Kati ya Programmer na I.T

Kati ya Programmer na I.T

Habari,
Aisee niende kwenye swali,
Ivi kati ya Programmer na IT yupi mwenye fursa nyingi za kujiajiri na kuajiriwa, na endapo wataajiriwa yupi ambae atapokea kiasi kikubwa cha mshahara kupita mwenzake???
cc. Chief-Mkwawa mchambawima1 MK254 snipa Isac M Barbarosa Na wengineo
Wote wana fursa za kujiajiri, inaegemea tu na capital uliyokuwa nayo.
1. Kama wewe ni IT na una capital ya kutosha unaweza kufungua biashara kisha ukajiri programmer na ukawa una wa supervise.
2. Kama capital yako ni ndogo, unaweza wewe kama programmer ukaingia msituni ukafungua biashara ukajiajiri mwenyewe kama programmer.

All in all watu wengi wanaojiajiri kama programmer unakuta ndio wako kwenye start-up stage za business ila wakisha expand huwa wanaajiri programmers maana ile kazi ni mzigo kufanya mwenyewe kila kitu.
 
kuliko kuingia kwenye Biashara kwa lengo la kupata fedha, bora ukatafute mtu akuajiri. Utaishia kuwa frustrated na pengine kujifia mapema. Kwa lugha rahisi ni kuwa kama motive yako ni kusoma ili upate fedha, CompSc na related branches are not for you!
 
Mtu anapouliza swali sikuzote sio tu kwa niaba yake, ni kwa niaba ya wote
na usidhani labda alikuwa hajui labda,
Hata ivyo nadhani ukipitia comment utaona lundo la watu waliokuwa wanahitaji msaada ila walikuwa wanahofia kuuliza.
Sio kwamba najua vyote NO,

''Ruksa kunitoa ushamba kwa kitu nisichokijua, nitakuwa mshamba kwa dakika kisha I am professional'' -Fid Q
Pole
 
Swali lako lina utata. IT anaweza kua programmer,hata mtu yoyote akisoma programming anakua programmer. Kwahyo sio cheo ni skill. IT na Comluter Engineer ndio wa kulinganishwa.

Lakini Ngoja ni assume nmekuelewa swali lako.

Programmer ndio ana fursa nyingi
 
kuliko kuingia kwenye Biashara kwa lengo la kupata fedha, bora ukatafute mtu akuajiri. Utaishia kuwa frustrated na pengine kujifia mapema. Kwa lugha rahisi ni kuwa kama motive yako ni kusoma ili upate fedha, CompSc na related branches are not for you!
Heshima yako bro!

So watu wanasoma CS ili wapate nini kama si pesa?? Najua kuna passion and all that but at the end what do you want to achieve? Money?
 
Heshima yako bro!

So watu wanasoma CS ili wapate nini kama si pesa?? Najua kuna passion and all that but at the end what do you want to achieve? Money?
They get paid because they solve problems. So chase problems and offer solutions and you get money. Chase money and you'll never catch them.

Basic business principle that harshly applies in Engineering/IT/CS soma kipande hiki:

endapo wataajiriwa yupi ambae atapokea kiasi kikubwa cha mshahara kupita mwenzake???
 
Ok kama I T ni teknolojia ya mawasiliano, unaitenga vp na programming.
Jamii forum ni sehem moja wapo tunapopata taharifa na kiwasiliana, je hapa haijatumika teknolojia ya habari? Ok na je programming haijatumika?
IT ni nani na proggramer ni nani?
Ninachojua kwny ofisi nyingi iwe za kiserikali au za kmpuni binafsi huwa wanatenga kitengo cha IT na si programming ingawa yaeeza kuwa ni ofisi ya kudeal na programming.
Mleta uzi naomba unijibu na mimi.
Kati ya fundi makanika na mtengeneza engine ya gari nani anapata deal nyingi.
 
They get paid because they solve problems. So chase problems and offer solutions and you get money. Chase money and you'll never catch them.

Basic business principal that harshly applies in Engineering/IT/CS soma kipande hiki:
Nimekupata sawia mkuu!! Get required skills, find problems, solve them and ultimately they'll pay you!! Thank you!
 
Njia moja rahisi ya kukumbana na deals kubwa hapa Afrika, ikiwemo kwetu Kenya na pia hata Bongo ni kama ukifanya kazi on sub-contractual basis. Ni vigumu kwa programmer akiwa mwenyewe kupata deals kubwa hususan za kiserakali maana lobbying ya manyang'au huwa kali sana na deals hazipokezwi kwa kufuata sifa.

Kawaida mimi huachia makampuni yashindane kupata deal halafu wenyewe wananijia nifanye implementation kwa kunipa kandarasi ya sub contract. Unawacha wanaandika winning proposal kwa tender, wanafanya lobbying balaa maana serikali na makampuni makubwa wanataka kuona proposals za kiajabu ajabu zenye kuonyesha watendaji wa kampuni wenye masters degrees na mambo makubwa ambayo hata hayahusiani na mradi wenyewe.

Sasa kampuni ikishinda, wanasaka programmer ambaye ataongoza implementation na shughuli inafanyika. Humu siwezi kutaja baadhi ya miradi ambayo nimetekeleza, lakini kwa kifupi nimehusika katika very top projects za kiserikali na mashirika binafsi.
Usiku huu wa leo hapa nafanya coding ya system ambapo nipo hotelini, nimekuja na wafanyi kazi 20 wa wizara fulani ambapo nipo nawapa darasa ya system fulani ambayo nimewatengenezea. Tutaishi hotelini humu siku 30 kila siku tunapitia system nikiifanyia maboresho kulingana na mapendekezo yao. Ni system nimeitengeneza ndani ya miezi sita.

So kwa kifupi, nawashauri madogo ambao wanataka kuingia kwa fani hii, wajifunze IT in general ndani na nje, halafu kisha wakomae na programming. Kazi zitawafuata tu... zipo, programmers ni wachache kwenye nchi zetu hizi. Tatizo wengi wanataka shortcuts, anajifunza programming language kwa mihemko na kujiita programmer.

Programming is a lifestyle, it's a way of life...ukianza inabidi ubadilishe maisha yako kabisa, unakua boring kwa marafiki maana huna muda wa kwenda kucheza cheza pool table kitaa.
Mk254 umeongea bonge la pointi, IT ni tamu sana ukiwa na passion waeza fanya chochote na pia ina ulingo mpana wa kuchezea popote utakapoamua kucheza kuna networking ukii mastet na ukapata certification yake utandunda, ipo sytem administration and security nayo ina itamu wake, kuna ishu za graphics and design pia huku ipo kali tu na kuna programming ambapo hapa inahitaji ujitoe roho na nafsi. Pesa utaipata popote pale kwenye IT. Note usiige wala kukurupuka kusomea hii course kama haupo tayari kujitoa na kama wewe sio mfuatiliaji wa mambo hasa ya IT TECHNOLOGY.
 
Ok kama I T ni teknolojia ya mawasiliano, unaitenga vp na programming.
Jamii forum ni sehem moja wapo tunapopata taharifa na kiwasiliana, je hapa haijatumika teknolojia ya habari? Ok na je programming haijatumika?
IT ni nani na proggramer ni nani?
Ninachojua kwny ofisi nyingi iwe za kiserikali au za kmpuni binafsi huwa wanatenga kitengo cha IT na si programming ingawa yaeeza kuwa ni ofisi ya kudeal na programming.
Mleta uzi naomba unijibu na mimi.
Kati ya fundi makanika na mtengeneza engine ya gari nani anapata deal nyingi.
fundi makenika...
I know yote ni mahindi lakini naongelea unga wa dona na sembe ni upi unaolika na watu kwa sana???
Umenipata?
 
Nimependezwa na mjadala huu,kwa kuzingatia swali,IT na Programmer wote wanafursa sawa za kuajiriwa aidha hakuna jibu LA moja kwa moja LA nani anapata mshahara mkubwa,inategemea wameajiriwa wapi yaani nchi ,kampuni,taasisi ,serikalini au sekta binafsi.Kwa mazingira ya Serikali ya Tanzania baadhi ya Wizara na Taasisi za Serikalu huajiri za wajuzi wa IT aidha zipoWizara zinajiri zaidi wajuzi wa Programming
 
Nitakujibu kwa maneno machache maana umeniita.
Binafsi nilizunguka mjini sana nikiwa muda mwingi nimefulia kipindi nafanya kazi general za IT kama vile computer and printer repairs, networking n.k.

Lakini baadaye nikaamua kukomaa na programming. Yaani sijajutia kwangu mimi kuwa coder. Inalipa na pia ina watu wachache maana wengi huanza kwa mihemko halafu wanaishia njiani. Lazima uwe na moyo wa chui, nguvu za simba na mvumilivu kama nyoka ili ufaulu kwenye taasisi ya programming.
Kubali kuwa chizi mwenye uwezo wa kufanya coding week yote huku unalala masaa machache sana.

Ukiwa na passion ya kihivyo utakua bingwa na kazi zitakufuata, wateja watakufuata, hutotaka kuajiriwa na mtu.
Soko la programming ni kama vipi? au ni kutengeneza programu tu?
 
Programming kwa Afrika bado mkuu!!.......hata kazi zinazohitaji programmer hapa Tanzania nafikiri pia ni chache sana!
Wat
Soko la programming ni kama vipi? au ni kutengeneza programu tu?
Moja ya shida ya tanzania watu wanawaza soko kwanza Na hela kabla hawajaanza ku appreciate Na kuelewa nini maana ya computing.Ndo maana ni nadra sana kuona system programmers hapa kwasababu most of them(wana IT na CS)hawataki kwenda deep into the system Na ku devote time and passion kuelewa vitu.soko ni muhimu lakini tunabidi kwaanza tuanze ku appreciate computing Alf soko Ndo litafuata baadaye
 
Labda hujanielewa, naomba urudie majibu yangu yote taratibu na utapata picha nzima ya nini ninachokisema. Fahamu kwamba chuo hakikufanyi uwe programmer, uwezo wa kuwa programmer ni juhudi zako mwenyewe. Ujifungie chumbani na kuyasahau ya dunia, wewe na vitendea kazi vyako hadi kieleweke.

Wapo watu wengi wenye shahada za sayansi ya kompyuta lakini kuandika software inakua shughuli, wamejaa nadharia tupu. Nilichokisema ni kwamba baada ya chuo kukuandaa kwenye mambo muhimu ya msingi, unafaa kuanza kutia bidii na kuhakikisha umekua programmer mwenyewe.

Wapo programmers wazuri ambao hawakupitia chuoni, lakini kila mmoja atakuambia ilibidi atumie nguvu nyingi sana ili kufanikiwa. Hivyo kama unao uwezo wa kupitia chuo, nenda kasome kwanza, lakini kama uwezo huo haupo, usikate tamaa, komaa, tafuta videos, download vitabu, andaa mazingira chumbani, jifungie ndani kitaa, ingia kwenye online forums za programmers, husika katika mijadala, pambana tu na kitaeleweka.
nataka kuwa programm lakini nataka niome mwenyewe kama ulivyosema bila kwenda chuo sasa unanishauri nianzeje mm kama beginner
 
Kwani wadau ujue sie wengine... ni pangu pakavu kabisa.....

Programming kazi zake ni zipi kwa ofisin... km ofisini anafanya nin na mitaan anafanya nin... then izo kazi zipo mara kwa mara katika maisha ya kawaida...

Pia.

I.T kazi zake ni zipi kwa ofisin... km ofisini anafanya nin na mitaan anafanya nin... then izo kazi zipo mara kwa mara katika maisha ya kawaida...

Naombwa nijuze then ntajua nani anapiga pesa
 
Back
Top Bottom