Kesi ya Saileth Vithlani wa kashfa ya Rada

Kesi ya Saileth Vithlani wa kashfa ya Rada

Status
Not open for further replies.
Akishatiwa mbaroni, mashtaka mengine yako mbeleni.. tunataka abambwe kwanza... ni lazima tuhakikishe kuwa hawezi kuunda Kikosi cha Kisasi, au kula Njama kuharibu uchunguzi. Kwa jinsi mambo yalivyo inaonekana huyu ndiye Malaika wa Shetani ambaye kwa hakika tuhuma anazokabiliwa nazo ni sawa na Salamu toka Kuzimu.

Yeyote ambaye anamfahamu au anafahamu alipo ahakikishe kuwa anampatia ujumbe toka serikali ya Tanzania ujumbe ambao ni sawa na Simu ya Kifo. Sina uhakika kama ana ulinzi wowote kiasi cha kuweza kuonekana ni Maskini Jeuri kwani jinsi anavyofahamika hapendi kuonekana mchana, mara nyingi utamkuta Dar-es-Salaam Usiku.

Kwa yeyote anayemtafuta lazima ahakikishe yeye mwenyewe anayo Hawala ya Fedha kwani endapo atahitaji tiketi aweze kurudi naye salama ama sivyo itakuwa ni Roho Mkononi. Huyu bwana kutokana na shughuli zake amekuwa kama kile kisa cha Ngoswe - Penzi kitovu cha Uzembe na watu kumuamini walifanya makosa.

Jitihada za kumtafuta zitakuwa ni kama Usiku wa Balaa ambapo hakuna kinachotabirika kwani hadi mwisho ni lazima wale wanaomtafuta wajiulize "Tutarudi na Roho Zetu?". Makosa kidogo tu yatakuwa yanawafanya wamtafutao wapotee kama yule bwana aliyepotea katika Mzimu wa Watu wa Kale. Ni lazima tuunganishe nguvu zetu na kudhamiria kama Kuli vinginevyo itakuwa ni kama mtu Aliyeonja Pepo au kama mambo ya nchi ya Kusadikika.

Nina uhakika huyu bwana atajaribu kutoa kitu kidogo ili asikamatwe lazima watu wamuambie "Pesa Zako Zinanuka". Hata hivyo isidhaniwe kuwa kwa kuwekwa mbaroni huyu bwana atakuwa amefikia Kikomo, kwani inasadikiwa anayo Roho ya Paka. Hata hivyo tusikubali geresha hizo na tufanye jitihada zetu za kumtia mbaroni ziwe ni za Kufa na Kupona.

Kwa hakika ndugu zangu kukamatwa kwa Vithlani na hatimaye kufikishwa Mahakamani na hatimaye kukutwa na hatia itakuwa ni jitihada zinazostahili Zawadi ya Ushindi! Wanausalama wetu watumie njia zote kumtia mbaroni kwa amani, lakini Akibisha, Mlipue!

Mwanakijiji asante sana kwa kunikumbusha hizo riwaya, umenifurahisha sana. Na jinsi ulivyopangilia huo mlolongo, hongera, imependeza.
 
plosi wa tanzania wamekuwa hivyo muda mrefu,unadhani hawajui alipo...?wahindi wamekuwa marafiki wa wakubwa muda mrefu..

Mkomboziufisadi, naomba usilete mambo yatakayo onekana ya kibaguzi katika hili swala. Wahindi ni watu kama Waafrika tu au asilia nyingine yoyote, na kama wako Tanzania na ni raia wana uhuru wa kuwa marafiki na yeyote yule aliyekaribu nao. Matendo yao ndiyo ya kuhoji. Basi ,tumtafute huyu mtuhumiwa kwa makosa yake na wala si Uhindi wake.

SteveD.
 
Mlioko UK mnaweza kuchapa na kubandika kiujanja ujanja kwenye notice bodi zenu hasa ile mitaa ya waasia..? au chini ya miembe na mipera?
 
Huyo sidhani kama anaweza kukimbilia UK, mimi nafikiri atakimbilia kwenye nchi mojawapo tu Afrika au basi India, maana kwa kutumia hela zake, serikali nyingi za kiafrika zinaweza kumkubali ajisitiri.

Mimi nitabandika picha yake kwenye mkia wa mudguard ya baiskeli yangu hapa Tosamaganga, just incase!!

SteveD.
 
..mwafrika,hizi siasa kali tena zenye hasira kali umezianza lini?

..taratibu,haya mambo yako mengi,halafu inaonekana hayaishi kila kukicha,yatakutia kichaa buree!punguza kidogo hasira!

..hiki kilio chetu sote!ingawa wengine wanacheka,ilihali hawajui kuwa wanalia!

Mkuu Dar si LAMU,

Haya mambo mbona yalishanitia ukichaa muda mrefu sana! Thanks GOD niko marekani na ikifika weekend kama hii kunakuwa na alot of activities kusafisha akili kidogo la sivyo ningekuwa nimerudi bongo na kujiunga na jeshi muda mrefu sana!

Nilikuahidi last time kuwa ninapunguza hasira zangu na kwa kweli nimekuwa kwenye therapy ya muda mrefu sasa toka kwa madaktari bingwa wa JF - Nyani Ngabu na SteveD - ambao wana secret drug inayofanya kazi within seconds. Usijali sana nina dozi yakutosha so hakuna watoto au wanyama watakaodhurika hapa.

Hii case ya this guy inachafua moyo na kwa kweli kwa maoni yangu inabidi this guy apigwe mishale kama sita yenye sumu kali sana na afe maramoja. Wakati mwingine, watu kama hawa wanahitaji kuuwawa tu maana mahakama na polisi haziwawezi.

nimefuatilia kwa muda sasa historia ya Mafia hapa US na nimegundua kuwa nguvu ya mafia ilipunguzwa sana walipoanza kuuwawa hadharani na sio kupelekwa polisi au magereza. The same thing can happen to mafia hawa wa kibongo na wapambe wao.

haya ni maoni yangu tu!
 
Wait A Minute, Mbona Haijatangazwa Zawadi Nono Itatolewa , Waseme How Much, Fasta Sana Wanaume Waache Vibarua Waingie Mzigoni Kumsaka ...toa Pesa Upate Pesa,nothing For Free!!!!!!!!
 
Mkuu Dar si LAMU,

Haya mambo mbona yalishanitia ukichaa muda mrefu sana! Thanks GOD niko marekani na ikifika weekend kama hii kunakuwa na alot of activities kusafisha akili kidogo la sivyo ningekuwa nimerudi bongo na kujiunga na jeshi muda mrefu sana!

Nilikuahidi last time kuwa ninapunguza hasira zangu na kwa kweli nimekuwa kwenye therapy ya muda mrefu sasa toka kwa madaktari bingwa wa JF - Nyani Ngabu na SteveD - ambao wana secret drug inayofanya kazi within seconds. 🙂 🙂 Usijali sana nina dozi yakutosha so hakuna watoto au wanyama watakaodhurika hapa.

Hii case ya this guy inachafua moyo na kwa kweli kwa maoni yangu inabidi this guy apigwe mishale kama sita yenye sumu kali sana na afe maramoja. Wakati mwingine, watu kama hawa wanahitaji kuuwawa tu maana mahakama na polisi haziwawezi.

nimefuatilia kwa muda sasa historia ya Mafia hapa US na nimegundua kuwa nguvu ya mafia ilipunguzwa sana walipoanza kuuwawa hadharani na sio kupelekwa polisi au magereza. The same thing can happen to mafia hawa wa kibongo na wapambe wao.


haya ni maoni yangu tu!

Very true, Mwafrika wa Kike na kubaliana nawe hapo juu kwa asilimia 200!!

Indirect but direct, way to go sometimes!

SteveD.
 
Wait A Minute, Mbona Haijatangazwa Zawadi Nono Itatolewa , Waseme How Much, Fasta Sana Wanaume Waache Vibarua Waingie Mzigoni Kumsaka ...toa Pesa Upate Pesa,nothing For Free!!!!!!!!

Are you in the WANT to redirect mabilioni ya Kikwete?! he he

SteveD.
 
Mkomboziufisadi, naomba usilete mambo yatakayo onekana ya kibaguzi katika hili swala. Wahindi ni watu kama Waafrika tu au asilia nyingine yoyote, na kama wako Tanzania na ni raia wana uhuru wa kuwa marafiki na yeyote yule aliyekaribu nao. Matendo yao ndiyo ya kuhoji. Basi ,tumtafute huyu mtuhumiwa kwa makosa yake na wala si Uhindi wake.

SteveD.

hauwezi kuzungumzia ubaguzi kama wewe sio mbaguzi,mie nimeelezea ukweli na wala sijasena mambo ya ubaguzi..
vp steve D,umetumwa.

mie nipo hapa nitabandika hapa hotelini hii picha ya huyu fedhuli
 
Kwi kwi kwi,

hilo libaba halihitaji kunyongwa bali linahitaji kupigwa kwa mishale ya sumu ya kimasai (ile ambayo hutumika kuua simba) ili lisipate nafasi ya kutibiwa hospitali.

Nilijua siku nyingi kuwa unatafuta kuniona na sasa umepata nafasi hiyo. Tuwasiliane kwenye PM maana krismas naenda bongo na labda nitapunguza siku za kukaa Amsterdam (kuvuta bangi kihalali) na kupitia UK ili "tusaini MOU memorandum of understanding" kati yangu na wewe.

Mwafrika wa Kike,

Mmmmmmhhhhh!!! kusign MOU tena? Hapo nimeshindwa mama, wajanja wakiiona hiyo MOU nitakuja itwa fisadi kama Karamangi.

Ila za huko Amsterdam, niulize, nikueleze coffee bar gani wana bangi nzuri.

Jamani ni weekend inaanza, inabidi kuangiza na utani kidogo!
 
hauwezi kuzungumzia ubaguzi kama wewe sio mbaguzi,mie nimeelezea ukweli na wala sijasena mambo ya ubaguzi..
vp steve D,umetumwa.

mie nipo hapa nitabandika hapa hotelini hii picha ya huyu fedhuli

Ndiyo nimetumwa na Watanzania walalahoi wasiopenda ubaguzi wa aina yoyote, matamshi, nakala wala maandishi yanayoweza kuonekana yana mlengo wa namna hiyo.


Mkombozi, hapo kwenye blue, hakikisha unabandika kwenye corridor zote, kwenye lift na misalani 🙂 Angalia wasikukamate tu wakasema unaendeleza graffiti...


SteveD.
 
yeah utani leo unaruhusiwa ila mtu akija kubondwa na rungu la mtu wa bush asije kulia "lele mama". Mali nyingine ni za kuangalia tu.. zina wenyewe...
 
Akishatiwa mbaroni, mashtaka mengine yako mbeleni.. tunataka abambwe kwanza... ni lazima tuhakikishe kuwa hawezi kuunda Kikosi cha Kisasi, au kula Njama kuharibu uchunguzi. Kwa jinsi mambo yalivyo inaonekana huyu ndiye Malaika wa Shetani ambaye kwa hakika tuhuma anazokabiliwa nazo ni sawa na Salamu toka Kuzimu.

Yeyote ambaye anamfahamu au anafahamu alipo ahakikishe kuwa anampatia ujumbe toka serikali ya Tanzania ujumbe ambao ni sawa na Simu ya Kifo. Sina uhakika kama ana ulinzi wowote kiasi cha kuweza kuonekana ni Maskini Jeuri kwani jinsi anavyofahamika hapendi kuonekana mchana, mara nyingi utamkuta Dar-es-Salaam Usiku.

Kwa yeyote anayemtafuta lazima ahakikishe yeye mwenyewe anayo Hawala ya Fedha kwani endapo atahitaji tiketi aweze kurudi naye salama ama sivyo itakuwa ni Roho Mkononi. Huyu bwana kutokana na shughuli zake amekuwa kama kile kisa cha Ngoswe - Penzi kitovu cha Uzembe na watu kumuamini walifanya makosa.

Jitihada za kumtafuta zitakuwa ni kama Usiku wa Balaa ambapo hakuna kinachotabirika kwani hadi mwisho ni lazima wale wanaomtafuta wajiulize "Tutarudi na Roho Zetu?". Makosa kidogo tu yatakuwa yanawafanya wamtafutao wapotee kama yule bwana aliyepotea katika Mzimu wa Watu wa Kale. Ni lazima tuunganishe nguvu zetu na kudhamiria kama Kuli vinginevyo itakuwa ni kama mtu Aliyeonja Pepo au kama mambo ya nchi ya Kusadikika.

Nina uhakika huyu bwana atajaribu kutoa kitu kidogo ili asikamatwe lazima watu wamuambie "Pesa Zako Zinanuka". Hata hivyo isidhaniwe kuwa kwa kuwekwa mbaroni huyu bwana atakuwa amefikia Kikomo, kwani inasadikiwa anayo Roho ya Paka. Hata hivyo tusikubali geresha hizo na tufanye jitihada zetu za kumtia mbaroni ziwe ni za Kufa na Kupona.

Kwa hakika ndugu zangu kukamatwa kwa Vithlani na hatimaye kufikishwa Mahakamani na hatimaye kukutwa na hatia itakuwa ni jitihada zinazostahili Zawadi ya Ushindi! Wanausalama wetu watumie njia zote kumtia mbaroni kwa amani, lakini Akibisha, Mlipue!



We bwana umebarikiwa...sina la kusema zaidi...swaaafii kabisa.


 
🙂 wewe Mtanzania achana na anga za watu... utazua bifu buree.....!!! Kumbuka Nyani nimeshamtungua mtini kutokana na antics zake katika hili........he he he


SteveD.

SteveD,

Nimegundua siri ya Mwafrika wa Kike, ukitaka kumchokoza basi fanya hivyo Ijumaa na Jumamosi, huwa mtulivu kama Simba aliyeshiba. Labda anakuwa tayari amesha yavuta majani yake kwa maandalizi ya kujirusha weekend.

Si umeona hata alivyojibu? Nilikuwa najaribu ku test hypothesis
yangu, naona inafanya kazi vizuri.
 
yeah utani leo unaruhusiwa ila mtu akija kubondwa na rungu la mtu wa bush asije kulia "lele mama". Mali nyingine ni za kuangalia tu.. zina wenyewe...

mwanakijiji,Lini Msola atang'oka?umeshachukua hatua gani
 
yeah utani leo unaruhusiwa ila mtu akija kubondwa na rungu la mtu wa bush asije kulia "lele mama". Mali nyingine ni za kuangalia tu.. zina wenyewe...

Mwanakijiji,

Mmmmmhhhhh!!! Basi mzee, nimesikiliza ushauri wako, nimeacha, maana rungu la kutoka kwa Bush linaweza kupasua kichwa cha mtu.
 
SteveD,

Nimegundua siri ya Mwafrika wa Kike, ukitaka kumchokoza basi fanya hivyo Ijumaa na Jumamosi, huwa mtulivu kama Simba aliyeshiba. Labda anakuwa tayari amesha yavuta majani yake kwa maandalizi ya kujirusha weekend.

Si umeona hata alivyojibu? Nilikuwa najaribu ku test hypothesis
yangu, naona inafanya kazi vizuri.

Guilt as charged!

Sikubishii Mtanzania kwani kulingana na msongo wa maisha haya inabidi kupata muda wa kusafisha akili. Nilipokea malamiko mengi sana toka kwa members hapa kuhusu ile mechi yangu kali kabisa kati yangu na Kada iliyofanyika jumamosi moja hapa JF back in the days ingawa ile mechi ilikuwa na washuhudiaji wa zaidi ya mia mbili kwa dakika. Toka wakati huo niliahidi kuwa nice on weekends na kutokuwa excessive kwenye threads kwa issue binafsi na members.

Nilikubaliana na ushauri toka kwa madaktari bingwa kabisa wa JF - Nyani ngabu na SteveD - wa kutumia ile special drug on weekends ili kujiandaa na mapambano ya wiki inayofuata.

Natumaini utanilipa kitu kidogo maana nimetumika kama sample na assistant katika research yako hii - teh teh teh
 
Jamaa ameshiba mihela ya kuwa middle man na dubious deals...PCB na serikali kwa kuanzia wafreeze assets za Vithcorp na Merlin Intl, alafu wamtumie meseji kupitia kwa mama yake pale West London. Yule Somaiya yeye amesalimika kwenye hili maana yeye alipewa $ 400,000.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom