Kati ya Programmer na I.T

Kati ya Programmer na I.T

Sikumbuki siku niliwahi kuagizwa cheti. Mara nyingi huwa reference tu, unakuta mteja kampa mtu namba yangu.
Yaani ukihakikisha umepokeza kazi ipasavyo watakufuata tu. Huwa hata sina muda wa ku-update CV yangu.
Mkuu, Unahisi ni sahihi kama mtu akiamua kujifunzia mtaani tu, labda kwa mtu mwenye ujuzi wa programming pasipo kwenda chuo?
 
Mkuu, Unahisi ni sahihi kama mtu akiamua kujifunzia mtaani tu, labda kwa mtu mwenye ujuzi wa programming pasipo kwenda chuo?

Ni muhimu sana kwa mtu kwenda chuo, upate vitu vya msingi na kustawi. Halafu hapo baadaye komaa na programming. Programmers wapo wengi wa kujifunza mtaani bila chuo, lakini wanatumia nguvu nyingi sana hadi ingekua bora akaandaliwa sehemu kwanza.

Elimu ya chuo inakuwezesha kuelewa binary logic, hii ni mojawapo wa issue ambayo huwatatiza programmers hususan ambao wamezoea IDE za drag and drop, inafaa kusoma na kuelewa mfumo mzima wa computer, jinsi vifaa vyote vimeunganika hadi kuwa computer. Mtiririko wa taarifa na mwendo kasi.

Chuo kitakufunza Operating Systems, na jinsi software yako ita interract nazo maana humo utakuta wana miundo mbinu tofauti na ulivyo kitaa na laptop yako. Utapata pia elimu iliyotulia ya data structures na algorithms.

Utafunzwa pia programming languages, historia na muundo. Jinsi zinahusiana, kuwiana na kutofautiana. Na pia utapata fursa ya kusoma na wenzio concepts za programming.

Yaani kuna mambo mengi ukipitia chuo utapata kuyajua ndani ya Software Design & Architecture.
 
Ni muhimu sana kwa mtu kwenda chuo, upate vitu vya msingi na kustawi. Halafu hapo baadaye komaa na programming. Programmers wapo wengi wa kujifunza mtaani bila chuo, lakini wanatumia nguvu nyingi sana hadi ingekua bora akaandaliwa sehemu kwanza.

Elimu ya chuo inakuwezesha kuelewa binary logic, hii ni mojawapo wa issue ambayo huwatatiza programmers hususan ambao wamezoea IDE za drag and drop, inafaa kusoma na kuelewa mfumo mzima wa computer, jinsi vifaa vyote vimeunganika hadi kuwa computer. Mtiririko wa taarifa na mwendo kasi.

Chuo kitakufunza Operating Systems, na jinsi software yako ita interract nazo maana humo utakuta wana miundo mbinu tofauti na ulivyo kitaa na laptop yako. Utapata pia elimu iliyotulia ya data structures na algorithms.

Utafunzwa pia programming languages, historia na muundo. Jinsi zinahusiana, kuwiana na kutofautiana. Na pia utapata fursa ya kusoma na wenzio concepts za programming.

Yaani kuna mambo mengi ukipitia chuo utapata kuyajua ndani ya Software Design & Architecture.
Ungekuwa karibu ningekuoffa hata Juice,
Umeelezea vizuri sana,
Na kwa hakika Comments zako zimewasaidia wengi sana.
Shukrani Mkuu.
Na kama kutakuwa na cha ziada usisite kushea nasi
 
Nitakujibu kwa maneno machache maana umeniita.
Binafsi nilizunguka mjini sana nikiwa muda mwingi nimefulia kipindi nafanya kazi general za IT kama vile computer and printer repairs, networking n.k.

Lakini baadaye nikaamua kukomaa na programming. Yaani sijajutia kwangu mimi kuwa coder. Inalipa na pia ina watu wachache maana wengi huanza kwa mihemko halafu wanaishia njiani. Lazima uwe na moyo wa chui, nguvu za simba na mvumilivu kama nyoka ili ufaulu kwenye taasisi ya programming.
Kubali kuwa chizi mwenye uwezo wa kufanya coding week yote huku unalala masaa machache sana.

Ukiwa na passion ya kihivyo utakua bingwa na kazi zitakufuata, wateja watakufuata, hutotaka kuajiriwa na mtu.
Mkuu uko wapi nikutafute?
 
Ungekuwa karibu ningekuoffa hata Juice,
Umeelezea vizuri sana,
Na kwa hakika Comments zako zimewasaidia wengi sana.
Shukrani Mkuu.
Na kama kutakuwa na cha ziada usisite kushea nasi

Anytime bro.
 
Ni muhimu sana kwa mtu kwenda chuo, upate vitu vya msingi na kustawi. Halafu hapo baadaye komaa na programming. Programmers wapo wengi wa kujifunza mtaani bila chuo, lakini wanatumia nguvu nyingi sana hadi ingekua bora akaandaliwa sehemu kwanza.

Elimu ya chuo inakuwezesha kuelewa binary logic, hii ni mojawapo wa issue ambayo huwatatiza programmers hususan ambao wamezoea IDE za drag and drop, inafaa kusoma na kuelewa mfumo mzima wa computer, jinsi vifaa vyote vimeunganika hadi kuwa computer. Mtiririko wa taarifa na mwendo kasi.

Chuo kitakufunza Operating Systems, na jinsi software yako ita interract nazo maana humo utakuta wana miundo mbinu tofauti na ulivyo kitaa na laptop yako. Utapata pia elimu iliyotulia ya data structures na algorithms.

Utafunzwa pia programming languages, historia na muundo. Jinsi zinahusiana, kuwiana na kutofautiana. Na pia utapata fursa ya kusoma na wenzio concepts za programming.

Yaani kuna mambo mengi ukipitia chuo utapata kuyajua ndani ya Software Design & Architecture.
Ina maana kama sina mda ua pesa ya kwenda chuo siwezi kuwa programmer au web developer?
 
Ina maana kama sina mda ua pesa ya kwenda chuo siwezi kuwa programmer au web developer?

Labda hujanielewa, naomba urudie majibu yangu yote taratibu na utapata picha nzima ya nini ninachokisema. Fahamu kwamba chuo hakikufanyi uwe programmer, uwezo wa kuwa programmer ni juhudi zako mwenyewe. Ujifungie chumbani na kuyasahau ya dunia, wewe na vitendea kazi vyako hadi kieleweke.

Wapo watu wengi wenye shahada za sayansi ya kompyuta lakini kuandika software inakua shughuli, wamejaa nadharia tupu. Nilichokisema ni kwamba baada ya chuo kukuandaa kwenye mambo muhimu ya msingi, unafaa kuanza kutia bidii na kuhakikisha umekua programmer mwenyewe.

Wapo programmers wazuri ambao hawakupitia chuoni, lakini kila mmoja atakuambia ilibidi atumie nguvu nyingi sana ili kufanikiwa. Hivyo kama unao uwezo wa kupitia chuo, nenda kasome kwanza, lakini kama uwezo huo haupo, usikate tamaa, komaa, tafuta videos, download vitabu, andaa mazingira chumbani, jifungie ndani kitaa, ingia kwenye online forums za programmers, husika katika mijadala, pambana tu na kitaeleweka.
 
Ukisoma IT huwezi kuikwepa programming japo ile basic ya kufanyia UE. Binafsi nimesoma IT ila sikuwa napenda code kabisa hasa C++, nilijikita zaidi kwenye networking. Watu wanaosoma computer science ndio maranyingi wanajikita kwenye programming
 
Labda hujanielewa, naomba urudie majibu yangu yote taratibu na utapata picha nzima ya nini ninachokisema. Fahamu kwamba chuo hakikufanyi uwe programmer, uwezo wa kuwa programmer ni juhudi zako mwenyewe. Ujifungie chumbani na kuyasahau ya dunia, wewe na vitendea kazi vyako hadi kieleweke.

Wapo watu wengi wenye shahada za sayansi ya kompyuta lakini kuandika software inakua shughuli, wamejaa nadharia tupu. Nilichokisema ni kwamba baada ya chuo kukuandaa kwenye mambo muhimu ya msingi, unafaa kuanza kutia bidii na kuhakikisha umekua programmer mwenyewe.

Wapo programmers wazuri ambao hawakupitia chuoni, lakini kila mmoja atakuambia ilibidi atumie nguvu nyingi sana ili kufanikiwa. Hivyo kama unao uwezo wa kupitia chuo, nenda kasome kwanza, lakini kama uwezo huo haupo, usikate tamaa, komaa, tafuta videos, download vitabu, andaa mazingira chumbani, jifungie ndani kitaa, ingia kwenye online forums za programmers, husika katika mijadala, pambana tu na kitaeleweka.
Nimekupata sana mkuu!! Swali lingine...katika back end development, php, django, rubby on rail na node js ipi ina future nzuri kwa hizi nchi zetu za dunia ya tatu??
 
Alafu naskia wanasema kujifunzia mtaani kwa mtu mwenye ujuzi ni bora zaidi kuliko vyuoni, hii kuna ukweli wowote?

Nta assume upo Tanzania na unataka Formal education with certification

kwanza nataka uliza unataka kusoma Bachelor au Diploma?
Nikiangalia katika TCU Guidebook mfano katika Chuo ambacho kina hizi Course mbili
Bachelor of Science in Information Technology(IT) na Bachelor of Science in Computer Science
Hii inanifanya kufikiri kwamba hizo ni speciality mbili tofauti kwa siku za nyuma nilikua na mdogo wangu alitaka kusoma hizi nkawa nafatilia Almanac ya UDSM na naweza kusema kwa research nilofanya mtu wa Computer Science ana coverage kuwbwa zaidi ya Programming kushinda huyo anayesoma Bsc in IT ila bado katika hiyo almanac vitu kama networking bado viko covered both sides i.e Bsc in IT na Bsc in CS.

Tukirudi kwenye base kabisa
"....An IT career involves installing, organizing and maintaining computer systems as well as designing and operating networks and databases. Computer science is focused entirely on efficiently programming computers using mathematical algorithms..." Source

Based kwenye hayo maelezo kama utapitia formal education ya hapa kwetu at one point kuna skills za IT utapata ukiwa umepitia CS na kuna matangazo ya kazi yana specify kabisa kama yanataka mtu wa degree yana specify iwe in Bsc in IT au Bsc in CS
 
Nta assume upo Tanzania na unataka Formal education with certification

kwanza nataka uliza unataka kusoma Bachelor au Diploma?
Nikiangalia katika TCU Guidebook mfano katika Chuo ambacho kina hizi Course mbili
Bachelor of Science in Information Technology(IT) na Bachelor of Science in Computer Science.....

Which is better to study between IT, computer Science or computer Engineering?

Tofauti kati ya IT, Computer Science na Computer Engineering



Computer Science vs IT jamiiforums.com - Google Search
 
Hapa JF huwa unaonekana wa matawi ya juu kumbe mwenzetu tu!
Mtu anapouliza swali sikuzote sio tu kwa niaba yake, ni kwa niaba ya wote
na usidhani labda alikuwa hajui labda,
Hata ivyo nadhani ukipitia comment utaona lundo la watu waliokuwa wanahitaji msaada ila walikuwa wanahofia kuuliza.
Sio kwamba najua vyote NO,

''Ruksa kunitoa ushamba kwa kitu nisichokijua, nitakuwa mshamba kwa dakika kisha I am professional'' -Fid Q
 
Nimekupata sana mkuu!! Swali lingine...katika back end development, php, django, rubby on rail na node js ipi ina future nzuri kwa hizi nchi zetu za dunia ya tatu??

Ulimwengu wetu wa tatu bado tuko nyuma sana, hatujafikia kiwango cha kuchagua ipi backend language yenye future nzuri kwetu maana hata hizi za sasa hatuja utilize ipasavyo. Itakua kujitakia makuu kwa yeyote kati yetu kubishana na wenzetu wa kule Ulaya wanapobishana ipi lugha yenye future nzuri. Utakuta mtu anang'ang'ania kutaja taja lugha za future, lakini ukimuuliza amefikia wapi na lugha anayoitumia sasa hivi, unashangaa hata 10% yake hajatumia vizuri.

Kwa kifupi, ni vigumu kutabiri siku za usoni za languages maana kuna ushindani mkubwa sana katika kuzibuni mpya na pia kuboresha zilizopo. Huwa nafuata mijadala ya wenzetu wakati wanajadili lugha za future hadi najikuta nasinzia. Japo kwa maisha yetu ya Kibongo bongo na Kikenya Kenya naona NodeJS ipo inakuja kwa kasi sana. Naitumia tumia na kuona ikinitimizia shughuli zangu vizuri sana tena kwa kasi ya ajabu.
 
Back
Top Bottom