Kawe leo hii kuanzia Saa 1 hadi Saa 3 Usiku kulitokea nini hadi MP wa JWTZ Kufurika, Kukamata Watu, Kutembeza Kichapo na Kuzua taharuki?

...Pamoja na uzibaji wa njia Sijui walijibishana nini kama muwajuavyo madereva bajaji na boda, keno akamlamba kibao kijana akaon sio kweli kaenda kweny bajaj yake katafuta silaha kaichukua, kwamba hapa naenda kujeruhi, kamchoma nayo" unasema kaua bila kukusudia? Basi Sheria ni pana aisee
Soma CPA kasome defensive factors ambazo zinaweza kukulinda usiwe liable.Utaelewa.
 
Mkuu mambo ya kisu au bisibisi ni yiming hata uwe vandame mtu akikutime anakuua
Boda boda na bajaji wengi wana bisibisi tena zile ndefu kabisa.

Ukiwa unabishana nae ukae kwa tahadhali.
Mara nyingi huwa wanatrmbea nazo kwa ajili ya kujitetea na majambazi ya pikipiki,

Huyo afande alifikiri cheo chake ndio kila kitu. Watu wamevurugwa kukuwahisha mbinguni hawaoni shida.

Ndio maana mimi siku zote hata mtoto mdogo anichokoze vipi sipigani nae maana najua linaweza kutokea lolote. Ni heri ionekane bwege mbele ya watu kuliko kujifanya kidume uishie kufa au jela
 
Shida sio hekima shida ni chuki, I'm telling you I know what I'm telling you raia punguzeni chuki na Jeshi lenu,
Huku kudharauliwa na kuchukiwa mmekutaka wenyewe.

Kwanini siku hizi mnapiga raia sana??
Utakuta jambo dogo tu la kutumia busara, nyie mnapiga. Zamani mlipendwa na kuheshimika....angalieni mlipokosea mrekebishe.
 
Kuna sababu, hawezi mtu akakuzaba makofi pasinakua na sababu yawezakua wewe ni mtovu wa nidhamu umemtusi km afanyavyo huyu member humu Don Vill hivi huyu aanze kuporomosha matusi mbele ya Askari na kumvimbia unadhani nini kitafuata? Mtu anatukana viungo vya mama yake anavitaja bila kua na staha unahisi nini kitafuata?,
Kama kakutukana ndio una haki ya kumpiga?
Huko jeshini ndivyo mnavyofundishwa?
Sasa muwapige wanyonge, ukikutana na mwamba au mtu wa silaha madhara yake ndio hayo.
 
Punguza chuki za kijinga, form 4 failure ndio mlivyokaririshwa kua kila Askari ni form 4 failure? Acha kua mjinga chagua kua mwerevu,
Askari mwenye shule havimbi hovyo. Nasikitika kanari alishindwa kucontrol hasira.
Mimi pale Lugalo nafika sana na nafanya nao mambo mengi sana.
Nafahamu vikosi vingi tu na wakuu wake.....kwenye barracks hadi ofisini.
Wakubwa wana heshima sana, sasa hawa ndugu zetu form 4 dah dah......walinzi wa magetini dah ndo wanavimba.
Mkome.
 
Duuh inasikitisha sana kama ni kweli ila hawa jamaa muda mwingi wanakosea mengi kwa kujiona hawagusiki........sasa kama nikweli mtu mwenye mafunzo mpaka cheo hiki anakufa kibwege namna hii? Kwasababu ya parking? Afande gani mwenye mafunzo na inaonyesha alikuwa senior jeshini anakosa busara na hekima kiasi hiki.
Tatizo ni kwamba kuna watu baadhi wakiwa na nyadhifa flani serikalini wanafikiri ndio wana title deed ya hii nchi kwamba they can do you whatever they want, na wala huwawezi Fanya chochote, sasa ona sasa, Mungu atujalie hekima na busara katika kufanya maamuzi.
 
Mkuu The Underdog X umejitahidi sana kutetea askari. Wewe ukiwa kama kiongozi huko uliko, fikishieni taarifa wenzenu kuwa siku hizi mambo yamebadilika. Zamani ni polisi na ninyi tu ndio mlikua mnatembea na silaha (ukiacha viongozi wakubwa wakubwa).

Siku hizi kuna raia kibao wanatembea na silaha kihalali na haramu pia. Watu wamevurugwa na mambo mengi, ukiwatibua wanafanya lolote. Majuto huja baadae both sides.

Lakini pia, jeshini mjitafakari. Kwanini wananchi hawaliheshimu jeshi, wanalichukia jeshi si kama zamani?

Kimebadilika nini?

Nakumbuka zamani ukiwa porini huko remote ukiona gari ya jeshi unasimamisha unaomba lift wanakubeba. Siku hizi mtu akiliona gari huko analipisha mbali, kwanini?

Ilikua mtu anasimamisha gari vijijini na kuwazawadia mazao mikungu ya ndizi, n.k, why not today?

Mmebadilika mno, mnaonea raia wakati mwingine bila sababu za maana. Mtu kakosea njia porini huko kaingia eneo la jeshi, msaidieni aondoke. Ninyi mnaanza kumuadhibu....raia watakosa kujenga chuki?

Badilikeni au tuendelee kushuhudia vita mitaani.
 
Magari yamepita asubuhi Mzee wewe umelala yamepita malori kibao yamebeba wanajeshi yanatoka Lugalo, endelea kulala wao hawalali wanakulinda wewe na mipaka ya Nchi yako
Mbona watu wengine ni washamba sana? Wanafanya kazi bure? Si ni kazi waliyoichagua na wanalipwa? Hujui kuna mgawanyo wa kazi? Unajua watu wanaokulisha wewe? Unajua watu wanaokutibu? Unajua watu wanaosafisha takataka? Una maana kwa vile mtu analinda ndiyo apige raia bila kufuata sheria?
 
Inasemekana ( kwa aliyenipa Taarifa Kamili kuwa ) Dereva Bajaji jana Usiku katika Baa Moja maarufu iliyo kwa ndani ( Mafichoni kidogo ) mkabala na Petro Station ya PUMA Kawe alipishana Kauli na Mwanajeshi ( tena Mkubwa wa Cheo cha Kanali ) kuhusu Kuzibiana njia ya kupita.

Ambapo Afande Kanali alikuwa Kapaki Gari lake lililokuwa limezuia njia kwa mbele na Dogo ( Dereva Bajaji ) kuhoji kwanini Afande aliziba njia hali iliyomkwaza Afande ( wa Cheo cha Kanali Muro kama sijalikosea Jina lake ) ambapo Afande Kanali akatoka ndani ya Gari lake na Kumzaba Makofi Dereva Bajaji huyo.

Kisha nae ( Dereva Bajaji ) kwa Hasira akaamua kwenda kuchukua Bisibisi Bajajini Kwake na kuja Kumchoma nayo Afande Kanali upande wa Moyo hali iliyomfanya akimbizwe Lugalo Hospital kwa Matibabu na Umauti kumkuta huko huko Wodini.
Duuh Kanali ni mtu mkubwa sana jeshini kwann alifanya kitu Cha kijinga namna hii? SI Bora angepiga simu kikosini awaite vijana wake kuliko alichokifanya au alikuwa amelewa?
 
Yaani inashangaza sana,unampiga mtu makofi,ili?
Sasa amekuchoma na bisibisi umekufa,wakati labda ungemuelimisha tu,kua dogo ngoja nipite,au unatumia saikolojia tu,mnayamaliza.Hii yakuamini askari anaweza akamdhibiti yeyote,inaleta changamoto.Hapo ukute kanali aliwaza tu kua kwasababu yeye ni mwanajeshi,akimpiga makofi,dogo ataomba msamaha,kumbe dogo kavurugwa,mwishowe ni kufa eti kwa kukitwa na bisibisi... aisee.
Na pengine hata huyo bajaji ukute alikuwa hajui kama Marehemu ni mwanajeshi, ila Cha kujifunza huku barabaran sio sehemu Nzuri kuvimbiana Bora uwe mpole tu hasa ukiwa kapuku
 
Back
Top Bottom