Karibuni kwa maswali yote ya kiafya

Karibuni kwa maswali yote ya kiafya

Mchubuko usiopona njia ya ajakubwa tatizo ni nini....choo kikiwa raini ni yaleyale kikiwa kigum kidog ndio kabisaaa....nakunywa maji mengi pia matunda nakula sana na choo mala nying napata si kigum ila hii hali haiishi....nisaidie
 
Kumekuwa na ongezeko kubwa sana la tatizo la uvimbe/ fibroids kwa kina Dada/ kina mama. Chanzo cha tatizo ni nini? Options za matibabu ni zip? Nini ushauri wako kwetu kuhusiana na hili? Asante kwa kuendelea kutuelimisha.
Habari.
Nikweli kumekua Na ongezeko kubwa la tatizo hilo zaidi kwa Wanawake. Na hii nikutokana sana na mambo ya Urembo.
Kwani kuna baadhi ya vipodozi Na dawa za nywele huchochea sana uzalishaji wa Oestrogen mwilini, kuliko kawaida.
Ongezeko hili la uzalishwaji wa oestrogen huchangia kwa kiasi kikubwa sana cha ukuaji wa fibroids

Kemikali hizi zinazoambatanishwa kwenye vipodozi au dawa za nywele hupenya kwenye ngozi kutokana Na matumizi wanayotumia Wanawake kwa lengo la kupendeza.
Kwa ujumla kemikali hizi. Hazimuathiri mtumiaji kwa matumizi Bali hata kwa kuvuta harufutu.
Ukichunguza wamama au wadada wengi hubadiri matumizi ya dawa kua vipodozi.

Kwamfano kuna dawa zilizo katika kundi la steroids kama vile hydrocortisone,Betamethasone,Dexamethasone,Beclometasone,Clobetasol,Prednisolin nk

Kimsingi dawa hizi ni dawa za allergy Na husaidia kupunguza nguvu za kinga za mwili.
Zinapokua katika mfumo wa Cream,Lotion au gelly husaidia kuondoa allergys kwenye ngozi.

Mbali Na kuondoa allergy bali pia huondoa ngozi ngumu Na rough ya nje. (Ngozi ambayo hutusaidia kutukinga Na miale mikali ya jua, kansa, michubuko Na kadhalika.

Dawa hizi kwa kawaida zinatakiwa zitumike kwa dozi maalum.Na kwa muda usiozidi wiki mbili.
Sasa kwa bahati mbaya wamama au wadada wamekua wakibadirisha matumizi ya dawa hizi Na kuzifanya kua vipodozi.

Kwa kawaida dawa hizi hunyonywa Na kuingia mwilini Na husababisha kwenda kuzuia tezi la adenal linalozalisha hormone ya adrenalin lisizalishe hormone hiyo.Na endapo matumizi hayo mabaya yataendelea, hufanya tezi hilo lisinyae Na kufa kabisa.

Matokeo ni mengi mabaya endapo tezi hili litakufa ambayo yanaweza kujitokeza mbali Na hayo ya fibroids niliotaja huko juu. Yakiwepo ya kupungua kinga za mwili, Na kupungua kwa kiwango cha homon ya Oestrogen.Na ikipungua umbo au shepu ya kike huanza kukimbia.
Hapo matokeo ni kuota ndevu Na sauti nzito kama mwanaume. Maziwa ya kifuani hunyauka. Na kuingia katika ukomo wa hedhi kabla ya umri. Na kua Na sura nzito kama mwanaume nk.

Sasa ili ujue upo katika kundi la waathiriwa. Tazama lotion yako ,Cream au gelly walipoandika "COMPOSISION"au INGREDIENTS ukiona kuna hizo dawa nilizozitaja hapo juu basi tambua upo katika hatari. Chukua hatua haraka kwa kuanza kuziacha

Na ukumbuke hutakiwi kuziacha ghafla, anza kuacha taratibu.kwani ukiacha ghafla kutokana Na nilioyaeleza huko juu utapata matatizo makubwa.
Kwani hapo ulipo kama vipodozi hivyo ushatumia muda mrefu basi huenda tezi ya adenal haifanyi kazi.
Hivyo itabidi uziache taratibu ili adrenal aanze kurudia majukumu yake ya kiutendaji kazi.

Kwa upande wa option za matibabu kwa waathirika fibroids, ziko option mbili.kutegemea Na chanzo chake
Ya kwanza ni matumizi ya dawa ikiwa ni pamoja Na kurekebisha mfumo wa homon.
Ya pili ni upasuaji ili kuiondoa fibroids yenyewe lakini pia mfumo wa homon ni lazima uangaliwe. Vinginevyo, baada ya upasuaji fibroids inaweza kurudi
Msweet nimatumaini yangu utakua umenufaika, karibu tena
 
Hili swal majibu yake vip?
Habari Mr Aymatu.
Awali ya yote nikuombe radhi kwa usumbufu ulioupata kwa kusubiri kwa muda mrefu.
Lakini lapili nikushukuru kwa kunikumbusha nakuendelea kunifuatilia.
Kwani safari ya huu Uzi ilipoanza tulikua pamoja Na mpaka hivi tuko pamoja
Hivyo basi, Mimi pamoja Na mawazo au mihemko yangu inayonisukuma kujibu maswali mbalimbali, Tunatoa shukurani kubwa kwako kwa ustamilivu wako.

Ama baada ya hayo niende kwenye swali lamsingi Na ningependa nijibu kwa lugha rahisi ili iwe pia faida kwa wengi.

Shahawa(Semen)hutengenezwa tofauti kabisa Na Mbegu.
1 Mbegu za kiume(Sperm) hutengenezwa kwenye Seminiferous tubules.
2 Shahawa (Semin) hutengenezwa kwenye Seminal visicle. Hivyo basi inabidi mbegu (Sperm) zisafiri kwenye mirija maalum (Epidydimis) hadi ziende kujichanganya Na shahawa (Semin) ndipo ziogelee humo.

Sasa basi Mbegu zikiwa zimefanikiwa kutoka kwenye Seminiferous tubules Na kwenda kwenye Seminal visicle.

Hapo shahawa zitaweza kua nzito Na hata rangi itabadirika Na kua nyeupe yenye muonekano kama Grey hivi.na matokeo ni kutungisha mimba.ikiwa kama tendo limefanyika na mmama ama mdada yupo katika Ovulation day.

Kwa hiyo pindi unapo jamiana Na mwanamke shahawa hutoka kwa njia ya (Ejaculation) huingia ukeni huku Mbegu zikiwa zinaogelea ndani yake.
Sasa kama mirija ya Epidydimis itakua imeziba ni kwamba Mbegu zitashindwa kwenda kwenye Seminal visicle.

Matokeo ya hapo yatakua hivi.Utapokua unajamiiana na mwanamke, shahawa(Semin)Zitawahi kukusanyika kwa haraka na
Ijaculation( kukojoa) itawahi sana.Kwa maana shahawa zitakua nyepesi, na ule muonekano wa kama Grey hautokuwepo na Mbegu ndani yake kutakua hamna.

Jingine ni kwamba kama mirija ya Epidydimis itakua imekonda, Mbegu zitasafiri kwa shida ili kufikia kwenye Seminal visicle.

Hali hiyo huzifanya Mbegu kupungua na kua chache katika safari ya kuelekea kwenye Seminal visicle, na zile zilizokua zimebaki. Zitakua zimejeruhiwa kutokana na kukonda kwa mrija huo.

Na katika kujeruhiwa huko kuna zingine hua zimekatika vichwa na zingine mikia.na zingine vichwa na mkia
Na kwa zile Mbegu ambazo hazito katika vichwa wala mikia kwa maana zina sehemu zote tatu kichwa mwili na mkia basi zitakua dhaifu, ila zote kwanzia zilizokatika vichwa na mikia na ambazo dhaifu zote zitafanikiwa kufika kwenye Seminal Visicle.

Matokeo ya hapo yatakua hivi.Ejaculation(kukojoa) hakuto wahi sana itakua ni kama kawaida hivi, kwanza shahawa hazitokua na tishio lolote lililo baya
1 Shahawa zitakua nzito kama kawaida na Rangi itakua nyeupe yenye kuelekea Grey ambayo ni ya kawaida.
2 Mbegu ndani ya shahawa zitakuwemo ila kutakua na makundi mawili ya Mbegu.
A kundi hili ni kundi la kwanza Ambalo Mbegu zake zinavichwa mwili na mkia ila nidhaifu.
B Kundi hili ni kundi la pili ambalo Mbegu zake zimekatika vichwa.na zingine zimekatika mikia.

Kwa ujumla makundi yote mawili hayana uwezo wa kutungisha mimba ingawa Muonekano wa shahawa na Rangi yake vinaonekana viko sawa

Mbegu Zile ambazo zilizokatika vichwa kwa kujeruhiwa njiani zikielekea kwenye Seminal visicle kutokana na kukonda mrija wa Epidydimis.
Hizo pindi Ejaculation itapokamilika hazitokua na uwezo wa kuogelea kabisa na kusonga mbele.
Lakini zile za pili zenye vichwa na mwili ila hazina mikia.
Ni kwamba zenyewe zitakua na uwezo wa kuogelea kusonga mbele ila hazitolifikia yai, kwani Na zenyewe hukatika vichwa muda mfupi baadae zikiwa safarini kulifuata yai

Lakini pia zile zenye vichwa mwili na mikia ila ni dhaifu zenyewe hua za mwisho kufa kwani zenyewe hujitahidi sana na hata kulifikia yai kabisa ila kwa bahati mbaya pale zinapokua katika hatua ya kupenya ndani ya yai nazo hukatika vichwa.

Na hiyo yote ni kwa sababu ya kujeruhiwa kutokana na wembamba wa mirija ya Epidydimis.

Kwa hiyo nivigumu kujua kama Mbegu nyeupe na nzito ndizo zenye uwezo wa kutungisha mimba kwa kuzitazama kwa macho. Ni vema kufanya uchunguzi wa afya ya uzazi.

Kwa kawaida Mbegu inatakiwa ionekane hivi wakati wa uchunguzi
1 kichwa
2 mwili
3 Mkia
Kama Mbegu ikiwa hivi basi wewe itakua na uwezo mkubwa wa kutungisha mimba

Na kiukweli matatizo huanzia hapa unakuta kuna mtu yeye Sperm zake zina kua ni vichwatu.
Mwingine Zinakua na mwilitu.
Mwingine Zinakua na mkiatu.
Mwingine mwili na mkiatu
Mwingine kichwa na mwilitu.

Ndugu Aymatu nimatumaini yangu umeelewa Karibu tena.





Naona limempiga chenga

Naona limempiga chenga
 
Nkingwamh Vip kuhusu viscosity,volume au comcetration ya mbegu je nazo katika kubaini mbegu salama haviangaliwi !

Asante sanaa kwa majibu yako mkuu.
 
Vip kuhusu viscosity,volume au comcetration ya mbegu je nazo katika kubaini mbegu salama haviangaliwi !

Asante sanaa kwa majibu yako mkuu.
Hizo hua Mara nyingi tunamshauri hata mtu binafsi kufanya uchunguzi yeye mwenyewe akiwa nyumbani, kwa hatua hizi.

Viscosity: hapa sperm za mwanaume ukizivuta kwa kidole zinatakiwa zivutike kama 2cm.
Ikivutika zaidi ya hapo humaanisha kuna tatizo katika Sperms hizo.
Sasa hapo kesi hiyo inabidi ituhusu

PH: Pia mtu anaweza Pima PH. Ya sperms yeye mwenyewe akiwa nyumbani kwa kutumia litms peper
Kwa kawaida zinatakiwa ziwe 7-8
Zisizidi ama kupumgua.
Kama hapo kutakua na utofauti wowote basi kesi hiyo itabidi ituhusu

COMSETRATION: Sperm hili itabidi lituhusu kwani ni muhimu kulitambua pia.
Na Sperm zinatakiwa zisipungue chini ya 1 milion. Zikiwa chini ya hapo majibu ni kwamba Sperm zimekua chini ya kiwango iko formular ya Ku culculate.

MORTILITY: Sperm zilizo sawa huwa na mwendo wa risasi.
 
Damu inanitoka mdomoni kirahisi tu ninapojaribu kuswaki au kujinyonya nyama za mdomoni. Je Nifanyeje
 
Dr I'm sorry nimeambiwa kuwa Nina tatizo la optical nerve na wanadai ndio linalochangia gani lakini pia masikio kutotulia kwa ndani yaani yanakuwa kama yanachemka, je ni kweli tiba sahihi ni IPI?
 
Mchubuko usiopona njia ya ajakubwa tatizo ni nini....choo kikiwa raini ni yaleyale kikiwa kigum kidog ndio kabisaaa....nakunywa maji mengi pia matunda nakula sana na choo mala nying napata si kigum ila hii hali haiishi....nisaidie
Habari Dada
Pia pole kwa tatizo hilo. tatizo hilo kwa kweli ni wengi wanahangaika nalo kutokana na kuona aibu.

Sababu ya tatizo hili ikiwa ni wa awali(acute) Mara nyingi huwa hauna sababu maalum. Lakini kuna wakati huweza kusababishwa na upataji wa choo kigumu Mara kwa Mara.

Lakini kama tatizo ni lamuda mrefu kidogo,( chronic) magonjwa kama kaswende TB Saratani Na madonda ya utumbo (chroho'ns disease) ni lazima yachunguzwe.

Kama tatizo sio lamuda sana Fanya kama ifuatavyo. Nunua Tablets Metronidazole 2x3x5/7 Pia nunua Caps Amoxilin 2x3x5/7 Pia nunua Tablets Paracetamol 2x3x5/7.
Hizo zote uwe ukimeza kabla kidogo ya kula. Baada ya kumaliza doese hizo, Nenda tena kanunue dawa hizo hizo.

Lakini awamu hii Metronidazole usimeze kwa mdomo.
Fanya hivi asubuhi ukiamka meza Caps Amoxilin pamoja na paracetamol.Kisha chukua maji moto moto kiasi pamoja na kitambaa safi.
Nenda bafuni uwe unakilowesha kitambaa maji hayo halafu unakibandika eneo la haja(Unyeo) kisha kandamiza kiasi ubaki umeshikilia kama. Dakika 2 kisha chovesha tena kitambaa hicho rudia hivyo kama Dakika kumi hivi.

Baada ya hapo chukua Tabs Metronidazole tembe mbili zisage vizuri kisha.
Unga huo ingiza ndani ya unyeo hasa eneo lile lililo na mchubuko.

Fanya hivyo kutwa Mara tatu na uwendelee kumeza Amoxilin na paracetamol 2x3.
Endelea na zoezi hilo muda wa siku tano, huku ukimeza hizo dawa.

UZINDUSHI:
Unapofanya hivyo hakikisha kama ulikua umeshikwa haja jihudumie kwanza swala hilo. Kisha jisafishe vizuri kabisa.
Baada ya hapo endelea na zoezi hilo.
Jingine ni kwamba, hakikisha ukisha weka jitahidi ukae mda mrefu kidogo bila kwenda haja ili dawa inyonywe
Jingine hakikisha umalizapo kujihudumia haja kubwa hakikisha umejisafisha vizuri na kujikausha vyema
Jingine kwakua tuna hitaji mchubuko upone inabidi mda wote wa dawa uwe ukijikinga na kupata haja ngumu kwa kunywa maji matamu tamu( Juice) na kula chakula ambacho ni rahisi kulainika.
Jingine hakikisha kitambaa kila umalizapo shuuri hiyo kifue vizuri kabla ya kukitumia tena.

Fanya hivyo kisha baada ya kumaliza siku tano ya zoezi hilo. Ulete mrejesho
Kama bado tutakupatia ushauri wa vipimo kubaini nilioeleza huko juu.
Asante na karibu tena.
 
Kama kichwa kinavyosema hapo nakaribisha maswali yanayo husu afya
1. Kuwashwa sehemu za siri baada ya kunyoa, nitumie dawa gani?
2. Mikono kupata ganzi na kuuma usiku baada ya kulala, nijaribu dawa gani.
Natanguliza shukran
 
Damu inanitoka mdomoni kirahisi tu ninapojaribu kuswaki au kujinyonya nyama za mdomoni. Je Nifanyeje
Habari Ndugu.
Hali kama hiyo ikiwa haiambatani na dalili zingine.
Huenda ukawa unasumbuliwa na mgonjwa ya fizi.

Kuna aina kubwa mbili za mgonjwa ya fizi ambayo ni
1. Gingivitis
2. Periodontitis
Ninakushauri ukaonane na daktari wa meno kwa uchunguzi zaidi.
Mimi sipendi kukwambia unaupungufu kua unaupungufu wa vitamin C.
Kwa maisha ya kawaida sio rahisi kua na upungufu namna hiyo
Kwanza tuanze na sababu ambazo ni tishio ndio tuje kumalizia na mambo ya vitamin.

Habari Dada
Pia pole kwa tatizo hilo. tatizo hilo kwa kweli ni wengi wanahangaika nalo kutokana na kuona aibu.

Sababu ya tatizo hili ikiwa ni wa awali(acute) Mara nyingi huwa hauna sababu maalum. Lakini kuna wakati huweza kusababishwa na upataji wa choo kigumu Mara kwa Mara.

Lakini kama tatizo ni lamuda mrefu kidogo,( chronic) magonjwa kama kaswende TB Saratani Na madonda ya utumbo (chroho'ns disease) ni lazima yachunguzwe.

Kama tatizo sio lamuda sana Fanya kama ifuatavyo. Nunua Tablets Metronidazole 2x3x5/7 Pia nunua Caps Amoxilin 2x3x5/7 Pia nunua Tablets Paracetamol 2x3x5/7.
Hizo zote uwe ukimeza kabla kidogo ya kula. Baada ya kumaliza doese hizo, Nenda tena kanunue dawa hizo hizo.

Lakini awamu hii Metronidazole usimeze kwa mdomo.
Fanya hivi asubuhi ukiamka meza Caps Amoxilin pamoja na paracetamol.Kisha chukua maji moto moto kiasi pamoja na kitambaa safi.
Nenda bafuni uwe unakilowesha kitambaa maji hayo halafu unakibandika eneo la haja(Unyeo) kisha kandamiza kiasi ubaki umeshikilia kama. Dakika 2 kisha chovesha tena kitambaa hicho rudia hivyo kama Dakika kumi hivi.

Baada ya hapo chukua Tabs Metronidazole tembe mbili zisage vizuri kisha.
Unga huo ingiza ndani ya unyeo hasa eneo lile lililo na mchubuko.

Fanya hivyo kutwa Mara tatu na uwendelee kumeza Amoxilin na paracetamol 2x3.
Endelea na zoezi hilo muda wa siku tano, huku ukimeza hizo dawa.

UZINDUSHI:
Unapofanya hivyo hakikisha kama ulikua umeshikwa haja jihudumie kwanza swala hilo. Kisha jisafishe vizuri kabisa.
Baada ya hapo endelea na zoezi hilo.
Jingine ni kwamba, hakikisha ukisha weka jitahidi ukae mda mrefu kidogo bila kwenda haja ili dawa inyonywe
Jingine hakikisha umalizapo kujihudumia haja kubwa hakikisha umejisafisha vizuri na kujikausha vyema
Jingine kwakua tuna hitaji mchubuko upone inabidi mda wote wa dawa uwe ukijikinga na kupata haja ngumu kwa kunywa maji matamu tamu( Juice) na kula chakula ambacho ni rahisi kulainika.
Jingine hakikisha kitambaa kila umalizapo shuuri hiyo kifue vizuri kabla ya kukitumia tena.

Fanya hivyo kisha baada ya kumaliza siku tano ya zoezi hilo. Ulete mrejesho
Kama bado tutakupatia ushauri wa vipimo kubaini nilioeleza huko juu.
Asante na karibu tena.
 
Dr I'm sorry nimeambiwa kuwa Nina tatizo la optical nerve na wanadai ndio linalochangia gani lakini pia masikio kutotulia kwa ndani yaani yanakuwa kama yanachemka, je ni kweli tiba sahihi ni IPI?
Habari ndugu.Katichi
Kabla sijaenda katika tatizo lako ningependa ujibu awali moja.
1 Katika matatizo yanayokusumbua kwanzia Ganzi, na masikio Je na macho hua yanakusumbua hasa upande wa Uoni?
 
Dr. Nkingwamh, tafadhali, kuna mwenye kidonda CHEUPEE, hakiwi chekundu wala hakitoki damu, hasikii maumivu hata kikiguswa ila kinatoa majimaji mepesi sana na hakinuki kabisa! Je hiki ni kidonda cha aina gani na dawa yake ni nini? Asante.
 
1. Kuwashwa sehemu za siri baada ya kunyoa, nitumie dawa gani?
2. Mikono kupata ganzi na kuuma usiku baada ya kulala, nijaribu dawa gani.
Natanguliza shukran
Habari ndugu Tatizo la kuwashwa sehemu hizo. Sijambo geni sana. Na ni watu wengi huwasumbua.
Kama haliambatani na Dalili nyingine basi ninachosema ondoa Presha.

Baadhi ya wataalamu wamekua wakihusisha tatizo hilo na magonjwa ya zinaa. Hasa kaswende.
Nikweli kaswende kuna wakati huanza na dalili kama vipele. ama vidonda isipokua sio lazima viwe sehemu za siri

Kumbuka vipele havichagui sehemu ya kukaa, vinaweza kukaa kichwani usoni ama sehemu yoyote ile ili mraditu pawe ni sehemu ya ngozi

Mbona vipele vikitokea usoni au miguuni watu hamshituki? Ila vikitoka kwenye eneo hilo. Haraka sana Asubuhi kwenye duka la dawa!

Uzoefu unaonyesha kua kama mtu hupenda kunyoa nywele hasa za maeneo laini kwa wembe wa kawaida.
Ni kwamba pale vinapoanza kuchomoza vinywele vipya lazima vipele vijitokeze.

Kwani mkuu vipi ukinyoa ndevu hivyo vipele hua havikuji?

Kama hakuna tatizo lingine hivyo vipele ni vya kawaida kabisa

Nimetoa Maelezo yote hayo kwa sababu mahusiano mengi yameharibika kwa sababu ya mpenzi mmoja kuonekana na vipele hivyo.
Kwa uwelewa Mdogo hudhaniwa ni magonjwa yazinaa.

Na kiukweli Mara nyingi watu wamekua wakitibiwa kwa gharama kubwa, kwa kudhaniwa ni magonjwa ya zinaa.
Biashara hii inafanyika sana huko kwenye Zahanati na maduka ya dawa mijini na hata vijijini.

Njia pekee ya kukaa kwa amani unapoona vipele hivyo Nenda ukafanye uchunguzi wa vipimo.
Usikubali kupewa au kununua dawa pasipo uchunguzi. Utaibiwa fedha na wakati mwingine unaweza kupata madhara kutokana na dawa hizo.

USHAURI WANGU
Ukinyoa nywele za sehemu laini badiri life style kwa muda hadi nywele zitoke kidogo.
1 Usivae boxer
2 Ukioga jikaushe maji kabisa ndio uvae
3 Usijipulizie Pafyum.
Kama ni makwapani
4 Penda kuvaa shati la mikono mifupi
5. Vaa mashati mepesi.
6 Ukiwa nyumbani penda kuvaa Sindlend

Kuhusu kufa ganzi mikono na kuuma wakati umelala Yawezekana kukawa na hitilafu kwenye neva zako.
Jaribu dawa hii kwanza ikiwa bado rudi hapa tutakupatia ushauri wa vipimo zaidi
Tabs Vitamin B-Comlex 1x3x5/7
Tabs Neurobian 1x2x5/7.
BBC karibu tena.
 
  • Thanks
Reactions: bbc
Hbar kiongz? Mungu akubarki sana! Kwanz kwa karne Kama hii kupata mtu kama ww ni ngumu!! Ww ni MAKONDA B ... Mm naitwa Raymond ninaishi Gmboto, ilala ,dar..
Nilikuwa na mambo kama mawili hivi au matatu unisaidie;
1. BIMA YA AFYA.
Nimejarb kufatilia google na kwa baadhi ya watu lkn bado wanashndwa kunipa majibu sahihi ya maswali yangu, kiufp nilitaka kujua faida za bima ya afya, (ii) Hipi nzuri hisiyozidi 150,000 kwa mwaka?
2. Nilitaka kujua kuhusiana na ULTRA SOUND na inafanyje kazi?
3. Nasumbuliwa na allegy zifuatazo
Food colour
Dust
Plastic material
Pollens za maua
Nyasi
Heat (Joto Kali)
Vitu vya baridi
Samaki
Mayai
Alluminium
Vitu vya shaba...
MATOKEO
1. Nawashwa sana nikimaliza Kuoga.
2.Maumivu ya kifua yaani vichomi
3. Moyo kuuma sana kama unavilia hasa wakati wa usiku..
4.Muwasho mtamu wakat wa usiku.. Je, nimatokeo ya hizo allegy?
3. Nilipima kama ninatatizo kwny Moyo kwa kipimo cha kutoa damu kwny mshipa.. Je, kuna kipimo kama hicho au nilitapeliwa?
Whatsup 0657 230355.. Mungu akubariki
Usimfananishe uyu Dokta na vitu vya ajabu
 
Dr. Nkingwamh, tafadhali, kuna mwenye kidonda CHEUPEE, hakiwi chekundu wala hakitoki damu, hasikii maumivu hata kikiguswa ila kinatoa majimaji mepesi sana na hakinuki kabisa! Je hiki ni kidonda cha aina gani na dawa yake ni nini? Asante.
Habari bwana Wajad.
Kabla ya kukupatia Maelezo Naomba nijue hicho kidonda kina mda gani na kilianza vipi.
 
Ukinyonywa uume na mwanamke mwenye virusi kwa sec 15 je,utapata maambukizi?
 
Habari ndugu Tatizo la kuwashwa sehemu hizo. Sijambo geni sana. Na ni watu wengi huwasumbua.
Kama haliambatani na Dalili nyingine basi ninachosema ondoa Presha.

Baadhi ya wataalamu wamekua wakihusisha tatizo hilo na magonjwa ya zinaa. Hasa kaswende.
Nikweli kaswende kuna wakati huanza na dalili kama vipele. ama vidonda isipokua sio lazima viwe sehemu za siri

Kumbuka vipele havichagui sehemu ya kukaa, vinaweza kukaa kichwani usoni ama sehemu yoyote ile ili mraditu pawe ni sehemu ya ngozi

Mbona vipele vikitokea usoni au miguuni watu hamshituki? Ila vikitoka kwenye eneo hilo. Haraka sana Asubuhi kwenye duka la dawa!

Uzoefu unaonyesha kua kama mtu hupenda kunyoa nywele hasa za maeneo laini kwa wembe wa kawaida.
Ni kwamba pale vinapoanza kuchomoza vinywele vipya lazima vipele vijitokeze.

Kwani mkuu vipi ukinyoa ndevu hivyo vipele hua havikuji?

Kama hakuna tatizo lingine hivyo vipele ni vya kawaida kabisa

Nimetoa Maelezo yote hayo kwa sababu mahusiano mengi yameharibika kwa sababu ya mpenzi mmoja kuonekana na vipele hivyo.
Kwa uwelewa Mdogo hudhaniwa ni magonjwa yazinaa.

Na kiukweli Mara nyingi watu wamekua wakitibiwa kwa gharama kubwa, kwa kudhaniwa ni magonjwa ya zinaa.
Biashara hii inafanyika sana huko kwenye Zahanati na maduka ya dawa mijini na hata vijijini.

Njia pekee ya kukaa kwa amani unapoona vipele hivyo Nenda ukafanye uchunguzi wa vipimo.
Usikubali kupewa au kununua dawa pasipo uchunguzi. Utaibiwa fedha na wakati mwingine unaweza kupata madhara kutokana na dawa hizo.

USHAURI WANGU
Ukinyoa nywele za sehemu laini badiri life style kwa muda hadi nywele zitoke kidogo.
1 Usivae boxer
2 Ukioga jikaushe maji kabisa ndio uvae
3 Usijipulizie Pafyum.
Kama ni makwapani
4 Penda kuvaa shati la mikono mifupi
5. Vaa mashati mepesi.
6 Ukiwa nyumbani penda kuvaa Sindlend

Kuhusu kufa ganzi mikono na kuuma wakati umelala Yawezekana kukawa na hitilafu kwenye neva zako.
Jaribu dawa hii kwanza ikiwa bado rudi hapa tutakupatia ushauri wa vipimo zaidi
Tabs Vitamin B-Comlex 1x3x5/7
Tabs Neurobian 1x2x5/7.
BBC karibu tena.
Kwanza nakushukuru sana kwa kuacha shughuli zako kuweza kunijibu namna hii, nakushukuru sana. Pili nikinyoa ndevu vipele havitokei wala kuwasha hakutokei ni sehemu za siri na ni wakati zinapoanza kuota nywele. Hapo hutamani hata kujikuna kwa gunzi lakini zikiishaota kuwasha kunaisha. Tatu nakushukuru kwa hizi dawa ulizoniandikia ngoja nijaribu. Naomba usituchoke sisi waulizaji. Shukran
 
Habari bwana Wajad.
Kabla ya kukupatia Maelezo Naomba nijue hicho kidonda kina mda gani na kilianza vipi.
Kilianza kama kichunusi kilichoota chenyewe halafu kikakatika, sasa kina ukubwa wa kama shilingi mia tano ya sarafu. Ni kama miezi mitatu sasa .
 
Back
Top Bottom