Wana JF, angalieni sana hawa buku7 wa Lumumba wanavyojadili mambo huku jamvini. Wanatafuta kila njia kukwepesha mada ili kutuvuruga tu.
Hivi, huyo mkewe Mbowe angewauliza hao wanao mkebehi Mh. Mbowe kwa habari za vimada wake, hayo yanahusianaje na maisha haya magumu hivi kwa Mtanzania? Hawa Tembo wetu wanaokwisha? Hao Wachina wanaokamatwa kila uchao na meno ya Tembo? Hao vijana wetu wanaokamatwa na Sembe huko China? Hivi vitu vinahusianaje na maisha ya Mh. Mbowe, hawa buku 7 humu jamvini wangejibu nini?
Tuache kujadili upuuzi wa mtu mmoja mmoja tujikite kwenye mambo mazito yanayoliangamiza Taifa hili. CCM wangeacha kuvivuruga vyama vya upinzani kwa gharama kuubwa kama hizo walizompa huyo ZZK wakazitumia hata kwenye;
Kuongeza mikopo ya vyuo vikuu
Kuongeza ufanisi wa hospitali moja tu Muhumbili
Kutoa ruzuku kwenye Umeme bei isituunguze hivyo
Kutoa ruzuku kwenye gesi bei ikapungua
Hata kina Nape wangekuwa na uhodari wa kuja humu JF na kujinadi kwa vitu hivyo walivyo fanya. Lakini mwisho wa siku, ni viongozi wa ccm kujitapa wakiwa wameshalewa wisky za Ikulu kuwa CDM itakufa kabla ya Pasaka ya mwaka huu.
Hawana chochote cha kujivunia hata kuonesha baada ya miaka 50 ya uhuru? Just let pie as pie, 2015 is not far.
Mtabaki kuelezea uzinzi wa Mbowe kama kwamba sote tunalala kwa Mbowe. Tena mwanzilishi ati ni Naibu Katibu Mkuu wa lichama koongwe.
Tunahitaji tabibu si bure. CCM memkosa hoja kabisa. Wangapi tunamfahamu huyo Lilian Mbowe, wangapi tunamfahamu huyo Joyce, tuna shida gani nao hao? Watatusaidia nini katika haya maisha magumu hivi tunayopambana nayo kila siku?
Watanzania, tusivurugwe na hawa watu walioishiwa sera. Uzinzi wa Mbowe haukuniletea haya maisha magumu. Nawasilisha.