Lucas Mwashambwa
JF-Expert Member
- Jul 28, 2022
- 36,349
- 23,757
Ndugu zangu Watanzania,
Unaweza kuniita majina yote mabaya ,unaweza nitukana kwa matusi yoyote yale utakayo,unaweza niita lichawa au likupe ,unaweza nitemea hata mate,unaweza kunichukia kuliko hata shetani .
Lakini pamoja na hayo yoote napenda kuwaambieni ukweli mchungu kabisa ambao pengine msingependa kuusikia wala kuukubali wala kuambiwa. Napenda kuwaambieni ya Kuwa suala la katiba mpya siyo kipaombele cha mamilioni ya watanzania, siyo kiu wala hitaji la msingi la watanzania.
Nenda kwa vijana waliomaliza vyuo vikuu na katika ngazi tofauti tofauti za Elimu,Nenda kwa watumishi wa Umma au wakulima au akina mama sokoni au vijana wa bodaboda vilingeni au wabeba mizigo stendi au maafisa usafirishaji barabarani au wanafunzi waliohitimu kidato cha sita au polisi au wanajeshi makambini.
Amini amini nawaambieni ndugu zangu Watanzania kwamba makundi yoote hayo na mengine mengi hakuna kundi litakuambia kuwa kipaombele chake au hitaji lake au kiu yake ni kupata katiba mpya. Hakuna atakaye kuambia jambo hilo. Sana sana utaambiwa na vijana juu ya kiu yao kubwa ya kupata ajira serikalini ili walitumikie Taifa lao kwa ujuzi walionao na walioupata.
Wakulima watakwambia wana tamani kuona serikali inaendelea kutoa ruzuku kwenye pembejeo kama vile mbolea za ruzuku pamoja na bei nzuri kwa mazao yao na soko la uhakika . Wafanyabiashara watakwambia wanatamani kuona makadirio ya kodi yenye kuendana na uhalisia ,mazingira mazuri ya kibiashara,sera na sheria nzuri zenye kuwajali na kuwasaidia wazawa katika uwekezaji na biashara kubwakubwa ,kupata fursa za mikopo ya riba nafuu na mengine ya aina hiyo.
Ukija mitaani utaambiwa habari za fursa za Elimu kwa vijana ,kupatiwa mikopo kwa wote wenye sifa kupata Elimu ya juu. Ukienda kwa watumishi wa umma utasikia habari za kuboreshewa maslahi yao ,kupandishwa madaraja kazini na kulipwa stahiki zao,kupewa nafasi za kujiendeleza kielimu na kuongeza ujuzi ,kupewa motisha mbalimbali kulingana na mazingira ya kazi, kuboreshewa mazingira ya kazi ikiwepo kujengewa makazi yenye hazi na staha na kulipwa viinua mgongo vyao kwa wakati.
Ukienda kwa askari wetu wavuni vya ulinzi na usalama utaambiwa habari za maslahi yao ,kuboreshewa mazingira ya kazi kwa kujengewa nyumba nzuri ,kupewa vifaa vya kisasa kwa ajili ya kukabiliana na maadui na majambazi,kulipwa posho na marupurupu mbalimbali kulingana na vitengo vyao na majukumu yao ya kazi na utayari wao.kupewa bima kubwa kubwa ili waweze kupata matibabu bora na ya hadhi ya juu wapatapo majeraha wawapo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kikazi na kioparesheni.
Ukienda kwa akina mama magengeni na sokoni utaambiwa habari za kupewa mikopo ya riba nafuu ili waepukane na mikopo kausha Damu. Ukienda kwa bodaboda utaambiwa habari za kusaidiwa kupata Bila za afya ili ziwasaidie wakipata majeraha au ajali ,kukopeshwa kupitia vikundi vyao na kuepukana na mikopo yenye riba kubwa na kuingia katika mtego wa madeni.
Habari za wananchi mitaani ni juu ya Maisha yao na namna ya kuyaboresha na kuyainua kupitia shughuli zao za kila siku, ni juu ya sera ,sheria , mikakati na mipango ya serikali kugusa shuguli zao na kuzipa nuru na matumaini ya kukua kila zianzishwapo. Ni juu ya huduma za kijamii kusogezwa karibu yao na kutolewa kwa ubora wa hali ya juu bila ubaguzi wala ukiritimba . Ni juu ya usawa wa fursa zipatikanazo katika maeneo yao,ni juu ya kuwashika mikono na kuwainua.ni juu ya kuwakwamua kiuchumi kupitia sera na sheria.
Hakuna Bibi utakayemkuta au kumsikia huko kijijini akizungumzia habari za katiba mpya au mahitaji ya katiba. Ndio maana leo hii mwanasiasa akisimama jukwaani na kuanza kuzungumza habari za katiba mpya kama kipaombele chake anakuwa anaonekana kama mtu anayewapotezea muda tu watu,anakuwa ni kama mtu mwenye kujadili habari za tumbo lake na maslahi yake binafsi.
Ndio maana hata leo uwaambie Watanzania kwamba hushiriki uchaguzi mpaka ipatikane katiba mpya unakuwa unajipotezea muda wako tu,unakuwa unampigia mbuzi gitaa tu. Watanzania wanaangalia zaidi yawahusuyo na kugusa Maisha yao kama nilivyoeleza hapo juu. Kwa hiyo asijetokea mtu au mwanasiasa akasema anawapigania watanzania kwa kutaka katiba mpya.
Kwa hakika atakuwa anajidaganya Mwenyewe na wala hatujamtuma kufanya kazi hiyo. Na wala siyo mahitaji yetu kwa sasa. Mahitaji yetu ya muhimu na msingi watanzania nimeshaeleza japo kwakifupi na hayo ndiyo ambayo yamekuwa yakitekelezwa na serikali ya Rais Samia usiku na mchana,ndio yamekuwa kipaombele cha serikali ya Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
Ndio Maana ya kuendelea kuungwa mkono na kupendwa na watanzania wote kutokana na kugusa Maisha yao. Kama huamini kuwa katiba mpya siyo kipaombele chetu watanzania jaribu uitishe hata maandamano leo hii uone kama kuna mtu atatokea barabarani kuandamana kuunga mkono. Nakuhakikishieni ya kuwa hakuna atakaye andamanaa zaidi ya watu kuendelea na shughuli zao kama kawaida tu.
Nimewapeni ukweli huo. Mkubali au mkatae,Mnune au mvimbe mashavu yenu lakini huo ndio unabakia kuwa ukweli wenyewe.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Unaweza kuniita majina yote mabaya ,unaweza nitukana kwa matusi yoyote yale utakayo,unaweza niita lichawa au likupe ,unaweza nitemea hata mate,unaweza kunichukia kuliko hata shetani .
Lakini pamoja na hayo yoote napenda kuwaambieni ukweli mchungu kabisa ambao pengine msingependa kuusikia wala kuukubali wala kuambiwa. Napenda kuwaambieni ya Kuwa suala la katiba mpya siyo kipaombele cha mamilioni ya watanzania, siyo kiu wala hitaji la msingi la watanzania.
Nenda kwa vijana waliomaliza vyuo vikuu na katika ngazi tofauti tofauti za Elimu,Nenda kwa watumishi wa Umma au wakulima au akina mama sokoni au vijana wa bodaboda vilingeni au wabeba mizigo stendi au maafisa usafirishaji barabarani au wanafunzi waliohitimu kidato cha sita au polisi au wanajeshi makambini.
Amini amini nawaambieni ndugu zangu Watanzania kwamba makundi yoote hayo na mengine mengi hakuna kundi litakuambia kuwa kipaombele chake au hitaji lake au kiu yake ni kupata katiba mpya. Hakuna atakaye kuambia jambo hilo. Sana sana utaambiwa na vijana juu ya kiu yao kubwa ya kupata ajira serikalini ili walitumikie Taifa lao kwa ujuzi walionao na walioupata.
Wakulima watakwambia wana tamani kuona serikali inaendelea kutoa ruzuku kwenye pembejeo kama vile mbolea za ruzuku pamoja na bei nzuri kwa mazao yao na soko la uhakika . Wafanyabiashara watakwambia wanatamani kuona makadirio ya kodi yenye kuendana na uhalisia ,mazingira mazuri ya kibiashara,sera na sheria nzuri zenye kuwajali na kuwasaidia wazawa katika uwekezaji na biashara kubwakubwa ,kupata fursa za mikopo ya riba nafuu na mengine ya aina hiyo.
Ukija mitaani utaambiwa habari za fursa za Elimu kwa vijana ,kupatiwa mikopo kwa wote wenye sifa kupata Elimu ya juu. Ukienda kwa watumishi wa umma utasikia habari za kuboreshewa maslahi yao ,kupandishwa madaraja kazini na kulipwa stahiki zao,kupewa nafasi za kujiendeleza kielimu na kuongeza ujuzi ,kupewa motisha mbalimbali kulingana na mazingira ya kazi, kuboreshewa mazingira ya kazi ikiwepo kujengewa makazi yenye hazi na staha na kulipwa viinua mgongo vyao kwa wakati.
Ukienda kwa askari wetu wavuni vya ulinzi na usalama utaambiwa habari za maslahi yao ,kuboreshewa mazingira ya kazi kwa kujengewa nyumba nzuri ,kupewa vifaa vya kisasa kwa ajili ya kukabiliana na maadui na majambazi,kulipwa posho na marupurupu mbalimbali kulingana na vitengo vyao na majukumu yao ya kazi na utayari wao.kupewa bima kubwa kubwa ili waweze kupata matibabu bora na ya hadhi ya juu wapatapo majeraha wawapo katika utekelezaji wa majukumu yao ya kikazi na kioparesheni.
Ukienda kwa akina mama magengeni na sokoni utaambiwa habari za kupewa mikopo ya riba nafuu ili waepukane na mikopo kausha Damu. Ukienda kwa bodaboda utaambiwa habari za kusaidiwa kupata Bila za afya ili ziwasaidie wakipata majeraha au ajali ,kukopeshwa kupitia vikundi vyao na kuepukana na mikopo yenye riba kubwa na kuingia katika mtego wa madeni.
Habari za wananchi mitaani ni juu ya Maisha yao na namna ya kuyaboresha na kuyainua kupitia shughuli zao za kila siku, ni juu ya sera ,sheria , mikakati na mipango ya serikali kugusa shuguli zao na kuzipa nuru na matumaini ya kukua kila zianzishwapo. Ni juu ya huduma za kijamii kusogezwa karibu yao na kutolewa kwa ubora wa hali ya juu bila ubaguzi wala ukiritimba . Ni juu ya usawa wa fursa zipatikanazo katika maeneo yao,ni juu ya kuwashika mikono na kuwainua.ni juu ya kuwakwamua kiuchumi kupitia sera na sheria.
Hakuna Bibi utakayemkuta au kumsikia huko kijijini akizungumzia habari za katiba mpya au mahitaji ya katiba. Ndio maana leo hii mwanasiasa akisimama jukwaani na kuanza kuzungumza habari za katiba mpya kama kipaombele chake anakuwa anaonekana kama mtu anayewapotezea muda tu watu,anakuwa ni kama mtu mwenye kujadili habari za tumbo lake na maslahi yake binafsi.
Ndio maana hata leo uwaambie Watanzania kwamba hushiriki uchaguzi mpaka ipatikane katiba mpya unakuwa unajipotezea muda wako tu,unakuwa unampigia mbuzi gitaa tu. Watanzania wanaangalia zaidi yawahusuyo na kugusa Maisha yao kama nilivyoeleza hapo juu. Kwa hiyo asijetokea mtu au mwanasiasa akasema anawapigania watanzania kwa kutaka katiba mpya.
Kwa hakika atakuwa anajidaganya Mwenyewe na wala hatujamtuma kufanya kazi hiyo. Na wala siyo mahitaji yetu kwa sasa. Mahitaji yetu ya muhimu na msingi watanzania nimeshaeleza japo kwakifupi na hayo ndiyo ambayo yamekuwa yakitekelezwa na serikali ya Rais Samia usiku na mchana,ndio yamekuwa kipaombele cha serikali ya Jemedari wetu kipenzi cha watanzania Mheshimiwa Daktari Mama Samia Suluhu Hasssan.
Ndio Maana ya kuendelea kuungwa mkono na kupendwa na watanzania wote kutokana na kugusa Maisha yao. Kama huamini kuwa katiba mpya siyo kipaombele chetu watanzania jaribu uitishe hata maandamano leo hii uone kama kuna mtu atatokea barabarani kuandamana kuunga mkono. Nakuhakikishieni ya kuwa hakuna atakaye andamanaa zaidi ya watu kuendelea na shughuli zao kama kawaida tu.
Nimewapeni ukweli huo. Mkubali au mkatae,Mnune au mvimbe mashavu yenu lakini huo ndio unabakia kuwa ukweli wenyewe.
Kazi iendelee, Mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa Maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.
Lucas Hebel Mwashambwa, Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.