Katibu wa CHADEMA Rungwe, Award Karonga akamatwa tuhuma za uchochezi

Katibu wa CHADEMA Rungwe, Award Karonga akamatwa tuhuma za uchochezi

Waufukweni

JF-Expert Member
Joined
May 16, 2024
Posts
4,393
Reaction score
14,500
Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linamshikilia Award Karonga, ambaye ni kiongozi mwandamizi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), kwa tuhuma za uchochezi na makosa mengine ya kijinai.

1769761875847.png
Award Karonga, ambaye ni mkazi wa Katumba, anashikilia nyadhifa za Katibu wa CHADEMA Wilaya ya Rungwe na Makamu Mwenyekiti wa Hamasa Taifa wa chama hicho, kwa mujibu wa taarifa rasmi iliyotolewa leo, Januari 30, 2026, na Ofisi ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya.

1769773181650.png
Kiongozi huyo ambaye baadhi ya viongozi wa CHADEMA kupitia mitandao mbalimbali ya kijamii wamemtaja pia kama mlinzi wa Tundu Lissu, Mwenyekiti wa CHADEMA taifa aliyeko gerezani kwa tuhuma za uhaini, alikamatwa, Januari 29, 2026, majira ya saa nne asubuhi katika maeneo ya Mtaa wa Katumba, Kata ya Ibighi, Tukuyu wilayani Rungwe.

Jeshi la Polisi limebainisha kuwa kukamatwa kwa Karonga kumetokana na tuhuma mbalimbali za kijinai zinazomkabili, ikiwemo uchochezi. Taarifa hiyo haikufafanua kwa kina matukio mahususi ya uchochezi anayotuhumiwa kwayo, lakini imesisitiza kuwa makosa hayo ni ya asili ya kijinai.

“Upelelezi unakamilishwa ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake”, imeeleza taarifa hiyo iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Benjamin Kuzaga.

==

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mbeya linapenda kujulisha kuwa limemkamata na linamshikilia Award Karonga, Mkazi wa Katumba ambaye ni Katibu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo [CHADEMA] Wilaya ya Rungwe na pia ni Makamu Mwenyekiti Hamasa Taifa wa chama hicho.

Alikamatwa Januari 29, 2026 saa 4 asubuhi maeneo ya Mtaa wa Katumba, Kata ya Ibighi Tukuyu Wilaya ya Rungwe kwa tuhuma mbalimbali za kijinai ikiwepo uchochezi.

Upelelezi unakamilishwa ili hatua zaidi za kisheria ziweze kuchukuliwa dhidi yake.

ASHIKILIWA KWA TUHUMA ZA UCHOCHEZI MBEYA.webp
 
Wameshakana kumshikilia! Haya majitu ni majinga mno,leo unasema ndiyo,kesho unasema siyo, au wameshammaliza? Just curious.
 
Daah jamaa wa Mbeya Mjini huyu anapatika huko Rungwe sasa hivi aisee Nchi ngumu hiyo wanauana kisa madaraka hata hao wanaokamatwa hawana madhara yeyote basi tu usumbufu wa kijinga jinga kwa sababu ya kukosa shule.
 
Back
Top Bottom