Katika shule bora 100, shule za seriakli ni 7 tu

Katika shule bora 100, shule za seriakli ni 7 tu

Kale ka salary na kenyewe ni tatizo pia , mwambie pia wazir waongezewe pia salary ili wawe na motisha ya kufundisha, hawezi kupata moraly ya kufundisha wakati mshahara haumaliz mwezi ikifika tarehe 18 tu hoi
Hivi kwani kuna mtu alilazimishwa kufanya kazi anayoifanya? Kamshahara kakiwa kadogo maana yake unakuwa umeona penye kamshahara kakubwa unakafuata tu.
 
Poa tu; tumetesa kwenye 100 za chini... orodha ikiwekwa upside down; lazima Top 100 zote tuwe sisi!!!
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Nilipokua alevel wakapandisha madalaja D ikaanzia 50 lengo lao likiwa kupandisha ufaulu....... Nikawaza kwa mtu mwenye akili timamu angeongeza walimu kwanza angeongeza upatikanaji wa vitabu vya mitaala ni aibu hii nchi haina vitabu vya kiada kwa masomo ya sayansi alevel fizikia kemia na baiolojia hakuna kabisa baada ya kufanya hivyo ndo apandishe ufaulu...... Asa mtu unakulupuka unapandisha ufaulu me shuleni nina mwl mmoja wa fizikia form five na six tunamtegemea huyo vitabu ni galama chands ina pop up kene 35k unataka nipate 50 sa cjuh nijifundishe au hiyo maksi inatoka mbinguni?????
 
mtoa post mpumbav kama wapumbav wengne, u advance utajuaje matatizo ya walimu wako,au we2 raha yako kufundishwa bila kujua maslah ya walimu wako? hv we2 kama unaakil timamu unaweza soma bila kula? kwa taarifa yako hata hio idadi kubwa sana haikupaswa kuwa hvyo n badala yake shule zote mia moja zilipaswa kuwa za shule binafsi kulingana na mahtaj wanayoyapata watumish wa shule binafsi! serikal iko bize na kuhakik watumish hewa na kuwasahau walimu na kada nyingne,wacha waendelee kuhakik.
 
mtoa post mpumbavu kama wapumbav wengne! unapo toa post ya kuwalaum walimu ulipaswa kufanyia utafit yakinifu! usiwaze kupata we2 wakt walimu wanamazingira magum!
 
Mleta mada hujatafakari kwa mapana. Umesema shule uliyosoma wewe, halafu unaleta mada inayogusa taifa kwa ujumla.

Anyway, untaka walimu wafundishe vipi? Mnawapa motisha gani ili wapate hamu ya kufundisha? Fanya kazi kwa bidii ili mwanao umpeleke Private.
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Nimeipenda hiyo ya mwisho kuwa walimu hawana Morali. Unadhani kwanini hawana morali ya kufundisha mkuu?
 
Halafu kuna wapuuzi wanatetea serikari izipangie hizi shule zinavyoendeshwa kusudi tuwe taifa la wajinga.
 
Mishahara midogo na mtalalamika sana.Walimu hawathamaniwi kabisa,na mtapiga kelele sana
 
kama una haraka na nia unataka kuona matokeo ya shule za sekondari za serikali, usianzie juu, unatakiwa uanzie chini kupanda juu.
 
Wala si ajabu,ni kawaida ya shule au vyuo vikuu vya taasisi za watu binafsi katika nchi za magharibi kufanya bora kuliko public schools and colleges.Kwetu wameanza na shule ili siku za mbeleni hata colleges zitaipiku public colleges.
 
Ndugu Dudus tatizo lingekuwa ni lugha pekee basi wanafunzi wote wangekuwa wanapata "A" kwenye Kiswahili. Nikitazama matokeo hata Kiswahili ni majanga. Tatizo ni kubwa zaidi ya lugha.
mkuu Tata nakubaliana na wewe ndio maana Dudus amesema 25% au zaidi kidogo hivyo asilimia zilizobaki ni mfano mishahara,posho,malimbikizo,vitendea kazi ,uhaba wa waalimu n.k
 
Madawa ya kulevya yanaweza kuwa chanzo cha kuanguka kwa ufaulu Dar es salaam
 
Tatizo ni "Kithungu" masomo yanafundishwa Kimalikia wakati walimu na wanafunzi hawaijui hiyo lugha!?
What do we expect?

Nashauri Shule zote (Form 1-6) waweke wakalimani
Hata hao wanaofundisha private nao wanatumia kizungu hicho hicho.... ila private wanafaulu, Gvt wanafeli. Ishu kubwa hapa ni motisha kwa waalimu...
 
Shule za serikali nyingi zinatiisha huruma. Huwa najiuliza unakimbiliaje kufuta ada hali ya kuwa miundombinu ya shule ni duni sana tena saana!!
Maabara na vifaa shida, maktaba ni tabu,madawati tatizo,madarasa hayatoshi na hayajakamilika, umeme na maji utata,vyoo Vya mashaka,chakula hakuna,michezo na vifaa vyake bado...yaani list hainamwisho!! Kubwa zaidi walimu wananyimwa stahili zao,wengi wamejaa madeni wanaishi kwenye vivyumba kwa shida na hata mlo niwatabu. Haya mambo yanahitaji kiongozi makini asiyejali sifa binafsi!! Unahangaikia madege huku shule hazina vyakula,vyoo wala madawati?? Vitimbi
 
Wakulaumiwa ni hii Serikali ambayo inadhoofidha elimu nchini na kuwanyanyasa walimu kwa kila namna.

katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
 
serikali kuwadharau walimu unategemea nini? na bado
 
wanafunzi wengi wanaosoma shule za serikali ni wale ambao baba zao au mama zao wameshindwa kuwapeleka shule za kulipia lakini kila mwenye mtoto ambae anajiweza kielimu mzazi wake anajitahidi kumpeleka shule za kulipia
 
Back
Top Bottom