Kati ya Programmer na I.T

Kati ya Programmer na I.T

Vipi kuhusu anayetaka kujifunza Data analysis/Data science.Je naye atahitaji kwanza kuwa programmer au kujifunza lugha ngapi ukiitoa lugha ya PYTHON.

Data analysis/data science kwanza uwe vizuri statistics ,pia hauwezi kufanya chochote hapo bila kuwa vizuri kwenye kutumia software za data analysis.maneno hayata kusaidia.

Lugha moja tu inatosha,ila kilichopo ni kwamba kuna software zimetengenezwa na hizo lugha kwa ajiri ya kufanya analysis Kwa hiyo unaweza kuishia kwenye software zilizotengenezwa tayari au usome language kabisa iliyotengeneza hiyo software ya analysis ni machaguo yako sasa hapo automatic wewe ni programmer tu lazima uandike code kitu kitokee .
 
Nitakujibu kwa maneno machache maana umeniita.

Binafsi nilizunguka mjini sana nikiwa muda mwingi nimefulia kipindi nafanya kazi general za IT kama vile computer and printer repairs, networking n.k.

Lakini baadaye nikaamua kukomaa na programming. Yaani sijajutia kwangu mimi kuwa coder. Inalipa na pia ina watu wachache maana wengi huanza kwa mihemko halafu wanaishia njiani. Lazima uwe na moyo wa chui, nguvu za simba na mvumilivu kama nyoka ili ufaulu kwenye taasisi ya programming.

Kubali kuwa chizi mwenye uwezo wa kufanya coding week yote huku unalala masaa machache sana.

Ukiwa na passion ya kihivyo utakua bingwa na kazi zitakufuata, wateja watakufuata, hutotaka kuajiriwa na mtu.

Maneno yako yanitie nguvu
 
Labda hujanielewa, naomba urudie majibu yangu yote taratibu na utapata picha nzima ya nini ninachokisema. Fahamu kwamba chuo hakikufanyi uwe programmer, uwezo wa kuwa programmer ni juhudi zako mwenyewe. Ujifungie chumbani na kuyasahau ya dunia, wewe na vitendea kazi vyako hadi kieleweke.

Wapo watu wengi wenye shahada za sayansi ya kompyuta lakini kuandika software inakua shughuli, wamejaa nadharia tupu. Nilichokisema ni kwamba baada ya chuo kukuandaa kwenye mambo muhimu ya msingi, unafaa kuanza kutia bidii na kuhakikisha umekua programmer mwenyewe.

Wapo programmers wazuri ambao hawakupitia chuoni, lakini kila mmoja atakuambia ilibidi atumie nguvu nyingi sana ili kufanikiwa. Hivyo kama unao uwezo wa kupitia chuo, nenda kasome kwanza, lakini kama uwezo huo haupo, usikate tamaa, komaa, tafuta videos, download vitabu, andaa mazingira chumbani, jifungie ndani kitaa, ingia kwenye online forums za programmers, husika katika mijadala, pambana tu na kitaeleweka.
Sana broo mafanikio ni juhudi tusipende shortcut nmekuelewa sana kaka
 
Back
Top Bottom