Kassim Majaliwa: Moyo wangu utulie niseme Magufuli alikuwa kiongozi Mzalendo

Kassim Majaliwa: Moyo wangu utulie niseme Magufuli alikuwa kiongozi Mzalendo

JanguKamaJangu

JF-Expert Member
Joined
Feb 7, 2022
Posts
3,177
Reaction score
7,472
Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa, amesema Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Magufuli, alikuwa kiongozi mzalendo aliyejengwa katika misingi ya uwajibikaji, uaminifu, uadilifu, na upendo.

Amesema Hayati Magufuli hakupenda mzaha katika kazi zake na alikuwa mkali, akikemea maovu, wizi, rushwa, na ubadhirifu wa mali za umma.

Majaliwa ameyasema hayo leo Machi 17, 2026, wakati wa kumbukizi ya miaka mitano ya kifo cha Dkt. Magufuli iliyofanyika Chato, mkoani Geita.

Aidha, Majaliwa amesema Watanzania wataendelea kumkumbuka Hayati Magufuli kwa busara na hekima zake katika kuongoza taifa na kusimamia rasilimali za nchi.

“Tunajiona kabisa tumempoteza, hatunae, nataka niwaambie kwamba yupo kwenye mioyo yetu, tuendelee kumuenzi,” amesema Waziri Mkuu Mstaafu Majaliwa.

Video: VIBES FM
 
Hotuba yake ameinajisi mwishoni alipochomekea propaganda na uchawa kumsifia mama yao
 
Kas
Majaliwa wa Magu angekutana na Majaliwa wa "Mama" wangepigana sana. Majaliwa lost both his Authority and influence under the so called Mama
Kasimu Majaliwa aliondoka na Magufuli aliyebaki kipindi cha mama ulikua Kama mzimu mpaka akawekewa Naibu
 
Waziri Mkuu Mstaafu, Kassim Majaliwa, amesema Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati Dkt. John Magufuli, alikuwa kiongozi mzalendo aliyejengwa katika misingi ya uwajibikaji, uaminifu, uadilifu, na upendo.

Amesema Hayati Magufuli hakupenda mzaha katika kazi zake na alikuwa mkali, akikemea maovu, wizi, rushwa, na ubadhirifu wa mali za umma.

Majaliwa ameyasema hayo leo Machi 17, 2026, wakati wa kumbukizi ya miaka mitano ya kifo cha Dkt. Magufuli iliyofanyika Chato, mkoani Geita.

Aidha, Majaliwa amesema Watanzania wataendelea kumkumbuka Hayati Magufuli kwa busara na hekima zake katika kuongoza taifa na kusimamia rasilimali za nchi.

“Tunajiona kabisa tumempoteza, hatunae, nataka niwaambie kwamba yupo kwenye mioyo yetu, tuendelee kumuenzi,” amesema Waziri Mkuu Mstaafu Majaliwa.

Video: VIBES FM
Sauti ya kimamlaka hii.
 
Msoga, Kizimkazi na Kolomije wote wamekwepa wenda Chato na hawa ndiyo watuhumiwa wakubwa kumtoa roho Jiwe, ama kweli the guilty are always afraid.
 
Back
Top Bottom