warumi
R I P
- May 6, 2013
- 16,213
- 18,455
- Thread starter
- #61
GoodNafikiri kosa la Shetani siyo kumdanganya Eve/Hawa bali ni KUFICHUA SIRI ZA MUNGU KWA MWANADAMU. Jiulize kama kweli Adamu alikuwa na maisha ya milele kwanini Mungu apande mti wa Uzima? Apa inaonesha Adamu alipungukiwa vitu viwili ili awe kama Mungu, kwanza ni MAARIFA( Ujuzi wa mema na mabaya) pili ni MAISHA YA MILELE.
Aya mambo mawili ya utimilifu wa Adamu, Mungu aliyafanya fumbo ili Adamu hasiwe nayo ili awe tegemezi kwa bwana Mungu wake. Ili fumbo Mungu aliliweka kama tunda japo siyo tunda kama tunda! Na akamwambia Adamu hasiguse apo maana alijua Adam akifumbua ayo Mafumbo mawili basi hataweza tena kumdhibiti Adamu maana atakuwa na Utimilifu wote.
Kwahiyo shetani alichofanya ni kufichua siri ya Mungu kwa Adamu akiamini Adamu akitimilika basi atapata kiumbe mwingine wa kushirikiana naye kupambana na Utawala wa Mungu. Mungu kwa kutambua hila za Shetani akamfukuza Adamu kwenye ile Bustani ili hasile tunda la pili(kufungua code namba mbili) za kuishi milele.
Kwahiyo Shetani hajasema uongo ni ukweli japo ni ukweli ambao Mungu hakutaka ujulikane kwa Adamu.
Sent using Jamii Forums mobile app
Sent from my iPhone using JamiiForums
