Missile of the Nation
JF-Expert Member
- May 24, 2018
- 16,817
- 62,027
Nimemsikiliza Mheshimiwa Warioba, amesema kuwa vijana wetu waliouawa na Iddi Amin ni wachache kuliko watanzania waliouawa na utawala wa samia kwa kutumia majeshi yetu.
Taarifa ya jambo hili imenitafakarisha sana, kunihuzunisha sana na kushangazwa sana kuona kuwa majeshi yetu yanaweza kufanya uharamia, mauaji na ukatili wa kutisha dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kiwango hiki.
Kwa mauaji haya, ni upi uhalali kwa jeshi kuendelea kuitwa jeshi la wananchi wa Tanzania, upo wapi uhalali huu?.
Kama Majeshi yanaua watanzania kuliko Iddi Amin, hayo majeshi yanwezaje kujipride kuwa ni majeshi ya wananchi?.
Kinachotafakarisha zaidi ni kuwa kauli ya ulinganifu huo kuwa adui aliua vijana wetu wachache kuliko watanzania waliouawa na majeshi yetu imetolewa na aliyewahi kuwa makamu wa rais, waziri mkuu na mwanasheria mkuu wa serikali. Hili jambo linashtusha mno!.
Mimi siku zote nimekuwa proud na majeshi yetu, hasa operesheni ya kumng'oa nduli Idd Amin dada, siku zote nimejisikia fahari kuwasoma makamada walioendesha vita hiyo wakiwa makao makuu na wale waliokuwa field akina jenerali Mwita Marwa, Selasie Mayunga, Imran Kombe, Musuguri, na wengineo wengi . Sasa leo Waziri mkuu mstaafu anaposema Amin hakufanya mauaji kama haya yaliyofanywa na majeshi ya sasa nachanganyikiwa kabisa nasema kweli akina Mayunga, Marwa na Msuguri wangekuewepo leo wangeruhusu haya mambo kutokea?. Bila shaka huko walipo makaburini mashujaa wetu hawa wanajipinduapindua kwa uchungu kushuhudia silaha walizoziinua kumpiga adui leo hii zimegeuzwa kuwapiga watanzania!.
Labda ndiyo maana Watazania wanapocomment katika page za mtandaoni za Jeshi la Wananchi, wanatoa kauli kali za kuonyesha kuchukia, kupiga vijembe.Hii yote naamini ni katika kuonyesha hali ya kukata tamaa. Hii yote huenda ni kwa sababu ya uchungu wa mauaji ya kutisha ya wananchi wasio na rungu, wala wembe!.
Na kimsingi ni kosa gani ambalo wananchi hawa walilifanya hadi wastahili kupigwa risasi za kivita na kuuawa kinyama namna ile?:
1. Wapo wengi tu waliuawa walikuwa hata hawamo katika masuala ya maandamano wao walikuwa mitaani na shughuli zao za kijamii ikiwemo kujitafutia riziki wameuawa bila haki.
2. Wapo wananchi waliandamana kutaka mambo ya utekaji yakome, wanataka chaguzi huru na haki ili waweze kuweka viongozi wao madarakani kwa mujibu wa katiba na wao hawakusalimika na risasi na mauaji holela.
3. Wapo waliouawa mitaani mwao, majumbani mwao ambao hawakuwamo kabisa katika ishu za maandamano. Hawa walifanya kosa gani hadi wastahiki kuuawawa?
Hapana aisee, Jeshi linao wajibu wa kuwaomba radhi Watanzania, na liseme kwa nini Kuna mauaji mengi hivi yalitokea, wao walikuwa wapi?. Na kwa kuwa operesheni ya kumng'oa Amin ilikuwa ni ya kijeshi, na kwa kuwa operesheni ya October 29 ilikuwa ni ya kijeshi (Ndiyo maana tulimuona mkuu wa majeshi kwenye TV akieleza kinachofanyika) basi tunalitaka jeshi litoe kauli kuhusu kauli hii ya waziri mkuu mstaafu kuwa watanzania waliouawa na majeshi yetu katika maandamano inazidi idadi ambayo mvamizi, nduli iddi Amin aliifanya kwa vijana wetu mwaka 1978.
c.c CDF JWTZ
Msikilize Mzee Warioba hapa akilisema jambo hili
Taarifa ya jambo hili imenitafakarisha sana, kunihuzunisha sana na kushangazwa sana kuona kuwa majeshi yetu yanaweza kufanya uharamia, mauaji na ukatili wa kutisha dhidi ya wananchi wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa kiwango hiki.
Kwa mauaji haya, ni upi uhalali kwa jeshi kuendelea kuitwa jeshi la wananchi wa Tanzania, upo wapi uhalali huu?.
Kama Majeshi yanaua watanzania kuliko Iddi Amin, hayo majeshi yanwezaje kujipride kuwa ni majeshi ya wananchi?.
Kinachotafakarisha zaidi ni kuwa kauli ya ulinganifu huo kuwa adui aliua vijana wetu wachache kuliko watanzania waliouawa na majeshi yetu imetolewa na aliyewahi kuwa makamu wa rais, waziri mkuu na mwanasheria mkuu wa serikali. Hili jambo linashtusha mno!.
Mimi siku zote nimekuwa proud na majeshi yetu, hasa operesheni ya kumng'oa nduli Idd Amin dada, siku zote nimejisikia fahari kuwasoma makamada walioendesha vita hiyo wakiwa makao makuu na wale waliokuwa field akina jenerali Mwita Marwa, Selasie Mayunga, Imran Kombe, Musuguri, na wengineo wengi . Sasa leo Waziri mkuu mstaafu anaposema Amin hakufanya mauaji kama haya yaliyofanywa na majeshi ya sasa nachanganyikiwa kabisa nasema kweli akina Mayunga, Marwa na Msuguri wangekuewepo leo wangeruhusu haya mambo kutokea?. Bila shaka huko walipo makaburini mashujaa wetu hawa wanajipinduapindua kwa uchungu kushuhudia silaha walizoziinua kumpiga adui leo hii zimegeuzwa kuwapiga watanzania!.
Labda ndiyo maana Watazania wanapocomment katika page za mtandaoni za Jeshi la Wananchi, wanatoa kauli kali za kuonyesha kuchukia, kupiga vijembe.Hii yote naamini ni katika kuonyesha hali ya kukata tamaa. Hii yote huenda ni kwa sababu ya uchungu wa mauaji ya kutisha ya wananchi wasio na rungu, wala wembe!.
Na kimsingi ni kosa gani ambalo wananchi hawa walilifanya hadi wastahili kupigwa risasi za kivita na kuuawa kinyama namna ile?:
1. Wapo wengi tu waliuawa walikuwa hata hawamo katika masuala ya maandamano wao walikuwa mitaani na shughuli zao za kijamii ikiwemo kujitafutia riziki wameuawa bila haki.
2. Wapo wananchi waliandamana kutaka mambo ya utekaji yakome, wanataka chaguzi huru na haki ili waweze kuweka viongozi wao madarakani kwa mujibu wa katiba na wao hawakusalimika na risasi na mauaji holela.
3. Wapo waliouawa mitaani mwao, majumbani mwao ambao hawakuwamo kabisa katika ishu za maandamano. Hawa walifanya kosa gani hadi wastahiki kuuawawa?
Hapana aisee, Jeshi linao wajibu wa kuwaomba radhi Watanzania, na liseme kwa nini Kuna mauaji mengi hivi yalitokea, wao walikuwa wapi?. Na kwa kuwa operesheni ya kumng'oa Amin ilikuwa ni ya kijeshi, na kwa kuwa operesheni ya October 29 ilikuwa ni ya kijeshi (Ndiyo maana tulimuona mkuu wa majeshi kwenye TV akieleza kinachofanyika) basi tunalitaka jeshi litoe kauli kuhusu kauli hii ya waziri mkuu mstaafu kuwa watanzania waliouawa na majeshi yetu katika maandamano inazidi idadi ambayo mvamizi, nduli iddi Amin aliifanya kwa vijana wetu mwaka 1978.
c.c CDF JWTZ
Msikilize Mzee Warioba hapa akilisema jambo hili