Robert Heriel Mtibeli
JF-Expert Member
- Mar 24, 2018
- 21,337
- 51,858
CHALAMILA KAULI ZAKE ZINAZUA MASWALI MENGI.
Na Robert Heriel.
Nani aliyemuambia wananchi wa Mwanza Wanakinyongo na Kifo cha Magufuli?
Chalamila hajamaliza hata wiki mbili tangu awe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, sasa je aliwezaje kuzipata taarifa za Wakazi wa Mwanza kwa muda mfupi tuu kuwa watu Wanakinyongo na Kifo cha Magufuli?
Je Chalamila alikuwa akiisemea nafsi yake au alikuwa akiwasilisha vinyongo vya watu wanaomzunguka kuhusu Kifo cha Magufuli?
Je Chalamila hakuwepo wakati msiba wa Magufuli na hakusikia Sababu zilizosababisha Umauti umfikie JPM?
Je nini dhamira ya Chalamila kusema kauli hiyo?
Chalamila kusema watu Waende na Mabango yenye jumbe zozote hata za MATUSI, alikuwa anajaribu Kueleza Uhuru wa namna gani?
Chalamila akiwa Mbeya aliwahi kusema hataki Mabango ya Aina yoyote yenye jumbe za hovyo, je nini kimebadilika alipofika Mwanza?
Nilishawahi kusema, Wale wote waliokuwa wakisapuza na kuhamasisha JPM aongezewe muda wa kuongoza wanapaswa waondolewe katika nafasi walizonazo. Na Kama ni wabunge mwaka 2025 wasirudi bungeni.
Bahati nzuri wanafahamika, na wanajifahamu. Hatuwezi kuwa na taifa la viongozi wasioweza kutumia akili zao vizuri.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa MOROGORO
Na Robert Heriel.
Nani aliyemuambia wananchi wa Mwanza Wanakinyongo na Kifo cha Magufuli?
Chalamila hajamaliza hata wiki mbili tangu awe Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, sasa je aliwezaje kuzipata taarifa za Wakazi wa Mwanza kwa muda mfupi tuu kuwa watu Wanakinyongo na Kifo cha Magufuli?
Je Chalamila alikuwa akiisemea nafsi yake au alikuwa akiwasilisha vinyongo vya watu wanaomzunguka kuhusu Kifo cha Magufuli?
Je Chalamila hakuwepo wakati msiba wa Magufuli na hakusikia Sababu zilizosababisha Umauti umfikie JPM?
Je nini dhamira ya Chalamila kusema kauli hiyo?
Chalamila kusema watu Waende na Mabango yenye jumbe zozote hata za MATUSI, alikuwa anajaribu Kueleza Uhuru wa namna gani?
Chalamila akiwa Mbeya aliwahi kusema hataki Mabango ya Aina yoyote yenye jumbe za hovyo, je nini kimebadilika alipofika Mwanza?
Nilishawahi kusema, Wale wote waliokuwa wakisapuza na kuhamasisha JPM aongezewe muda wa kuongoza wanapaswa waondolewe katika nafasi walizonazo. Na Kama ni wabunge mwaka 2025 wasirudi bungeni.
Bahati nzuri wanafahamika, na wanajifahamu. Hatuwezi kuwa na taifa la viongozi wasioweza kutumia akili zao vizuri.
Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
0693322300
Kwa sasa MOROGORO