Kauli ya Mnyika, Inakatisha tamaa...

Kauli ya Mnyika, Inakatisha tamaa...

sasa cha ajabu ni nini mimi naona amemanisha wote majembe na tunataka watu kama hao bungeni

kwa hiyo unakubali serikali itakuwa ya ccm? kama ni serikali yao vipi aitikise?
 
Mnyika akifanikiwa kurudi bungeni, Akatoe sadaka ya shukrani kwanza kanisani kwake, maana amekalia kuti bovu.

huyu mgombea wenu wa ubungo asahau kabisa, maana yeye ndio tunahasira naye sana ya kutudanganya wananchi, tena wengine wengi tunamchukia mamvi kwa sababu ya magazeti yake, alikuwa mwandishi wa habari pekee kutuaminisha wananchi kuwa Lowasa ni fisadi, leo anataka aniaminishe otherwise? asahau kupata ubungo.
 
John Mnyika, Mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jana alitoa kauli ambayo kidogo ilitufanya wachache tufikirie tofauti na dhamira kuu ya UKAWA kuwaondoa CCM.

Mnyika alisema, wananchi wa Ubungo na Kibamba wafikirie juu ya uwepo wake na Kubenea ndani ya bunge utakavyoitikisa serikali...
Kwa kauli hii inamaanisha kuwa Mnyika haamini kama Ukawa watachukua nchi!!
Au alimaanisha wataitikisa serikali yao wenyewe watakaoiunda?

It means hawaamini kama Serikali ya CCM itatoka madarakani, wakati sisi wananchi wa kawaida tushaliona anguko kubwa la Chama cha Mapinduzi.

Kubenea naye nasikia kasema akipata Ubunge atawataja waliochota pesa za escrow bungeni, kama anaamini serikali itakuwa ya UKAWA nilitaraji aseme watawashughurikia maana si itakuwa serikali yao, au akitutajia sisi ndo tufanye nini wakati wanaenda kuchukua serikali?
 
John Mnyika, Mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jana alitoa kauli ambayo kidogo ilitufanya wachache tufikirie tofauti na dhamira kuu ya UKAWA kuwaondoa CCM.

Mnyika alisema, wananchi wa Ubungo na Kibamba wafikirie juu ya uwepo wake na Kubenea ndani ya bunge utakavyoitikisa serikali...
Kwa kauli hii inamaanisha kuwa Mnyika haamini kama Ukawa watachukua nchi!!
Au alimaanisha wataitikisa serikali yao wenyewe watakaoiunda?

It means hawaamini kama Serikali ya CCM itatoka madarakani, wakati sisi wananchi wa kawaida tushaliona anguko kubwa la Chama cha Mapinduzi.

Mkuu inaonekana umeathiriwa saana na namna wabunge wa ccm wanavyofanya kazi wakiwa bungeni. Na kusahau majukumu ya mbunge kwamba ni:
1) Kuisimamia serikali.
2) Kushauri serikali.
3)Kuitwanga masuali magumu serikali.
4) Kuelezea shida na kero zinawakabili wananchi wao wanawawakilisha.
Pamoja na mambo mengine meeengi. Hayo ndio majukumu ya mbunge yoyote yule bila kujali kama anatoka chama tawala au upinzani.
John Mnyika na Kubenea wanayajua vyema majukumu yao kama wabunge na wataisimamia vyema serikali ya UKAWA hata kama wao wanatoka UKAWA.
 
Mnyika akifanikiwa kurudi bungeni, Akatoe sadaka ya shukrani kwanza kanisani kwake, maana amekalia kuti bovu.

huyu mgombea wenu wa ubungo asahau kabisa, maana yeye ndio tunahasira naye sana ya kutudanganya wananchi, tena wengine wengi tunamchukia mamvi kwa sababu ya magazeti yake, alikuwa mwandishi wa habari pekee kutuaminisha wananchi kuwa Lowasa ni fisadi, leo anataka aniaminishe otherwise? asahau kupata ubungo.

wanadhani kuchoka kwetu ndo watufanyie chochote, wataisoma namba.
 
John Mnyika, Mgombea ubunge kwa tiketi ya Chadema jana alitoa kauli ambayo kidogo ilitufanya wachache tufikirie tofauti na dhamira kuu ya UKAWA kuwaondoa CCM.

Mnyika alisema, wananchi wa Ubungo na Kibamba wafikirie juu ya uwepo wake na Kubenea ndani ya bunge utakavyoitikisa serikali...
Kwa kauli hii inamaanisha kuwa Mnyika haamini kama Ukawa watachukua nchi!!
Au alimaanisha wataitikisa serikali yao wenyewe watakaoiunda?

It means hawaamini kama Serikali ya CCM itatoka madarakani, wakati sisi wananchi wa kawaida tushaliona anguko kubwa la Chama cha Mapinduzi.

Kulingana na maalezo yako sijaona mahali aliposema serikali ya ccm
Anaweza akaitikisa hata serikali ya ukawa.
 
Mkuu inaonekana umeathiriwa saana na namna wabunge wa ccm wanavyofanya kazi wakiwa bungeni. Na kusahau majukumu ya mbunge kwamba ni:
1) Kuisimamia serikali.
2) Kushauri serikali.
3)Kuitwanga masuali magumu serikali.
4) Kuelezea shida na kero zinawakabili wananchi wao wanawawakilisha.
Pamoja na mambo mengine meeengi. Hayo ndio majukumu ya mbunge yoyote yule bila kujali kama anatoka chama tawala au upinzani.
John Mnyika na Kubenea wanayajua vyema majukumu yao kama wabunge na wataisimamia vyema serikali ya UKAWA hata kama wao wanatoka UKAWA.

Mkuu, hiyo serikali ya UKAWA kama Mnyika hatakuwa waziri ni nani atakuwa waziri sasa!!
 
Ukawa wangekuwa wana nafasi ya kushinda uchaguzi Dr. Slaa na Lipumba wasingeondoka.

Kubenea aliwatangazia watu kuwa Chadema ilijua kuwa haiwezi kushinda uchaguzi mwaka huu ndio maana wakamtosa Dr. Slaa. Lowassa wamemchukua ili awape pesa za kampeni tu. Ukisoma ilani ya uchaguzi ya chadema ya uchaguzi uliopita 2010 waliandika kuwa hawatashinda uchaguzi wa 2015, sijui walitumia kigezo gani ila walishajua hilo.

Tumia akili angalau kidogo tu...
 
Kazi ya Bunge ni kutikisa serikali iwe yako au si yako, japo nina uhakika aliitumia kumaanisha serikali ya ccm
 
Lowassa ndiye anayejua nani atakuwa Waziri katika serikali yake.

kwa hiyo tufanye mchezo wa kubahatisha? kiongozi ambaye hatujui kesho ataamka na lipi ni hatari sana, kijana kama Mnyika hapashwi kukosa serikali ya UKAWA.
 
Hueleweki wewe maana katika nyanja za bungeni makali ya Mnyika hayana shaka. Na katika taaluma ya habari za uchunguzi Kubenea hana mpinzani. Akifikisha bungeni hizo taarifa, srikali lazima itatikisika
 
Ya Ngoswe Kuitwa Ngoswe Muachie Ngoswe Mwenyewe......Ya UKAWA kushinda au kushindwa uchaguzi wa okitoba waachie wenyewe.....hawa na magufuli yao....wale na luwassa wao.....hehehehehe laazma mtu ang'olewe jino bila ganzi mwaka huu....
.
...na wale wa lichama lenye kunguni wallllllllllllllllllahi tunalichoma moto okitoba ishirini na tano...
.
....hahahahah natania tu
 
Endeleeni kuwaamini Ukawa wawatie UKIWA.
 
Huwezi kuitoa ccm madarakani hata siku moja

Mimi si mwanachama wa chama chochote na mara zote nimekuwa nikichagua mtu bila kujali anatoka ccm au upinzania ili mradi anajitambua kama kiongozi. katika lugha ambazo sizipendi na ninazichulia ni kusema "CCM HAITATOKA MADARAKANI KAMWE" na hii lugha imejaa kiburi na kujikweza kusiko na maana na ndio inafanya ccm kubweteka na kushindwa kuwahudumia wananchi wake kama inavyostahili. Lakini kumbuka methali isemayo Kila chenye mwanzo kina mwisho Kama CCM haina mwazo basi tusitegeme kutoka madaraka kamwe lakini kama ina mwazo Lazima ifikie ukomo. katika ulimwengu huu asiye na mwisho/ukomo ni mmoja tu naye ni MUNGU ALIYE HAI
 
Hueleweki wewe maana katika nyanja za bungeni makali ya Mnyika hayana shaka. Na katika taaluma ya habari za uchunguzi Kubenea hana mpinzani. Akifikisha bungeni hizo taarifa, srikali lazima itatikisika

sasa mkuu kama ataitikisa hata serikali ya chama chake mwenyewe huoni kama kashaona weakness kubwa katika serikali watakayoiunda hata kabla hawaingia madarakani?
 
Ukawa ikishinda mnyika lazima awe waziri, na waziri hawezi kuitikisa serikali ambapo yeye ni sehemu ya serikali, kauli hii inamaanisha mnyika hana uhakika wa kuwa lowassa ata muangusha mzee john pombe magufuli.Kwaiyo wataitikisa serikali wakiwa wapinzani imara.
 
Back
Top Bottom