monde arabe
JF-Expert Member
- Oct 22, 2017
- 8,490
- 13,022
Habar za muda huu ndugu wanajukwaa
Sote tunafahamu yanayoendelea hapa nchini kwetu,ukiachana na suala la Ngorongoro Conservation suala la moto kwa Taifa hili ni kesi ya Freeman Aikaeli Mbowe
Kesi hii inamtesa kiongozi mkuu wa nchi, inawatesa viongozi wa vyama na serikali na inavitesa vyombo vya ulinzi na usalama kuliko inavyomtesa Mbowe na wenzake
Kesi hii,inawatesa wengi kwa kuwa mazingira ya kuitunga na watu walioitunga hawakutumia akili.Mkubwa wa nchi anataka kuifuta lkn,anahisi itamdhalilisha kwa kuwa alishasema "wengine walishafungwa" lkn, ukweli ni kwamba hakuna mtu ambaye alikuwa tayar ameshafungwa kutokana na kesi hii.
MATOKEO YA KESI YA MBOWE KWA SERIKALI NA MIHIMILI YAKE
Kwa upande wa serikali, kesi hii inaondoa hali ya serikali kuaminiwa na raia wake wa ndani na nje ya nchi na hata wageni (wasio raia) waliondani na nje ya nchi hawawezi kuiamini serikali tena kutokana na utungwaji wa kesi hii. Serikali imewatumia watu kutoka ndani ya idara ya usalama wa Taifa ambao ni Kidando, Jaji Tiganga na wengineo (mawakili wote wa serikali kwenye kesi hii ni watu kutoka idara ya usalama wa Taifa kutoka kwenye desk ya mahakama) kwa hiyo kwa watu wenye akili timamu hawawezi kuiamini serikali kwakuwa inatumia watu kutoka kwenye organs za serikali kutesa raia wake.
Muhimili wa mahakama umepoteza imani yake kwa wananchi kutokana na mwenendo wa kesi yenyewe lkn,muhimili huu utapoteza imani kwa wananchi zaidi endapo utamfunga Mbowe na wenzake.
HATUA INAYOFUATIA
Hatua pekee iliyobaki kwa ccm na serikali yake ni kumfunga Mbowe kwa kulazimisha na baada ya muda fulani Mkuu wa nchi atatoa msamaha ili ionekane kuwa Mbowe alikuwa na hatia ndyo maana serikali ilimfunga pia,serikali itatumia kigezo kuwa imemsamehe Mbowe kwa kuwa alipanga kufanikisha ugaidi lkn,hakuwa amefanya ugaidi pia,alipokuwa gerezani alionyesha nidhamu njema
USHAURI KWA MBOWE NA CHADEMA
Kamwe, msikubali kumuomba Lucifer (CCM na Serikali yake) msamaha kwa kuwa huo msamaha utaambana na masharti magumu (attached with difficult conditionalities) miongoni mwa masharti hayo itakuwa ni pamoja na kuandika barua ya kukiri kuwa mlishiriki kwenye njama za kupanga ugaidi na baada ya hapo Chama kinaweza kufutiwa usajili kwa kuwa kitaonekana kama ni chama cha kigaidi ndyo maana Zitto anang'ang'ania sana suala la Mbowe kuachiwa kwa njia ya msamaha maana anajua kitakachofuatia ni Chadema kufutiwa usajili kama chama cha upinzani then,chama chake ndyo kitakuwa chama kikuu cha upinzani
Mbowe akiomba msamaha ataonekana kama kweli ni gaidi so,atazuiwa kufanya siasa kwa maisha yake yote yaliyobaki chini ya jua,ataishi chini ya uangalizi maalum wa jeshi la polisi na mbaya zaidi kuna baadhi ya nchi anaweza kuzuiwa kuingia.
USHAURI KWA SERIKALI
Rais futa kesi hiyo kwa kutumia akili,muagize hata Jaji wako Tiganga aifute kwa kuwa nafasi bado inaruhusu kwa wewe kufanya hivyo
MWISHO
Kesi hii inatengeneza doa kwa serikali,inawapa wananchi hasira na hali ya kuichukia nchi yao pamoja na kutokuwa na imani na nchi yao
Kesi hii, inawafanya wawekezaji kutokuleta mitaji yao Tanzania kwa kuwa ni kesi iliyobeba sura ya nchi kwenye angle ya usalama na haki (hakuna muwekezaji makini anayeweza kupeleka mtaji wake kwenye Taifa ambalo haliwezi kutenda haki) Kesi hii, inalichafua Taifa kwenye mipaka ya kimataifa,inawachafua viongozi wa vyama na serikali
Katika ulimwengu wa kiroho, kesi hii inaliletea Taifa laana na kuondoa baraka za Mungu Muumba wa vyote kwenye uso wa ardhi. Kumbukeni kipnd Pharaoh alipowazuia wana wa Israel kwenye nchi ya ahadi Mungu alileta mapigo kwa raia wote wa Misri so yatakuja mapigo mengi kwa Taifa na watawala. Pia, Mungu hatapokea maombi yenu ninyi watawala na wala sadaka zenu kwa kuwa vitabu vinasema "kama umekosana na jirani yako urudi ukapatane nae ndipo utoe sadaka yako"
"Maombi ya mwenyedhambi ni machukizo mbele za Mungu"
Mbowe siyo gaidi, tunahitaji katiba mpya
Asanteni!
Sote tunafahamu yanayoendelea hapa nchini kwetu,ukiachana na suala la Ngorongoro Conservation suala la moto kwa Taifa hili ni kesi ya Freeman Aikaeli Mbowe
Kesi hii inamtesa kiongozi mkuu wa nchi, inawatesa viongozi wa vyama na serikali na inavitesa vyombo vya ulinzi na usalama kuliko inavyomtesa Mbowe na wenzake
Kesi hii,inawatesa wengi kwa kuwa mazingira ya kuitunga na watu walioitunga hawakutumia akili.Mkubwa wa nchi anataka kuifuta lkn,anahisi itamdhalilisha kwa kuwa alishasema "wengine walishafungwa" lkn, ukweli ni kwamba hakuna mtu ambaye alikuwa tayar ameshafungwa kutokana na kesi hii.
MATOKEO YA KESI YA MBOWE KWA SERIKALI NA MIHIMILI YAKE
Kwa upande wa serikali, kesi hii inaondoa hali ya serikali kuaminiwa na raia wake wa ndani na nje ya nchi na hata wageni (wasio raia) waliondani na nje ya nchi hawawezi kuiamini serikali tena kutokana na utungwaji wa kesi hii. Serikali imewatumia watu kutoka ndani ya idara ya usalama wa Taifa ambao ni Kidando, Jaji Tiganga na wengineo (mawakili wote wa serikali kwenye kesi hii ni watu kutoka idara ya usalama wa Taifa kutoka kwenye desk ya mahakama) kwa hiyo kwa watu wenye akili timamu hawawezi kuiamini serikali kwakuwa inatumia watu kutoka kwenye organs za serikali kutesa raia wake.
Muhimili wa mahakama umepoteza imani yake kwa wananchi kutokana na mwenendo wa kesi yenyewe lkn,muhimili huu utapoteza imani kwa wananchi zaidi endapo utamfunga Mbowe na wenzake.
HATUA INAYOFUATIA
Hatua pekee iliyobaki kwa ccm na serikali yake ni kumfunga Mbowe kwa kulazimisha na baada ya muda fulani Mkuu wa nchi atatoa msamaha ili ionekane kuwa Mbowe alikuwa na hatia ndyo maana serikali ilimfunga pia,serikali itatumia kigezo kuwa imemsamehe Mbowe kwa kuwa alipanga kufanikisha ugaidi lkn,hakuwa amefanya ugaidi pia,alipokuwa gerezani alionyesha nidhamu njema
USHAURI KWA MBOWE NA CHADEMA
Kamwe, msikubali kumuomba Lucifer (CCM na Serikali yake) msamaha kwa kuwa huo msamaha utaambana na masharti magumu (attached with difficult conditionalities) miongoni mwa masharti hayo itakuwa ni pamoja na kuandika barua ya kukiri kuwa mlishiriki kwenye njama za kupanga ugaidi na baada ya hapo Chama kinaweza kufutiwa usajili kwa kuwa kitaonekana kama ni chama cha kigaidi ndyo maana Zitto anang'ang'ania sana suala la Mbowe kuachiwa kwa njia ya msamaha maana anajua kitakachofuatia ni Chadema kufutiwa usajili kama chama cha upinzani then,chama chake ndyo kitakuwa chama kikuu cha upinzani
Mbowe akiomba msamaha ataonekana kama kweli ni gaidi so,atazuiwa kufanya siasa kwa maisha yake yote yaliyobaki chini ya jua,ataishi chini ya uangalizi maalum wa jeshi la polisi na mbaya zaidi kuna baadhi ya nchi anaweza kuzuiwa kuingia.
USHAURI KWA SERIKALI
Rais futa kesi hiyo kwa kutumia akili,muagize hata Jaji wako Tiganga aifute kwa kuwa nafasi bado inaruhusu kwa wewe kufanya hivyo
MWISHO
Kesi hii inatengeneza doa kwa serikali,inawapa wananchi hasira na hali ya kuichukia nchi yao pamoja na kutokuwa na imani na nchi yao
Kesi hii, inawafanya wawekezaji kutokuleta mitaji yao Tanzania kwa kuwa ni kesi iliyobeba sura ya nchi kwenye angle ya usalama na haki (hakuna muwekezaji makini anayeweza kupeleka mtaji wake kwenye Taifa ambalo haliwezi kutenda haki) Kesi hii, inalichafua Taifa kwenye mipaka ya kimataifa,inawachafua viongozi wa vyama na serikali
Katika ulimwengu wa kiroho, kesi hii inaliletea Taifa laana na kuondoa baraka za Mungu Muumba wa vyote kwenye uso wa ardhi. Kumbukeni kipnd Pharaoh alipowazuia wana wa Israel kwenye nchi ya ahadi Mungu alileta mapigo kwa raia wote wa Misri so yatakuja mapigo mengi kwa Taifa na watawala. Pia, Mungu hatapokea maombi yenu ninyi watawala na wala sadaka zenu kwa kuwa vitabu vinasema "kama umekosana na jirani yako urudi ukapatane nae ndipo utoe sadaka yako"
"Maombi ya mwenyedhambi ni machukizo mbele za Mungu"
Mbowe siyo gaidi, tunahitaji katiba mpya
Asanteni!