AdvocateFi
JF-Expert Member
- Jan 15, 2012
- 11,492
- 5,050
Ni kweli wako vizuri lakini bado wanakosa watu wa content hasa suala la news,vipindi na documentaries.
Azam wamewekeza sana katika suala la 'watangazaji' lakini issue ni je watatangaza nini? kinachouza kituo siyo watangazaji bali kinachotangazwa.
Aljazeera English ilipoanzishwa walichukua watu wengi kutoka CNN,BBC ,PRES TV nk lakini hawakuchukua watangazaji wengi bali 'wazalishaji wa content''.
Tangu kuanza kwa AZAM TV ni habari gani kubwa waliyowahi kuibua au ni kipindi gani cha nje (nje ya studio) kinachowauza mbali na kipindi cha Uchaguzi?'
Nafikiri nguvu kubwa wangewekeza katika suala la content badala ya kutafuta watangazaji maarufu duniani.
Tido alipoingarisha TBC hakuwa na watagazaji wapya au maarufu bali aliwekeza katika suala la content.
M.Byabato
Tv Journalist
Great thinker.