Naomba kufahamu kwa undani zaidi, madhara ya mtoto anapozaliwa na kunywa yale "maji machafu"..... in layman's language... 'Maji machafu'... Maji hayo ni nini???? Nini madhara anayoyapata mtoto kiafya, kiakili, na mambo ya ziada ambayo kitaalamu unaweza kuyazungumzia. Nini cha kufanya kuweza kuweza kuzuia hali hii....
Asante.
Habari msweet
Kwanza kabla ya kujua madhara.
Ningependa tumjue kwanza mtoto alietumboni.
Anaishije huko, na kwanini anakua!.
Mama au Dada anapo bahatika kushika mimba. Kutoka siku ya kwanza hadi wiki ya 8, ile mimba hutambuliwa kama "Embryo" yaani humaanisha 'kukua ndani'.
Wakati kama huu kwa yule mama mjamzito hujulikana kama Embryonic Period. Huhusishwa na kuumbwa kwa mifumo muhimu ya viungo vya mwili.
Kwanzia wiki ya 8 hadi mwisho wa Mimba, kiumbe hicho hutambuliwa kama Fetus(kijusi) au kwa lugha yetu ni mwana ambae hajazaliwa. Na wakati kama huu hujulikana kama Fetal Period.(wakati wa kijusi) yani mwili kuanza kukua na sehemu Fulani za mwili kuanza kufanya kazi.
Baada ya wiki ya kwanzatu ya kuingia mimba, chembe mrundiko ya ndani, huunda nusu mbili.
Ya kwanza huitwa hypoblast, na yapili huitwa Epiblast.
Hizi zote zina kazi tofauti katika maendeleo ya kukua kwa mtoto.
HYPOBLAST
Hii huzalisha ule mfumo wa maji ambao ni sehemu muhimu moja wapo ya muundo wa kupitisha chakula kutoka kwa mama kwenda kwa mtoto.
EPIBLAST
Huunda mfumo mwepesi (Membrane) ufunikae mtoto. Na kuhifadhi Amnion fluids, ambayo kijusi kitalelewa humo hadi kuzaliwa.
Baada ya hapo Epiblast pia huendelea kuunda chembe tatu maalum au miundo chipukizi.
Ambazo ni.
1 Ectoderm
2 Endoderm
3 Mesoderm
Ectoderm:
hufanya kazi ya kuchipuza na kuzifanya sehemu muhimu nyingi, ikiwemo Ubongo, Uti wa mgongo,Vichocheo, Ngozi, Vidole, na Nywele,
Endoderm:
Huzalisha au kuunda sehemu za ndani za mfumo wa Pumzi na mmeng'enyo na huzalisha sehemu kubwa muhimu kama vile Ini na Pancries.
Mesoderm:
Huunda Moyo, Figo, Mifupa, Ufupa mwororo, Misuli, Chembe za Damu. Na viungo zingine.
Wakati chembe za damu zinapojitokeza katika ule Mfuko wa maji. Mifereji ya damu, huundwa kote kote kwenye embryo na Sehemu ya mwanzo ya Moyo huanza kuchipuza.
Karibu Mara moja ule moyo unaanza kukua kwa haraka, huanza kujikunja na Sehemu zake muhimu huanza kuumbika.
Moyo huanza kupiga kwazia wiki 3 na siku moja. baada ya kutunga mimba.
Mfumo wa kuzungusha damu, ni mfumo wa kwanza wa mwili. Au kundi la viungo vya kwanza kuanza kufanya kazi.
Kati ya wiki ya 3 na ya 4. Mpangilio wa Umbo la mwili huanza kuchipuza
Huku Ubongo na Uti wa mgongo na Moyo huanza kutambulika Pamoja na ule mfuko wa maji.
Ukuaji wa haraka husababisha kujikunja kwa kijitoto, ambavyo kwa kawaida hua kimenyooka
Mfanyiko huu hujumuisha sehemu ya ule mfuko wa maji na kua sehemu ya kuta ya mmeng'enyo.
Na kuunda kifua na sehemu za mmeng'enyo wa huyu binadamu chipukizi.
Maendeleo hayo ya kibiolojia ya ukuaji wa mtoto yenye kustaajabisha huendelea hivyo hadi kufikia kipindi cha wiki 16 (miezi minne.) Hapo kijusi au kiumbe hicho kipya huanza kufanya kazi karibu viungo vyote.
Na hisia mbalimbali zinazoendelea nje huanza kuhisi na kusikia.
Kipindi hiki sasa Amniotic fluids hutengenezwa kwa wingi kabisa kwa ajili ya kumlinda mtoto dhidi ya maambukizi na kufanya maendeleo ya ukuaji wake yawe bora.
Pia amniotic fluid humpa joto mtoto na kulihifadhi. Pia humsaidia mtoto kwenye mmeng'enyo na upumuaji
MATOKEO YA DHARULA
Kuna matokeo ya dharula ambayo ni hatari kwa kiumbe hicho.
Matukio ya hatari yanapo onyesha viashiria ni haraka mama awahi hospitali.
Ili dactari alichunguze tukio hilo na kulichukulia hatua Mara moja.
1 Chupa ama fuko linalomhifadhi mtoto kupasuka kabla ya wiki 37(Prematura repture of membranes) hali hii ni hatari sana mama inabidi awahi hospitali haraka sana.
Sababu mtoto hapo atakua katika hatari ya kupata maambukizi.
Na usalama wake utakua ni mdogo kwakua Yale maji yanayomlinda yamewahi kutoka.
Hapo dactari atachukua vipimo kubaini chanzo cha tatizo pamoja na maelezo ya mama mwenyewe.
Dactari anaweza akam bed rest ama kumwanzishia uchungu haraka ili ajifungue kama mimba itakua na zaidi ya wiki 34. Yote hayo yanaweza kufanyika endapo dactari atavyoliona tukio lenyewe.
Endapo Dactari ataamua mama arudi nyumbani. Basi anaweza kumpatia antibiotic ili kuumlinda mtoto dhidi ya bacteria. Pamoja na kumchoma mama sindano Fulani za steroid ili kumsaidia mtoto kwenye ukuaji wa mapafu.
Pia wakati chupa hiyo imepasuka na ni kabla ya siku kama nilivyoeleza. Mama inambidi. Awe makini ajiepushe kutumia vyoo vya paplic. Na endapo atatumia awe makini sana.
Vile vile mama asifanye mapenzi kabisa mpaka atapojifungua. Pia mama asijiweke vidole ukeni. Pia asioge kwenye tub bath.Kwani hivyo vyote huweza kumuweka mama katika hatari ya kuongeza maambukizi.
Lakini wa mama inawabidi kua makini pindi mnapoona chupa imepasuka kabla ya muda na kuchunguza Yale maji yaliotoka. Kwani utapokwenda hospitali na maelezo ukatoa kadiri ulivyoona husaidia sana kupata huduma kwa haraka.
Kwani humrahisishia daktari kutokutumia muda mkubwa wa kuamua.
Kwa kawaida maji ya chupa hua hayana rangi wala harufu.
Endapo mama ataona rangi ya kijani au brown na harufu. Hiyo ni dalili ya maambukizi.
Au huenda mtoto amejisaidia choo kubwa. Ama alipata risk Fulani iliopelekea kujisaidia choo kubwa.
Au kama utaona wekundu huenda yakawa maji hayo yamechanganika na damu.
Yote hayo mama atapoeleza humrahisishia daktari kukuwahishia huduma.
Kwa mama aliefikisha wiki 36 chupa ikipasuka daktari huanzisha uchungu ili mama ajifungue kuliko kumwacha. au kumfanyia C- section itategemea na afya ya mama kwa kipindi hicho.
2 Kuna tukio lingine ambalo mama kisha pata uchungu na chupa ime pasuka lakini mtoto anakua kachelewa kutoka. Tukio hili hupelekea mtoto kunywa maji hayo. Ambayo Mara nyingi huwaathiri watoto kwenye mapafu na mfumo wa upumuaji.
Ima kuna wakati mwingine mtoto anaweza kutoka akiwa kichwa kimetazama juu. Hili nalo huweza kusababisha mtoto kuonja au kunywa maji hayo. Maji hayo yakaingia kwenye mapafu huathiri mfumo wa upumuaji.
Baada yakua ushatoka hospitali, kisha ukamuona mtoto ngozi inabadirika rangi kua kama blue hivi. Huenda ikawa mfumo wa upumuaji hauko sawa au alikunywa maji hayo. Rudi hospitali haraka kamweleze daktari.
Hayo yote kama mama atajifungulia katika kituo cha afya Dactari anaweza kuondoa hatari hizo kwa asilimia 80.
Kwa hiyo wamama ninawashauri pale unapohisi mjamzito na kuthibitika mjamzito. Pageuzeni katika vituo vya afya kua ni nyumbani.
Namaanisha chochote utachokiona tofauti wahi haraka katika kituo cha afya na Mara utapoona leba inaanza nenda kajifungulie hospitali.
Hiyo itakusaidia kuondoa hatari hizo nilizo zitaja.
Kwako msweet natumaini utakua umeelimika na Umma kwa ujumla.