Kenyatta na ICC; Watu na Maraisi wa Africa wana uwezo mdogo wa kufikiria?

nakuhakikishia kua as long as you and i are alive hakuna rais au rais wa zamani wa marekani au uingereza atapelekwa ICC. Hilo hata wewe unalijua
inawezekana ni kweli unachosema, sina uhakika lakini habari za juu juu zinasema kuwa sheria za marekani zimetengenezwa kuwalinda watu wao na ICC, kwasababu sijazisoma izo sheria zao niiache tu hewani. however, laiti kama Bush na Ramsfed wangekuwa wamefanya makosa hayo baada ya mwaka 2002 icc statute ilipoanza kufanya kazi, international community ingewapigia kelele sana na kuna uwezekano marekeni wangeona hakuna jinsi ila kusalenda. pia ingewanyima ujasiri katika mambo mengi sana ya kidiplomasia. kitu kingine ni kwamba, wenzetu wakienda kupigana vita pamoja na kwamba wanavunja sana sheria za vita, wanapigana kisomi sana, wako radhi hata kutumia mabilioni ya dola alimradi kile wanachokifanya wajustify na sheria waonekane hawajavunja, wanaziba mianya yote ya ushahidi na wao wanajizatiti kwasababu wameforsee what might happen to them after the war, hivyo kwa viongozi wa marekani au hata uingereza kushitakiwa na mahakama hii ni vigumu kidogo. hata hivyo, sioni kama ni kitu kibaya hata kama icc ingekuwa kwa waafrika pekee alimradi inawashughulikia watu ambao kweli walifanya ukatili na mauaji kwa raia wasio na hatia. angalia Bagbo wa ivory coast, alivyo kataa kuachia madaraka baada ya uchaguzi, angalia hata kibaki alivyokataa kuachia madaraka pamoja na kwamba yeye hayuko kule, hivyo ni vitendo ambavyo utaviona africa tu, sehemu zingine za dunia huwezi kuviona, na hata kama icc ingekuwa inalalia upande mmoja wa waafrica tu, hiyo sio hasara kwetu wala si ukoloni mamboleo kwasababu inashughulikia viongozi ambao sisi waafrica wenyewe tusingeweza kuwashughulikia. HAYO NI MAWAZO YANGU TU LAKINI.
 
Nimeshangaa sana jinsi Maraisi wa Africa wamekuwa wanaalamika juu ya suala la Kenyatta wa Kenya na suala la kushitakiwa Mahakama ya Kimataifa (ICC). Wanadai yafuatayo;

"There shouldn't be a court in the north judging people from the south" - Au security commissioner Ramtane Lamamra

“What then is the problem of the ICC when the Kenyan people have spoken through their vote”. President Museveni

Hivi watu wenye akili wanaweza kuongea ujinga wa namna hii?

Hivi sisi Waafrika tuna akili nzuri kweli? Yaani ushahidi kwamba Kenyatta hakuhusika na mauaji Kenya ni kuwa alishinda uchaguzi? Katika kisa cha Yesu na mhalifu Barnabas, ina maana Barnabas alikuwa hana hatia na Yesu kuwa na hatia kwa kuwa tu watu walichagua Barnabas ili aachiwe huru na sio Yesu?

Na pia viongozi wa Afrika watalalamikaje kwamba ICC isihukumu watu wa kusini wakati viongozi wa Afrika wenyewe kwa hiari walisaini makubaliano ya ICC? Kama ICC ilikuwa sawa kwa wauaji wa Rwanda, kwa nini isiwe sawa kwa Kenyatta? Kama wanaona ICC haifai si wajitoe kwanza ndio wapinge kina Kenyatta kushitakiwa ICC?

Hivi Waafrika tuna laana ya kutoweza kufikiri na kutumia akili? Hawa viongozi wa namna hii ndio tunategemea walikomboe bara letu kutokana na umasikini na ukandamizazi demokrasia?

Jamani Afrika bara langu nakulilia! Mbona viongozi wako wanakubaka na kukunajisi sana?

wengi wa viongozi wa Afrika walishajua watapelekwa ICC baada ya kumaliza muda wa urais wao, hapa wamekubaliana kusimama na kufa pamoja, wanajua wanachofanya wala usiwashangae. huo ndio mfumo wa kuendesha hata serikali, huwezi kuipinga wakati uko madarakani vinginevyo ujiuzulu kwanza ndipo uipinge
 
Mimi Siungi mkono, mahakama ya ICC kwa inaonekana ina makando kando mengi yanayohitaji kupatiwa ufumbuzi, Lakini, kwanza nimevutiwa na taarifa iliyotolewa kwenye gazeti la daily nation la Kenya toleo la kenya ambapo mwendesha mashitaka mkuu wa ICC anaonekana kuwashangaa viongpzi wa AU

kwamba kwanini wao wanaonekana kuwatetea zaidi wanaotuhumiwa na kuwasahau waathiri wa matendo yaliyopelekea kufunguliwa kwa kesi za wahusika? kwamba kwanini hatutaki haki itendeke kwa waliouawa, kuwa walemavu au kuharibiwa mali zao wakati wa vurugu za kenya za mwaka 2007, lakini tunawatetea waliofunguliwa mashitaka kutokana kuchochea uhalifu huo?

kingine ni kuwa bara a afria ndilo lenye idadi kubwa zaidi ya wananchama wa ICC, wako 44 kati ya 122 waliosaini kuanzishwa kwa mahakama husika. iweje leo walalamike hivyo wakati walikubali kusain hatia ya kuanzihwa kwake?

kadhalika nchi nane za kiafrika zimewasilisha maombi kwa ICC ikiitaka kufanya uchunguzi na hatimaye kufungua mashitaka dhidi ya waafrika wenzao wanaotuhumiwa kwa makosa mbalimbali!

Kiroja kingine(kwangu) ni kwanini leo Au ispokuwa Botswana, inataka kesi za akina kenyatta ziondolewe kwa kisingizio cha kudhalilisha utaifa wa nchhi ya amkifrika wakati tunafahamu kuna waafrika wengine wanaotakiwa katika mahakama hiyo na hatujaona nguvu kama inayotumika sasa?. rais wa Sudan anatafutwa na mahakaa hiyo kwa zaidi ya miaka mitano sasa kwa nini nguvu hizo hazijatumika? kwanini Kenya na kenyata tena wakati huu

hii inanipelekea katikan hoja nyingine kuwa ni wakenya wenywe ambao walipewa wajibu wa kuunda mahakama maalum ya kuwashughulikia watuhumiwa wa machafuko ya 2007/8 lakini wanasiasa wao ikiwa ni pamoja na Kenyattta walishindwa kufanya hivyo na kuipelekea ICC kufungua mashitaka husika, leo kimetokea nini?
 
Jamani kama chombo kilichoundwa kuwashtaki wakiukaji wa haki za binadamu duniani kinaonyesha bias openly ya kuwa tayari kumwajibisha muAfrika na sio mzungu halafu bado miAfrika humu ndani inakishabikia mimi inanshangaza sana.
Inferiority complex yetu lazima itakua geneticaly inherited.
Sawa viongozi waAfrika wali sign hayo makubaliano wakijua hicho chombo hakitakua na upendeleo wowote na kitafanya kazi kama kilivyobainisha.
Wanashangaa kuwa kumbe ni kwa ajili ya kuwa wajibisha maskini wao na sio nchi tajiri!

ICC haifanyi kazi kishabiki kama unavyotuonyeha hapa. Kosa la Bush ni nini sasa, kwamba alivamia Iraq? Hata kama ushahidi wa kuvamia Iraq haukuwa wa kweli, suala linabaki kwamba ilikuwa ni katika vita ya kuzuia ugaidi.

Viongozi wa Afrika wanasema ICC inaonea Afrika bila kutaja nani kutoka nje ya Afrika amekiuka haki za binadamu bila kushitakiwa.
 
ICC haifanyi kazi kishabiki kama unavyotuonyeha hapa. Kosa la Bush ni nini sasa, kwamba alivamia Iraq? Hata kama ushahidi wa kuvamia Iraq haukuwa wa kweli, suala linabaki kwamba ilikuwa ni katika vita ya kuzuia ugaidi.

Viongozi wa Afrika wanasema ICC inaonea Afrika bila kutaja nani kutoka nje ya Afrika amekiuka haki za binadamu bila kushitakiwa.

Hehe sidhani kama tuko pamoja kwenye viwango vya fikra!
 
Nchi za Magharibi ziliishajiwekea utaratibu mzuri katika KATIBA zao za kuwashtaki marais pindi wakikabiliwa na tuhuma, wawe madarakani au wawe wameishatoka madarakani. Kwa hivyo, Rais wa nchi kama Marekani akituhumiwa kuvunja haki za binadamu dhidi ya raia wa nchi yake atafunguliwa mashtaka kwa utaratibu waliojiwekea. Kwa mfano, Rais Bill Clinton wakati akiwa bado madarakani alifikishwa 'mahakamani' (impeachment) yaani Senate ya Marekani inafanya kazi kama mahakama katika suala hilo kwa mujibu wa Katiba yao. Alishinda kesi na hivyo kuendelea na urais wake. Kwetu sisi Afrika na mataifa mengine ambayo bado yanajikokngoja kiutawala wa sheria hakuna utaratibu uliojengwa katika Katiba zetu (na hatuko tayari kufanya hivyo - angali Rasimu ya Warioba) za kuwashitaki marais (hata kama wametuhumiwa kushiriki katika kuvunja haki za kibinadamu dhidi ya RAIA wao!!!). ICC ilikuja kama njia ya kujaribu kuziba hilo pengo. Ndio maana practically inaonekana kana kwamba ICC imeundwa kwa ajili ya nchi za Afrika tu. Watu kama Museveni haishangazi kuipiga vita ICC maana tayari ni mmojawapo ya candidates kama haki ingekuwa inafuata mkondo wake.
 
Back
Top Bottom