Kuumwa na kichwa Mara kwa Mara tatizo nini
Habr Mr.Miraji. Kuumwa nakichwa Mara kwa mara, Mara nyingi hakusababishwi Na sababu za hatari, au hakumaanishi kua kuna ugonjwa mbaya sana unaoendelea mwilini.
Lakini wakati mwingine kunaweza kumaanisha kua kuna ugonjwa wa hatari mwilini unao hitaji matibabu ya haraka.
Kuumwa Na kichwa kunaweza kugawanyika katika makundi kadhaa kutokana Na visababishi kama ifuatavyo.
1 Maumivu ya kichwa ya awali (Primary headache)
Maumivu haya husababishwa Na kuongezeka kwa hisia za maumivu katika viungo vinavyo tambua maumivu ndani ya ubongo.
Mfumo wa kemikali katika ubongo, mishipa ya fahamu, mishipa ya damu ya nje ya fuvu ama misuli ya shingo Na kichwa, huchangia kusababisha maumivu ya kichwa ya awali.
Kuna baadhi ya watu wao wamebeba vinasaba vinavyo sababisha wao kupata maumivu haya maishani mwao.
Aina hii ya maumivu ya kichwa nayo imegawanyika katika makundi makubwa mawili.
( A )MAUMIVU YA KICHWA YA MIGRAINE(MIGRAINE HEADACH)
Aina hii ya maumivu ya kichwa ndio ambayo imeenea sana. Na watu wengi wanaosumbuliwa Na maumivu ya kichwa ya Mara kwa Mara hua Na tatizo hili la migraine.
Maumivu haya yanaweza kua ya upande mmoja.lakini yanaweza kua katika paji la Uso.pia Na kusikika katika eneo lote la paji la uso Na shingo.
Aina hii Mara nyingi hua ni ya kichwa kugonga"(throbbing pain) Na huambatana Na dalili kama vile kichefu chefu au kutapika, kizunguzungu, macho kushindwa kuona vizuri, Na macho kuuma pindi yanapoangalia mwanga.
Na mgonjwa wa maumivu haya hujisikia nafuu pindi akipumzika.
Pia mtu mwenye tatizo la migraine endapo atakua anatumia vitu kama vinywaji vyenye kemikali ya caffeine au pombe( alcohol)Sigara husababisha kuchochea zaidi kumwa kwa maumivu hayo.
Pia Mawazo, Uchovu,Hasira, nayo ni miongoni mwa mambo yanayochochea maumivu haya.
Aina hii pia huweza kuwasumbua wanawake ambao wako katika umri wa kuweza kushika mimba.
Ambao ndio wameanza kupata hedhi zao hivi karibuni.
(B) MAUMIVU YA KICHWA CHA MGANDAMIZO."(TENSION HEADACH).
Maumivu haya ya kichwa kwa kawaida hua ya kugangamiza,/kukaza(Pressing /tightening) Na hua yanatokea kwenye pande zote za paji la uso, kuelekea utosini.( Frontal-occipital).Na haya hua hayaongezeki pindi mgonjwa anapotembea kama ilivyo kwa migraine.
Pia hayaambatani Na dalili za kichefu chefu ama kutapika, ama kizunguzungu.
Lakini Mara nyingi maumivu haya huanza pale mtu anapokua Na msongo wa mawazo, au kukosa usingizi.(Insomnia)
MAUMIVU YA KICHWA (SECONDARY HEADACH)
Aina hii ya tatizo Mara nyingi husababishwa na Tatizo ambalo liko ndani ya damu Na mgonjwa hupata maumivu haya kama matokeo au ishara ya tatizo katika mwili.
Maumivu ya namna hii Mara nyingi yamekua yakiambatana Na dalili zingingine ambazo pia zimekua zikisababishwa Na tatizo la msingi.ambazo ni
1 Homa
2 kutapika
3 kupungua uzito
4 Dalili za mfumo wa fahamu (kuchanganikiwa, kuzimia,kupungua kwa hali ya ufahamu,macho kushindwa kuona,mwili au sehemu ya mwili kupooza)
5 Maumivu ya viungo/ mifupa.
Mara nyingi sababu za maumivu haya hua ni maambukizi ya bacteria au virusi.
Kuna wakati mwingine maumivu ya kichwa huchangia sana Na mifumo ya maisha tunayoishi ambayo ni kinyume Na kanuni za afya.
Kama vile kutokunywa maji ya kutosha,kutopata usingizi wa kutosha,kufanya kazi sana kupita kiasi kupelekea uchovu uliopitiliza,Na matumizi ya vinywaji vyenye caffeine Na Pombe Na Sigara.
Hivyo basi nibora kuishi kwa kufuata kanuni za afya ili kujikinga Na maumivu haya ya kichwa ya Mara kwa mara.
Na kama unafuata kanuni za afya Na bado unashambuliwa Na maumivu haya.
Kua ukijibu maswali haya wewe mwenyewe kabla ya kwenda Hosp.
1 kichwa kinauma,Je kinaambatana Na Homa?
2 kichwa kinauma kinaambatana Na dalili za mfumo wa fahamu?
3 kichwa kinauma kinaambatana Na maumivu ya viungo Na mifupa?
4 kichwa kinauma kinaambatana Na kupungua uzito?.
Kichwa Kikiwa kinauma Na ikiwa unajibu maswali haya "ndio" zikapatikana basi ninashauri fika katika kituo cha afya haraka ili uchunguzi zaidi ufanyike.Mr. Miraji Na Umma kwa ujumla nimatumaini yangu mmeelewa.
Kama kuna maswali mengine Mimi kwenu ni wito Na ninawakaribisha tena.
Sent from my itel it1556 Plus using
JamiiForums mobile app