Hatangalii umbali tunaangalia je ipo ndani yake ? kutoka Dar na Morogoro town ni karibu zaidi kushinda hata kutoka pale Moro town kwenda wilaya nyingine ila hatuwezi kusema Moro ni Dar kwa kuzingatia ukaribu.
Elewa kwamba iyo Charambe na Mbande jina la zamani lililojulikana ilikuwa ni Mbagala Mbande ,Mbagala Charambe ila baada ya mji kukua jina la Mbagala likatoka sasa inaitwa Mbande tu lakini tukija 2008/9 mpk 2010 kote palijulikana kama Mbagala Maji matitu pekee ndio imeMaintain jina la Mbagala mpaka leo inaitwa Mbagala Majimatitu ila jina hilo linapotea mdogo mdogo .Hiyo case ni sawa na Buza jina la Buza limekuja sasa ila nyuma kidogo ilikuwa sehemu ya Yombo pamoja na Yombo Dovya Buza ilikuwa ikiitwa Yombo Buza ilikuwa nadra sana mtu kusema naenda Buza hata kiwalani nayo mpaka sasa ni Yombo Kiwalani.
Ila tukiwa kwa Goms Kitunda ,kivule hata Banana nk toka kitambo haina uhusiano na Goms kijina ,kiserikali hata raia wa kawaida hawachukulii kuwa wapo Gongo la mboto . Na ukija kiserikali maeneo yote niliyotaja kuwa yanauhusiano na Mbagala yapo Jimbo la Mbagala.
Na hitimisha kuwa Goms sio pa kufananisha na Mbagala na mnakimbilia polisi kujumlisha Goms na Airport na maeneo ya jirani .