono ikiwemo hoja kwamba hakiutaki Muungano na kwamba pindi kikishika madaraka kitauvunja Muungano huo. Hoja hii ni dhaifu mno inayolenga kutimiza malengo ya kisiasa badala ya kushughulikia hasa kiini cha matatizo ya msingi ya Muungano.


Si siri kwamba kwa kushindwa kushughulikia kiini cha matatizo haya kumewapelekea wananchi kuona kwamba Muungano huu haupo kwa maslahi yao. Na kwa Wazanzibari, kutokana na Serikali ya Muungano kila uchaguzi unaopokaribia kuamua kumimina maelfu kwa maelfu ya askari wa vikosi vyake ambao, kwa kushirikiana na askari wa vikosi vya SMZ, wamekuwa wakitumika kuwaadhibu Wazanzibari kwa kujaribu kutumia haki yao ya kidemokrasia na kikatiba kuchagua viongozi wanaowataka, wanafikia hatua hata ya kuuona ni Muungano wa kikandamizaji. Hisia za namna hii zinapata nguvu zaidi pale wanapomuona Rais wa Jamhuri ya Muungano anafikia kujua na kukiri kwamba chama chake hakina nafasi ya kushinda uchaguzi huru na wa haki lakini viongozi wake watatumia mabavu kubaki madarakani na yeye akashirikiana nao kufanikisha hilo. Mwandishi mashuhuri wa kimataifa, Jonathan Power, anaripoti:


"The governing party [in Zanzibar] is part of the mainland's goverining CCM, but, as [President] Mkapa says, there are some militant people in my party. They don't want to lose power even if it means fiddling the vote." [13]


"Chama kinachotawala [Zanzibar] ni sehemu ya chama cha CCM kinachotawala Bara, lakini kama anavyosema [Rais] Mkapa, kuna wahafidhina katika chama changu. Hawako tayari kuachia madaraka hata kama hiyo inamaanisha wizi wa kura."


Yaliyofuata katika utekelezaji wa mpango huo yataingia katika historia ya Tanzania kama mojawapo ya matukio ya unyama mkubwa kuwahi kufanywa na askari wazalendo dhidi ya wananchi wenzao kwa sababu tu ya itikadi tofauti za kisiasa na kuwazuia wasitekeleze haki yao ya kidemokrasia na kikatiba. Matukio hayo yenyewe ni matokeo ya kupuuzwa kwa njia ya mazungumzo na makubaliano ya Muafaka ambayo awali Rais mstaafu Mkapa aliahidi mbele ya Watanzania na ulimwengu kwamba atayasimamia kikamilifu.


Wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa 2005, niliandika makala katika gazeti la Mwananchi Jumapili nikiwa na lengo la kuwaondolea mashaka wenzetu wa chama kinachotawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) na wananchi kwa ujumla kuhusu mambo kadhaa tunayotuhumiwa nayo. Kuhusu Muungano niliandika:


"&[HASHTAG]#8230[/HASHTAG]; Muungano ni nguzo moja nyengine ya nguvu na maslahi ya Zanzibar na ya Wazanzibari wenyewe. Wanaosema kwamba CUF haitaki Muungano na kwamba itauvunja ni waongo. CUF, kama ilivyo CCM, ni chama chenye nguvu Visiwani na Bara. Na kama CCM ina uwezo wa kutawala pande zote, CUF ina uwezo huo mara mbili zaidi. Msimamo wetu ni kwamba kuna hitilafu na kasoro mbali mbali katika Muungano lakini hizo tutazijadili kwa pamoja na Serikali ya Muungano na naamini tutaweza kuzipatia ufumbuzi."[14]


Na huo unabaki kuwa ndiyo msimamo wa CUF katika kutatua hizi zinazoitwa kero za Muungano. Mazungumzo makini, ya kina na yenye kuambatana na nia njema kwa wahusika wote ndiyo njia pekee ya matumaini katika kuyapatia ufumbuzi matatizo yanayolikabili Taifa letu. Hakuna mbadala wa mazungumzo. Nje ya mazungumzo ni fujo.


Lakini wakati tunazungumzia namna ya kutatua matatizo haya kwa lengo la kuwa na Muungano imara, ni vyema tuelewe kwamba tunahitaji kwanza kuhakikisha kuwa tumetatua tatizo la mgogoro wa kisiasa Zanzibar ambao unaendelea kumong'onyoa misingi ya umoja wa visiwa hivi na kuathiri maendeleo yake. Tunahitaji kuwa na Zanzibar imara isiyoyumba ili kuwa na Muungano imara usiyoyumba. Naomba nifikie Hitimisho kwa kunukuu kutoka katika Utangulizi wa Manifesto ya Uchaguzi ya CUF, pale tuliposema:


"Mtazamo wetu ni kwamba Wazanzibari tutakuwa na nguvu na sauti licha ya udogo wetu ikiwa tutakuwa na mfumo shirikishi badala ya tenganishi na kwamba tunaweza kuyafikia, kwa umoja wetu, mengi ambayo hatukuweza kuyafikia kwa kugawanyika kwetu."[15]

Mfumo Kristo: KHATIMA YA ZANZIBAR NA MUSTAKBALI WA MUUNGANO

Mzee Tajo daima ntakukumbuka, ingawa mahasimu wako na vizazi vyao wametumia nguvu nyingi kukufuta kwenye siasa na historia ya Zanzibar.Kwa kweli ulikuwa muakilishi mahiri,mwalimu na mtumishi kwa watu wako. Uliona mbali sana,
ulivyo amua kuwashauri wasikimbilie kudai uhuru, wakasomeshe vijana kwanza, na hapo wakamua kuziba masikio yao. Ulienda mbele zaidi ukaamua kuunganisha chama chako na wa afro. Jitihada zako za kuona umuhimu wa elimu kwenye taifa, ulijaribu kuzungumza na wachina na wengineo, ili vijana wa kizanzibar wakosome, na hapo wakakufukuza na kuanza kukejeli na kukuchezea ngoma na kukuita chachandu. Matokeo yake sasa tunayaona, Ile chachandu ambayo waliokuwa wakikuchezea hapo nyumbani, sasa hivi ndio wanatupaka kwenye macho, hatuoni hatuelewi, macho yanawasha kwa pilipili. Mungu akulaze pema Tajo,na sisi utuombee huko kwa mola tuweze tatua hii Project ya Mungano.
 
Back
Top Bottom