Katika shule bora 100, shule za seriakli ni 7 tu

Katika shule bora 100, shule za seriakli ni 7 tu

This is a very serious issue; lina-contribute more than 25% ya matokeo mabovu shule za Serikali. Mtoto aliyeanzia English medium tangu vidudu huwezi kumfananisha na aliyetokea Kiswahili medium wanapoingia F.I. Nina kibinti changu kiko Class V; hizo nondo wanazopewa ni balaa; kuanzia Mathematics, English, etc. For sure it is great; acha tu watupige hizo ada ni halali yao na naomba Serikali isiingilie kabisa hili suala kwa shule binafsi kama walivyotaka kufanya. Waboreshe zao tutapeleka watoto huko.
Kama tatizo ni lugha tungetegemea somo la kiswahili liongoze kwa ufaulu!? Is that the case?
 
Kama tatizo ni lugha tungetegemea somo la kiswahili liongoze kwa ufaulu!? Is that the case?
Exactly; that is the case. Matokeo ya 2016 yanaonesha Kiswahili ndilo somo lililoongoza kwa ufaulu; the last likiwa Mathematics kama kawaida.
 
Kuboresha elimu ni kumjali mwalimu kwanza kwa mshahara mzuri unaokidhi mahitaji ya msingi. Hii ni kwa waalimu wote kuanzia shule za msingi mpaka kwa wale wa vyuo vya ualimu na wakaguzi wote. Baada ya hapo ni kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia. Ukianza kuboresha mazingira ya kufundishia na kujifunzia kama vile madawati nk hakuwezi kuleta mabadiliko chanya!
Ukiboresha maslahi ya waalimu kwanza wanapata heshima katika jamii kuliko ilivyosasa!
Hata kuchumbia ni mbinde! Mkigongana kwa binti vijana wawili, mmoja mwalimu wa sekondari mwenye shahada mwingine ni MHASIBU mwenye shahada, mwalimu anapigwa chini fasta!
 
Kwa hiyo elimu bora ni zaidi ya madawati na elimu bure?! Taaluma ya ualimu na maslahi ya walimu kwa upana wake viangaliwe pia, kuendelea kuwatazama walimu kama vitendea kazi vya kushinda uchaguzi na kuvitelekeza ni kiama cha taifa!
 
Tatizo ni "Kithungu" masomo yanafundishwa Kimalikia wakati walimu na wanafunzi hawaijui hiyo lugha!?
What do we expect?

Nashauri Shule zote (Form 1-6) waweke wakalimani
Shule nyingi zimefaulu kwa kishindo kwa kiwango cha F katika somo la KISWAHILI .Je nacho chafundishwa kwa kithungu ?
 
Unajitambulisha kuwa "advanced level" halafu unaleta bandiko na kuliacha linaning'inia kama popo bila hata kutoa "the way forward" ya kukabiliana na mtanziko huu wa kielimu tulionao?

Utakuwa ni form six failure toka "kidete secondary" pale Mjimwema Wilaya ya Kigamboni au Somangila Day ya huko huko Kigamboni.
huyu itakuwa wa nyeburu secondary
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Yafanyike haya kama hatutaona mabadiliko:
-Mishahara ya walimu iongezwe
-Mazingira ya kufundisha yaboreshwe...mfano vifaa vya kufundishia vitabu...maabara na mfunzo kwa vitendo yawepo
-Walimu wapewe ration kama wanavyopewa maaskari(hapa ndio mtakuwa mmewaweza waalimu walai...na kufanya fani ivutie watu bora zaidi badala ya sasa ilivyo kimbilio la wakosaji.
-Walimu wajengewe nyumba za kulala za kutosha.
-Michezo iboreshwe mashuleni..
-Kila wilaya kama kuna uwezekano ziwepo shule mbili ya wasichana na wavulana za mifano ambazo zitakuwa na vifaa vyote na Walimu na kupangiwa wanafunzi waliofaulu vizuri ngazi ya wilaya au hata moja kwa kuanzia
-Mtihani wa mchujo wa kidato cha pili upewe msisitizo wa hali ya juu na wanafunzi wasipitishwe,wafaulu kweli kuendelea na masomo ya kidato cha tatu...Mimi kwa maoni yangu naona ni vizuri hata ule wastani ukaongezwa kidogo mpaka thelathini
-Waalimu wawe na warsha na semina za mara kwa mara za ndani na nje ili kuboresha ufundishaji wao na kuwapa Walimu hamasa ya kufundisha na kuipenda kazi yao..
-Wanasiasa wasiingilie hii fani ...ufaulu unapungua kwasababu ya siasa...na wakati mwingine wanasiasa na serikali inawatumia Walimu pale wanapotaka kutekeleza majukumu yao na wakishafanikiwa wanawasahau..
-Serikali iwalipe Walimu madeni yao na hela zao za kupanda madaraja na wale wanaostahili kupanda madaraja wapande kwa wakati....wengi wanafanya kazi kishingo upande,wakiwa na manung'uniko mengi...wapi ufanisi hapo sasa....
 
Jiulize ni kwa nini shule za binafsi zinafanya vizuri kuliko za serikali? kama kweli unataka kuja na kitu ambacho kitasaidia elimu ya nchi hii hasa katika shule za serikali fanya utafiti
 
Binafsi nilitegemea kuona ya kwamba utafiti unaonyesha ya kuwa shule za serikali hazifanyi vizuri kwa sababu 1, 2, 3 n,k na siyo walimu kulala n,k. Kufanya hivyo kunaweza kumsaidia waziri wa elimu kufanyia kazi utafiti wako na hivyo kusaidia kuimarisha shule zetu za serikali
 
Kuna mambo mengi sana yanayofanya shule za serikali zisifanye vizuri. Na mjadala wa kuzifanya ziwe shindani kama za binafsi hauwezi kufikia mwafaka bila baadhi ya watoto na wazazi kuhathirika kwa namna moja au nyingine.
 
Mwalimu private analipwa m1.3\5 na full resources alaf inalingana na mwalimu wa serikali wa laki5 matatizo lukuki
 
Kuna mambo mengi sana yanayofanya shule za serikali zisifanye vizuri. Na mjadala wa kuzifanya ziwe shindani kama za binafsi hauwezi kufikia mwafaka bila baadhi ya watoto na wazazi kuhathirika kwa namna moja au nyingine.
Kunawatu wanasema kwamba sababu kubwa ya shule za serekali kutokufanya vizuri ni.
  1. Walimu hawaandai maandalio ya Kazi.
  2. Walimu waserikalin wengi wao matokeo yao ya shule kuanzia sekondari hadi chuo ni walifeli kwhyo wanashindwa kulimudu somo.
  3. Wakuu wa shule hizo wengiwao wameteuliwa kwakujuana na si kwa maadili au sifa za uchapa Kazi.
 
Motisha! MOTISHA jamani ni kila kitu kwenye elimu! Wizara ijaribu kutoa dozi ya motisha kwa Walimu kwa mwaka mmoja tu halafu tuangalie matokeo yake!!
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Umesema hawana morali halafu unasema ni wavivu. Kipi ni kipi!!!
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Walivyo wa ajabu suluhu la tatizo hili watazifungia za watu binafsi 93, ili 7 za serikali ziwe za kwanza.
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Nikatagemea ungezitaja hizo shule 7
 
katika shule mia bora za matokeo shule za serikali ni saba tu
Profesa Ndalichako walimu wa serikali wanalala sana Mimi advance nimesoma serikali walimu wengi wa serikali ni wavivu kufundisha na awana morali pia wakuu wa shule wanashindwa kuwasimamia walimu
Acha uchochezi serikali imeboresha elimu kwenye shule zake,hahahahahah!
 
Nashindwa kuelewa mwenzenu hii ni tungo tata kwangu naomba mnieleweshe zaidi
 
Back
Top Bottom