GHIBUU
JF-Expert Member
- Jan 13, 2011
- 4,432
- 3,016
Uko sawa mkuu maana hata Tanganyika haina kiti UN.
Kipo ndo hio tanzania, Zaire kuita Congo.
Uko sawa mkuu maana hata Tanganyika haina kiti UN.
sijakuelewa hapa. unataka tena muendelee kubebwa hata kwa baraza lenu la mawaziri lije huku bara kula posho? hivi hamtosheki na hawa akina nahodha vuai, dr.hatib, dr. mwinyi, dr. bilal na wengineo wengi wanaokula ruzuku za wabara bila ya kuzitolea jasho? maajabu haya.
masikini tanganyika yangu.
Huyu Kesissy ni mpuuzi tu hata posho wanazopeana huko bungeni nani kawapa ruksa angeanza kwanza kupambana nazo kama ana uchungu na Tanganyika.Duuh!! Kessy..Huyu kwa CCM hakuna wa kumsogelea..Anasimamia anacho Amini..Siyo maigizo ya Mwingulu kuvaa matambara shingoni ndiyo Uzalendo
Well said..tunamshukuru Mhe Keissy kwa haya maono. Huyu ni mmoja wa wateule wachache waliobaki mjengoni kwa ajili ya kuikomboa Tanganyika huruMawazo kama ya KESSY hamuwezi kuyamaliza kwa kupigana naye nje ya Bunge yeye ndivyo anavyoamini hata upande mwingine mwa shilingi wanasema Tanganyika imevaa koti la muungano.Rasmu ya katiba ya Mzee Warioba iliweka misigi mizuri ya kumaliza dukuduku kama hizo.Mambo yote ni serikali tatu kama ilivyoainishwa na kamati ya Mzee Warioba hata ukisoma kitabu cha Dr Mwakyembe kinafafanua vizuri dukuduku za akina Kessy na Duni suala ni serikali tatu.Mwl OLUOCHI amewambia hata katiba yetu ikipinda haitashi zaidi ya miaka 10.Tunahitaji Zanzibar na Tanganyika zenye serikali kamili si ujaja ujanja wa akina LUKUVI na WASIRA.Malikia miaka mingi alikuwa na mawazo mgando lakini kabla mwezi huu haujaisha tegemea kupata SCOTLAND huru.SITTA,LUKUVI,WASIRA mpo hapo
Ama kweli ukistaajabu ya musa!Wabunge wa Zanzibar wanachangia hoja zaidi ya hao wa Bara ambao kila kukicha wanaonekana wamelala tena wengine wakisha weka saini ya mahudhurio wanarudi mahotelini kujirusha na mabinti. Huyu Mjumbe Kessy ni jinga la wajinga kwa sababu bunge letu ni bunge la JMT sio bunge la Tanganyika. Hao wajumbe 83 wanawakilisha majimbo yao sawa kabisa na wabunge 300 wetu ambao kwa upumbavu wetu wameenda pale kuchuma na kugombea nafasi za kuingia mabaraza ya Bunge kuvuta Posho. Kama kuna mambo ya Tanganyika ambayo wabunge wa Zanzibar hawatakiwi kujadili basi na uiundwe Congress yenye wajumbe wake toka pande mbili ili kupitia yale ya Muungano, kisha hilo bunge la Tanganyika libakie na magarasha wake.
Akumbuke tu kwamba Katiba inayojadiliwa ni ya Tanzania hivyo kila kinachpitishwa na bunge hilo ni kwa ajili ya Tanzania sio Tanganyika, Sheria za Tanganyika ndizo hutumika kama sheria mama. hivyo ni wao Wazanzibar wamefungwa na matakwa ya Tanganyika kuingia moja kwa moja kuwa sheria mama na ndio maana wanaitaka serikali 3 (ya Tanganyika) ili sheria mama ya JMT iwe tofauti na ile ya Tanganyika.
Ama kweli ni taabu kubwa sana akili ndogo kuongoza akili kubwa.
Kwa kuongezea hapo ikitokea CUF wamechukua nchi Zanzibar na CCM bara. Kwa hiyo lazima wawe na coalition government? na unavyosema ikatokea Rais wa Bara amekufa automatic CUF ndio itakuwa inaongoza nchi.. Hawa jamaa sijui kama wana akili aiseeKessy yupo sahihi. Tena anatakiwa apongezwe kwa kuwasemea watanganyika ambao siku zote wanashindwa kuongea ukweli kuhusu utata wa muungano. Mwenye busara yeyote lazima ajiulize,hivi zanzbar wanachangia sh ngapi kwenye gharama za muungano. Jibukeshatoa Benno Ndulu gavana kwamba hawachangii kitu!. Kingine pia tujiulize,tunapomufanya rais wa zanzbar kuwa makamu wa kwanza wa rais,hivi tuna akili kweli? Ikitokea rais wa Tanzania bahati mbaya kafa,huyo makamu wa kwanza ndiye atakua rais. Sasa kichekesho ni kwamba huyo makamu kachaguliwa na watu laki kadhaa wa Zanzbar tu,watanganyika wote milioni 44 hawajamchagua wala hawajashirikishwa kumpata! Haya ni maajabu na mbunge Kessy ana ujasiri wa kuyaelezea haya na tumemuelewa.
Huyu Kesissy ni mpuuzi tu hata posho wanazopeana huko bungeni nani kawapa ruksa angeanza kwanza kupambana nazo kama ana uchungu na Tanganyika.
Cha kuchekesha huyu Keissy, kawashikia akili watu na kumuona ana uchungu na taifa lakini yeye na wenzake wanakula kodi zetu huku wanagonga meza na kukoroma bungeni huku kwenye akanti zao wanawekewa pesa.Miezi 6 posho sio mchezo, eti leo ananguruma, unafiki tu.
Eti wazenji walimsubiri Keissy nje ya ukumbi ili wambonyeze kizenji? Wanatafuta balaa hao. Wajue kuwa Keissy anawakilisha kwa kiasi kikubwa mtazamo wa watanganyika walio wengi.
Cha kuchekesha huyu Keissy, kawashikia akili watu na kumuona ana uchungu na taifa lakini yeye na wenzake wanakula kodi zetu huku wanagonga meza na kukoroma bungeni huku kwenye akanti zao wanawekewa pesa.
miaka 50 ya kudanganyana ifike mahali tuwe wakweli ccm wamezoea vya dhuluma hawawezi kuishi ktk ukweli ..huyu mzee Nkasi namuunga mkono hatuwezi kubeba mzigo uliobebeka tena kila mtu ababe mzigo wake hawa wanzazibar tunalisha kwa pesa zetu hawana faida yoyote kwetu... back tanganyika