Katika hili, namwamini Shetani

Mimi naombeni kuuliza swali:

Hivi kutoka kuumbwa kwa akina Adamu na Hawa, mpaka kula tunda na mwishowe kufukuzwa, ilipita miaka mingapi hapo!?

Na Je, walipokula tunda, wakafukuzwa siku hiyohiyo!?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sema wewe papa kasema nini. Halafu hiyo habari hajaandika FaizaFoxy hiyo ni BBC.

Wewe una hallucinate nakushauri kaonane na Psychiatric haraka sana.
 
Kwani mama, Adamu alimaliza siku baada ya kula tunda alilokatazwa?
Adamu hakufikisha miaka 1000 ambayo ndo siku moja kwa Mungu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ee3e.:


Sent from my iPhone using JamiiForums
 

Mbona kila kitu nimeeleza, jaribu kutuliza akili yako na andika kwa paragraph mkuu.

Mungu yupo kama binadamu , siku zote binadamu anataka ufanikiwe ila sio kufanikiwa kumzidi, huyo Ndo Mungu , na kumbuka alisema yeye ni Mungu mwenye wivu , hakati tumwabudu Miungu yeyote zaidi yake , apo inamaanisha kuna miungu mingine powerful kumzidi


Aliwafukuza adam na hawa bustanini kwa kuhofia watakula mti wa uzima na kuishi milele, Sasa hapo ndo ujiulize why Mungu hakutaka tuishi milele? Na anasema anatupenda


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Kupata ufahamu wa kujua mema na mabaya hiyo haiwezi kufanya uwe sawa na Mungu hapo inadhibitisha hata shetani mwenyewe alikua mwongo kwa kuwaambia wakila wangekua sawa na Mungu.

Mwanzo 3:22 inasema " bwana Mungu akasema, basi mtu huyu amekua kama sisi kwa kujua mema na mabaya, na Sasa asije kunyoosha mkono wake akatwaa matunda ya mti wa uzima, akala akaishi milele"

Umeona Sasa hofu ya Mungu aliyokua nayo kwa binadamu baada ya kula tunda?, na kwa nini aliwafukuza akina adam bustan ya Eden kama wangekua hawana madhara kwke? Yeye c Ndo aliyewaumba


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Mkuu jibu maswali yangu niliyokuuliza,kuna vitu naona unajichanganya mwenyewe,Mungu aliposema yeye ni Mungu mwenye wivu ni kweli imeandikwa hivyo,wewe unatoa wapi maelezo kwamba kama ni mwenye wivu maana yake anaonea wivu miungu wengine wenye nguvu kuliko yeye?Wewe ni wapi kwenye biblia imeandikwa hao miungu wengine wana nguvu kuliko yeye?Hapo ndipo unakua unakosea .
Unaelewa maana ya Mungu Mwenyezi?Almighty God?Kasome biblia vizuri kisha jitahidi kuelewa majina aliyokuwa anayatumia Mungu yana maana gani.Kumbuka maswali yangu kwako yajibu mkuu.Mwanadamu ameumbwa kwa mfano wa Mungu hii haimanishi mwanadamu analingana kila kitu na Mungu,kasome biblia yako kwanini anasema njia zake si kama njia za wanadamu na akili ya juu ya mwanadamu haifikii hata upumbavu wa Mungu ingawa Mungu si mpumbavu hapa anajaribu kuelezea kuna knowledge gap kubwa sana kati ya Mungu na wanadamu.Sasa wewe naona unasoma biblia kweli ila kuna kitu kimezuiwa kwako na ndiyo maanda nikauuliza wewe ni devoted christian au unasoma biblia kwa sababu zako fulanifulani?

Mpango wa Mungu ni tuishi milele na kwa taarifa yako unaposema kifo kuna vifo vya aina mbili kuna kifo cha mwili kwa maana ya mwili kutengana na nafsi na mwili hiki tulichokizoea na kuna kifo cha nafsi na Roho ambayo ni kutupwa katika ziwa la moto.
Ndiyo maana Mungu akasema msimwogope awezaye kuangamiza mwilil tu bali mwogopeni awezaye kuangamiza mwili pamoja na Roho,Mungu pekee anaweza akaangamiza mwili na Roho wengine ni mwili tu.
Mkuu piamkumbuka Mungu wa kwenye biblia ni Mungu wa miungu,hapa sijui kama unaelewa,ni kweli anatambua uwepo wa miungu wengine lakini hawana uwezo kama yeye na wala hao miungu wengine hawakuumba bali yeye ndiye aliyetuumba.Sasa anakuwa na wivu akiona mwanadamu anaabudu miungu wengine na kumwacha yeye.
Kama unataka kuishi milele mbona solution yake ipo ni kumpokea Yesu kufanyika kuwa Bwana na mwokozi wako,ishi maisha matakatifu kama ambavyo biblia inatufundisha utaulithi uzima wa milele.

Unajua sikuelewi kama kweli unasoma biblia kwa nia ya kujifunza au kuikosoa injili,Yesu alipokutana na mwanamke msamaria alimwambia yeye ni maji ya uzima.Kifo cha kwanza kinatokana na dhambi ya Adam na Hawa,lakini Mungu aliamua kumtoa mwanaye wa pekee ili kila amwaminiye asipotee bali awe na uzima wa milele.Haya maandiko hujawahi kukutana nayo au ni ubishi tu mkuu?
Mimi nikushauri endelea kusoma biblia,ukitaka maelezo just pm me nitakusaidia kuliko kuja hapa ,kuandika vitu ambavyo vitawapotosha wengine wasiosoma maandiko na mwishoni uwe na cha kujibu mbele ya Jehova.Sikuzuii kuandika ila nakutahadhalisha kuna adhabu kubwa kwa walimu,unapokuwa unawafundisha watu make sure una uhakika na unachoandika.
Mambo haya tunayoyaandika na kuyaongea yatatumika juu yetu kama ushahidi mbele za Mungu hata kama unatumia jina ambalo si lako lakini Mungu ananijua mimi ni nani na wewe ni nani na nitatoa hesabu ya yote ninayoyafanya kwenye mitandao.

Waswahili wanasema ukitaka kujua utamu wa ngoma ingia ucheze,tumeona matendo makuu ya Bwana,tumeona mapepo yakiomba yapelekwe kwa miungu wengine huko hakuna moto ila huku kwetu tukiliita jina la Yesu moto unawaka.Sasa huwezi kuwa nje kisha ukadai unayajua sana ya ndani,ingia full na si mguu nje mguu ndani,you will never know the full picture.
Mkuu nilitumia muda sana kufuatilia haya mambo njoo pm ukitaka kujua zaidi nitakuambia na vitu uvifuatilie mwenyewe katika dunia hii ndiyo utajua Jehova ni Mungu mwenye uweza na nguvu wala hakuna mwingine kama yeye.
Shida ya siku hizi za mwisho watu wanataka watumie akili zao kureason mambo ya Mungu ,huwezi kuujua ukweli utapotea.
Kasome kumbukumbu la torati29:29.Kuna mambo Mungu ameyafunua kwetu na mengine hajayafunua kwetu,kuwa makini hapo shetani hata leo ameendelea kuwakamata watu kwa kuwaletea elimu mpya,nao wanaona ni uhuru waomkujifunza hayo mambo bila kujali chanzo chake ni nini Mungu au shetani.
 
Mkuu wewe ni mpotoshaji,kama wale jamaa tabia zao husoma maandiko hawayamalizii,umesema Mwanzo 3:22 mimi nakuomba uendelee usome mpaka Mwanzo 3:24
"Na basi akamfukuza huyo mtu, akaweka upande wa mashariki wa bustani ya Edeni+ makerubi+ na upanga unaowaka ambao ulikuwa unajizungusha-zungusha ili kuilinda njia ya kwenda kwenye ule mti wa uzima. "
Mungu alimwambia Adam hakika siku utakayokula tunda utakufa,kwa hiyo Neno litokalo kinywani mwa Bwana lazima litimie,hivyo angewaacha kwenye bustani wangekula tunda la uzima na kuishi milele.Na sababu aliyowafukuza ni ili wasiweze kula tunda la uzima wakaishi milele kitu ambacho kingefanya kile alichowaambia mwanzo kisitimie ndiyomaana aliweka malaika kuilinda njia ya kwenda kwenye mti wa uzima,Mungu huliangalia Neno lake apate kulitimiza.

Nakuuliza tena wewe ni Mkristo?Je ni msom,aji wa biblia mara kwa mara?Je umejazwa Roho Mtakatifu?
 
Umeacha habari za umbea?
 
Lakini ukiangalia vizuri kifo kililazimika kuwepo, jiulize je kisingekuwepo wengine wangezaliwaje? Na dunia hii sasa hivi tungekuaje?
 
Nafikiri kosa la Shetani siyo kumdanganya Eve/Hawa bali ni KUFICHUA SIRI ZA MUNGU KWA MWANADAMU. Jiulize kama kweli Adamu alikuwa na maisha ya milele kwanini Mungu apande mti wa Uzima? Apa inaonesha Adamu alipungukiwa vitu viwili ili awe kama Mungu, kwanza ni MAARIFA( Ujuzi wa mema na mabaya) pili ni MAISHA YA MILELE.

Aya mambo mawili ya utimilifu wa Adamu, Mungu aliyafanya fumbo ili Adamu hasiwe nayo ili awe tegemezi kwa bwana Mungu wake. Ili fumbo Mungu aliliweka kama tunda japo siyo tunda kama tunda! Na akamwambia Adamu hasiguse apo maana alijua Adam akifumbua ayo Mafumbo mawili basi hataweza tena kumdhibiti Adamu maana atakuwa na Utimilifu wote.

Kwahiyo shetani alichofanya ni kufichua siri ya Mungu kwa Adamu akiamini Adamu akitimilika basi atapata kiumbe mwingine wa kushirikiana naye kupambana na Utawala wa Mungu. Mungu kwa kutambua hila za Shetani akamfukuza Adamu kwenye ile Bustani ili hasile tunda la pili(kufungua code namba mbili) za kuishi milele.

Kwahiyo Shetani hajasema uongo ni ukweli japo ni ukweli ambao Mungu hakutaka ujulikane kwa Adamu.

Sent using Jamii Forums mobile app
 

Sz


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
KATIKA HILI NAMUAMINI SHETANI.

ALAFU UNAKUTA ANAANZA NA

Kwanza kabisa nimshukuru Mungu kwa huruma na neema yake kwa kunifanya mpaka dakika hii naendelea kupumua na kuwa mzima wa afya. Pia kwa mamlaka aliyotupa viumbe wake ya kutawala samaki wa Baharini na ndege wa angani , wanyama na kwa kutuumba kwa mfano wake. MWANZO1:26. Hakika huu ni upendo wa ajabu sana , sifa na utukufu viende kwake.

UWAGA SISOMI KABISA!![emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 

Zsz0zspzzz3ps../.pzi//s::


Sent from my iPhone using JamiiForums
 

Well said mkuu , safi sana umenisoma


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Naona kuna haja ya somo la theolojia kuwa mandatory kwa wakristo wote hivi mpaka leo kuna watu wanaamini tunda lilioliwa ni Tunda as Tunda??

Jamani lugha iliyotumika hapa ni figurative yaani lugha ya picha ila haina maana ni mti kma hii miti yetu au tunda kama haya matunda yetu kama watu mnadai hii miti ya Eden ni miti ya kawaida naomba mnielezee hii sura

Ezekiel 31:9
9 Nalimfanya kuwa mzuri kwa wingi wa matawi yake; hata miti yote ya EDEN, iliyokuwa ndani ya bustani ya Mungu, ilimwonea wivu.


18 Umefanana na nani, hivi katika utukufu na ukuu, kati ya miti ya EDEN? Lakini utashushwa pamoja na miti ya EDEN, hata pande za chini za nchi; utalala kati ya hao wasiotahiriwa; pamoja na hao waliouawa kwa upanga.

SWALI
Je ni miti gani ya Eden imepelekwa kuzimu wakati kuzimu ni kwa ajili ya shetani na wafuasi wake??

Je miti inaweza kuoneana wivu kama wanadamu?

Je miti inaweza kuhukumiwa na Mungu kisa inaKIBURI yaani miti ina character za kibinadamu?

Biblia ni figurative otherwise mkisema mti ni mti wa kawaida basi mnisaidie hayo maswali angu hapo juu!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…