Erythrocyte
JF-Expert Member
- Nov 6, 2012
- 117,651
- 218,131
Kesi ya Ugaidi inayomkabili Mbowe na Wenzake watatu inaendelea tena leo , ambapo Shahidi wa tatu ambaye anajulikana kama Konstebo Msemwa ataendelea kutoa Ushahidi wake ,
Tukumbuke kwamba mashahidi wa Jamhuri zaidi ya 20 ni askari Polisi
===
Jaji ameingia..
Watu wanasimama,
Kesi inatajwa, watu wanaketi..
Jaji: Wakili wa Serikali Wakili wa Serikali anatambulisha Mawakili wa Jamhuri..
Adv. Kibatala anatambulisha Jopo la mawakili wa utetezi..
Peter Kibatala
Jonathan Mndeme
Fredrick Kihwelo
Dickson Matata
John Mallya
Sisty Aloyce
Alex Masaba
Idd Msawanga
Gaston Garubindi
Evaresta Kisanga
Hadija Aron
Faraj Mangula
Maria Mushi
George Masoud
Michael Lugina
Jaji: nimeona mawakili wa utetezi wapo upande huu, Je mpo sawa?
Wakili wa Serikali: Tupo sawa
Wakili Peter Kibatala: Tupo sawa
Jaji: Wakili Kidando wakili wa serikali: shauri limekuja kwa ajili ya kusikiliza na mpaka sasa tumeshaleta mashahidi 3 kati ya 7, na tunaomba hairisho mpaka Jumatatu.. tunaomba kupata muda wa kupitia ushahidi uliowasilishwa
Wakili wa serikali: tunaomba kuondoa mashahidi wengine waliobakia kwa dhumuni la kesi ndogo. tubakie na hao hao watatu Wakili wa Serikali anakaa chini.. Jaji: kuna lolote upande wa utetezi? Jaji anaendelea kuandika.
Kibatala: Hakuna mheshimiwa Jaji.. Jaji anaendelea kuandika..
Jaji: Shauri hili dogo kwa upande wa Jamhuri limefungwa, Nitamsikiliza wakili John Mallya...
Wakili Mallya: Mshtakiwa wa pili atajitetea mwenyewe na mashahidi wengine watatu pamoja na yeye watakuwa jumla wanne
Jaji: Kuna kingine?
Mallya: Mheshimiwa ni hayo
Jaji: Mpo tayari kuanza utetezi hata sasa? au Mngehitaji muda wa kujiandaa?
Mallya: tupo tayari Jaji anaandika. Mahakama kimya, Nje mvua inapiga kidogo
Jaji: Shahidi wa kwanza wa shauri dogo la utetezi aje kwenye kizimba.
- Shahidi anaenda kizimbani anasindikizwa na askari Magereza
Jaji: tutajie majina yako kwa ukamilifu wako unaitwa nani?
Shahidi: Adam Kasekwa
Picha: Katikati ni Adam Kasekwa(Adamoo Komando)
Jaji: Kuna Jina limekuwa likitumika la Adamoo unalitambua?
Shahidi: Nalitambua
Jaji: Dini yako Mkristo?
Shahidi: ndiyo
Jaji: Apa
Shahidi: Naapa mbele ya mahakama hii, yote nitakayosema yatakuwa kweli tupu, Eeh! Mwenyezi Mungu nisaidie.. Jaji unaweza kutoa ushahidi wako ukiwa umesimama au umekaa, Wakili John Mallya unaweza kuendelea.
Mallya: Shahidi umetoka kuapa, unaweza kututambulisha ulipokuja mahakamani umetokea wapi?
Shahidi: nimetokea gereza la Segerea.
Mallya: Siku za nyuma ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuwa askari wa JWTZ kikosi namba 72 Sangasanga Morogoro
Mallya: ni Kikosi cha namna gani?
Shahidi: zamani kikosi cha Makomandoo siku hizi kinaitwa SPECIAL FORCE
Mallya: umehudumu kwa miaka gani?
Shahidi: Miaka sita kuanzia 2012 mpaka 2018
Mallya: Kipi kilikufanya uache kazi?
Shahidi: sikuacha bali niliachishwa na wakuu wangu
Jaji: sijui mnasikia maana naona kelele za mvua zinaingilia, KILA MTU ANAYO HAKI YA KUSIKILIZA HII KESI
Jaji: Jamani Mnasikia Wote: tunasikiaaaaaa
Jaji: Kama mkiona hamsikii tunaweza ku' break kidogo, Hasa mawakili na washitakiwa muwe free tafadhali.
Mallya: Mwaka 2016 mpaka 2017 nilikuwa kwenye misheni KONGO na Kurejek salama nchini kwangu na kuendelea na kazi.. wakuu wangu wakagundua kuwa nina tatizo la BATTLE CONFUSION
Mallya: Unaweza kumueleza, Jaji Battle Confusion inakuwaje?
Shahidi: siwezi kujijua sana lakini ni hali ya Askari anaposikia milio ya mizinga na risasi kwa wingi anakuwa hafanyi vile anavyotakiwa na wakubwa wake
Mallya: Kwenye Afya ana athiri mfumo gani? Shahidi: mfumo wa akili.
Mallya: sasa umeshafukuzwa kazi baada ya Battle Confusion, Je ulikuwa unafanya shughuli gani?
Shahidi: nilikuwa nafanya biashara ya kununua maharage huko Morogoro sehemu inaitwa Nongwe na kuuza soko la Lubeho, kote Morogoro
Mallya: unamfahamu mshtakiwa namba 4?
Shahidi: simfahamu sana ila nilitakiwa nikafanye kazi ya VIP PROTECTION
Mallya: kazi ya VIP PROTECTION ni kazi unayoweza kuifanya?
Shahidi: Ndiyo Wakili wa Serikali: OBJECTION
Mallya: naondoa swali Mallya ulifanya nini?
Shahidi: nilikuwa kwenye hatua ya mazungumzo ya kazi
Mallya: yalikuwa yanahusisha nini?
Shahidi: kuhusiana na majukumu ya kazi na malipo yetu
Mallya: ilikuwa lini?
Shahidi: Mwishoni wa mwezi wa 7 mwaka 2020
Mallya: Makubaliano ya kufanya kazi na mshtakiwa wa 4 mlikuwa mnafanya wapi?
Shahidi: mara ya kwanza tulifanya Moshi
Mallya: nakupeleka tarehe 05 Mwezi 08 mwaka 2020 kilitokea nini?
Shahidi: siku hiyo nikiwa na mshtakiwa mwenzangu namba 03 Mohammed Ling'wenya sehemu inaitwa maduka, tukavamiwa na watu kama watano, walinivamia mimi kwanza wakaanza kunipiga, mshtakiwa mwenzangu akaja kuniokoa.
Shahidi: alipofika akawauliza "Mbona mnapiga huyu mtu?".. wakamuuliza wewe unamfahamu huyu, akajibu ndiyo namfahamu.. wakachukua madawa na silaha, nikawasikia wakisema ana madawa.. wakati Mimi wakiendelea kunishambulia.
Shahidi: Mshitakiwa mwenzangu akawawahi akitoa vitu mfukoni, nikasikia kwa maneno akisema huyu mmeshamuwekea madawa? akiwa anamaanisha mimi... mmemuweka madawa na silaha? Mimi natoa vitu vyangu kabisa msije mkaniweka na mimi, Wakati huo mimi wakiendelea kunishambulia.
Mallya: unaweza Kuwakumbuka watu hao ukiwa hapa Mahakamani?
Shahidi: Mahakamani nimeshawaona watu 2
Jaji: Subiri kidogo, anaendelea kuandika.
Mallya: ni nani umewaona hapa mahakamani?
Shahidi: Ramadhani Kingai na Mahita ambao nimekuja kuwafahamu majina yao hapa mahakamani
Mallya: hawa watu wawili ambao umewataja walikuwa na majukumu gani?
Shahidi: nilikuwa nawatambua kwa sura na matendo yote ya kunipiga na kuniwekea Madawa na silaha.
Jaji: Ukisema kuwekewa madawa na silaha nini kilichotokea?
Shahidi: Wakati wananipiga na wamenibana, akaingiza mkono wake kwenye suruali akasema ana madawa na mwingine akaingiza kitu nyuma ya mkanda akatoa kitu akasema ana silaha
Mallya: hili eneo ambalo tukio limetokea lilikuwa ni eneo la wazi?
Shahidi: pana maduka ya kubadilisha pesa. M-pesa na tiGoPesa na Grocery pembeni
Mallya: Wewe ulikuwa sehemu gani?
Shahidi: nilikuwa katikati upande kulia maduka na upande wa kushoto Grocery..
Mallya: Ulikuwa umekwenda kufanya nini?
Shahidi: kuagiza chakula, Nilikuwa naandaliwa nyama ya kuchoma lakini hata kulipa bado
Mallya: nini kilifuata,?
Shahidi: baada ya mwenzangu kusema natoa vitu vyangu msije kuniwekea kama mlivyo muwekea huyu, wakatukamata na wakatufunga pingu na kutuingiza kwenye gari yao..
Mallya: baada ya kuingizwa kwenye gari waliwapeleka wapi?
Shahidi: Muda wote tulikuwa tunapigwa, hatukujua tunaelekea wapi, baadae wakatufikisha kituo cha polisi
Mallya: kituo gani?
Shahidi: nilikuaa sikijui, lakini baada ya kuongea mahakamani nimegundua ni Central Moshi
Mallya: Baada ya kupelekwa Central Moshi kitu gani kilifuata?
Shahidi: walinitoa pale ndani kituoni kuna chumba cha pembeni palikuwa na jopo la watu wengi wakanivua nguo zote, nikawa ninaning'inizwa kwenye kichuma fulani mithili ya MSHIKAKI au POPO
Shahidi: nikiwa siwezi kusimama wakanitoa pingu wakanivalisha suruali na shati, wakaanza kunikokota
Jaji: umezungumzia kuvaa!
Shahidi: Ndiyo walinivalisha suruali. wakawa wananikokota kunipeleka mahabusu, baada ya kufika mahabusu wakanifunga pingu za mikono wakaniacha ndani
Mallya: jambo gani lilifuata? Shahidi: ndani ya mahabusu kuna chumba kidogo cha mlango wa nondo wakawatoa watu mule wakanifungia mimi..
Mallya: ulijua hatima ya yule mtuhumiwa mwingine?
Shahidi: sikujua hatima yake Mallya: nini kilifuata?
Shahidi: niliendelea kukaa ndani
Mallya: kuna ushahidi umetolewa kuwa mlizunguka maeneo mbalimbali Moshi na Hai
Shahidi: hapana sikutolewa kwenda popote
Shahidi: Ndani ya chumba kuna Askari alikuja kumwaga maji
Mallya: nini kiliendelea
Shahidi: kesho yake nilikuja kugundua ni kesho tayari baada ya kuona Jua
Shahidi: wakanitoa wakinilazimisha nitembee lakini nikawa nikawa siwezi Simu inaita kwa VIBRATION (mithili ya Philips)
Jaji: naomba kila Mtu aweke simu yake katika mazingira ambayo hayaathiri kazi yangu au ya shahidi, Msilazimishe niongee Jambo ambalo sitaki kuongea..
Shahidi: sikujua naenda wapi, nilitambua tu nipo kwenye gari na ikaanza kutembea
Mallya: kitu gani kiliendelea?
Shahidi: nikiwa ndani ya gari kabla haijatoka kwa muda wa nusu saa, mateso yaliendelea kwa kunichoma choma na bisibisi
Shahidi: wakawa wananiambia "Leo ndiyo mwisho wa maisha yako, na kwamba hapa tulipo unamjua nani, nikajibu simjui Mtu, wakasema basi na wewe hakuna anayejua upo na nani"
Mallya: Endelea
Shahidi: nilikuwa nimelazwa kwenye floor ya gari, siyo kwenye siti..
Shahidi: baada ya safari ya muda mrefu sana, tukafika sehemu wakanishusha kwa kunikokota vievile na tulipofika kwenye kachumba wakanitoa Jacket wakaniuliza "Unajua upo wapi hapa?" nikawaambia "hapana sifahamu" wakafunga mlango nikiwa ndani nikiwa na pingu lakini Jacket wamenitoa
Mallya: unamkumbuka aliyekuwa anakuuliza hayo?
Shahidi: namkumbuka ni Goodluck
Mallya: Jambo gani lingine lilitokea kwenye kile chumba?
Shahidi: nikiwa na pingu nikajikokota kusogea mlangoni bahati nzuri nikaona watu wengine wamefungiwa kwenye chumba kingine kidogo mule
Shahidi: nilikaa pale tarehe 7, 8 na 9 na ilipofika tarehe 9 usiku wakaja kunichukua usiku.
Mallya: umesema umekamatwa Moshi tarehe 05 je kati ya tarehe 5 Mpaka tarehe 7 kuna nini kilitokea?
Shahidi: tarehe 05 - 7 nilikamatwa Moshi na kuteswa kisha nikasafirishwa kuja TAZARA
Shahidi: tarehe 09 wakanitoa usiku, siku hiyo angalau nilikuwa na uwezo wa kutembea, Lakini wakaniambia huku tunakoenda yanaenda kukuta yaleyale ya Moshi, sasa UJIANDAE Mallya: Tarehe 09 nini KILIFUATIA?
Shahidi: Wakinitoa wakanipandisha kwemye gari, safari ikaanza..
Shahidi: haikuchukua muda kama Moshi. Siku hiyo sikuwekwa chini kama walivyonisafirisha kutoka Moshi. wakaniingiza kwenye chumba wakanifungua
Jaji: Subiri kidogo..
Jaji: unasema mlipofika wakakushusha?
Shahidi: walifikisha mpaka kwenye chumba, Kilipofunguliwa wakanitoa Jacket usoni, wakaniamuru niingie ndani
Jaji: Ndiyo
Mallya: rudi nyuma kidogo shahidi baada ya kuambiwa kuwa upo TAZARA, Ulifanya jambo lolote kuthibitisha upo TAZARA?
Shahidi: ilipofika jioni nilikuwa nasikia mlio wa honi ya TRENI,nikagundua nipo MAENEO yanayofanana na TAZARA
Mallya: sasa tayari upo sehemu nyingine umefumguliwa koti machoni
Shahidi: niligundua umeshaingia usiku, kesho yake usiku tena akaja Kingai na Goodluck wakanitoa ndani
Mallya: Taratibu Shahidi Jaji aandike
Shahidi: wakanipeleka Kwenye chumba kilichokuwa kina meza, Goodluck akawa mlangoni na Kingai akakaa mbele yangu tukawa tunatazamana
Jaji: NDIYO
Mallya: Pingu unazozungumzia ni zipi
Shahidi: pingu za chuma
Mallya: kuna wakati wowote walikutoa Pingu tangu utoke Moshi?
Shahidi: akamuamuru Goodluck anifungua mkono mmoja, wakanifungua wa kulia wakaendelea kufunga wa kushoto, wa kulia ukawa upo FREE..
Shahidi: Kingai akaniambia "mateso yanapopungua ujue kuna kuna mambo mazuri yamekaribia" m tunataka uwe mstaarabu, hapa kuna nyaraka tunakuja mnazo tunataka usaini..
Mallya: Mkono wa kushoto na pingu, wa kulia na kalamu, nini kilifuata!
Shahidi: akawa ananionyesha sehemu za kuandika kama "NATHIBITISHA" au KUSAINI
Mallya: Ulipata Kujua Kimeandikwa kitu gani ktk kile kingai anachokuoatia Kuthibitisha au Kusaini
Shahidi: Hapana
Mallya: Moshi umetuambia walikupiga, wakakulaza kwenye Floor sehemu yenye Joto kwenye gari, Je unauthibisho wowote unaoweza kuonyesha mahakamani?
Shahidi: naweza Kuthibitisha kwa kuonyesha sehemu nilizoumizwa, Makovu yanayoeleka kupona na mguu nimeumia leo siwezi kutembea vizuri
Jaji: kabla hajatuonyesha atueleze yapo sehemu gani, isije ikawa sehemu ambayo yanaweza kutweza utu wake
Mallya: Shahidi tueleze maeneo ya mwili ambayo umeumia
Shahidi: Mguu wangu wa kushoto na mkono wamgu wa kushoto
Jaji: sina tatizo na maeneo hayo, Wakili unaweza kuendelea
Mallya: unaweza kusimama kuonyesha mahakama?
Jaji: unaweza kusimama na mimi nitasogea kuweza kuona..
Jaji: hiyo ni mguuni (anaonyeshwa)
Jaji: sawasawa anarudi kukaa sehemu yake
Shahidi: Anarudi sehemu yake pia Mahakama ipo kimyaaa!
Mallya: kuna wakati ulitaka kumueleza Jaji kuna vingine ulitaka kumueleza nini hivyo?
Shahidi: Takribani Mwaka 1 na mwezi sasa tangu niteswe na kuumizwa, sikuwahi kupelekwa hospitali kwa matibabu na mpaka sasa nahisi maumivu makali
Mallya: Je ulipata kutambua kuwa upo kituo gani cha polisi?
Shahidi: nilikuja kujua nipo kituo cha polisi MBWENI
Mallya: Ulijuaje kuwa upo Mbweni?
Shahidi: kuna askari polisi alikuwa zamu, alisema hamtakiwi kujua mpo wapi, lakini mpo kituo cha Polisi Mbweni
Mallya: Utofauti wa majina yako Mbweni ulijuaje?
Shahidi: siku ya kwanza nafika Mbweni nilifika pale Mlangoni nikakabidhiwa kikaratasi kuwa kuanzia siku hiyo naitwa VICENT JUMA na wakikikuuliza umekamatiwa wapi sema TABORA na useme kesi ya UNYANG'ANYI, ukiseme Majina yako tutajua
Mallya: baada ya kujua upo Mbweni nini kiliendelea?
Shahidi: niliendelea kukaa Mbweni muda wote mpaka siku nafikishwa mahakamani na muda wote sikufunguliwa pingu
Mallya: unakumbuka ilikuwa siku gani? Mahakama gani?
Shahidi: ilikuwa Tarehe 19 Mwezi 08 Mwaka 2020
Shahidi: Nilipofika mahakamani ndipo nilikutana na mshtakiwa mwenzangu ambaye tulikamatwa pamoja Moshi na mshtakiwa namba 1..
Jaji: Kama naelewa tangu mtoke Moshi hamkuwahi kuonana
Shahidi: ndiyo hatukuwahi kuonana kwa macho
Mallya: Je mliwahi kuwasiliana?
Shahidi: tukiwa TAZARA tuliwasiliana kwa sauti akitokea chumba kingine lakini hatuonani
Mallya: tarehe 05 RAU Madukani, Moshi ukisema wamekuwekea vitu, Je wewe Binafsi ulikuwa na nini mfukoni?
Shahidi: nilikuwa na pesa Laki 2 na 60 taslimu, simu ya Itel na line ya Halotel
Mallya: hivyo vitu vipo wapi?
Shahidi: tangu wavichukue sijavipata
Mallya: nani alichukua.+?
Shahidi: alichukua mfukoni Goodluck akampatia Kingai
Jaji: Shahidi bado unayo maji mkononi, Kama utahitaji break utasema maana kuulizwa maswali kunatumia sana akili na kuchosha mwili
Shahidi: Asante Mheshimiwa Jaji
Mallya: ukiondoa Kingai na Goodluck kuna mtu mwingine unamkumbuka alikuja Mbweni?
Shahidi: nilimuona Mahita
Mallya: alikuja kufanyeje?
Shahidi: nilimuona wakati wanakuja kuniona, Lakini hakuhusika kuingia katika kile chumba
Jaji: chumba kipi?
Shahidi: chumba kile ambacho kilikuwa na Meza mbili na Kingai
Jaji: nimekuelewa
Mallya: Umesikia wakitoa ushahidi hapa,kwamba walikuwa wanawapa matunzo mazuri na walikuwa wanatunza utu wenu
Shahidi: si kweli
Mallya: walisema waliharibikiwa gari Himo je unasemaje kuhusu hilo?
Shahidi: kwangu ni ngumu kuhusu kuelezea kwa sababu tulikuwa tunasimama sehemu nyingi lakini nilikuwa nimefungwa usoni nisione kitu
Mallya: je unakumbuka tangu tarehe 05 mpaka Kingai anakuletea maelezo yako usaini zilikuwa zimepita siku ngapi
Shahidi: Siku 06
Wakili Mallya: Kwa sasa sina la zaidi Mheshimiwa Jaji
Jaji: Wakili Malya unafikiri Shahidi wako anaweza Kuendelea.?
Mallya: it depends
Jaji: nimekupa wewe kuamua nilikuwa naweza kuendelea bila kukuuliza
Mallya: Anaweza kuendelea Mheshimiwa
- Anaingia wakili Nashon Nkungu
Nashoni: Je ni kweli baada ya kupata Battle Confusion hukupatiwa matibabu?
Shahidi: hapana nilipatiwa kwa maana nilipelekwa hospitali ya Lugalo
Nashoni: kwenye maelezo watu hawa walikwambia sisi hautufahamu na wewe hutufahamu ni sahihi?
Shahidi: ni sahihi.?
Nashoni: Ulipata hisia gani kuwa na watu hao?
Shahidi: wasiwasi nikaona roho yangu ipo mkononi
Wakili wa Serikali: MHESHIMIWA JAJI HISIA NI KITU GANI
Jaji: hilo linamuhusu mwenyewe, kuhusu hisia zake, haliwezi kuathiri Jambo lolote
Jaji: rudia hisia ulisikiaje hisia zako
Shahidi: niliogopa kwamba naweza kuteswa sana
Nashon: umeeleza kuwa ulikuwa unachomwa BISIBISI, Je ni maeneo gani sasa?
Shahidi: Maeneo ya MBAVU na MATAKONI
Nashoni: Ukisafirishwa kutoka ulipokamatwa Moshi kuja Dar es salaam, TAZARA..
Shahidi: baada ya siku MOJA
Nashon: Uliambiwa kuwa mnaanza safari ya kuja Dar es salaam au popote.?
Shahidi: Hapana sikuambiwa
Nashon: unaweza kujua kwanini hamkuanza safari ya kuja Dar es salaam baada tu ya kukamatwa?
Shahidi: Hapana
Nashon: Unakumbuka kuwa mlifika Arusha baada ya kukamatwa?
Shahidi: Sikumbuki na wala halikwepo jambo hilo
Nashon: unasema ulikuwa na Pesa,260,000/= unakumbuka kuandikiwa risiti ya pesa hizo?
Shahidi: Hapana
Nashon: Mheshimiwa Jaji yangu ni hayo tu
Jaji: Wakili Fred na Matata mtauliza maswali wote 2 au 1 kwa niaba ya mshtakiwa wa 3?
Wakili Fred Kihwelo: Kwa niaba ya mshtakiwa wa tatu hatutokuwa na maswali yoyote
Jaji: Kibatala kwa niaba ya mshtakiwa wa nne
Wakili Kibatala: nataka utuambie kwa vitendo Ulikabwaje pale RAU MADUKANI..
Shahidi: nilikuwa naongea na simu nikiwa nimevaa Jacket naongea na simu, akatokea mtu kwa nyuma akashika mkono wenye simu na Jacket wakati najitetea akatokea kwa mbele mwingine, Mwingine akatokea akanishika mkanda hapa kiunoni..
Kibatala: unaweza kutonyesha?
Shahidi: bahati nzuri suruali niliyovaa siku ile nakamatwa ndiyo niliyovaa leo, haina hata
RUSKI KIBATALA: naweza KUONA?
Shahidi: Ndiyo unaweza kusogea Kibatala: sawa lakini pia mahakama inataka kuona
Kibatala: Wakati wanakukamata hapo ikawaje
Shahidi: akatokea mtu mbele akanipiga ngumi
Kibatala: unamkumbuka?
Shahidi: ndiyo alikuwa dereva wa gari tuliyopanda
Kibatala: Kingai alikwepo eneo la tukio.+?
Shahidi: ndiyo
Kibatala: alikuwa anafanya nini?
Shahidi: yeye ndiyo ALICHUKUA PESA ZANGU BAADA YA kusachiwa
Kibatala: Afande anayeitwa Mahita alikwepo wakati unakamwata.l?
Shahidi: alikwepo na yeye ndiye alikuwa wa kwanza kunikaba wakati naongea na simu
Kibatala: uliwezaje kuona tukio hilo la kukabwa?
Shahidi: niliona kwa sababu ilikuwa mchana na nilikuwa na akili timamu
Kibatala: Wakati wanafika kukukamata waliijitambulisha kwa mujibu wa PGO na sheria.l?
Shahidi: Hapana hawakufanya hilo..
Kibatala: na ni kweli kwamba wakati wanakukamata hawakuwa wameshika Ki' Notebook?
Wakili wa Serikali: MHESHIMIWA OBJECTION anachokifanya Wakili Msomi siyo kinacholekezwa kwa mujibu wa TRIAL WITHIN a TRIAL pamoja kwamba haijasema UKOMO wa maswali.. Matters ambazo ni Mpya zitaipotezea Muda Mahakama
JAJI: Wakili Kibatala..
Kibatala: Kwa heshima na taadhima wakili Msomi mwenzangu HANA HOJA, Shahidi analindwa na Jaji kama ningemuuliza SWALI ambalo lingemdhalilisha ningezuiwa, sijui anamaanisha nini?
Jaji: tuendeleee Shahidi ni wa Utetezi siyo wa mashtaka ,Labda iwe kwa maswali yanayo dhalilisha
Jaji: Tuendeleeeeeeeee Kibatala: uliwahi kuona mtu ameshika NOTEBOOK wakati wa zoezi kukukaba na kukukamata linaendelea?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: wakati unakamatwa ni eneo la wazi bila shaka watu wengi walishuhudia wakati wa Kukamatwa kwako
Shahidi: ndiyo walikuwa wengi
Kibatala: je uliona wakati wowote Kingai anaita watu washuhudie kukamatwa kwako?
Shahidi: Hapana Kibatala: uliona hapa mahakamani kitabu chochote ambacho mahakamani kimeletwa kinaeleza ni aina gani ya silaha ulikamatwa nayo Moshi?
Shahidi: hapana
JAJI: wakili naomba tu' break ni takribani masaa mawili sasa, na tutaendelea saa 7 kamili mchana.. natoa Break ya nusu saa kisha tutarejea kuendelea... Jaji ananyanyuka anatoka Tunasimama.
- Jaji ameingia..
- Kesi inatajwa..
- Mafaili yanapelekwa kwa jaji
Jaji: Wakili wa Serikali kuna mabadiliko yoyote?
Wakili wa Serikali: Hapana
Jaji: Kuna mabadiliko yoyote upande wa utetezi?
Kibatala: Hapana Mheshimiwa
Jaji: Nakuita sasa shahidi navnina kukumbusha upo chini ya kiapo
Kibatala: kwa Kumbukumbu zako kuna shahidi yoyote aliwahi kuwasilisha hapa mahakamani kwamba bastola imeingia kama sehemu ya ushahidi?
Shahidi: Hapana sijaona.
Kibatala: umesikia mashahidi wa serikali wamesema walipokuchukua Moshi kwamba waliwachukua kwenda kumtafuta Moses Lijenje kwa sababu ya upelelezi?
Shahidi: Hapana sijaona
Kibatala: kuna nyaraka yoyote imetolewa ushahidi wa upande wa mashitaka kwamba kuna nyaraka inaonyesha gari iliharibika na kutengenezwa
Shahidi: Hapana Kibatala: ushawahi kuona shahidi kutoka Moshi Central Polisi Station Moshi kuwa uliingia na kutoka mara kadhaa ukiwa kituoni
Kibatala: Ulimsikia Jumanne ndiyo alikupekua Moshi, uliwahi kumuona Jumanne mahakamani kama shahidi muhimu?
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulimsikia shahidi kutoka central Police Station DSM kuwa alikabidhiwa watuhumiwa ikiwemo wewe kutoka kwa Jumanne, je Jumanne umemuona Mahakamani
Shahidi: Hapana sijamuona
Kibatala: Umemuona Shahidi ambaye ni dereva ambaye gari lake liliharibika Himo na ndiye aliyewaendesha kutoka sehemu mbalimbali
Shahidi: Hapana
Kibatala: Umemuona RPC ambaye baada ya gari kuharibika ndiye alitoa gari yake kuwaleta DSM kuthibitisha hilo
Shahidi: hapana sijamuona
Kibatala: Ushawahi kumuona mahakamani dereva wa RPC ambaye aliwachukua na gari yake kutoka Himo — Dar.?
Shahidi: Sijamuona
Kibatala: hapa Mahakamani ulishawahi kuona kithibitisho chochote kinacho onyesha gari ya RPC imeruhusiwa kutoka Moshi - DSM?
Shahidi: Hapana sijaona
Kibatala: kwanza kwa uelewa wako wewe ulitekwa au ulikamatwa?
Shahidi: nilitekwa
Kibatala: Je Ulishawahi kusikia hapa Mahakamani Kingai au wenzie wanazungumzia kuhusu pesa zako?
Shahidi: Hapana
Kibatala: umesikia Mashahidi wa serikali wanasema waliwakamata mkiwa mnakula?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Utakubaliana na mimi kama mlienda kula bila shaka ulikuwa na pesa, Je umesikia hapa mahakamani wamezungumzia kuhusu Pesa ulizokuwa unataka kununulia chakula?
Shahidi: Hapana
Jaji: Kama nilivyosema wiki iliyopita, Jambo hili linahusu ushahidi gani upokelewe au ushahidi gani usipokelewe, kwa hiyo najipa tena dakika chache kabla sijaamua.. kwa hiyo nita' break na kuamua.. Jaji ananyanyuka anatoka mahakamani.
Shahidi: Hapana
Kibatala: wakati unatoka RAU Madukani kwenda Central Police station Moshi ulifungwa kitambaa usoni?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwa hiyo ulifungwa kitambaa machoni wakati wa kutoka Moshi kwenda Dar es salaam na wakati kutoka TAZARA kwenda Mbweni?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulisema ulipokuwa kituoni TAZARA ulipafahamu kwa kusikia honi ya treni?
Shahidi: Ndiyo Kibatala: nini kingine kilikufanya utambue kuwa upo TAZARA
Shahidi: kwa sababu niliuliza MAHABAUSU wenzangu
Kibatala: unawakumbuka hao Mahabusu?
Shahidi: ndiyo nakumbuka mmoja alikuwa anavaa kanzu mrefu kama msomali, na mwingine alikuwa mwanajeshi kutoka kambi ya TWALIPO na wote walikuwa na MASHTAKA ya UGAIDI pia
Kibatala: Je kwa kesi hii hii.+?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Umesikia shahidi wa serikali amesema rumande aliwaletea uji ilikuwa shimoni, Je rumande ya TAZARA ipo shimoni
Shahidi: Hapana haipo Shimoni
Kibatala: je mlipokuwa TAZARA walikuja maafisa wawili wa JWTZ je unawafahamu
Shahidi: Siwafahamu kwa majina ila nawakumbuka kwa sura kwa sababu nilifanya nao kazi kikosi cha 92KJ
Kibatala: je unafahamu walikuwa wanahusika na nini pamoja na kina Kingai
Shahidi: sifahamu
Kibatala: wakati unakwenda Mbweni ulijua kuwa unaenda kwenye MATESO?
Shahidi: Ndiyo ni sahihi.
Kibatala: ni kweli au si kweli kwa askari aliyekwambia hapa upo Mbweni ingawa hukutakiwa kujua upo wapi, alionyesha utu na kwamba unaonewa?
Shahidi: Ni sahihi Kabisa
Kibatala: Ni sahihi wakati unahojiwa, Afande kingai anakulazimisha usaini maelezo na kupelekea kesi ndogo katika kesi kubwa, Kule Mbweni, muelezee Mheshimiwa Jaji, Goodluck alipokuwa mlangoni alikuwa ameshika bastola?
Shahidi: Sahihi kabisa
Jaji: kufupisha muda, unaelewa nini kuhusiana na ADVERSE PARTY?
Wakili wa Serikali: OBJECTION. Sheria ya ushahidi kifungu 146(1) na (2) kwamba Cross Examination inafanywa na upande wa pili, kwa madhumuni kama haya tunakubaliana, ila madhumuni yake ni kwamba anayefanya mahojiano (Cross examination) awe kwa ushahidi ambao umesemwa,
Wakili wa Serikali: najua mahakama ndiyo ina haki ya ku' Control m Cross examination ila tuliruhusu hili sisi tutakosa nafasi ya Kuhoji, Tulitegemea wenzetu wangeuliza kwa kielelezo ambacho wamekigusa wao
Jaji: Kuna kingine?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni kweli Cross examination haina mipaka, Lakini sheria imeaininisha masuala yapi yataulizwa kwenye Cross examination.. Sheria ya ushahidi kifungu namba 151 (6) a,b,c
Jaji: kwa tafsiri yako je?
Wakili wa Serikali: Maana yake ni kwamba anaweza shahidi akaulizwa maswali, lakini maswali hayo lazima yajikite katika mambo yafuatayo kutikisa ushahidi yaelekezwe katika kuvumbua ni nani na nafasi yake katika maisha ni Ipi, yaende katika kutikisa uadilifu wake na uadilifu wake
Jaji: umesoma 155 na ngapi?
Wakili wa Serikali: 155 yenyewe tu ila ina a,b na c
Wakili wa Serikali: kabla, hujaamua tunaomba turejee kifungu cha sheria ya Ushahidi 146 mahakama inayoamua kipi kiiingie katika Ushahidi, anachokiuliza Kibatala hakitakiwi kuingia kwenye ushahidi
Wakili wa Serikali: Swali alililouliza Kibatala "upo Mbweni lakini hutakiwi kujua kama hapa upo wapi" na kauliza swali linalofuata kuwa "Je alikuonea huruma" Je swala hilo linaweza kuthibitishwa? Kifungu kidogo cha( 3) Mahakama ndipo ushahidi huo unaweza kupokelewa Jaji: NDIYO
Wakili wa Serikali: inaenda kwa maswali aliyokuwa anam' lead shahidi kuwa Je ushahidi uliletwa au haukuletwa,Je ukiwa haukuletwa wataweza kuleta?
Jaji: Kibatala, unaweza kujibu?
Kibatala: Wenzangu Wamechanganya Dhumuni la Ushahidi. wamechanganya Kujua nafasi yao katika kesi hii
Kibatala: Wamechanganya kujua mimi na Mallya ni akina nani.. Sisi sote ni adverse Party tupo upande mmoja na ndiyo maana tulitengana.. Kwa hiyo sisi interest zetu ni adverse party Niende kwa Kifungu cha 155 Shahidi anapohojiwa maswali ya dodoso anaweza, ukiongezea maswali yoyote
Kibatala: Kifungu 152 maswali ya kumuongoza shahidi yanaruhusiwa wakati wa kufanya Dodoso, hakuna mipaka. kwa sababu wa leading huenda kuna mitego, unapouliza maswali yao dodoso unaruhusiwa kuuliza maswali yanayomtega, kwa hiyo kifungu 155 wenzetu wamekisoma visivyo
Kibatala: Hapana tuna discuss mchakato wa kielelezo siyo bielelezo, shahidi yupo Free na hawa siyo Mawakili wa mshtakiwa kwamba mshtakiwa amelalamika nimemtesa na maswali, na mwisho Mallya mwenyewe mteja wake hajalalamila kuwa namtesa shahidi wake..
Kibatala: halafu kuhusu Goodluck aliongea Mallya wakati wa kuhoji ushahidi wake hawakuhoji, sasa ikipita imeshapita.. Kuhusu Relevance nimemuuliza kitu kilichoingia kwenye ushahidi wa kwanza Kuhusu kumuita huyo Goodluck mimi naweza kumuita kwa kupitia mshtakiwa wa nne
Kibatala: walitakiwa kumzuia Mallya kuhusu kumuongelea Goodluck, ilishapita imepita. Ujumla Mh Jaji yalipo ni maoni binafsi ya mawakili wenzetu siyo maoni ya sheria, Hatuwezi kufunika haki kwa sababu upande fulani unakereketwa, katazo au ruhusa lazima lipimwe katika vigezo hivyo
- Mawakili wa upande wa utetezi wanaingia..
- Mawakili wa Serikali pia wamerejea na kuketi swadakta..
- Washtakiwa wao mara hii hawakutolewa kwenda mahabusu..
- Walibakizwa..
- Jaji amerejea
- Kesi inatajwa tena
- Mafaili yanapelekwa mezani kwa Jaji Jaji anatania anasema askari wake wasikate pumzi ya kelele za 'kooooooooortiii' kabla yeye ajakaa, ili aongeze mazoezi..
Jaji: nimechukua muda mrefu kutafakari hoja zilizoibuliwa na mawakili wasomi Mawazo yangu kifungu cha 252, 165 na kifungu 161 cha sheria ya ushahidi kinatoa nafasi ya shahidi kuulizwa maswali yoyote isipokuwa yale yanayoteza utu wa mtu
Jaji: yapo maamuzi ya mashauri mbalimbali na mengi ya hayo mashauri yanayosema Contradict, Ku shake au kupunguza thamani ya ushahidi uliokwisha kutolewa. Kwa maoni yangu mtu anapokuwa ana contradict au kupunguza thamani ya ushahidi wake, si vyema maneno hayo yaanze na neno KWELI
Jaji: kwa sababu Ukiuliza KWELI au SI KWELI unamnyima Shahidi nafasi yaa kuuliza.. Unaweza kuondoa neno si kweli hivi na hivi, lakini sizuii kuuliza swali lolote...
Jaji: Wakili kibatala unaweza kuendelea..
Kibatala: naomba Shahidi arudi kizimbani
Kibatala: Nakuuliza kuhusu Afisa wa polisi Goodluck alikuwa ameshika nini mkononi akiwa mlangoni?
Shahidi: alikuwa na Pistol mkononi
Kibatala: Pistol umeijuaje?
Shahidi: ninaifahamu kwa sababu nimeisoma sana
Kibatala: kwani Goodluck kwa kusimama na bastola mlangoni kulikuwa na shida gani?
Shahidi: Sikuona shida yoyote lakini walisha ni Alert kabla kuwa wakiona siwapi ushirikiano basi hali ya amani itakuwa imekaribia
Kibatala: ACP kingai anasema alikufuata Central Police Station akakupandisha floor ya kwanza na kwenda kukuchukua maelezo
Shahidi: Siyo kweli Kibatala: kama ungepewa nafasi wakati wa kutoa Maelezo ungemuita au usingemuita Mwajiri wako Freeman Mbowe?
Shahidi: Ningemuita..
Kibatala: kwani Goodluck kwa kusimama na bastola mlangoni kulikuwa na shida gani?
Shahidi: Sikuona shida yoyote lakini walisha ni Alert kabla kuwa wakiona siwapi ushirikiano basi hali ya amani itakuwa imekaribia
Kibatala: kama Freeman Mbowe asingekuwa na nafasi, mwingine wa kumuita kukusaidia kwenye matatizo?
Shahidi: ningemuita mke wangu
Kibatala: Mke wako yupo wapi?
Shahidi: Chalinze
Kibatala: nakurudisha Moshi, Mahabusu ilimwagiwa maji, tatizo lako lipo wapi, Je kama wanasafisha?
shahidi: nilijua mateso yanaendelea kwa sababu sikuweza kulala tena
Kibatala: ukawa unafanyeje?
Shahidi: nilikuwa nimekaa usiku kucha
Kibatala: Ulipewa chakula lini na wapi?
Shahidi: TAZARA
Kibatala: Moshi hukupewa chakula?
Shahidi: Sikupewa chakula Moshi..
Kibatala: Ulipewa chakula TAZARA muda gani?
Shahidi: Chakula cha mchana cha mahabusu wote, ugali na mboga za majani
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama wakati wote ulipokuwa Moshi ulipewa chakula
Shahidi: Hapana sikupewa chakula
Kibatala: Wanasema mlipokuwa Himo, gari baada ya kuharibika mkala chakula na kuja Dar es salaam, je kwa kumbukumbu zako, uliwahi kula chakula HIMO?
Shahidi: Hapana Kibatala: Je, unakumbuka kama uliibadilisha na kupanda gari nyingine?
Shahidi: Sikumbuki, nakumbuka baada ya kutoka Moshi nilikuja kushuka baada ya kufika DSM
Kibatala: Unasema Moshi ulipigwa na kuteswa kama mishikaki au popo kwenye chuma, ulipigwa kipigo gani?
Shahidi: Nilikuwa napigwa kwenye unyayo, magotoni, nikiwa miguu juu kichwa chini.
Kibatala: Zoezi lilichukua muda gani?
Shahidi: lilichukua dakika 45
Kibatala: husianisha kati ya kipigo chako na kwenye nyayo na hilo chuma na kushindwa kutembea mpaka kurudishwa mahabusu, ikabidi wakuburuze.
Shahidi: Kuna uhusiano nilipopigwa miguu ilivimba nikawa nashindwa kukanyaga chini, nikikanyaga chini miguu inakuwa inauma kama nimepigwa shoti
Kibatala: Kupigwa kuna uhusiano gani na kupoteza fahamu kwenda kwenye ubongo?
Shahidi: Kupigwa kwenye unyayo ni TORTURE unayasikia maumivu kutoka kwenye miguu mpaka kichwani
Kibatala: Hapa kuna maelezo, kielelezo nataka kujua kweli ulisaini maelezo yako?
Shahidi: nilishasema mwanzo kuwa nilitaarifiwa tangu mwanzo, ndapo nitaenda kinyume, nitakuwa nayatafuta mengine, kwa kuwa nilishakuwa nimeteswa sana ikabidi kukubaliana nao.
Kibatala: unasema suruali uliyovaa leo ndiyo suruali uliyovaa 05 August ambayo haina (Ruksi) Je, dhumuni lako lilikuwa kuja kuonyesha makusudi mahakama?
Shahidi: Hapana kwa sababu leo sikuwa nimejiandaa kuja kutoa ushahidi, wala sikutegemea kuwa leo nitatoa ushahidi.
Kibatala: kwani kwa unavyojua upande wa mashtaka watakuwa na mashahidi wangapi?
Shahidi: Mashahidi 7 Kibatala: leo ulitegemea nini?
Shahidi: waendelee kutoa ushahidi..
Kibatala: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu..
Jaji: Upande wa Mashtaka W.S: Unaitwa Adam Hassan Kasekwa?
Shahidi: Naitwa Adam Hassan Kasekwa na Pia kama nilivyomwambia Jaji
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya kazi gani
Shahidi: ni MWANAJESHI, KOMANDOO
Wakili wa Serikali: Wewe ni KOMANDOO mahiri sana?
Shahidi: KOMANDOO.. Mahiri gani?
Wakili wa Serikali: Umahiri wa ujuzi?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: umesema ulikuwa VIP PROTECTION?
Shahidi: ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unaajiriwa kwenda vitani?
Shahidi: Hapana Niliajiriwa kwenda kumlinda MBOWE
Wakili Mallya: OBJECTION Mheshimiwa naomba distance kati ya wakili na mteja wangu, kwa sababu za ki Afya akae mbali kidogo, wakili amevua barakoa makusudi
Jaji: Sababu za Ki Afya KAA MBALI KIDOGO
Wakili wa Serikali: Kwakuwa wewe ni Komandoo uliyefuzu na miongoni mwa mafunzo uliyofuzu ni kuvumilia hali ya mateso?
Shahidi: NDIYO, NA NDIYO MAANA UNANIONA HAPA
Wakili wa Serikali: Makomandoo ni watu siyo legelege ni watu wenye kuhimili shida mazingira watakayo kumbana nayo?
Shahidi: NDIYO
Wakili wa Serikali: Kwa kuwa +Makomandoo ni watu wanaohimili shida ni nadra kumkuta Komandoo analalamika
Shahidi: Si Kweli
Jaji: wakili,Hebu rudia swali unaposema hali ngumu, hali ngumu, ni hali ngumu ya Maisha, Fedha au Mateso?
Wakili wa Serikali: Kwa kuwa maomandoo ni watu wanaohimili Shida ni nadra kumkuta Komandoo analalamika
Shahidi: nimekwambia NDIYO, kwa Sababu MAKOMANDOO na wao wanadamu..
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Unataka kuiambia mahakama kwamba makomandoo si wastahimilivu
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Katika mafunzo ya ukomandoo ulifuzu kukaa na njaa kwa muda mrefu?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Hatutegemei kusikia unalalamika kukaa njaa kwa muda wa siku 2
Shahidi: Si Kweli
Wakili wa Serikali: Ni kweli Kwambaaaaaaa
Mallya: Objection kama nimekuelewa Rulling yako ya maswali kuanza, ni kweli ilikuwa inatuhusu wote
Wakili wa Serikali: Unakumbukumbu nzuri sana
Shahidi: Ndiyo kabisa
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unakumbuka mlolongo wa kesi vizuri sana?
Shahidi: Ndiyo sahihi kabisa
Wakili wa Serikali: Yaliyojiri kule Moshi na kule Mbweni ulimuuliza wakili wako kabla kesi haijaanza
Shahidi: Si kweli
Jaji: Subiri kidogo, Shahidi ukiona kichwa kinapata moto unaeeza kuomba maji, naona unayo uongezwe maji
Shahidi: Ndiyo niongezewe mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Kwamba mpaka kesi inaanza ulikuwa hujamwambia wakili wako kuhusu yaliyotokea Moshi mpaka tarehe 09 Mbweni?
Shahidi: Sijamwambia
Wakili wa Serikali: ulimweleza wakati gani?
Shahidi: wakati kesi inatolewa Kisutu
Wakili wa Serikali: Kuanzia siku Ramadhani Kingai anatoa ushahidi mpaka Leo hii unatoa ushahidi wako wakili wako alikuwa anafahamu mambo yaliyokusibu?
Shahidi: sahihi kabisa
Wakili wa Serikali: Ulishawahi kutuhumiwa makosa ya utovu wa nidhamu ukiwa Jeshini?
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Jeshini wakati wa misheni DRC unazitambua kamati za kinidhamu zilizopo Jeshini?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Unapotuhumiwa kwa jambo lolote unatakiwa kupewa Haki ya KUSIKILIZWA?
Shahidi: ni HAKI ndiyo..
Wakili wa Serikali: kule Jeshini wakikutuhumu wakakupeleka kwenye kamati, kwanini wewe lazima uwepo?
Shahidi: Unapoitwa kwenye Jambo kama hilo, wanataka kujua kutoka upande wako
Wakili wa Serikali: Usipoitwa utakuwa umenyimwa Haki?
Shahidi: NDIYO
Wakili wa Serikali: kwa hiyo haifai Kumtuhumu Mtu wakati haupo
Shahidi: ndiyo
Wakili wa Serikali: Hata wewe huwezi kukubali tunazungumza maneno dhidi yako, Kasekwa kafanya 1,2,3,4,5 Wakati wewe haupo
Shahidi: Hilo mimi siwezi kulijibia, inategemea hao wenyewe
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Kama hali ipo hivyo kama Usilopenda kufanyiwa wewe Usimfanyie Mwenzio,Kingai wakati anatoa ushahidi wake wakati wanakukamata wewe tarehe 05, RAU Madukani, walipokukamata walikupekua na wakakuta na KETE 58 za Madawa ya kulevya na wakakukuta pistol
Shahidi: Ndiyo alivyoeleza unayarudia tu yote
Wakili wa Serikali: Usilete kujua sana
Mallya: OBJECTION maneno hayo kujua sana yana lengo yakumtoa shahidi wangu nje ya lengo
Jaji: Maneno hayo ya kujua sana nafikiri yasirudiwe tena
Wakili wa Serikali: Wakati wa ushahidi wa Kingai alieleza kuwa alikuandikisha MAELEZO na akaita mashahidi wawili wanawake wakati wa upekuzi
Shahidi: Ndiyo alieleza
Wakili wa Serikali: Kingai hakueleza suala lolote la kuhusu kukupiga?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Wakili wako hakumweleza Kingai Kuwa Wewe Kingai ulimuwekea Madawa ya kulevya na Pistol
Mallya: OBJECTION wakili anauliza mambo ambayo mimi na mteja tulikuwa tunaongea
Jaji: Upande wa mashtaka jibu
Wakili wa Serikali: Nilichomuuliza kuhusu kutoka moshi Mpaka hapa siyo jambo la siri
Wakili wa Serikali: nimeuliza kwamba Kingai hakuhojiwa unayoyaleta leo..
Jaji: Sijaona tatizo katika namna ambayo wakili wa serikali amemuuliza shahidi
Wakili wa Serikali: Shahidi narejea tena maneno yangu Adhana inapigwa, Jaji anaomba tusubiri Kidogo Jaji tunaweza KUENDELEA.....
Wakili wa Serikali: Kingai wakati anatoa ushahidi wake hakuulizwa suala lolote kuhusiana kukutilia wewe madawa ya kulevya na kukuwekea wewe Pistol na siku ile walikupiga eneo lile la RAU Madukani
Shahidi: SIVYO
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo hali ilikuwaje?
Shahidi: aliulizwa na wakili Kibatala
Wakili wa Serikali: Kingai anasema wakati wana kukamata uliwapa ushirikiano, wakafanya walichofanya, si ndivyo walivyosema?
Shahidi: Sijaelewa
Mallya: Maneno ya KWELI au SI KWELI ulishayatolea muongozo
Shahidi: Si kweli nilisikia hapa ingawa mimi siyo Mwanasheria yaliulizwa
Wakili wa Serikali: Maneno haya ni sawa na kusema kukamatwa na kupigwa ni Kinyume na sheria na vile vile na kupigwa ni kinyume cha sheria
Shahidi: Sijakuelewa
Jaji Hebu subiri Kidogo, Adamoo upo sawa?
Shahidi: nipo timamu Mheshimiwa Jaji
Jaji: Mallya
Mallya: Shahidi yupo sawa sawa
JAJI: nadhani nimeweka bayana yasitumike Mwanzoni inakuwa kama mangigizo ila mwishoni yanaweza kutumika.
Wakili wa Serikali: Leo hii ndiyo mara ya kwanza Mahakama inaelezwa wakati unakamatwa palikuwa na hali ya vurumai, Madawa yakawekwa kiunoni kwako, Pistol Ikawekwa kiunoni kwako pia ulipigwa
Wakili wa Serikali: Namwambia mtu kitendo cha kukamata na kumpiga mtu ni kinyume na sheria, na huyo Bwana akasema ni kweli sheria haziruhusu kumpiga mtu wakati unamkamata, Swali linakuja kitendo cha kumwambia kukamatwa na kupigwa ni kinyume na sheria ni vitendo tofauti?
Shahidi: vinaoana
Jaji: Wakili usiweke story ndefu sana, Uliza maswali Direct, Usizunguke sana mtaulizana maswali mpaka asubuhi na bado sitoelewa, Go straight...
Wakili wa Serikali: Kitendo cha kukiuka utaratibu na kusema ni Kitendo..
Shahidi: Hakuna Tofauti
Wakili wa Serikali: Kingai kasema mlipofika kituoni mkawashusha wakina mama mkarudi mitaani kumtafuta Moses Lijenje
Shahidi: Ndivyo alivyoeleza
Wakili wa Serikali: Kingai akasema kuwa baadae wakawarudisha kituoni baada ya kumkosa Moses Lijenje
Shahidi: Ndivyo alivyoeleza
Wakili wa Serikali: Ni kweli kuwa Kingai hakuhojiwa kuwa alikuwa anadanganya, isipokuwa mlipofika kituoni mkaenda kuteswa, hili suala hakuhojiwa wala hukuhojiwa
Shahidi: Sijakuelewa, kuhojiwa na nani
Wakili wa Serikali: Wakati mnamuuliza Kingai maswali kama haya ya Dodoso
Jaji: nafikiri kuna tatizo hapa na hali haijabadilika, bado wakili unaweka explanation, ndiyo maana kila wakati anarudi kusema rudia swali sijakuelewa.
- Mahakama Kimyaaaaaa
Jaji: Mkishindwa kueleza nitasema tuje Jumatatu
Wakili wa Serikali: Kwanini maswali mengi ninayokuuliza hutaki kujibu
Shahidi: Yana, mlolongo, Mreeeeefu swali halijukikani lipo wapi
- Mahakama: Wote kichekooooo
Wakili wa Serikali: Wakati Kingai anahojiwa hakuulizwa kuhusu wewe kuteswa
Shahidi: si kweli, alihojiwa
Wakili wa Serikali: Umeleeza kuwa walikutesa wakawa wanakuchoma na bisibisi matakoni na tumboni
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo baada ya kuchomwa na bisibisi ulitokwa na damu nyingi sana!
Shahidi: Si kweli
Wakili wa Serikali: Kwa kuwa hukutokwa na damu nyingi Majeraha yalikuwa madogo sana
Shahidi: sahihi
Wakili wa Serikali: Kama majeraha haya yalikuwa Madogo, Uliweza kuyavumilia?
Shahidi: sahihi
Wakili wa Serikali: Majereha hayo Madogo ambayo uliyavumilia hayakuwa kitu kikubwa
Shahidi: Yalikuwa kitu kikubwa ndiyo maana nimeiambia mahakama
Wakili wa Serikali: Mwanzo ulisema Kitu kilichokufanya Majeraha yalikuwa madogo, sababu ya kuvumilia ilikuwa sababu hayakutoa damu au Kwa sababu ya mazingira
Mallya: OBJECTION kumuharasi Shahidi kwa Jambo ambalo Shahidi ameshajibu ni kupoteza muda wa mahakama
Wakili wa Serikali: Sawasawa Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Kwa sababu majeraha yale hayakutia Damu hayakuweka Vidonda kwenye Matako yako
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Ulichomwa sana bisibisi kwenye matako yako, Damu haikutoka na majeraha hayakutoka, Je ni kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Jaji: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kwa ruhusa yako naomba tushauriane hapa
Jaji: sawa na ukirudi tumalize juu ya bisibisi za matako
Wakili wa Serikali: Nishamliza Mheshimiwa Jaji Mahakama Kimyaaaaaa Kidogo
Wakili wa Serikali: Wale waliokuwa wamekuzingira na kukufanyia uhalifu tarehe 05 hakuna hata mmoja uliweza kumtambua?
Shahidi: Ni kweli kabla ya pale sikuwa namfahamu hata mtu mmoja
Wakili wa Serikali: hukuwahi kuwaona kabla ya hapo?
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali: Kabla ya hapo hukuwahi Kugombana, kurushiana maneno kwa namna yoyote ambayo inaweza kuleta chuki?
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Sikuwahi kuwa na kinyongo nao kabla ya wakati ule
Shahidi: Sahihi kabisa
Wakili wa Serikali: Watu hawa licha ya kuwa huna kinyongo, Walikuja kukufanyia UBAYA
Shahidi: ndiyo
Wakili wa Serikali: Hakika HALI hii ni ya kustaajabisha sana
Mallya: OBJECTION maneno hayo anayotumia wakili anajaribu kumlisha maneno kabla ya Swali
Jaji: Nafikiri SHAHIDI Mwenyewe anaweza KUJIBU
Shahidi: ni kweli
Wakili wa Serikali: Watu waliokuvamia siku ile, ukiachia Ramadhani Kingai na Mahita wengine wote huwakumbuki wala huwafahamu?
Shahidi: si kweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wote unawakumbuka na kuwafahamu
Shahidi: Siyo wote
Wakili wa Serikali: ieleze MAHAKAMA kuanzia siku ile wanakukamata RAU Madukani tarehe 05 mwezi wa 8, Mpaka tarehe 07 Mwezi 08 hukuwa unawafahamu majina yao, Ndiyo maana umekuja kuwafahamu hapa wakina Ramadhani Kingai kwa sababu hakukwambia majina yao
Shahidi: Sahihi Kabisa
- Kimya kidogo wanashauriana Upande wa Serikali
Jaji: nafikiri inatosha kwa leo Siku ya Jumatatu tunaeweza kuendelea Jaji upande wa utetezi mnasemaje?
Kibatala: Tutakuwa na nafasi
Wakili wa Serikali: Tutakuwa na nafasi Mheshimiwa
-Jaji anaandika kidogo,
- Mahakama ipo kimya
Jaji: tutakuwa na shahidi mwingine upande wa Utetezi?
Mallya: Ni Mshitakiwa
- Jaji anainama na kuendelea kuandika, Mahakama ipo kimya
Jaji: nahairisha mpaka Jumatatu, kwa sababu ya MUDA umekuwa changamoto, natarajia tutaanza SAA 3 Mpaka Jumatatu, nawashukuru Mawakili wa pande zote pamoja na kuvutana
NAWASHUKURU WOTE WANAOTUMIA MUDA WAO KUFUATILIA SHAURI HILI
- Jaji ananyanyuka anatoka..
=== Mwisho ===
Tukumbuke kwamba mashahidi wa Jamhuri zaidi ya 20 ni askari Polisi
===
Jaji ameingia..
Watu wanasimama,
Kesi inatajwa, watu wanaketi..
Jaji: Wakili wa Serikali Wakili wa Serikali anatambulisha Mawakili wa Jamhuri..
Adv. Kibatala anatambulisha Jopo la mawakili wa utetezi..
Peter Kibatala
Jonathan Mndeme
Fredrick Kihwelo
Dickson Matata
John Mallya
Sisty Aloyce
Alex Masaba
Idd Msawanga
Gaston Garubindi
Evaresta Kisanga
Hadija Aron
Faraj Mangula
Maria Mushi
George Masoud
Michael Lugina
Jaji: nimeona mawakili wa utetezi wapo upande huu, Je mpo sawa?
Wakili wa Serikali: Tupo sawa
Wakili Peter Kibatala: Tupo sawa
Jaji: Wakili Kidando wakili wa serikali: shauri limekuja kwa ajili ya kusikiliza na mpaka sasa tumeshaleta mashahidi 3 kati ya 7, na tunaomba hairisho mpaka Jumatatu.. tunaomba kupata muda wa kupitia ushahidi uliowasilishwa
Wakili wa serikali: tunaomba kuondoa mashahidi wengine waliobakia kwa dhumuni la kesi ndogo. tubakie na hao hao watatu Wakili wa Serikali anakaa chini.. Jaji: kuna lolote upande wa utetezi? Jaji anaendelea kuandika.
Kibatala: Hakuna mheshimiwa Jaji.. Jaji anaendelea kuandika..
Jaji: Shauri hili dogo kwa upande wa Jamhuri limefungwa, Nitamsikiliza wakili John Mallya...
Wakili Mallya: Mshtakiwa wa pili atajitetea mwenyewe na mashahidi wengine watatu pamoja na yeye watakuwa jumla wanne
Jaji: Kuna kingine?
Mallya: Mheshimiwa ni hayo
Jaji: Mpo tayari kuanza utetezi hata sasa? au Mngehitaji muda wa kujiandaa?
Mallya: tupo tayari Jaji anaandika. Mahakama kimya, Nje mvua inapiga kidogo
Jaji: Shahidi wa kwanza wa shauri dogo la utetezi aje kwenye kizimba.
- Shahidi anaenda kizimbani anasindikizwa na askari Magereza
Jaji: tutajie majina yako kwa ukamilifu wako unaitwa nani?
Shahidi: Adam Kasekwa
Picha: Katikati ni Adam Kasekwa(Adamoo Komando)
Jaji: Kuna Jina limekuwa likitumika la Adamoo unalitambua?
Shahidi: Nalitambua
Jaji: Dini yako Mkristo?
Shahidi: ndiyo
Jaji: Apa
Shahidi: Naapa mbele ya mahakama hii, yote nitakayosema yatakuwa kweli tupu, Eeh! Mwenyezi Mungu nisaidie.. Jaji unaweza kutoa ushahidi wako ukiwa umesimama au umekaa, Wakili John Mallya unaweza kuendelea.
Mallya: Shahidi umetoka kuapa, unaweza kututambulisha ulipokuja mahakamani umetokea wapi?
Shahidi: nimetokea gereza la Segerea.
Mallya: Siku za nyuma ulikuwa wapi?
Shahidi: Nilikuwa askari wa JWTZ kikosi namba 72 Sangasanga Morogoro
Mallya: ni Kikosi cha namna gani?
Shahidi: zamani kikosi cha Makomandoo siku hizi kinaitwa SPECIAL FORCE
Mallya: umehudumu kwa miaka gani?
Shahidi: Miaka sita kuanzia 2012 mpaka 2018
Mallya: Kipi kilikufanya uache kazi?
Shahidi: sikuacha bali niliachishwa na wakuu wangu
Jaji: sijui mnasikia maana naona kelele za mvua zinaingilia, KILA MTU ANAYO HAKI YA KUSIKILIZA HII KESI
Jaji: Jamani Mnasikia Wote: tunasikiaaaaaa
Jaji: Kama mkiona hamsikii tunaweza ku' break kidogo, Hasa mawakili na washitakiwa muwe free tafadhali.
Mallya: Mwaka 2016 mpaka 2017 nilikuwa kwenye misheni KONGO na Kurejek salama nchini kwangu na kuendelea na kazi.. wakuu wangu wakagundua kuwa nina tatizo la BATTLE CONFUSION
Mallya: Unaweza kumueleza, Jaji Battle Confusion inakuwaje?
Shahidi: siwezi kujijua sana lakini ni hali ya Askari anaposikia milio ya mizinga na risasi kwa wingi anakuwa hafanyi vile anavyotakiwa na wakubwa wake
Mallya: Kwenye Afya ana athiri mfumo gani? Shahidi: mfumo wa akili.
Mallya: sasa umeshafukuzwa kazi baada ya Battle Confusion, Je ulikuwa unafanya shughuli gani?
Shahidi: nilikuwa nafanya biashara ya kununua maharage huko Morogoro sehemu inaitwa Nongwe na kuuza soko la Lubeho, kote Morogoro
Mallya: unamfahamu mshtakiwa namba 4?
Shahidi: simfahamu sana ila nilitakiwa nikafanye kazi ya VIP PROTECTION
Mallya: kazi ya VIP PROTECTION ni kazi unayoweza kuifanya?
Shahidi: Ndiyo Wakili wa Serikali: OBJECTION
Mallya: naondoa swali Mallya ulifanya nini?
Shahidi: nilikuwa kwenye hatua ya mazungumzo ya kazi
Mallya: yalikuwa yanahusisha nini?
Shahidi: kuhusiana na majukumu ya kazi na malipo yetu
Mallya: ilikuwa lini?
Shahidi: Mwishoni wa mwezi wa 7 mwaka 2020
Mallya: Makubaliano ya kufanya kazi na mshtakiwa wa 4 mlikuwa mnafanya wapi?
Shahidi: mara ya kwanza tulifanya Moshi
Mallya: nakupeleka tarehe 05 Mwezi 08 mwaka 2020 kilitokea nini?
Shahidi: siku hiyo nikiwa na mshtakiwa mwenzangu namba 03 Mohammed Ling'wenya sehemu inaitwa maduka, tukavamiwa na watu kama watano, walinivamia mimi kwanza wakaanza kunipiga, mshtakiwa mwenzangu akaja kuniokoa.
Shahidi: alipofika akawauliza "Mbona mnapiga huyu mtu?".. wakamuuliza wewe unamfahamu huyu, akajibu ndiyo namfahamu.. wakachukua madawa na silaha, nikawasikia wakisema ana madawa.. wakati Mimi wakiendelea kunishambulia.
Shahidi: Mshitakiwa mwenzangu akawawahi akitoa vitu mfukoni, nikasikia kwa maneno akisema huyu mmeshamuwekea madawa? akiwa anamaanisha mimi... mmemuweka madawa na silaha? Mimi natoa vitu vyangu kabisa msije mkaniweka na mimi, Wakati huo mimi wakiendelea kunishambulia.
Mallya: unaweza Kuwakumbuka watu hao ukiwa hapa Mahakamani?
Shahidi: Mahakamani nimeshawaona watu 2
Jaji: Subiri kidogo, anaendelea kuandika.
Mallya: ni nani umewaona hapa mahakamani?
Shahidi: Ramadhani Kingai na Mahita ambao nimekuja kuwafahamu majina yao hapa mahakamani
Mallya: hawa watu wawili ambao umewataja walikuwa na majukumu gani?
Shahidi: nilikuwa nawatambua kwa sura na matendo yote ya kunipiga na kuniwekea Madawa na silaha.
Jaji: Ukisema kuwekewa madawa na silaha nini kilichotokea?
Shahidi: Wakati wananipiga na wamenibana, akaingiza mkono wake kwenye suruali akasema ana madawa na mwingine akaingiza kitu nyuma ya mkanda akatoa kitu akasema ana silaha
Mallya: hili eneo ambalo tukio limetokea lilikuwa ni eneo la wazi?
Shahidi: pana maduka ya kubadilisha pesa. M-pesa na tiGoPesa na Grocery pembeni
Mallya: Wewe ulikuwa sehemu gani?
Shahidi: nilikuwa katikati upande kulia maduka na upande wa kushoto Grocery..
Mallya: Ulikuwa umekwenda kufanya nini?
Shahidi: kuagiza chakula, Nilikuwa naandaliwa nyama ya kuchoma lakini hata kulipa bado
Mallya: nini kilifuata,?
Shahidi: baada ya mwenzangu kusema natoa vitu vyangu msije kuniwekea kama mlivyo muwekea huyu, wakatukamata na wakatufunga pingu na kutuingiza kwenye gari yao..
Mallya: baada ya kuingizwa kwenye gari waliwapeleka wapi?
Shahidi: Muda wote tulikuwa tunapigwa, hatukujua tunaelekea wapi, baadae wakatufikisha kituo cha polisi
Mallya: kituo gani?
Shahidi: nilikuaa sikijui, lakini baada ya kuongea mahakamani nimegundua ni Central Moshi
Mallya: Baada ya kupelekwa Central Moshi kitu gani kilifuata?
Shahidi: walinitoa pale ndani kituoni kuna chumba cha pembeni palikuwa na jopo la watu wengi wakanivua nguo zote, nikawa ninaning'inizwa kwenye kichuma fulani mithili ya MSHIKAKI au POPO
Shahidi: nikiwa siwezi kusimama wakanitoa pingu wakanivalisha suruali na shati, wakaanza kunikokota
Jaji: umezungumzia kuvaa!
Shahidi: Ndiyo walinivalisha suruali. wakawa wananikokota kunipeleka mahabusu, baada ya kufika mahabusu wakanifunga pingu za mikono wakaniacha ndani
Mallya: jambo gani lilifuata? Shahidi: ndani ya mahabusu kuna chumba kidogo cha mlango wa nondo wakawatoa watu mule wakanifungia mimi..
Mallya: ulijua hatima ya yule mtuhumiwa mwingine?
Shahidi: sikujua hatima yake Mallya: nini kilifuata?
Shahidi: niliendelea kukaa ndani
Mallya: kuna ushahidi umetolewa kuwa mlizunguka maeneo mbalimbali Moshi na Hai
Shahidi: hapana sikutolewa kwenda popote
Shahidi: Ndani ya chumba kuna Askari alikuja kumwaga maji
Mallya: nini kiliendelea
Shahidi: kesho yake nilikuja kugundua ni kesho tayari baada ya kuona Jua
Shahidi: wakanitoa wakinilazimisha nitembee lakini nikawa nikawa siwezi Simu inaita kwa VIBRATION (mithili ya Philips)
Jaji: naomba kila Mtu aweke simu yake katika mazingira ambayo hayaathiri kazi yangu au ya shahidi, Msilazimishe niongee Jambo ambalo sitaki kuongea..
Shahidi: sikujua naenda wapi, nilitambua tu nipo kwenye gari na ikaanza kutembea
Mallya: kitu gani kiliendelea?
Shahidi: nikiwa ndani ya gari kabla haijatoka kwa muda wa nusu saa, mateso yaliendelea kwa kunichoma choma na bisibisi
Shahidi: wakawa wananiambia "Leo ndiyo mwisho wa maisha yako, na kwamba hapa tulipo unamjua nani, nikajibu simjui Mtu, wakasema basi na wewe hakuna anayejua upo na nani"
Mallya: Endelea
Shahidi: nilikuwa nimelazwa kwenye floor ya gari, siyo kwenye siti..
Shahidi: baada ya safari ya muda mrefu sana, tukafika sehemu wakanishusha kwa kunikokota vievile na tulipofika kwenye kachumba wakanitoa Jacket wakaniuliza "Unajua upo wapi hapa?" nikawaambia "hapana sifahamu" wakafunga mlango nikiwa ndani nikiwa na pingu lakini Jacket wamenitoa
Mallya: unamkumbuka aliyekuwa anakuuliza hayo?
Shahidi: namkumbuka ni Goodluck
Mallya: Jambo gani lingine lilitokea kwenye kile chumba?
Shahidi: nikiwa na pingu nikajikokota kusogea mlangoni bahati nzuri nikaona watu wengine wamefungiwa kwenye chumba kingine kidogo mule
Shahidi: nilikaa pale tarehe 7, 8 na 9 na ilipofika tarehe 9 usiku wakaja kunichukua usiku.
Mallya: umesema umekamatwa Moshi tarehe 05 je kati ya tarehe 5 Mpaka tarehe 7 kuna nini kilitokea?
Shahidi: tarehe 05 - 7 nilikamatwa Moshi na kuteswa kisha nikasafirishwa kuja TAZARA
Shahidi: tarehe 09 wakanitoa usiku, siku hiyo angalau nilikuwa na uwezo wa kutembea, Lakini wakaniambia huku tunakoenda yanaenda kukuta yaleyale ya Moshi, sasa UJIANDAE Mallya: Tarehe 09 nini KILIFUATIA?
Shahidi: Wakinitoa wakanipandisha kwemye gari, safari ikaanza..
Shahidi: haikuchukua muda kama Moshi. Siku hiyo sikuwekwa chini kama walivyonisafirisha kutoka Moshi. wakaniingiza kwenye chumba wakanifungua
Jaji: Subiri kidogo..
Jaji: unasema mlipofika wakakushusha?
Shahidi: walifikisha mpaka kwenye chumba, Kilipofunguliwa wakanitoa Jacket usoni, wakaniamuru niingie ndani
Jaji: Ndiyo
Mallya: rudi nyuma kidogo shahidi baada ya kuambiwa kuwa upo TAZARA, Ulifanya jambo lolote kuthibitisha upo TAZARA?
Shahidi: ilipofika jioni nilikuwa nasikia mlio wa honi ya TRENI,nikagundua nipo MAENEO yanayofanana na TAZARA
Mallya: sasa tayari upo sehemu nyingine umefumguliwa koti machoni
Shahidi: niligundua umeshaingia usiku, kesho yake usiku tena akaja Kingai na Goodluck wakanitoa ndani
Mallya: Taratibu Shahidi Jaji aandike
Shahidi: wakanipeleka Kwenye chumba kilichokuwa kina meza, Goodluck akawa mlangoni na Kingai akakaa mbele yangu tukawa tunatazamana
Jaji: NDIYO
Mallya: Pingu unazozungumzia ni zipi
Shahidi: pingu za chuma
Mallya: kuna wakati wowote walikutoa Pingu tangu utoke Moshi?
Shahidi: akamuamuru Goodluck anifungua mkono mmoja, wakanifungua wa kulia wakaendelea kufunga wa kushoto, wa kulia ukawa upo FREE..
Shahidi: Kingai akaniambia "mateso yanapopungua ujue kuna kuna mambo mazuri yamekaribia" m tunataka uwe mstaarabu, hapa kuna nyaraka tunakuja mnazo tunataka usaini..
Mallya: Mkono wa kushoto na pingu, wa kulia na kalamu, nini kilifuata!
Shahidi: akawa ananionyesha sehemu za kuandika kama "NATHIBITISHA" au KUSAINI
Mallya: Ulipata Kujua Kimeandikwa kitu gani ktk kile kingai anachokuoatia Kuthibitisha au Kusaini
Shahidi: Hapana
Mallya: Moshi umetuambia walikupiga, wakakulaza kwenye Floor sehemu yenye Joto kwenye gari, Je unauthibisho wowote unaoweza kuonyesha mahakamani?
Shahidi: naweza Kuthibitisha kwa kuonyesha sehemu nilizoumizwa, Makovu yanayoeleka kupona na mguu nimeumia leo siwezi kutembea vizuri
Jaji: kabla hajatuonyesha atueleze yapo sehemu gani, isije ikawa sehemu ambayo yanaweza kutweza utu wake
Mallya: Shahidi tueleze maeneo ya mwili ambayo umeumia
Shahidi: Mguu wangu wa kushoto na mkono wamgu wa kushoto
Jaji: sina tatizo na maeneo hayo, Wakili unaweza kuendelea
Mallya: unaweza kusimama kuonyesha mahakama?
Jaji: unaweza kusimama na mimi nitasogea kuweza kuona..
Jaji: hiyo ni mguuni (anaonyeshwa)
Jaji: sawasawa anarudi kukaa sehemu yake
Shahidi: Anarudi sehemu yake pia Mahakama ipo kimyaaa!
Mallya: kuna wakati ulitaka kumueleza Jaji kuna vingine ulitaka kumueleza nini hivyo?
Shahidi: Takribani Mwaka 1 na mwezi sasa tangu niteswe na kuumizwa, sikuwahi kupelekwa hospitali kwa matibabu na mpaka sasa nahisi maumivu makali
Mallya: Je ulipata kutambua kuwa upo kituo gani cha polisi?
Shahidi: nilikuja kujua nipo kituo cha polisi MBWENI
Mallya: Ulijuaje kuwa upo Mbweni?
Shahidi: kuna askari polisi alikuwa zamu, alisema hamtakiwi kujua mpo wapi, lakini mpo kituo cha Polisi Mbweni
Mallya: Utofauti wa majina yako Mbweni ulijuaje?
Shahidi: siku ya kwanza nafika Mbweni nilifika pale Mlangoni nikakabidhiwa kikaratasi kuwa kuanzia siku hiyo naitwa VICENT JUMA na wakikikuuliza umekamatiwa wapi sema TABORA na useme kesi ya UNYANG'ANYI, ukiseme Majina yako tutajua
Mallya: baada ya kujua upo Mbweni nini kiliendelea?
Shahidi: niliendelea kukaa Mbweni muda wote mpaka siku nafikishwa mahakamani na muda wote sikufunguliwa pingu
Mallya: unakumbuka ilikuwa siku gani? Mahakama gani?
Shahidi: ilikuwa Tarehe 19 Mwezi 08 Mwaka 2020
Shahidi: Nilipofika mahakamani ndipo nilikutana na mshtakiwa mwenzangu ambaye tulikamatwa pamoja Moshi na mshtakiwa namba 1..
Jaji: Kama naelewa tangu mtoke Moshi hamkuwahi kuonana
Shahidi: ndiyo hatukuwahi kuonana kwa macho
Mallya: Je mliwahi kuwasiliana?
Shahidi: tukiwa TAZARA tuliwasiliana kwa sauti akitokea chumba kingine lakini hatuonani
Mallya: tarehe 05 RAU Madukani, Moshi ukisema wamekuwekea vitu, Je wewe Binafsi ulikuwa na nini mfukoni?
Shahidi: nilikuwa na pesa Laki 2 na 60 taslimu, simu ya Itel na line ya Halotel
Mallya: hivyo vitu vipo wapi?
Shahidi: tangu wavichukue sijavipata
Mallya: nani alichukua.+?
Shahidi: alichukua mfukoni Goodluck akampatia Kingai
Jaji: Shahidi bado unayo maji mkononi, Kama utahitaji break utasema maana kuulizwa maswali kunatumia sana akili na kuchosha mwili
Shahidi: Asante Mheshimiwa Jaji
Mallya: ukiondoa Kingai na Goodluck kuna mtu mwingine unamkumbuka alikuja Mbweni?
Shahidi: nilimuona Mahita
Mallya: alikuja kufanyeje?
Shahidi: nilimuona wakati wanakuja kuniona, Lakini hakuhusika kuingia katika kile chumba
Jaji: chumba kipi?
Shahidi: chumba kile ambacho kilikuwa na Meza mbili na Kingai
Jaji: nimekuelewa
Mallya: Umesikia wakitoa ushahidi hapa,kwamba walikuwa wanawapa matunzo mazuri na walikuwa wanatunza utu wenu
Shahidi: si kweli
Mallya: walisema waliharibikiwa gari Himo je unasemaje kuhusu hilo?
Shahidi: kwangu ni ngumu kuhusu kuelezea kwa sababu tulikuwa tunasimama sehemu nyingi lakini nilikuwa nimefungwa usoni nisione kitu
Mallya: je unakumbuka tangu tarehe 05 mpaka Kingai anakuletea maelezo yako usaini zilikuwa zimepita siku ngapi
Shahidi: Siku 06
Wakili Mallya: Kwa sasa sina la zaidi Mheshimiwa Jaji
Jaji: Wakili Malya unafikiri Shahidi wako anaweza Kuendelea.?
Mallya: it depends
Jaji: nimekupa wewe kuamua nilikuwa naweza kuendelea bila kukuuliza
Mallya: Anaweza kuendelea Mheshimiwa
- Anaingia wakili Nashon Nkungu
Nashoni: Je ni kweli baada ya kupata Battle Confusion hukupatiwa matibabu?
Shahidi: hapana nilipatiwa kwa maana nilipelekwa hospitali ya Lugalo
Nashoni: kwenye maelezo watu hawa walikwambia sisi hautufahamu na wewe hutufahamu ni sahihi?
Shahidi: ni sahihi.?
Nashoni: Ulipata hisia gani kuwa na watu hao?
Shahidi: wasiwasi nikaona roho yangu ipo mkononi
Wakili wa Serikali: MHESHIMIWA JAJI HISIA NI KITU GANI
Jaji: hilo linamuhusu mwenyewe, kuhusu hisia zake, haliwezi kuathiri Jambo lolote
Jaji: rudia hisia ulisikiaje hisia zako
Shahidi: niliogopa kwamba naweza kuteswa sana
Nashon: umeeleza kuwa ulikuwa unachomwa BISIBISI, Je ni maeneo gani sasa?
Shahidi: Maeneo ya MBAVU na MATAKONI
Nashoni: Ukisafirishwa kutoka ulipokamatwa Moshi kuja Dar es salaam, TAZARA..
Shahidi: baada ya siku MOJA
Nashon: Uliambiwa kuwa mnaanza safari ya kuja Dar es salaam au popote.?
Shahidi: Hapana sikuambiwa
Nashon: unaweza kujua kwanini hamkuanza safari ya kuja Dar es salaam baada tu ya kukamatwa?
Shahidi: Hapana
Nashon: Unakumbuka kuwa mlifika Arusha baada ya kukamatwa?
Shahidi: Sikumbuki na wala halikwepo jambo hilo
Nashon: unasema ulikuwa na Pesa,260,000/= unakumbuka kuandikiwa risiti ya pesa hizo?
Shahidi: Hapana
Nashon: Mheshimiwa Jaji yangu ni hayo tu
Jaji: Wakili Fred na Matata mtauliza maswali wote 2 au 1 kwa niaba ya mshtakiwa wa 3?
Wakili Fred Kihwelo: Kwa niaba ya mshtakiwa wa tatu hatutokuwa na maswali yoyote
Jaji: Kibatala kwa niaba ya mshtakiwa wa nne
Wakili Kibatala: nataka utuambie kwa vitendo Ulikabwaje pale RAU MADUKANI..
Shahidi: nilikuwa naongea na simu nikiwa nimevaa Jacket naongea na simu, akatokea mtu kwa nyuma akashika mkono wenye simu na Jacket wakati najitetea akatokea kwa mbele mwingine, Mwingine akatokea akanishika mkanda hapa kiunoni..
Kibatala: unaweza kutonyesha?
Shahidi: bahati nzuri suruali niliyovaa siku ile nakamatwa ndiyo niliyovaa leo, haina hata
RUSKI KIBATALA: naweza KUONA?
Shahidi: Ndiyo unaweza kusogea Kibatala: sawa lakini pia mahakama inataka kuona
Kibatala: Wakati wanakukamata hapo ikawaje
Shahidi: akatokea mtu mbele akanipiga ngumi
Kibatala: unamkumbuka?
Shahidi: ndiyo alikuwa dereva wa gari tuliyopanda
Kibatala: Kingai alikwepo eneo la tukio.+?
Shahidi: ndiyo
Kibatala: alikuwa anafanya nini?
Shahidi: yeye ndiyo ALICHUKUA PESA ZANGU BAADA YA kusachiwa
Kibatala: Afande anayeitwa Mahita alikwepo wakati unakamwata.l?
Shahidi: alikwepo na yeye ndiye alikuwa wa kwanza kunikaba wakati naongea na simu
Kibatala: uliwezaje kuona tukio hilo la kukabwa?
Shahidi: niliona kwa sababu ilikuwa mchana na nilikuwa na akili timamu
Kibatala: Wakati wanafika kukukamata waliijitambulisha kwa mujibu wa PGO na sheria.l?
Shahidi: Hapana hawakufanya hilo..
Kibatala: na ni kweli kwamba wakati wanakukamata hawakuwa wameshika Ki' Notebook?
Wakili wa Serikali: MHESHIMIWA OBJECTION anachokifanya Wakili Msomi siyo kinacholekezwa kwa mujibu wa TRIAL WITHIN a TRIAL pamoja kwamba haijasema UKOMO wa maswali.. Matters ambazo ni Mpya zitaipotezea Muda Mahakama
JAJI: Wakili Kibatala..
Kibatala: Kwa heshima na taadhima wakili Msomi mwenzangu HANA HOJA, Shahidi analindwa na Jaji kama ningemuuliza SWALI ambalo lingemdhalilisha ningezuiwa, sijui anamaanisha nini?
Jaji: tuendeleee Shahidi ni wa Utetezi siyo wa mashtaka ,Labda iwe kwa maswali yanayo dhalilisha
Jaji: Tuendeleeeeeeeee Kibatala: uliwahi kuona mtu ameshika NOTEBOOK wakati wa zoezi kukukaba na kukukamata linaendelea?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: wakati unakamatwa ni eneo la wazi bila shaka watu wengi walishuhudia wakati wa Kukamatwa kwako
Shahidi: ndiyo walikuwa wengi
Kibatala: je uliona wakati wowote Kingai anaita watu washuhudie kukamatwa kwako?
Shahidi: Hapana Kibatala: uliona hapa mahakamani kitabu chochote ambacho mahakamani kimeletwa kinaeleza ni aina gani ya silaha ulikamatwa nayo Moshi?
Shahidi: hapana
JAJI: wakili naomba tu' break ni takribani masaa mawili sasa, na tutaendelea saa 7 kamili mchana.. natoa Break ya nusu saa kisha tutarejea kuendelea... Jaji ananyanyuka anatoka Tunasimama.
- Jaji ameingia..
- Kesi inatajwa..
- Mafaili yanapelekwa kwa jaji
Jaji: Wakili wa Serikali kuna mabadiliko yoyote?
Wakili wa Serikali: Hapana
Jaji: Kuna mabadiliko yoyote upande wa utetezi?
Kibatala: Hapana Mheshimiwa
Jaji: Nakuita sasa shahidi navnina kukumbusha upo chini ya kiapo
Kibatala: kwa Kumbukumbu zako kuna shahidi yoyote aliwahi kuwasilisha hapa mahakamani kwamba bastola imeingia kama sehemu ya ushahidi?
Shahidi: Hapana sijaona.
Kibatala: umesikia mashahidi wa serikali wamesema walipokuchukua Moshi kwamba waliwachukua kwenda kumtafuta Moses Lijenje kwa sababu ya upelelezi?
Shahidi: Hapana sijaona
Kibatala: kuna nyaraka yoyote imetolewa ushahidi wa upande wa mashitaka kwamba kuna nyaraka inaonyesha gari iliharibika na kutengenezwa
Shahidi: Hapana Kibatala: ushawahi kuona shahidi kutoka Moshi Central Polisi Station Moshi kuwa uliingia na kutoka mara kadhaa ukiwa kituoni
Kibatala: Ulimsikia Jumanne ndiyo alikupekua Moshi, uliwahi kumuona Jumanne mahakamani kama shahidi muhimu?
Shahidi: Hapana
Kibatala: ulimsikia shahidi kutoka central Police Station DSM kuwa alikabidhiwa watuhumiwa ikiwemo wewe kutoka kwa Jumanne, je Jumanne umemuona Mahakamani
Shahidi: Hapana sijamuona
Kibatala: Umemuona Shahidi ambaye ni dereva ambaye gari lake liliharibika Himo na ndiye aliyewaendesha kutoka sehemu mbalimbali
Shahidi: Hapana
Kibatala: Umemuona RPC ambaye baada ya gari kuharibika ndiye alitoa gari yake kuwaleta DSM kuthibitisha hilo
Shahidi: hapana sijamuona
Kibatala: Ushawahi kumuona mahakamani dereva wa RPC ambaye aliwachukua na gari yake kutoka Himo — Dar.?
Shahidi: Sijamuona
Kibatala: hapa Mahakamani ulishawahi kuona kithibitisho chochote kinacho onyesha gari ya RPC imeruhusiwa kutoka Moshi - DSM?
Shahidi: Hapana sijaona
Kibatala: kwanza kwa uelewa wako wewe ulitekwa au ulikamatwa?
Shahidi: nilitekwa
Kibatala: Je Ulishawahi kusikia hapa Mahakamani Kingai au wenzie wanazungumzia kuhusu pesa zako?
Shahidi: Hapana
Kibatala: umesikia Mashahidi wa serikali wanasema waliwakamata mkiwa mnakula?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: Utakubaliana na mimi kama mlienda kula bila shaka ulikuwa na pesa, Je umesikia hapa mahakamani wamezungumzia kuhusu Pesa ulizokuwa unataka kununulia chakula?
Shahidi: Hapana
Jaji: Kama nilivyosema wiki iliyopita, Jambo hili linahusu ushahidi gani upokelewe au ushahidi gani usipokelewe, kwa hiyo najipa tena dakika chache kabla sijaamua.. kwa hiyo nita' break na kuamua.. Jaji ananyanyuka anatoka mahakamani.
Shahidi: Hapana
Kibatala: wakati unatoka RAU Madukani kwenda Central Police station Moshi ulifungwa kitambaa usoni?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Kwa hiyo ulifungwa kitambaa machoni wakati wa kutoka Moshi kwenda Dar es salaam na wakati kutoka TAZARA kwenda Mbweni?
Shahidi: Ndiyo
Kibatala: ulisema ulipokuwa kituoni TAZARA ulipafahamu kwa kusikia honi ya treni?
Shahidi: Ndiyo Kibatala: nini kingine kilikufanya utambue kuwa upo TAZARA
Shahidi: kwa sababu niliuliza MAHABAUSU wenzangu
Kibatala: unawakumbuka hao Mahabusu?
Shahidi: ndiyo nakumbuka mmoja alikuwa anavaa kanzu mrefu kama msomali, na mwingine alikuwa mwanajeshi kutoka kambi ya TWALIPO na wote walikuwa na MASHTAKA ya UGAIDI pia
Kibatala: Je kwa kesi hii hii.+?
Shahidi: Hapana
Kibatala: Umesikia shahidi wa serikali amesema rumande aliwaletea uji ilikuwa shimoni, Je rumande ya TAZARA ipo shimoni
Shahidi: Hapana haipo Shimoni
Kibatala: je mlipokuwa TAZARA walikuja maafisa wawili wa JWTZ je unawafahamu
Shahidi: Siwafahamu kwa majina ila nawakumbuka kwa sura kwa sababu nilifanya nao kazi kikosi cha 92KJ
Kibatala: je unafahamu walikuwa wanahusika na nini pamoja na kina Kingai
Shahidi: sifahamu
Kibatala: wakati unakwenda Mbweni ulijua kuwa unaenda kwenye MATESO?
Shahidi: Ndiyo ni sahihi.
Kibatala: ni kweli au si kweli kwa askari aliyekwambia hapa upo Mbweni ingawa hukutakiwa kujua upo wapi, alionyesha utu na kwamba unaonewa?
Shahidi: Ni sahihi Kabisa
Kibatala: Ni sahihi wakati unahojiwa, Afande kingai anakulazimisha usaini maelezo na kupelekea kesi ndogo katika kesi kubwa, Kule Mbweni, muelezee Mheshimiwa Jaji, Goodluck alipokuwa mlangoni alikuwa ameshika bastola?
Shahidi: Sahihi kabisa
Jaji: kufupisha muda, unaelewa nini kuhusiana na ADVERSE PARTY?
Wakili wa Serikali: OBJECTION. Sheria ya ushahidi kifungu 146(1) na (2) kwamba Cross Examination inafanywa na upande wa pili, kwa madhumuni kama haya tunakubaliana, ila madhumuni yake ni kwamba anayefanya mahojiano (Cross examination) awe kwa ushahidi ambao umesemwa,
Wakili wa Serikali: najua mahakama ndiyo ina haki ya ku' Control m Cross examination ila tuliruhusu hili sisi tutakosa nafasi ya Kuhoji, Tulitegemea wenzetu wangeuliza kwa kielelezo ambacho wamekigusa wao
Jaji: Kuna kingine?
Wakili wa Serikali: Mheshimiwa Jaji ni kweli Cross examination haina mipaka, Lakini sheria imeaininisha masuala yapi yataulizwa kwenye Cross examination.. Sheria ya ushahidi kifungu namba 151 (6) a,b,c
Jaji: kwa tafsiri yako je?
Wakili wa Serikali: Maana yake ni kwamba anaweza shahidi akaulizwa maswali, lakini maswali hayo lazima yajikite katika mambo yafuatayo kutikisa ushahidi yaelekezwe katika kuvumbua ni nani na nafasi yake katika maisha ni Ipi, yaende katika kutikisa uadilifu wake na uadilifu wake
Jaji: umesoma 155 na ngapi?
Wakili wa Serikali: 155 yenyewe tu ila ina a,b na c
Wakili wa Serikali: kabla, hujaamua tunaomba turejee kifungu cha sheria ya Ushahidi 146 mahakama inayoamua kipi kiiingie katika Ushahidi, anachokiuliza Kibatala hakitakiwi kuingia kwenye ushahidi
Wakili wa Serikali: Swali alililouliza Kibatala "upo Mbweni lakini hutakiwi kujua kama hapa upo wapi" na kauliza swali linalofuata kuwa "Je alikuonea huruma" Je swala hilo linaweza kuthibitishwa? Kifungu kidogo cha( 3) Mahakama ndipo ushahidi huo unaweza kupokelewa Jaji: NDIYO
Wakili wa Serikali: inaenda kwa maswali aliyokuwa anam' lead shahidi kuwa Je ushahidi uliletwa au haukuletwa,Je ukiwa haukuletwa wataweza kuleta?
Jaji: Kibatala, unaweza kujibu?
Kibatala: Wenzangu Wamechanganya Dhumuni la Ushahidi. wamechanganya Kujua nafasi yao katika kesi hii
Kibatala: Wamechanganya kujua mimi na Mallya ni akina nani.. Sisi sote ni adverse Party tupo upande mmoja na ndiyo maana tulitengana.. Kwa hiyo sisi interest zetu ni adverse party Niende kwa Kifungu cha 155 Shahidi anapohojiwa maswali ya dodoso anaweza, ukiongezea maswali yoyote
Kibatala: Kifungu 152 maswali ya kumuongoza shahidi yanaruhusiwa wakati wa kufanya Dodoso, hakuna mipaka. kwa sababu wa leading huenda kuna mitego, unapouliza maswali yao dodoso unaruhusiwa kuuliza maswali yanayomtega, kwa hiyo kifungu 155 wenzetu wamekisoma visivyo
Kibatala: Hapana tuna discuss mchakato wa kielelezo siyo bielelezo, shahidi yupo Free na hawa siyo Mawakili wa mshtakiwa kwamba mshtakiwa amelalamika nimemtesa na maswali, na mwisho Mallya mwenyewe mteja wake hajalalamila kuwa namtesa shahidi wake..
Kibatala: halafu kuhusu Goodluck aliongea Mallya wakati wa kuhoji ushahidi wake hawakuhoji, sasa ikipita imeshapita.. Kuhusu Relevance nimemuuliza kitu kilichoingia kwenye ushahidi wa kwanza Kuhusu kumuita huyo Goodluck mimi naweza kumuita kwa kupitia mshtakiwa wa nne
Kibatala: walitakiwa kumzuia Mallya kuhusu kumuongelea Goodluck, ilishapita imepita. Ujumla Mh Jaji yalipo ni maoni binafsi ya mawakili wenzetu siyo maoni ya sheria, Hatuwezi kufunika haki kwa sababu upande fulani unakereketwa, katazo au ruhusa lazima lipimwe katika vigezo hivyo
- Mawakili wa upande wa utetezi wanaingia..
- Mawakili wa Serikali pia wamerejea na kuketi swadakta..
- Washtakiwa wao mara hii hawakutolewa kwenda mahabusu..
- Walibakizwa..
- Jaji amerejea
- Kesi inatajwa tena
- Mafaili yanapelekwa mezani kwa Jaji Jaji anatania anasema askari wake wasikate pumzi ya kelele za 'kooooooooortiii' kabla yeye ajakaa, ili aongeze mazoezi..
Jaji: nimechukua muda mrefu kutafakari hoja zilizoibuliwa na mawakili wasomi Mawazo yangu kifungu cha 252, 165 na kifungu 161 cha sheria ya ushahidi kinatoa nafasi ya shahidi kuulizwa maswali yoyote isipokuwa yale yanayoteza utu wa mtu
Jaji: yapo maamuzi ya mashauri mbalimbali na mengi ya hayo mashauri yanayosema Contradict, Ku shake au kupunguza thamani ya ushahidi uliokwisha kutolewa. Kwa maoni yangu mtu anapokuwa ana contradict au kupunguza thamani ya ushahidi wake, si vyema maneno hayo yaanze na neno KWELI
Jaji: kwa sababu Ukiuliza KWELI au SI KWELI unamnyima Shahidi nafasi yaa kuuliza.. Unaweza kuondoa neno si kweli hivi na hivi, lakini sizuii kuuliza swali lolote...
Jaji: Wakili kibatala unaweza kuendelea..
Kibatala: naomba Shahidi arudi kizimbani
Kibatala: Nakuuliza kuhusu Afisa wa polisi Goodluck alikuwa ameshika nini mkononi akiwa mlangoni?
Shahidi: alikuwa na Pistol mkononi
Kibatala: Pistol umeijuaje?
Shahidi: ninaifahamu kwa sababu nimeisoma sana
Kibatala: kwani Goodluck kwa kusimama na bastola mlangoni kulikuwa na shida gani?
Shahidi: Sikuona shida yoyote lakini walisha ni Alert kabla kuwa wakiona siwapi ushirikiano basi hali ya amani itakuwa imekaribia
Kibatala: ACP kingai anasema alikufuata Central Police Station akakupandisha floor ya kwanza na kwenda kukuchukua maelezo
Shahidi: Siyo kweli Kibatala: kama ungepewa nafasi wakati wa kutoa Maelezo ungemuita au usingemuita Mwajiri wako Freeman Mbowe?
Shahidi: Ningemuita..
Kibatala: kwani Goodluck kwa kusimama na bastola mlangoni kulikuwa na shida gani?
Shahidi: Sikuona shida yoyote lakini walisha ni Alert kabla kuwa wakiona siwapi ushirikiano basi hali ya amani itakuwa imekaribia
Kibatala: kama Freeman Mbowe asingekuwa na nafasi, mwingine wa kumuita kukusaidia kwenye matatizo?
Shahidi: ningemuita mke wangu
Kibatala: Mke wako yupo wapi?
Shahidi: Chalinze
Kibatala: nakurudisha Moshi, Mahabusu ilimwagiwa maji, tatizo lako lipo wapi, Je kama wanasafisha?
shahidi: nilijua mateso yanaendelea kwa sababu sikuweza kulala tena
Kibatala: ukawa unafanyeje?
Shahidi: nilikuwa nimekaa usiku kucha
Kibatala: Ulipewa chakula lini na wapi?
Shahidi: TAZARA
Kibatala: Moshi hukupewa chakula?
Shahidi: Sikupewa chakula Moshi..
Kibatala: Ulipewa chakula TAZARA muda gani?
Shahidi: Chakula cha mchana cha mahabusu wote, ugali na mboga za majani
Kibatala: Mwambie Mheshimiwa Jaji kama wakati wote ulipokuwa Moshi ulipewa chakula
Shahidi: Hapana sikupewa chakula
Kibatala: Wanasema mlipokuwa Himo, gari baada ya kuharibika mkala chakula na kuja Dar es salaam, je kwa kumbukumbu zako, uliwahi kula chakula HIMO?
Shahidi: Hapana Kibatala: Je, unakumbuka kama uliibadilisha na kupanda gari nyingine?
Shahidi: Sikumbuki, nakumbuka baada ya kutoka Moshi nilikuja kushuka baada ya kufika DSM
Kibatala: Unasema Moshi ulipigwa na kuteswa kama mishikaki au popo kwenye chuma, ulipigwa kipigo gani?
Shahidi: Nilikuwa napigwa kwenye unyayo, magotoni, nikiwa miguu juu kichwa chini.
Kibatala: Zoezi lilichukua muda gani?
Shahidi: lilichukua dakika 45
Kibatala: husianisha kati ya kipigo chako na kwenye nyayo na hilo chuma na kushindwa kutembea mpaka kurudishwa mahabusu, ikabidi wakuburuze.
Shahidi: Kuna uhusiano nilipopigwa miguu ilivimba nikawa nashindwa kukanyaga chini, nikikanyaga chini miguu inakuwa inauma kama nimepigwa shoti
Kibatala: Kupigwa kuna uhusiano gani na kupoteza fahamu kwenda kwenye ubongo?
Shahidi: Kupigwa kwenye unyayo ni TORTURE unayasikia maumivu kutoka kwenye miguu mpaka kichwani
Kibatala: Hapa kuna maelezo, kielelezo nataka kujua kweli ulisaini maelezo yako?
Shahidi: nilishasema mwanzo kuwa nilitaarifiwa tangu mwanzo, ndapo nitaenda kinyume, nitakuwa nayatafuta mengine, kwa kuwa nilishakuwa nimeteswa sana ikabidi kukubaliana nao.
Kibatala: unasema suruali uliyovaa leo ndiyo suruali uliyovaa 05 August ambayo haina (Ruksi) Je, dhumuni lako lilikuwa kuja kuonyesha makusudi mahakama?
Shahidi: Hapana kwa sababu leo sikuwa nimejiandaa kuja kutoa ushahidi, wala sikutegemea kuwa leo nitatoa ushahidi.
Kibatala: kwani kwa unavyojua upande wa mashtaka watakuwa na mashahidi wangapi?
Shahidi: Mashahidi 7 Kibatala: leo ulitegemea nini?
Shahidi: waendelee kutoa ushahidi..
Kibatala: Mheshimiwa Jaji ni hayo tu..
Jaji: Upande wa Mashtaka W.S: Unaitwa Adam Hassan Kasekwa?
Shahidi: Naitwa Adam Hassan Kasekwa na Pia kama nilivyomwambia Jaji
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unafanya kazi gani
Shahidi: ni MWANAJESHI, KOMANDOO
Wakili wa Serikali: Wewe ni KOMANDOO mahiri sana?
Shahidi: KOMANDOO.. Mahiri gani?
Wakili wa Serikali: Umahiri wa ujuzi?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: umesema ulikuwa VIP PROTECTION?
Shahidi: ndiyo
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unaajiriwa kwenda vitani?
Shahidi: Hapana Niliajiriwa kwenda kumlinda MBOWE
Wakili Mallya: OBJECTION Mheshimiwa naomba distance kati ya wakili na mteja wangu, kwa sababu za ki Afya akae mbali kidogo, wakili amevua barakoa makusudi
Jaji: Sababu za Ki Afya KAA MBALI KIDOGO
Wakili wa Serikali: Kwakuwa wewe ni Komandoo uliyefuzu na miongoni mwa mafunzo uliyofuzu ni kuvumilia hali ya mateso?
Shahidi: NDIYO, NA NDIYO MAANA UNANIONA HAPA
Wakili wa Serikali: Makomandoo ni watu siyo legelege ni watu wenye kuhimili shida mazingira watakayo kumbana nayo?
Shahidi: NDIYO
Wakili wa Serikali: Kwa kuwa +Makomandoo ni watu wanaohimili shida ni nadra kumkuta Komandoo analalamika
Shahidi: Si Kweli
Jaji: wakili,Hebu rudia swali unaposema hali ngumu, hali ngumu, ni hali ngumu ya Maisha, Fedha au Mateso?
Wakili wa Serikali: Kwa kuwa maomandoo ni watu wanaohimili Shida ni nadra kumkuta Komandoo analalamika
Shahidi: nimekwambia NDIYO, kwa Sababu MAKOMANDOO na wao wanadamu..
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo Unataka kuiambia mahakama kwamba makomandoo si wastahimilivu
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Katika mafunzo ya ukomandoo ulifuzu kukaa na njaa kwa muda mrefu?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Hatutegemei kusikia unalalamika kukaa njaa kwa muda wa siku 2
Shahidi: Si Kweli
Wakili wa Serikali: Ni kweli Kwambaaaaaaa
Mallya: Objection kama nimekuelewa Rulling yako ya maswali kuanza, ni kweli ilikuwa inatuhusu wote
Wakili wa Serikali: Unakumbukumbu nzuri sana
Shahidi: Ndiyo kabisa
Wakili wa Serikali: Ulikuwa unakumbuka mlolongo wa kesi vizuri sana?
Shahidi: Ndiyo sahihi kabisa
Wakili wa Serikali: Yaliyojiri kule Moshi na kule Mbweni ulimuuliza wakili wako kabla kesi haijaanza
Shahidi: Si kweli
Jaji: Subiri kidogo, Shahidi ukiona kichwa kinapata moto unaeeza kuomba maji, naona unayo uongezwe maji
Shahidi: Ndiyo niongezewe mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Kwamba mpaka kesi inaanza ulikuwa hujamwambia wakili wako kuhusu yaliyotokea Moshi mpaka tarehe 09 Mbweni?
Shahidi: Sijamwambia
Wakili wa Serikali: ulimweleza wakati gani?
Shahidi: wakati kesi inatolewa Kisutu
Wakili wa Serikali: Kuanzia siku Ramadhani Kingai anatoa ushahidi mpaka Leo hii unatoa ushahidi wako wakili wako alikuwa anafahamu mambo yaliyokusibu?
Shahidi: sahihi kabisa
Wakili wa Serikali: Ulishawahi kutuhumiwa makosa ya utovu wa nidhamu ukiwa Jeshini?
Shahidi: Hapana
Wakili wa Serikali: Ulipokuwa Jeshini wakati wa misheni DRC unazitambua kamati za kinidhamu zilizopo Jeshini?
Shahidi: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Unapotuhumiwa kwa jambo lolote unatakiwa kupewa Haki ya KUSIKILIZWA?
Shahidi: ni HAKI ndiyo..
Wakili wa Serikali: kule Jeshini wakikutuhumu wakakupeleka kwenye kamati, kwanini wewe lazima uwepo?
Shahidi: Unapoitwa kwenye Jambo kama hilo, wanataka kujua kutoka upande wako
Wakili wa Serikali: Usipoitwa utakuwa umenyimwa Haki?
Shahidi: NDIYO
Wakili wa Serikali: kwa hiyo haifai Kumtuhumu Mtu wakati haupo
Shahidi: ndiyo
Wakili wa Serikali: Hata wewe huwezi kukubali tunazungumza maneno dhidi yako, Kasekwa kafanya 1,2,3,4,5 Wakati wewe haupo
Shahidi: Hilo mimi siwezi kulijibia, inategemea hao wenyewe
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Kama hali ipo hivyo kama Usilopenda kufanyiwa wewe Usimfanyie Mwenzio,Kingai wakati anatoa ushahidi wake wakati wanakukamata wewe tarehe 05, RAU Madukani, walipokukamata walikupekua na wakakuta na KETE 58 za Madawa ya kulevya na wakakukuta pistol
Shahidi: Ndiyo alivyoeleza unayarudia tu yote
Wakili wa Serikali: Usilete kujua sana
Mallya: OBJECTION maneno hayo kujua sana yana lengo yakumtoa shahidi wangu nje ya lengo
Jaji: Maneno hayo ya kujua sana nafikiri yasirudiwe tena
Wakili wa Serikali: Wakati wa ushahidi wa Kingai alieleza kuwa alikuandikisha MAELEZO na akaita mashahidi wawili wanawake wakati wa upekuzi
Shahidi: Ndiyo alieleza
Wakili wa Serikali: Kingai hakueleza suala lolote la kuhusu kukupiga?
Shahidi: ni sahihi
Wakili wa Serikali: Wakili wako hakumweleza Kingai Kuwa Wewe Kingai ulimuwekea Madawa ya kulevya na Pistol
Mallya: OBJECTION wakili anauliza mambo ambayo mimi na mteja tulikuwa tunaongea
Jaji: Upande wa mashtaka jibu
Wakili wa Serikali: Nilichomuuliza kuhusu kutoka moshi Mpaka hapa siyo jambo la siri
Wakili wa Serikali: nimeuliza kwamba Kingai hakuhojiwa unayoyaleta leo..
Jaji: Sijaona tatizo katika namna ambayo wakili wa serikali amemuuliza shahidi
Wakili wa Serikali: Shahidi narejea tena maneno yangu Adhana inapigwa, Jaji anaomba tusubiri Kidogo Jaji tunaweza KUENDELEA.....
Wakili wa Serikali: Kingai wakati anatoa ushahidi wake hakuulizwa suala lolote kuhusiana kukutilia wewe madawa ya kulevya na kukuwekea wewe Pistol na siku ile walikupiga eneo lile la RAU Madukani
Shahidi: SIVYO
Wakili wa Serikali: Kwa hiyo hali ilikuwaje?
Shahidi: aliulizwa na wakili Kibatala
Wakili wa Serikali: Kingai anasema wakati wana kukamata uliwapa ushirikiano, wakafanya walichofanya, si ndivyo walivyosema?
Shahidi: Sijaelewa
Mallya: Maneno ya KWELI au SI KWELI ulishayatolea muongozo
Shahidi: Si kweli nilisikia hapa ingawa mimi siyo Mwanasheria yaliulizwa
Wakili wa Serikali: Maneno haya ni sawa na kusema kukamatwa na kupigwa ni Kinyume na sheria na vile vile na kupigwa ni kinyume cha sheria
Shahidi: Sijakuelewa
Jaji Hebu subiri Kidogo, Adamoo upo sawa?
Shahidi: nipo timamu Mheshimiwa Jaji
Jaji: Mallya
Mallya: Shahidi yupo sawa sawa
JAJI: nadhani nimeweka bayana yasitumike Mwanzoni inakuwa kama mangigizo ila mwishoni yanaweza kutumika.
Wakili wa Serikali: Leo hii ndiyo mara ya kwanza Mahakama inaelezwa wakati unakamatwa palikuwa na hali ya vurumai, Madawa yakawekwa kiunoni kwako, Pistol Ikawekwa kiunoni kwako pia ulipigwa
Wakili wa Serikali: Namwambia mtu kitendo cha kukamata na kumpiga mtu ni kinyume na sheria, na huyo Bwana akasema ni kweli sheria haziruhusu kumpiga mtu wakati unamkamata, Swali linakuja kitendo cha kumwambia kukamatwa na kupigwa ni kinyume na sheria ni vitendo tofauti?
Shahidi: vinaoana
Jaji: Wakili usiweke story ndefu sana, Uliza maswali Direct, Usizunguke sana mtaulizana maswali mpaka asubuhi na bado sitoelewa, Go straight...
Wakili wa Serikali: Kitendo cha kukiuka utaratibu na kusema ni Kitendo..
Shahidi: Hakuna Tofauti
Wakili wa Serikali: Kingai kasema mlipofika kituoni mkawashusha wakina mama mkarudi mitaani kumtafuta Moses Lijenje
Shahidi: Ndivyo alivyoeleza
Wakili wa Serikali: Kingai akasema kuwa baadae wakawarudisha kituoni baada ya kumkosa Moses Lijenje
Shahidi: Ndivyo alivyoeleza
Wakili wa Serikali: Ni kweli kuwa Kingai hakuhojiwa kuwa alikuwa anadanganya, isipokuwa mlipofika kituoni mkaenda kuteswa, hili suala hakuhojiwa wala hukuhojiwa
Shahidi: Sijakuelewa, kuhojiwa na nani
Wakili wa Serikali: Wakati mnamuuliza Kingai maswali kama haya ya Dodoso
Jaji: nafikiri kuna tatizo hapa na hali haijabadilika, bado wakili unaweka explanation, ndiyo maana kila wakati anarudi kusema rudia swali sijakuelewa.
- Mahakama Kimyaaaaaa
Jaji: Mkishindwa kueleza nitasema tuje Jumatatu
Wakili wa Serikali: Kwanini maswali mengi ninayokuuliza hutaki kujibu
Shahidi: Yana, mlolongo, Mreeeeefu swali halijukikani lipo wapi
- Mahakama: Wote kichekooooo
Wakili wa Serikali: Wakati Kingai anahojiwa hakuulizwa kuhusu wewe kuteswa
Shahidi: si kweli, alihojiwa
Wakili wa Serikali: Umeleeza kuwa walikutesa wakawa wanakuchoma na bisibisi matakoni na tumboni
Shahidi: Kweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo baada ya kuchomwa na bisibisi ulitokwa na damu nyingi sana!
Shahidi: Si kweli
Wakili wa Serikali: Kwa kuwa hukutokwa na damu nyingi Majeraha yalikuwa madogo sana
Shahidi: sahihi
Wakili wa Serikali: Kama majeraha haya yalikuwa Madogo, Uliweza kuyavumilia?
Shahidi: sahihi
Wakili wa Serikali: Majereha hayo Madogo ambayo uliyavumilia hayakuwa kitu kikubwa
Shahidi: Yalikuwa kitu kikubwa ndiyo maana nimeiambia mahakama
Wakili wa Serikali: Mwanzo ulisema Kitu kilichokufanya Majeraha yalikuwa madogo, sababu ya kuvumilia ilikuwa sababu hayakutoa damu au Kwa sababu ya mazingira
Mallya: OBJECTION kumuharasi Shahidi kwa Jambo ambalo Shahidi ameshajibu ni kupoteza muda wa mahakama
Wakili wa Serikali: Sawasawa Mheshimiwa
Wakili wa Serikali: Kwa sababu majeraha yale hayakutia Damu hayakuweka Vidonda kwenye Matako yako
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Ulichomwa sana bisibisi kwenye matako yako, Damu haikutoka na majeraha hayakutoka, Je ni kweli au si Kweli
Shahidi: Kweli
Jaji: Ndiyo
Wakili wa Serikali: Kwa ruhusa yako naomba tushauriane hapa
Jaji: sawa na ukirudi tumalize juu ya bisibisi za matako
Wakili wa Serikali: Nishamliza Mheshimiwa Jaji Mahakama Kimyaaaaaa Kidogo
Wakili wa Serikali: Wale waliokuwa wamekuzingira na kukufanyia uhalifu tarehe 05 hakuna hata mmoja uliweza kumtambua?
Shahidi: Ni kweli kabla ya pale sikuwa namfahamu hata mtu mmoja
Wakili wa Serikali: hukuwahi kuwaona kabla ya hapo?
Shahidi: Ni sahihi
Wakili wa Serikali: Kabla ya hapo hukuwahi Kugombana, kurushiana maneno kwa namna yoyote ambayo inaweza kuleta chuki?
Shahidi: Sahihi
Wakili wa Serikali: Sikuwahi kuwa na kinyongo nao kabla ya wakati ule
Shahidi: Sahihi kabisa
Wakili wa Serikali: Watu hawa licha ya kuwa huna kinyongo, Walikuja kukufanyia UBAYA
Shahidi: ndiyo
Wakili wa Serikali: Hakika HALI hii ni ya kustaajabisha sana
Mallya: OBJECTION maneno hayo anayotumia wakili anajaribu kumlisha maneno kabla ya Swali
Jaji: Nafikiri SHAHIDI Mwenyewe anaweza KUJIBU
Shahidi: ni kweli
Wakili wa Serikali: Watu waliokuvamia siku ile, ukiachia Ramadhani Kingai na Mahita wengine wote huwakumbuki wala huwafahamu?
Shahidi: si kweli
Wakili wa Serikali: kwa hiyo wote unawakumbuka na kuwafahamu
Shahidi: Siyo wote
Wakili wa Serikali: ieleze MAHAKAMA kuanzia siku ile wanakukamata RAU Madukani tarehe 05 mwezi wa 8, Mpaka tarehe 07 Mwezi 08 hukuwa unawafahamu majina yao, Ndiyo maana umekuja kuwafahamu hapa wakina Ramadhani Kingai kwa sababu hakukwambia majina yao
Shahidi: Sahihi Kabisa
- Kimya kidogo wanashauriana Upande wa Serikali
Jaji: nafikiri inatosha kwa leo Siku ya Jumatatu tunaeweza kuendelea Jaji upande wa utetezi mnasemaje?
Kibatala: Tutakuwa na nafasi
Wakili wa Serikali: Tutakuwa na nafasi Mheshimiwa
-Jaji anaandika kidogo,
- Mahakama ipo kimya
Jaji: tutakuwa na shahidi mwingine upande wa Utetezi?
Mallya: Ni Mshitakiwa
- Jaji anainama na kuendelea kuandika, Mahakama ipo kimya
Jaji: nahairisha mpaka Jumatatu, kwa sababu ya MUDA umekuwa changamoto, natarajia tutaanza SAA 3 Mpaka Jumatatu, nawashukuru Mawakili wa pande zote pamoja na kuvutana
NAWASHUKURU WOTE WANAOTUMIA MUDA WAO KUFUATILIA SHAURI HILI
- Jaji ananyanyuka anatoka..
=== Mwisho ===