Kenyatta amtumia Lowassa kuwapasha Watanzania

Kenyatta amtumia Lowassa kuwapasha Watanzania

Abelyon

Member
Joined
Aug 17, 2016
Posts
31
Reaction score
6
TUTAFAKARI

Jana kwenye mazishi ya William Ole Ntimama kiongozi wa kabila la maasai Kenya na mwanasisia wa Upinzani mkongwe ambayo pia ilihudhuriwa na Msemaji wa chama Mh.Ole Sendeka na Mh.Edward Lowassa.

Rais wa Kenya Mh.Uhuru Kenyatta alipata kunena maneno haya alipokuwa akizungumza

" Yupo pia Waziri mkuu mstaafu wa Tanzania Mh.Lowasa mapenda kumwambia ukirudi huko nyumbani waambie kiti ni cha moto lakini nimekikalia sawasawa"

Kwa sisi ambao babu zetu walifanya kazi kipindi cha kikoloni na baada ya Uhuru wazee wetu walitueleza ujumbe kama huu sio wa kupuuzia ukilinganisha na mzungumzaji na lengo la ujumbe kwa undani.

Tusisahau pia kuwa kama ilivyo ada kwa wakenya na wanasisia walitumia tukio hilo kuuza maneno yao kuelekea kinyang'anyiro cha August 2017 ambapo kutakuwa na mtifuano kati ya CORD chini ya Raila Odinga,Moses Watengula na Kalonzo Musyoka na JUBILEE PARTY chini ya Uhuru Kenyatta na Dp William Rutto


[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]sijui kenyatta alimaanisha nini?
 
Ikumbukwe kwamba Raila alimtembelea Magufuli. Sasa Lowassa kaambiwa......."ukirudi huko nyumbani waambie kiti ni cha moto lakini nimekikalia sawasawa."
My take.......nadhani Uhuru anasema......challenge ipo kubwa kutoka kwa wapinzani lakini yeye anajihami kubaki madarakani.
Hili litakuwa dongo kwa Magufuli kwa sababu inawezekana Uhuru kashasoma uhusiano wa wake (Magu) na Raila.
 
baada ya kina raila kurusha madongo ,lowasa ilipofika zamu yake alisema mr president nakuonea huruma kule kwetu hii tunaita kitimoto ndipo baadae kenyata akaongea hivyo..ila wakenya noma aisee kina raila walikuwa free tu kurush avijembe pale,kiukweli wako mbele yetu angalau kwenye ka uhuru fulani,tukoje sijui huku,duh.
 
baada ya kina raila kurusha madongo ,lowasa ilipofika zamu yake alisema mr president nakuonea huruma kule kwetu hii tunaita kitimoto ndipo baadae kenyata akaongea hivyo..ila wakenya noma aisee kina raila walikuwa free tu kurush avijembe pale,kiukweli wako mbele yetu angalau kwenye ka uhuru fulani,tukoje sijui huku,duh.
Sisi tuko mbele ya wakenya...hayo mambo ya uhuru wa kuongea tulishayaishi miaka mingi toka enzi za kina JK..sasa tuko katika zama tofauti
 
Sisi tuko mbele ya wakenya...hayo mambo ya uhuru wa kuongea tulishayaishi miaka mingi toka enzi za kina JK..sasa tuko katika zama tofauti

tuko mbele yao kwa fitna, woga na ujinga. lakini wako mbele yetu tena sana kwenye viwanda, elimu, demokrasia nk, Sisi tumebaki kukimbiza mwenge na kuwaambia wananchi tuna amani na hatuna ukabila.
 
TUTAFAKARI

Jana kwenye mazishi ya William Ole Ntimama kiongozi wa kabila la maasai Kenya na mwanasisia wa Upinzani mkongwe ambayo pia ilihudhuriwa na Msemaji wa chama Mh.Ole Sendeka na Mh.Edward Lowassa.

Rais wa Kenya Mh.Uhuru Kenyatta alipata kunena maneno haya alipokuwa akizungumza

" Yupo pia Waziri mkuu mstaafu wa Tanzania Mh.Lowasa mapenda kumwambia ukirudi huko nyumbani waambie kiti ni cha moto lakini nimekikalia sawasawa"

Kwa sisi ambao babu zetu walifanya kazi kipindi cha kikoloni na baada ya Uhuru wazee wetu walitueleza ujumbe kama huu sio wa kupuuzia ukilinganisha na mzungumzaji na lengo la ujumbe kwa undani.

Tusisahau pia kuwa kama ilivyo ada kwa wakenya na wanasisia walitumia tukio hilo kuuza maneno yao kuelekea kinyang'anyiro cha August 2017 ambapo kutakuwa na mtifuano kati ya CORD chini ya Raila Odinga,Moses Watengula na Kalonzo Musyoka na JUBILEE PARTY chini ya Uhuru Kenyatta na Dp William Rutto

[emoji1][emoji1][emoji1][emoji1]sijui kenyatta alimaanisha nini?


KENYATA NILIMUELEWA, LAKINI JAMANI LOWASSA SIJUI ALISEMA NINI, SIJUI KAMA KUNA YEYOTE ALIMUELEWA. YAANI NI KITUKO
 
tuko mbele yao kwa fitna, woga na ujinga. lakini wako mbele yetu tena sana kwenye viwanda, elimu, demokrasia nk, Sisi tumebaki kukimbiza mwenge na kuwaambia wananchi tuna amani na hatuna ukabila.

Ujumbe wako ni mzito.......
 
Uhuru tukiacha umungiki ni kiongozi msikivu Sana.
 
Hapa uchanganyaji wa karata ndiyo utawaponyesha.
 
Back
Top Bottom