Course Coordinator
JF-Expert Member
- Jul 27, 2019
- 1,685
- 3,074
Haya mambo ya kuzushiana ugonjwa na vifo hayajaanza leo, yalikuwepo enzi na enzi. Kuzushiana vifo sio jambo geni katika Ulimwengu huu, kuna mlolongo wa matukio mengi ya watu mashuhuri na watu maarufu waliowahi kuzushiwa kuumwa au vifo.
Sababu mojawapo hutokana ama na siasa zenye chuki na uadui ama usiri wa taarifa pale ambapo wahusika wanaposhindwa kutoa taarifa sahihi kwa wakati.
Mfano wiki hizi mbili kumetokea taarifa kuwa MWENYEKITI WA CHADEMA NDUGU FREEMAN MBOWE na MKURUGENZI wa Habari na itikadi wa CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO(CHADEMA) kuwa wamefariki. Kwa vile ile ni taharuki na inagusa mioyo ya watu, wahusika walijitokeza na kuujulisha umma kuwa wao ni wazima wa afya.
Lakini hivi karibuni kumeibuka taarifa za alipo Rais wetu na afya yake ikoje, hizo tuziache.
Marehemu mzee Mkapa Rais wa awamu tatu nae alipata kuugua na kwenda kutibiwa nje, sasa chama chake cha Mapinduzi kilikataza serikali isitoe taarifa ya Mzee Mkapa kama ni mgonjwa hii ilipelekea taharuki kwa sababu ya usiri ule wa kuumwa kwake, hivyo wapinzani wakachukua advantage ile kuwa Mzee Mkapa amefariki.
Mzee Mkapa alitaka umma ujulishwe ila CCM chini ya Makamu Mwenyekiti Philip Mangula walikataa, kuzushiwa ugonjwa au kifo kunaweza tokana na sababu mbalimbali za kutaka ama kujitakia.
Tuwaombee wagonjwa wale wote wanaumwa na wale wasioumwa waendelee kupata afya njema.
Jumapili njema ya leo.
Sababu mojawapo hutokana ama na siasa zenye chuki na uadui ama usiri wa taarifa pale ambapo wahusika wanaposhindwa kutoa taarifa sahihi kwa wakati.
Mfano wiki hizi mbili kumetokea taarifa kuwa MWENYEKITI WA CHADEMA NDUGU FREEMAN MBOWE na MKURUGENZI wa Habari na itikadi wa CHAMA CHA DEMOKRASIA NA MAENDELEO(CHADEMA) kuwa wamefariki. Kwa vile ile ni taharuki na inagusa mioyo ya watu, wahusika walijitokeza na kuujulisha umma kuwa wao ni wazima wa afya.
Lakini hivi karibuni kumeibuka taarifa za alipo Rais wetu na afya yake ikoje, hizo tuziache.
Marehemu mzee Mkapa Rais wa awamu tatu nae alipata kuugua na kwenda kutibiwa nje, sasa chama chake cha Mapinduzi kilikataza serikali isitoe taarifa ya Mzee Mkapa kama ni mgonjwa hii ilipelekea taharuki kwa sababu ya usiri ule wa kuumwa kwake, hivyo wapinzani wakachukua advantage ile kuwa Mzee Mkapa amefariki.
Mzee Mkapa alitaka umma ujulishwe ila CCM chini ya Makamu Mwenyekiti Philip Mangula walikataa, kuzushiwa ugonjwa au kifo kunaweza tokana na sababu mbalimbali za kutaka ama kujitakia.
Jumapili njema ya leo.