unijui sikujui bora ukae kimya
Wala sihitaji nikujuwe,nimejadili hoja yako,ingependeza kama ungetumia hiyo Elimu unayojisifu kuwa nayo kutoa mchango wako wa nini kifanyike ili Ku "rescue situations",huo ndiyo usomi,kuja na takwimu tu kuwa kati ya Shule 100 bora Shule za serikali ni 7 tu haiwezi kuleta tija katika kizazi hiki chenye wazazi wanaohimizwa wafyatue watoto tu kwa sababu Elimu ni bure.
Elimu ni moja ya hitaji la msingi la mtoto,kama yalivyo mahitaji mengine,msimamizi mkuu wa Elimu ya mtoto ni Mzazi mwenyewe.Kama Mzazi hatawekeza muda wake katika kufuatilia maendeleo ya mwanaye darasani,akaishia kumtelekeza mwanaye kwa walimu na yeye asishiriki kwa namna yeyote ile kufuatilia na kuwezesha ufanisi wa mtoto wake darasani,Mwalimu hata afanyeje,bado mwanafunzi husika hawezi kuleta matokeo bora.
Shule kama Kidete Sec.hata upeleke walimu magwiji wa taaluma ya ualimu,bado haiwezi kufanya vizuri.Haiwezekani Shule yenye watoto wahuni,waliokosa malezi bora ya wazazi,watoto wanaozurula katika fukwe za bahari pale Mjimwema badala ya kuwa darasani,watoto wanaojificha kwenye vichaka vilivyoko pembezoni mwa bahari na kufanya uchafu,kisha wanadandia malori ya mchanga/kokoto na kurudi kwao uwategemee wafanye vizuri darasani.
Wengi wa wanafunzi tulionao darasani siku hizi hawana sifa stahiki za kuwepo darasani,wamefika hapo kwa msaada wa mfumo mbovu wa Mitihani yetu ya darasa la VII,tangu tulipoamua kuifanya Mitihani ya VII iwe ya kuchagua,tuliua vipaji vya watoto wetu na kuasisi Taifa lisilokuwa na uwezo wa kutumia vipawa katika kufikiri,tukazalisha "kizazi cha kubet", sasa watoto waliochaguliwa kujiunga sekondari kupitia Mitihani ya " kubet"(multiple choice),unatarajia waweje darasani?
Haiwezekani serikali ihamishe Attendance registers za Shule ya msingi Maweni,Mjimwema,Ungindoni,Kibugumo,Mikwambe na Mizimbini na kuzihamishia Kidete Sekondari,kisha utarajie watoto hao waliopelekwa Kidete bila sifa stahiki waweze kufanya vizuri.
Tuache kucheza na Elimu ya watoto wetu kwa kutafuta umaarufu wa kisiasa,tuwaache wataalamu waziendeshe Shule kitaalamu,serikali ijikite katika kuziwezesha Shule kwa kuzipatia vitendea Kazi na walimu wa kutosha,iboreshe mazingira ya upatikanaji wa Elimu,na iache kuhamisha Attendance registers toka Shule za msingi na kuzipeleka sekondari,katika hali ya kawaida haiwezekani darasa zima likafaulu,wapewe nafasi wale tu wenye uwezo,tujikite zaidi katika ubora badala ya wingi,tukifanya hivyo serikali itakuwa na wanafunzi wachache wenye uwezo mzuri,na itawasomesha vizuri,vinginevyo tukiendekeza siasa katika mambo ya msingi,tutaendelea kufanya vibaya kila uchwao.