Kauli ya Mnyika, Inakatisha tamaa...

Kauli ya Mnyika, Inakatisha tamaa...

John Mnyika, Mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jana alitoa kauli ambayo kidogo ilitufanya wachache tufikirie tofauti na dhamira kuu ya UKAWA kuwaondoa CCM.

Mnyika alisema, wananchi wa Ubungo na Kibamba wafikirie juu ya uwepo wake na Kubenea ndani ya bunge utakavyoitikisa serikali...
Kwa kauli hii inamaanisha kuwa Mnyika haamini kama Ukawa watachukua nchi!!
Au alimaanisha wataitikisa serikali yao wenyewe watakaoiunda?

It means hawaamini kama Serikali ya CCM itatoka madarakani, wakati sisi wananchi wa kawaida tushaliona anguko kubwa la Chama cha Mapinduzi.

Sorry wewe ndo kichwa chako hakitumii akili, yeye naomba ubunge na kazi ya mbunge sio kutetea serikali yake ni kutetea wananchi. Shida iko wapi hata kama UKAWA itakuwa ndo serikal Mbunge makini atatetea wananchi tuuuu
 
hivi kwani kuna binadamu mwenye akili timamu ambae amewahi kufikiria kuwa ukawa watashinda uchaguzi huu?
hivi kuna binadamu mwenye nakili timamu ambae amewahi kufikiria kuwa ccm itashinda uchaguzi huu.
 
Bunge kazi yake ni kusimamia serikali sio kuitetea kwa kila hoja wanaoleta wabunge waccm tatizo lao wao wanajiona ni sehemu ya serikali ni kosa na ndio maana hatupigi hatua big up 2 mnyika na kubenea viva ukawa viva lowasa
 
Inamaana bado unafuata Mkumbo kuwa lowassa fisad mkuu atakuwa Rais !!!
 
Rabboni

Kwani wabunge wa ccm hawakuwa wakiitetemesha serikali yao?
 
Last edited by a moderator:
Naaam Mnyika anajua anachofuata Bungeni gvmnt ikikosea hajalishi ni chama chako wewe mbunge au si chako lazima uikosoe ili mambo yaende sawa.. kasumba ya kuikumbatia serikali eti kisa ni chama chako ndo imetufiisha hapa pabaya tulipo.. big up Mnyika..
 
Hueleweki wewe maana katika nyanja za bungeni makali ya Mnyika hayana shaka. Na katika taaluma ya habari za uchunguzi Kubenea hana mpinzani. Akifikisha bungeni hizo taarifa, srikali lazima itatikisika

serikali ipi sasa? yakwao wenyewe... ama serikali ipi.
 
sasa mkuu kama ataitikisa hata serikali ya chama chake mwenyewe huoni kama kashaona weakness kubwa katika serikali watakayoiunda hata kabla hawaingia madarakani?
Nikuelimishe

Serikali inafanya kazi chin ya Makatibu Wakuu. CCM imepora mfumo na taratibu stahili na kuwapachika mawaziri majukumu feki. Ndiyo sababu kuu ya kuhitaji MABADIRIKO ili kila mtu awajibike kivyake.

Kwenye mfumo sahihi bunge litaitikisa serikali kwa kushindwa kuwajibika biila kujali ni mbunge wa upande gani
 
Ukawa ikishinda mnyika lazima awe waziri, na waziri hawezi kuitikisa serikali ambapo yeye ni sehemu ya serikali, kauli hii inamaanisha mnyika hana uhakika wa kuwa lowassa ata muangusha mzee john pombe magufuli.Kwaiyo wataitikisa serikali wakiwa wapinzani imara.

chadema/ukawa ni serikali ijayo hii nilazima
 
Yaweza kuwa hukuelewa au huelewi kazi za mbunge. Kazi kubwa ya mbunge ni kuisimamia serikali....Hata kama ni serikali ya chama chako lazima isimamiwe. Kwa hali hiyo wakiingia bungeni wataisimamia vizuri serikali yao chini ya CDM kwa mwamvuli wa UKAWA hivyo kuleta ufanisi
Uko sahihi kabisa.

Jukumu kubwa la wabunge wote bila kujali itikadi zao za kisiasa ni kuisimamia serikali.

Kwa hiyo haijalishi kama serikali itakayoingia madarakani ni ya CCM au Ukawa, bado jukumu kuu la wabunge wote watakaochaguliwa Oktoba 25 mwaka huu, whether watakuwa wa CCM au Ukawa, bado wote kwa pamoja watatakiwa kuisimamia serikali na kuichachafya serikali iwapo itafanya madudu.

Ndiyo maana Ukawa inapohubiri mabadiliko ni kwa maana hiyo ya kwamba hata wabunge wa CCM, hawapaswi kurudi bungeni kwa kuwa wao wanachoamini ni kuwa iwapo chama chao ndicho kitakachokuwa madarakani, basi ni 'dhambi' kubwa kuikosoa serikali yao ya CCM wanapokuwa bungeni.
 
John Mnyika, Mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jana alitoa kauli ambayo kidogo ilitufanya wachache tufikirie tofauti na dhamira kuu ya UKAWA kuwaondoa CCM.

Mnyika alisema, wananchi wa Ubungo na Kibamba wafikirie juu ya uwepo wake na Kubenea ndani ya bunge utakavyoitikisa serikali...
Kwa kauli hii inamaanisha kuwa Mnyika haamini kama Ukawa watachukua nchi!!
Au alimaanisha wataitikisa serikali yao wenyewe watakaoiunda?

It means hawaamini kama Serikali ya CCM itatoka madarakani, wakati sisi wananchi wa kawaida tushaliona anguko kubwa la Chama cha Mapinduzi.

Hakuna ubaya mkuu kwa hiyo kauli. Hapo alikuwa na maana kwamba hao mawaziri wa serikali ya UKAWA lazima wajipange sawasawa kukabiliana na hoja za akina Mnyika na Kubenea endapo wenyewe hawatateuliwa kuwa mawaziri. Kumbuka hata ccm kwenyewe walipokuwa madarakani kulikuwa na mibunge ilikuwa inaitikisa serikali ya yenyewe!!
 
Hakuna ubaya mkuu kwa hiyo kauli. Hapo alikuwa na maana kwamba hao mawaziri wa serikali ya UKAWA lazima wajipange sawasawa kukabiliana na hoja za akina Mnyika na Kubenea endapo wenyewe hawatateuliwa kuwa mawaziri. Kumbuka hata ccm kwenyewe walipokuwa madarakani kulikuwa na mibunge ilikuwa inaitikisa serikali ya yenyewe!!

i got you, je, unadhani Ukawa ikichukua madaraka Mnyika hatapewa Wizara?
 
kwani hujaelewa nini hapo? serekali si anamaanisha ccm na serekali yake kabla yakukabidhi madaraka kwa ukawa itatikisika hapo October watakapo ona jimbo la ubungo na kibangu chini ya mnyika na kubenea
 
kwani hujaelewa nini hapo? serekali si anamaanisha ccm na serekali yake kabla yakukabidhi madaraka kwa ukawa itatikisika hapo October watakapo ona jimbo la ubungo na kibangu chini ya mnyika na kubenea

Jimbo la Kibangu ndiyo lipi?
 
Thread yako ni sawa na kukombeleza ukoko.
Huna hoja
 
Back
Top Bottom