Roving Journalist
JF Roving Journalist
- Apr 18, 2017
- 4,783
- 14,975
Ameyasema hayo katika akiwa mgeni rasmi katika maadhimisho ya Miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima ambayo kilele chake kinafanyika leo Agost 25, 2025 Jijini Dar es Salaam, ambapo wakati anahitimisha hotuba yake amesema kwamba wananchi wanayo haki ya kushiriki zoezi hilo kwa amani hali ambayo amedai kuwa Serikali imejipanga kuhakikisha kunakuwepo amani.
Sanjari na hilo, akizungumzia maadhimisho hayo, Majaliwa ameipongeza taasisi hiyo kwa hatua mbalimbali ambazo imeendelea kuzipiga katika kuhakikisha elimu ya watu wazima inakuwa na tija kwa jamii na kuwafikia watu wengi wa makundi mbalimbali katika jamii hususani suala la kutoa ujuzi.
Lakini pia Majaliwa ametoa kwa taasisi kutanua wigo kwa kuwafikia wananchi wengi zaidi hasa walioko maeneo ya pembezoni, ambapo ameeleza kuwa hatua hiyo itaongeza tija zaidi kwenye jamii.
Sambamba na wito huo pia ameelekeza Wizara kwa kushirikiana na taasisi husika kuhakikisha wanaendelea kuboresha mazingira ya kujifunzia, kutafuta vifaa vya kisasa ikiwemo matumizi ya Tehama ili kuwezesha wananchi kunufaika na elimu hiyo.
Aidha Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia Mhe. Prof. Adolf Mkenda ameeleza kuwa tokea Rais wa Jamhuri alipotoa maelekezo ya Wanafunzi wa Kike ambao walikuwa wamekumbana na changamoto mbalimbali ambazo zilipelekea kusitisha masomo ikiwemo kupata ujauzito kurejea tena masomoni, amesema kuwa zaidi ya 13,000 tayari wamejitokeza kuendelea na masomo.
Maadhimisho hayo yamebebwa na kauli mbiu isemayo "Elimu bila ukomo kwa maendeleo endelevu" huku mijadala mbalimbali ya tathimini ikiwa sehemu ya matukio.