Nimetafakari, nikaona nipate pia mawazo wanafikra weledi juu ya baadhi ya kauli zenye utata za viongozi kwa wananchi
Je, huu ni uungwana kweli?
Kauli tata za vingozi wa Tanzania
Je, huu ni uungwana kweli?
Kauli tata za vingozi wa Tanzania
- Mtakula nyasi lakini ndege ya Rais lazima inunuliwe (MRAMBA)
- Ukitaka kula inabidi ukubali na wewe kuliwa (J Kikwete)
- Foleni Dar ni ishara ya maisha bora (J Kikwete)
- Hata mimi sielewi kwa nini Tanzania ni maskini! (J Kikwete)
- Ningekuwa mvua ningenyeshea mabwawa (J Kikwete)
- Wafanyakazi hata wakigoma miaka 100 ila mshahara kima cha chini 350,000 haiwezkani (J Kikwete)
- Wanafunzi kupata mimba ni viherehere vyao (J Kikwete)
- Acheni wivu wa kike (MSEKWA)
- Asiyeweza nauli mpya kwenda kigamboni apige mbizi (MAGUFULI)
- Baada ya kutumia helikopta ya jeshi kwenda kwetu urambo mlitaka nipande punda(KAPUYA)
- Wabunge wa Dar wanafikiri kwa kutumia makalio(Dr Didas Ma------)
- Mnaniuliza mvua kwani mimi waziri wa mvua?(WASIRA)
- Ngeleja kila siku ananinunulia chai wakati nina uwezo (ANNE KILANGO)
- Posho za wabunge lazima zipande kwa sababu maisha ya Dodoma yapo juu (Spika Makinda)
- Wakati huu ambapo nchi inakabiliwa na janga la njaa nawashauri wakulima wahifadhi hata pumba maana zinaweza kusaidia (John Malecela)
- Kila mtu atabeba mzigo wake mwenyewe - Cleopa Msuya
- Mheshimiwa Lema, ninakuagiza ifikapo Jumatatu asubuhi uwasilishe Bungeni ushahidi kwamba mheshimiwa waziri mkuu asema uongo bungeni (Anna Makinda)
- Wapinzani wanapenda mambo ya ovyoovyo wanafiki hawa wataendelea kuwa wapinzani tu (Samwel Sita)
- Graduates msio na kazi fugeni kuku biashara hiyo inalipa sana (Mwantumu MAHIZA)
- Kinachomsumbua Slaa (Dr) ni wivu, wivu kuona ndege inapaa, ndege ya uchumi wa TZ inapaa"- (Edward Lowasa)
- Tanzania ni muungano wa visiwa viwili, Tanganyika na Zimbabwe (Philip Mulugo)
- Siongei na mbwa mi naongea na mwenye mbwa (Juma Ngamia)
- Hakuna Rais atakayetoka Kaskazini (Ridhiwan Kikwete)
- Waliotoka Bara na kuja Dar es Salaam wafute kwanza tongotongo (Ukiwaona Ramadhan Mwinshehe Ditopile Mzuzuri)
- Mbowe amekuja hapa kajamba-jamba halafu kaondoka (Seif Khatib)
- (Billioni 1.2) - Hivyo ni vijisenti tu (Andrew Chenge)