katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
unijui sikujui bora ukae kimya
Sasa wewe umeleta hoja ijadiliwe, kabla ya kuanza mjadala member mwenzio kakuambia umeleta hoja ambayo inaning'inia mno, kitu ambacho ni cha kweli na wala siyo tusi hata kidogo...
Binafsi naiona hoja yako ni nzuri sana kwa mjadala, lakini ni kweli kabisa kwa upande mmoja ina mapungufu ya kimantiki ktk uwasilishaji wake.
Umeshangaa vyema kuwa ktk shule bora 100 kitaifa ni kwa nini za serikali/umma ziwe 7 kati ya hizo na zinazobaki zote 93 zitoke ktk sekta binafsi...
Ukaanza kulivuruga bandiko lako wewe mwenyewe kwa kutoa hitimisho kuwa, sababu ni shule za serikali/umma kuwa
na WALIMU WAVIVU (nadhani ulimaanisha, wasiojituma ktk kazi yao) na WALIMU WAKUU/WAKUU WA SHULE wasio na uwezo bila hata kufafanua uwezo gani kwa sbb walimu walioko ktk shule za binafsi na zile za serikali wote wamezalishwa na vyuo hivi hivi vilivyopo nchini....
Hiki ndicho kinachokufanya ushambuliwe na wachangiaji wengi na wewe kukosa uvumilivu na kutoa majibu ya mkato na kuudhi ambayo yatakufanya usipate michango ya maana ktk hoja nzuri sana uliyoianzisha...
Mwisho basi, ingekuwa vyema sana kama hoja yako usingeitolea hitimisho wewe mwenyewe kwa sbb kwa vyovyote vile hizo sababu mbili za UVIVU WA WALIMU na UWEZO MDOGO WA W/WAKUU haziwezi kuwa sababu pekee za shule za serikali/umma kuburuzwa na shule za binafsi japo zaweza kuwa moja ya sababu nyingi ambazo wana JF wenzako wanaweza kusaidia kuzitoa....
Kumbuka kuwa humu ndani ya jukwaa hili wapo wataalamu wa mambo ya elimu, walimu, wachambuzi wa sera na kila aina ya wataalamu wa fani mbalimbali ambapo ukiweka wazo ama hoja yako vizuri, utanufaika kupata michango mizuri sana na kuwa shule kwako na sisi wengine pia!!
Haikuwa busara kumjibu member mwenzio kama ulivyojibu hapo kwa sababu, vyovyote iwavyo hakuna mtu mwenye shida ya kumjua ama kutomjua mwenzie humu, na akikaa kimya kama ulivyomwambia hapo juu na wengine wakakaa kimya, lengo lako la kuanzisha mjadala linakuwa halina maana. Ni bora wewe ndiye ungekaa kimya na wazo lako!!