Kelele za upinzani hazinisumbui-JK

machafuko hayawezi kuletwa na approach, yataletwa na wale wanaodhania kuwa nchi hii ni ya kwao peke yao na ambao kwa vile hawafurahishwi na "approach" basi wanajifanya miungu watu. "Mbona hamkupiga magoti mlipoomba".. hatapigiwa mtu magoti tena katika TAnzania, na sadaka ya sifa za uongo haitatolewa tena! CCM bora ing'amue hilo mapema.

Kile wananchi wanakitaka watakisema bila kuambiwa ni "jinsi gani waseme". CCM haiwezi na haina uwezo wa kuamulia ujumbe wa wananchi utolewe vipi! Kama ameamua kukaa kimya hilo ni uamuzi wake, lakini kwa kukaa kwake kimya haina maana ametuamulia ni jinsi gani tumfikishie ujumbe!

Tanzania haina wafalme, na hatuwezi kuruhusu viongozi watende kama wafalme! Hilo tumewakatilia na tutaendelea kuwakatalia, ndio maana nilishatoa pendekezo huko nyuma kuwa kama hawafurahishwi na ujumbe na jinsi ujumbe unatolewa, na kama wanaona wanapigiwa kelele za msingi waamue kututangazia tu kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kiimla ili na sisi tujue! Lakini kama nchi yetu ni huru na watu wake ni huru na wenye hadhi sawa, watawala wetu watambue kuwa hata ufalme wa Alexander ulivunjika na majeshi ya farao yalitumbukia bahari ya shamu! Wasijidanganya hata kidogo kuwa wataondoka madarakani on their own terms.. hapana, wataondoka kwani wananchi hawatafuata masharti ya "approach" gani itumike!!

this is what i was talking about ! CCM/WAPINZANI, CCM, CCM, CCM, CCM, CCM , CCM , CCM CCM, CCM, CCM, CCM, CCM, !! Mwanakijiji unaweza ukawa na point nzuri lakini wewe kuihusisha CCM na kila jambo baya basi huondoa maana kabisa ya ujumbe uliokuwa unataka kufikisha. Mentality yako i guess will take another 10 years to clear up, maana inaelekea una imani fulani hivi kwamba something ni wrong hata kama ni right, unaona mabaya tu na sio mazuri !

Ushauri wa bure: Utazeeka mapema, so i suggest you as your fellow mate to sometimes give up space to your mind, rather than kufikiria hivyo (mentality) which will benefit you for a short term period !
 
Ahadi kuwa ni deni, na kama Rais ameahidi kufanya jambo ni bora afuatilie na kuona linafanyika. Ndiyo sehemu mojawapo ya Urais wake, sasa kusema tumuache bila kuulizia ni kumpa kibali cha kutawala kwa amri! Kama anataka kufanya mambo kimya kimya anaweza lakini akitoa ahadi hadharani basi wananchi wanayo haki na sababu ya kuuliza ahadi hiyo imefikiwa wapi. So, Icadon endelea kuuliza!!

Heheeee, do you feel being bullied ? Are you still thinking about that person who tool your lunch money at lunch time and insulted you ? Nitakwambia kitu kimoja, process za uchunguzi huchukua muda kukamilika from what i know, otherwise kama mnataka itokee ripoti bogus inaweza ikatolewa hata kesho na rais akiwa huko aliko !

Icadon endelea kuuliza lakini jua kwamba ripoti haijakamilika ndio maana yupo kimya ! mkimuuliza sana, definitely jibu litakuwa ni kwamba hiyo ishu inashuhulikiwa. Kuna mambo mengi tu yanashuhulikiwa which costs our leaders time, money and their energies too !

Keep posted !
 
hoja hujibiwa kwa hoja! Kama CCM inachukua credit ya mambo mazuri yanayoendelea nchini... nadhani haina uchaguzi isipokuwa na kubeba lawama pia!
 
hoja hujibiwa kwa hoja! Kama CCM inachukua credit ya mambo mazuri yanayoendelea nchini... nadhani haina uchaguzi isipokuwa na kubeba lawama pia!

VIZURI SANA....Lakini ndipo hapo ninaposhangaa iweje msione yale mazuri pia yanayofanywa under ccm !na sio ccm tu bali kitu chochote kinachopata lawama kinastahili kubeba hiyo lawama, lakini hapa big ishu wanayoona ni ccm na sio lawama ! many people make CCM as a bigger issue worse than the problems themselves !
 
machafuko hayawezi kuletwa na approach, yataletwa na wale wanaodhania kuwa nchi hii ni ya kwao peke yao na ambao kwa vile hawafurahishwi na "approach" basi wanajifanya miungu watu. "Mbona hamkupiga magoti mlipoomba".. hatapigiwa mtu magoti tena katika TAnzania, na sadaka ya sifa za uongo haitatolewa tena! CCM bora ing'amue hilo mapema.

Kile wananchi wanakitaka watakisema bila kuambiwa ni "jinsi gani waseme". CCM haiwezi na haina uwezo wa kuamulia ujumbe wa wananchi utolewe vipi! Kama ameamua kukaa kimya hilo ni uamuzi wake, lakini kwa kukaa kwake kimya haina maana ametuamulia ni jinsi gani tumfikishie ujumbe!

Tanzania haina wafalme, na hatuwezi kuruhusu viongozi watende kama wafalme! Hilo tumewakatilia na tutaendelea kuwakatalia, ndio maana nilishatoa pendekezo huko nyuma kuwa kama hawafurahishwi na ujumbe na jinsi ujumbe unatolewa, na kama wanaona wanapigiwa kelele za msingi waamue kututangazia tu kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kiimla ili na sisi tujue! Lakini kama nchi yetu ni huru na watu wake ni huru na wenye hadhi sawa, watawala wetu watambue kuwa hata ufalme wa Alexander ulivunjika na majeshi ya farao yalitumbukia bahari ya shamu! Wasijidanganya hata kidogo kuwa wataondoka madarakani on their own terms.. hapana, wataondoka kwani wananchi hawatafuata masharti ya "approach" gani itumike!!

Mwanakijiji,

- Machafuko yanaweza kuletwa na "approach", sidhani kama una uelewa mdogo mpaka nielezee hili kwa undani.

- CCM sio chama cha wafalme. Wabunge wa CCM kama wabunge wa vyama vingine hugombea nafasi zao na kupigiwa kura. The same goes for the president. Labda, wapinzani wana dhana ya kwamba kama wao watashinda kwenye mashindano ya kurusha matope basi wapewe nafasi. Hata kwenye hizo enzi za ufalme, watu hawakupata utawala kwa njia hii. Hapa nimetumia neno "matope" kwa sababu ya kuchukua TUHUMA na kuzisambaza kama HUKUMU. Opposition has a long way to go in learning democracy.

- Ujumbe wa wapinzani kama ungemuudhi sana Rais kama ambavyo umeandika hapa, quote "...kama hawafurahishwi na ujumbe na jinsi ujumbe unatolewa, na kama wanaona wanapigiwa kelele za msingi waamue kututangazia tu kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kiimla ili na sisi tujue!..." NA kama angekuwa anataka nchi ya kiimla basi angetangaza kama ulivyoshauri, lakini, democracy ni ngumu na hii inakwenda hand in hand with burden of proof. Rais hawezi KUKURUPUKA kama vile upinzani unavyopressurize na aanze kufanya kweli.

Nimesema hapo awali, tuwe na subra. Binadamu asiyekuwa na subra hafai kwa Uongozi...Naamini kazi inafanyika. Hivi ile ripoti ya BoT si ni baada ya siku 60 tokea zoezi lianze...hivi zimefika...?
 
Mwanakijiji,

- Machafuko yanaweza kuletwa na "approach", sidhani kama una uelewa mdogo mpaka nielezee hili kwa undani.

- CCM sio chama cha wafalme. Wabunge wa CCM kama wabunge wa vyama vingine hugombea nafasi zao na kupigiwa kura. The same goes for the president. Labda, wapinzani wana dhana ya kwamba kama wao watashinda kwenye mashindano ya kurusha matope basi wapewe nafasi. Hata kwenye hizo enzi za ufalme, watu hawakupata utawala kwa njia hii. Hapa nimetumia neno "matope" kwa sababu ya kuchukua TUHUMA na kuzisambaza kama HUKUMU. Opposition has a long way to go in learning democracy.

- Ujumbe wa wapinzani kama ungemuudhi sana Rais kama ambavyo umeandika hapa, quote "...kama hawafurahishwi na ujumbe na jinsi ujumbe unatolewa, na kama wanaona wanapigiwa kelele za msingi waamue kututangazia tu kuwa Tanzania imekuwa nchi ya kiimla ili na sisi tujue!..." NA kama angekuwa anataka nchi ya kiimla basi angetangaza kama ulivyoshauri, lakini, democracy ni ngumu na hii inakwenda hand in hand with burden of proof. Rais hawezi KUKURUPUKA kama vile upinzani unavyopressurize na aanze kufanya kweli.

Nimesema hapo awali, tuwe na subra. Binadamu asiyekuwa na subra hafai kwa Uongozi...Naamini kazi inafanyika. Hivi ile ripoti ya BoT si ni baada ya siku 60 tokea zoezi lianze...hivi zimefika...?

what a good conclusion ! You made it clearer. Uchaguzi huwa huru, kwa watu wote, kampeni safi hufanyika, baada ya hapo wananchi huru waliopiga kura huchagua viongozi wanaowaamini, mara nyingi hutokea viongozi wa ccm videdea. sasa kosa la nani hapo wakati uchaguzi ulikuwa huru, wote wameanza kampeni wakatia mmoja n.k ? anyway tuongeleeni zaidi kuletea wananchi maendeleo.
WATU TUNATAKA CHANGES LEO, LAKINI CHANGES HAZIWEZI KUTOKEA TANZANIA IN THE NEXT 50 YEARS, IT WILL TAKE TIME AND PAIN TO DO ALL THE WORK, NDIO MAANA NILISEMA TUFANYENI KAZI KWA AJILI YA VIZAZI VIJAVYO NA SIO KWA AJILI YETU SIE, TUKISEMA HIVYO TUTAKUWA TUNAJIDANGANYA ! TANZANIA TUNAYOITAKA SISI SIDHANI KAMA TUTAIFAIDI SISI WA SASA HIVI BALI VIZAZI VYETU ! am sorry to be the bearer of this bad news lakini huo dnio ukweli ! KAMA JK,MBOWE,SLAA WANATAKA KUONEKANA KAMA MALCOM X,SIJUI NANI....THEY BETTER FORGET IT MAANA HATUTOFANIKIWA MPAKA OPPISITON LEARNS DEMOCRACY AND THAT WILL TAKE TIME ! WE HAVE TO WORK OUT ASS*ES OUT PEOPLE !
Lakini mkuu thats really a good conclusion you made !
 
1.
KadaMpinzani
JF Senior Expert Member Join Date: Wed Jan 2007
--------------------------------------------------------------------------------
atatoa ripoti tu baada ya uchunguzi kumalizika ! so tumuache kwa sasa
.



2.
Insurgent
Nimesema hapo awali, tuwe na subra.

ahsante mkuu, ni kweli tunahitaji subira!
 
what a good conclusion ! You made it clearer. Uchaguzi huwa huru, kwa watu wote, kampeni safi hufanyika, baada ya hapo wananchi huru waliopiga kura huchagua viongozi wanaowaamini, mara nyingi hutokea viongozi wa ccm videdea. sasa kosa la nani hapo wakati uchaguzi ulikuwa huru, wote wameanza kampeni wakatia mmoja n.k ? anyway tuongeleeni zaidi kuletea wananchi maendeleo.
WATU TUNATAKA CHANGES LEO, LAKINI CHANGES HAZIWEZI KUTOKEA TANZANIA IN THE NEXT 50 YEARS, IT WILL TAKE TIME AND PAIN TO DO ALL THE WORK, NDIO MAANA NILISEMA TUFANYENI KAZI KWA AJILI YA VIZAZI VIJAVYO NA SIO KWA AJILI YETU SIE, TUKISEMA HIVYO TUTAKUWA TUNAJIDANGANYA ! TANZANIA TUNAYOITAKA SISI SIDHANI KAMA TUTAIFAIDI SISI WA SASA HIVI BALI VIZAZI VYETU ! am sorry to be the bearer of this bad news lakini huo dnio ukweli ! KAMA JK,MBOWE,SLAA WANATAKA KUONEKANA KAMA MALCOM X,SIJUI NANI....THEY BETTER FORGET IT MAANA HATUTOFANIKIWA MPAKA OPPISITON LEARNS DEMOCRACY AND THAT WILL TAKE TIME ! WE HAVE TO WORK OUT ASS*ES OUT PEOPLE !
Lakini mkuu thats really a good conclusion you made !

Hatuhitaji miaka yote hiyo ni mingi sana, kama tungeweza kukomesha watu kama Karamagi na kundi lake la mafisadi haya madini pamoja na utalii unaweza kuibadili Tanzania in the next 15 to 20 years.
 
Hatuhitaji miaka yote hiyo ni mingi sana, kama tungeweza kukomesha watu kama Karamagi na kundi lake la mafisadi haya madini pamoja na utalii unaweza kuibadili Tanzania in the next 15 to 20 years.

this is what am talking about, Dua unataka kufaidi wewe ? Kwani unadhani roma ilijengwa ndani ya siku 2 ? najua ni mingi sana tena sana, lakini angalia mataifa makubwa how long did it take for them to be where they are now ! wee acha tu lakini yote historia !

After all Dua, hizo ni approximations tu ambazo i made myself, so usishangae hata ikachukua miaka 200 kuendelea !!
 
this is what am talking about, Dua unataka kufaidi wewe ? Kwani unadhani roma ilijengwa ndani ya siku 2 ? najua ni mingi sana tena sana, lakini angalia mataifa makubwa how long did it take for them to be where they are now ! wee acha tu lakini yote historia !

After all Dua, hizo ni approximations tu ambazo i made myself, so usishangae hata ikachukua miaka 200 kuendelea !!

Mimi sina haja ya kufaidi nawaonea huruma wale ambao wanadhulumiwa na hii mifisadi kama vile hakuna wenye utu. Huwa najiuliza kama hawa mafisadi wana dini. Wamezaliwa kama kuku na watakufa kama mwewe na mali zote wataziacha hapa hapa, what a shame!
 
Mimi sina haja ya kufaidi nawaonea huruma wale ambao wanadhulumiwa na hii mifisadi kama vile hakuna wenye utu. Huwa najiuliza kama hawa mafisadi wana dini. Wamezaliwa kama kuku na watakufa kama mwewe na mali zote wataziacha hapa hapa, what a shame!

ndio hapo, lakini mafisadi wako kote kote hivyo hata leo the so called mafisadi wakitoka watakuja wa aina nyingine either in another form/style or whatever lakini watakuja ! walikuja mitume/manabii tofauti ndai ya miaka tofauti kuleta maendeleo lakini hiyo haikumaanisha ulikuwa mwisho wa mafirauni !
 
Usiwajali hao mafisadi wa baadaye tunataka ku-deal na hawa kwanza maana wajukuu hawawezi kutuelewa. Unakumbuka enzi za utumwa mibaba yenye afya inabeba kazungu kamoja tena kana bunduki moja. What a shame, more or less like this one.
 
Usiwajali hao mafisadi wa baadaye tunataka ku-deal na hawa kwanza maana wajukuu hawawezi kutuelewa. Unakumbuka enzi za utumwa mibaba yenye afya inabeba kazungu kamoja tena kana bunduki moja. What a shame, more or less like this one.

sawa, but thats the truth mkuu ! niliposema vile sikuwa na maana ya kuvunja nguvu maana hata mie binafsi nataka kufaidi hayo maendeleo !
 
Slaa na wenzake, walipoitisha mkutano pale Mwembeyanga na kutoa list ya mafisadi na ndani ya list ile wakamtaja JK walitegemea nini?

Leo wanasema mbona rais amenyamaza? Walitegemea nini? Hata mimi nikiwa najijua ni msafi halafu ukaniweka kwenye list ya wachafu na kutaka nichukue hatua, siwezi.
Sababu inayomfanya awapuuzie ni kwamba anajijua yeye ni msafi, sasa anaona inawezekana hata wale waliotajwa kwenye ile list wakawa wamepakaziwa kama yeye.

Approach ya Slaa na wenzake inaweza kuleta machafuko na kuturudisha miaka kadhaa nyuma. Wanaweza kuwa na akili sana lakini hawana BUSARA. Sasa rais hajasema kitu, nini kinawazuia kwenda mahakamani? Au huko Hague?

Tatizo ni kwamba siyo tu wapinzani wanaquestion usanii wa huyu jamaa bali hata ndani ya CCM tayari kuna viongozi na wanachama wengi wanamuona ni bomu. Ni lazima abadilike ili kurudisha imani ya wananchi kwake au vinginevyo histori itamkumbuka kuwa ni kiongozi aliyeisambaratisha CCM.

Ni haki ya Slaa kuhoji dhidi ya upotevu wa $250 millioni pale BOT. Kamwe kuhoji huko hakuna nia yoyote ya kuleta machafuko. Wananchi na wapinzani kuhoji dhidi ya mikataba bomu ambayo haina maslahi kwa Watanzania kamwe hakuonyeshi nia ya kuleta machafuko au kumwaga damu.

Mtu anayetaka machafuko au kumwaga damu utamsikia anatafuta silaha za aina yoyote ile ili aingie msituni, na hili sijalisikia likitamkwa na wananchi wala wapinzani. Ndiyo tabia ya CCM hiyo badala ya kujibu tuhuma nzito dhidi ya viongozi wao, basi hutaka kupoteza lengo kwa kuanza kuleta vitisho vya machafuko na umwagaji wa damu.

Watanzania si wajinga wanaona vitendo vyake na kusikia kauli zake sidhani kuna chochote kinachowaridhisha kati ya wanayoyaona na wanayoyasikia.
 
this is what i was talking about ! CCM/WAPINZANI, CCM, CCM, CCM, CCM, CCM , CCM , CCM CCM, CCM, CCM, CCM, CCM, !! Mwanakijiji unaweza ukawa na point nzuri lakini wewe kuihusisha CCM na kila jambo baya basi huondoa maana kabisa ya ujumbe uliokuwa unataka kufikisha. Mentality yako i guess will take another 10 years to clear up, maana inaelekea una imani fulani hivi kwamba something ni wrong hata kama ni right, unaona mabaya tu na sio mazuri !

Ushauri wa bure: Utazeeka mapema, so i suggest you as your fellow mate to sometimes give up space to your mind, rather than kufikiria hivyo (mentality) which will benefit you for a short term period !


Mawazo yako Kada hayawezi,hata siku moja,tenga chungu chakula kikaiva.

SISIEMU wametawala kwa miaka zaidi ya 46 mfululizo bila chama chcochote kile kuwa mshiriki.

Kwahiyo SISIEMU inahusika kwa kila jambo baya au zuri nchini Tanzania.
Ni unafiki, ni kujikana, ni uzandiki na uzushi usio na msingi wa kujikita kukataa kwamba kila jambo Tanzania haliihusu SISIEMU.

Juu ya yote ni ukosefu wa fadhira kwa SISIEMU kuelekeza sifa za jambo lolote lilowahi kufanyika Tanzania kwa jumuia,kundi la watu au chama chochote zaidi ya SISIEMU.

Kitendo cha kukataa na kukikingia SISIEMU kifua ili isibebe sifa za mambo yote Tanzania ni sawa na juhudi za kuchanganya Maji na mafuta, wote tunajua hazitafanikiwa.

Hoja Huru kwako KadaMpinzani;

Kuzeeka ni Biological and enviromental process.
Pamoja na urithi uliopata kutoka kwa wazazi wako wa kuishi kwa muda mrefu, jinsi ujionavyo na uionavyo jamii katika kioo cha fahamu na fahisi ya maisha yako husaidia kuongeza au kuimega Lifespan yako.
Furaha na raha ya kukubali kila jambo bila kuipa akili yako fursa ya kuchambua,kutafakari na kutoa mapendekezo katika maisha yako si kigezo pekee kikuwezeshacho kuongezea umri wa kuishi.
Pia, kupinga mambo mengi yaliyokuwepo yaliyopo na yajayo kwa kuchemsha Bongo na kutoa sababu zenye afya,ushawishi na mwelekeo si sababu ya kuzeeka mapema.

Elimu ,Sayansi na Teknolojia yote hapa Dunia imeweza kufikia hapa kwa sababu ya watu waliochemsha na waendeleao kuchmsha Bongo zao na kuyaelezea mambo kutokana na matokeo ya utafiti wao kuliko kukubali na kuunga mkono mambo kiimla na kimazoea.

Si zamanai sana elimu sahihi ilikuwa;

Jua linaizunguka Dunia na Dunia ni sawa na Meza pana ambayo ukifika ukingoni unaporomoka katika maporomoko marefu kwenda kusiko julikana na pengine kwenda ahera.

Kada Unadhani hoja kwamba Dunia ni ya mviringo na kwamba yenyewe ndiyo ilizungulo jua ilikuja kwa kukubali na kuunga mkono kila jambo???
 
Subira hipo, ila ukiangalia ni kama muungwana majibu yake yanatofautiana, akiwa na nchi wahisani anatoa jibu hili akiwa na watanzania anatoa jibu lile.Alafu nadhani lingekuwa jambo la busara kama angewatangazia wananchi akiwa nyumba(Jumba jeupe la pale magogoni) kuwa uchunguzi unaendelea maana watanzania ndio waliompigia kura sio Condi na wenzake wa pale The Hill, kwa kifupi nadhani walipa kodi wa Tanzania wangetulizana kama rais wao angewathamini na kuwaambia live kwenye hotuba zake za kila mwezi. All in all I wish him all the best kwenye hili.
 
haha,Kingwendu anatia aibu kweli,kusema hakosi usingizi na kelele za wapinzani,nani kamuuliza kuwa anakosa usingizi?Ukiona mtu anaisifia mvua jua imemnyea,huu jamaa hapati usingizi hata kidogo,kabanwa kila kona,wananchi wamembana,wapinzani wamembana,wafadhali wamembana,ccm kwenyewe wamembana,sasa hivi kuna vuguvugu la mambo ndani ya ccm baada ya kuona Kingwendu anawaharibia chama,kwa hiyo msije kushangaa anapigwa chini kwenye kura za maoni 2010,hilo lipo kabisa,kwa hiyo tumuonee huruma,sijawahi kuona rais anashindwa kazi ndani ya 2 baada ya kuchaguliwa.Kingwendu umejenga ufa mkubwa sana ndani ya chama,Mbeya wanakusubiri uende wakupashe,tumia sleeping pills,vinginevyo utakufa kwa mawazo Kingwendu,ikulu ni mzigo.
 
Duh, mimi nafikiri JK ana matatizo makubwa zaidi ya vile wananchi wanafikiria. nashindwa kabisa kuelewa kiongozi anapoozungumzia Kelele za Upinzani wakati kuna viongozi wa juu ktk kamati kuu ya chama chake CCM wamesimama na kumtaka achukue hatua.
Ikiwa Mwinyi, Malecela, Salim A. Salim, Prof. Shivji na Butiku wote hawa wametaja maswala tofauti yanayohusiana na tuhuma tofauti ambazo zinaweza kujenga chuki baina ya serikali na wananchi, yeye anachukulia swala hili kuwa dogo kiasi cha kutomkosesha usingizi - inanipa picha tofauti kabisa.
Something is going on! I can't point it out lakini ukisoma hotuba yake utagundua kwamba anajaribu sana kukwepa kutoa msimamo wake ktk maswala haya yote.
Hizi report zote hazikutungwa na Dr. Slaa ama Zitto ni report zilizotoka nje ya vyama kabisa, tena zimetoka jikoni mwao wenyewe leo imekuwaje hawa jamaa wapike majungu?
Wananchi tunafahamu siasa ni kitu gani na mara nyingi zinahusiana na vyama sio watu binafsi, leo wanashtumiwa wao kundi dogo sana la watu ktk viongozi na wanachama wa CCM limekuwa swala la Chama!..
Je, ni wakati gani tutaweza tenganisha mtu na chama chake ikiwa viongozi hawa hulindwa hadi wanapostaafu?..Na sijaona mahala ktk report ile likizungumzia chama CCM kama ndio nguzo ya ufisadi huo.
Hayo maswala mengine yote alozungumza hayana uzito mkubwa kwa wananchi ikiwa kuna tobo ktk pakacha la maendeleo yetu..swala hapa sio nguvu na jitihada zinazotumika kulijaza pakacha hili la maendeleo bali wananchi wanazungumzia hizo tobo zinazomwaga kinachoingia.
Ni muhimu afahamu kwamba kwa kila tunachofanya kamwe hatuwezi kujaza maji ktk hilo pakacha na hata kidogo tulichojitahidi kuweka kitakwisha kutokana na tobo hizo.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom