Kauli ya Mch. Mtikila kuhusu katiba mpya hii hapa

Mwenyekiti wa DP, Mchungaji Christopher Mtikila amesema Chadema ilikurupuka na kudandia hoja ya Katiba mpya ya nchi bila kuzingatia maslahi ya Watanzania na kuonya kuwa mchakato wa kuunda Katiba unaweza kushindwa kama utafanywa kwa lengo la kukidhi matakwa ya watu wachache wanaoshinikizwa na wageni.

Akizungumza kwa simu jana, Mtikila alisema si viongozi wa Chadema wenye dhamira ya dhati ya uundaji wa Katiba mpya kwa maslahi ya Watanzania, kwa kuwa wanataka Katiba iundwe, kwa maslahi binafsi kwa lengo la kuendeleza zama za ukoloni.

“Mimi nilipojaribu kuzungumzia Katiba mpya na haja ya kuwa na Serikali tatu, watu waliniona kichaa, jambo ambalo lilisababisha kampeni ya kutaka Katiba kuwa ngumu na isiyo na mafanikio … sasa watu hao hao wanataka Katiba mpya kwa maslahi yao,” alisema.

Hata hivyo Mtikila alimwomba Rais Kikwete, asisahau kumjumuisha kwenye Tume atakayoiunda kwa kuzingatia kuwa ametumia muda mwingi kudai Katiba mpya ya nchi akiwa na dhamira ya dhati.

niliposoma muanzishaji wa huu uzi na kugundua kuwa ni wewe nilijua tu contents zitakuwa ni crap!!!

Anyway heri Chadema wanaodai Katiba kwa maslahi ya Tanzania kuliko yeye (Mtikila) aliyekuwa anadai katiba kwa kutaka umaarufu.
 
Kama udandiaji wao ndo umefikisha hatua ya katiba kupatikana basi HAWA NI WADANDIAJI WAZURI

kama mwanaume hana hata ubavu wa kudandia basi huyo ni mwanaume suruali.

Bravo Chadema. Hawali wakanya wakalala bila kulitaja neno Chadema.

Na bado!!
 
Shida ya Mtikila ndo hii tu '' KUTAKA UMAARUFU '' !! Ona sasa hapa anawaona Chadema kama wa Binafsi!!! Bila kujua kuwa Nguvu ya Chadema kwa sasa ndio inayoleta mabadiliko yote tuyaonayo sasa...Mtikila nitamsifu kwa kitu kimoja tu.....''' Ni migania uhuru mzuri....anaifahamu mahakama vizuri na anaitumia vizuri'' shida yake mbinafsi!!! akubali kuwa Chadema ni Chama Mbadala ashirikiane nacho ili Watanzania wote wafikie lengo moja ambalo ni katiba Mpya. Pili asikimbilie kuomba raisi amjumuishe kwenye tume ya katiba...Bali ashirikiane kushinikiza raisi kuhusu ujumuishaji wa wananchi wote katika mchakato wa katiba kama walivyofanya ndugu zetu wa Kenya....
 
Back
Top Bottom