Karibuni kwa maswali yote ya kiafya

Karibuni kwa maswali yote ya kiafya

Naomba kufahamu vertigo na tiba yake
Habari ndugu;
Vertigo ni ishara au ashirio la kua kuna kitu Fulani hakipo sawa mwilini hivyo kupelea mtu kuona kizungu zungu.
Hali hiyo huweza kumtokea mtu yoyote.
Sababu ziko nyingi, inaweza kua ni upungufu wa damu, kuongeka kusiko kawaida kwa damu,maambukizi kwenye uti wa mgongo, hitilafu katika mfumo wa kinga mwili.na hitilafu Fulani maeneo ya kichwa n.k
Tiba inategemea na chanzo cha tatizo lenyewe cha msingi hapo ni kufika hospitali na kufanyiwa uchunguzi. Asante
 
Habari Dr. Naweza sema nina tatizo au sijui ni nini maana ninasumbuliwa na maumivu ya korodani (Pumbu). Huwa inanitokeaga nikiwa na malaria pale homa inapopanda, na wiki mbili zilizopita niliumwa kama siku nzima hadi kutembea ni shida. Je tatizo au chanzo ni nini maana nishawahi sikia redioni wakisema maumivu ya mara kwa mara ya korodani yanaweza sababisha upungufu kama sio ukosefu wa nguvu za kiume.
Habari ndugu GRU:
Maumivu ya korodani Ni ashirio la kua katika vifuko vilivyo hifadhi korodani hakuko sawa.
Inaweza kua korodani zimejinyonga au kuna maambukizi yalio sababisha uvimbe ndani ya kifuko hicho na kutumia nafasi kubwa. Hivyo kupelekea kuzibana korodani zenyewe au inaweza kua unaziumiza wewe mwenye korodani kwa kuzibana na kusababisha kusagana zenyewe.
Na hilo ni kutokana na haya mambo ya kizungu. Yani wakati unapokutana kimwili na mwanamke kunakua na style ambazo zina kwenda kuziumiza korodani moja kwa moja.

Ninakushauri fika katika vituo vyetu vya afya ili ufanyiwe uchunguzi. Hasa chunguza magonjwa ya zinaa.
Kama kutakua hakuna unaweza rudi tukasonga mbele zaidi kwa ushauri zaidi.
Asante.
 
Habari Dr,
Tunashukuru kwa Ukarimu wako kuendelea kutuelimisha habari ya afya,
Naomba msaada, Mume wangu ana shida ya tumbo kwa muda mrefu, akila chakula anasema ni kama kinakwama kwenye "chembe ya moyo"- hapa chini ya kifua kidogo, na huchukua muda kuyeyushwa,
Pili kuna wakati anakuwa hana apetite ya kula anakula kwa kujilazimisha tu,
Tatu kwa kipindi hiki kuna baadhi ya vyakula anashindwa kula anasema vinampa kichefu chefu kama dagaa, samaki n.k.
Tulienda hosptl akapima kipimo kile cha kuingizwa sijui ni mrija mdomoni mpaka tumboni ikaonekana vidonda vya tumbo ni kama vinamuanza, pia aliambiwa ana tatizo la acid nyingi tumboni, hapati kiungulia.
kuna baadhi ya dawa ambazo huwa anapewa zinatuliza kwa muda then anaendelea kuumwa,
NAOMBA UNISAIDIE:
1. inawezekana kuna shida nyingine inayopelekea matatizo haya na afanye nini? kila siku hana raha yaani
2. Ni vyakula gani anaweza kutumia vinavyoweza kupunguza kiasi cha acid tumboni?
Ahsante.
Habari Dada:
Pole kwa tatizo la mumeo. Katika maelezo yako hapa, hujanieleza baada ya kugundulika vidonda kama kuna Shambulio la H.pylori.
Lakini kwakua lishakua linamuda mrefu ni lazima shambulio hilo Lita kuwepo.

Mi kabla ya kukueleza kua ni chakula gani. Napenda nikueleze kua mumeo usitake awe mtumwa wa tatizo hilo.
Ninamaanisha kwamba kutaka kujua vyakula ambavyo akila havito mletea shida ni kuruhusu yeye aendelee kushambuliwa.
Halafu wewe ukimtengenezea mazingira ya kutokusikia maumivu. Hii ni njia isio sahihi kabisa.

Cha msingi kwakua tatizo ni la muda mrefu, dawa za antibiotic zinahitajika sana kwake kwa ajili ya kushambuliwa H.pylori bacterial.
Ambazo ni hizi hapa!
1 Tablets Metronidazole
2x3x7/7
2 Caps Amoxilin
2x3x7/7
Lakini kwakua asidi imekua ikizalishwa kwa wingi sasa, inabidi atumie dawa Proton pump inhibitors
'PPIs' kama Omeprazole.Esomeprazole,na lansoprazole.
Hapo ni kufanya chaguzi ya dawa aina moja, kwani hizo zote hufanya kazi moja.
Proton pump inhibitors hufanya kazi kwa kuvunja / kuzuia kazi ya proton ziitwazo proton pump ambazo huhusika katika utengenezaji wa asidi tumboni.

Sasa wakati kama huu ukiwa katika kutumia dawa za kuzuia uzalishwaji wa asidi, ni vema sasa kuupunguzia mwili ongezeko la asidi

Kuna vyakula ambavyo hatakiwi kutumia ili kuupunguzia mwili ongezeko la asidi. vyakula hivyo ni
Vyakula vyenye viungo vingi. Malimau, ukwaju.na Jamii nzima ya vitu vikali kama limau.nk
Viungo kama pili pili kina sababisha kidonda chenyewe kiwe na maumivu makali.
Jamii ya caffein na Pombe pia ni hatari kwa mgonjwa wako
Pia ni vema kula chakula kikiwa na hali ya ulaini ili kuepusha ongezeko la michubuko kwenye vidonda.
Asante.
 
niliwah kuwa na tabia ya kuwa kujizonga tishu kwenye uume kutokana na wasisi wa majiji baada ya kutoka chooni, nilikua nikifanya ivo mpaka ninapohisi pamekauka. Mda mwengine nikijisahau mpaka kufika jioni mpaka unakuta ile tishu au toilet paper imeganda na ngozi. ikafika mda ikawa nikijigusisha tishu au toilet paper tu nahisi maumivu ya mchonoto. Nikaacha kabisa hiyo tabia na miaka imepita. Lakini mpaka hii leo ikitokea hata bahati mbaya kugusisha Toilet paper na uume nahisi maumivu.
Naomba msaada juu ya hili. hofu yangu ni kuja kupata maradhi au kua na dalili za maradhi.
 
Doctor naomba msaada mke wangu ana tatizo la kuganda kwa damu
Naomba msaada ni dawa gani atumie
 
Mke wangu ana kilo 82
Habari bwana mawese nimejaribu:
kuhusisha tatizo lako kwa mambo mbalimbali naona inakua ngumu kupata majibu ya moja kwa moja, zaidi ya kukueleza mambo haya yafuatayo.
Kwakua hupati Homa na tatizo lenyewe ni la mda mrefu ni kwamba tatizo hilo liko nje ya uti wa mgongo na nimehusisha na vifupa spines hivi hapa LO1 vertebra kwenye Lumbar spine ni kifupa mwiba cha tano kutoka chini.
Hapo katika kifupa hiki kuna kona kubwa ambayo imekimbilia nyuma zaidi. Ambapo ukisema unyooke vizuri kifupa mwiba hicho kinagusana na LO2 vertebra ambacho ni kifupa mwiba cha nne kutoka chini.

kwa hivyo hapo kuna kua hakuna space zinazoachiana zaidi ya kusagana.
Na vikisagana maumivu yanaanzia hapo, na kusambaa kwenye eneo lote la uti wa mgongo.

Ushauri wangu kwako, mkeo huyo ulienae kwa uzito alionao ndio atakua dawa kwako.
Kila siku muda wa kulala pamoja na asubuhi kabla ya kwenda kazini
Lalia tumbo kisha mkeo awe akikukalia mgongoni katikati. Maeneo ya usawa wa mbavu. Pale juu sio bondeni kuelekea kiunoni.

Na awe akikukalia akitazama miguuni kwako.na akae kwa kujiachia, huku akinesa nesa kama kakalia kiti chenye springi.
Afanye hivyo kama dakika 20 kila siku na wakati huo uwe ukitumia dawa hii yenye mchanganyiko wa dawa mbili.
Glucosamine sulfate 500mg
And chondroitin 400mg
Dawa hii tumia 1x1 kwa siku,kwa muda wa wiki 2

Pia Zingatia haya.
1 Unapokutana na mkeo kimwili, hakikisha awe juu yako na asikae akanyooka, atapokua juu yako halafu akulalie kifua chote.
2 Hakikisha usiinue kifua kumfuata aliko, kua na style hiyo hadi wote mmalize haja za miili yenu.
Kufanya hivyo ni kwa ajili ya kujaribu kuipunguza ile kona iliopo kwenye kifupa mwiba cha tano(LO1 vertebra).
2. Usijaribu kukutana na mkeo kimwili ukiwa upo juu yae. Kufanya hivyo kutaruhusu ile kona iendelee kuwepo. Na kusababisha kusagana kati ya LO1 vertebra na LO2 vertebra.

Mr. Mawese nadhani utakua umeelewa. Asante
 
Mama Yangu anasumbuliwa na ugonjwa ambao anahisi anaungua kwenye mashavu, mabwegani, na kichwani usawa wa utosi.
Wakati mwingine akiwa anaungua hivyo kuna vitu vinamchoma kama vichomi kichwani.
Pia anakuwa anakaukiwa shingoni kama ana kikohozi kikavu.
Hali hii ya kuhisi kuungua ni ya muda mrefu sasa. Hata mwaka jana ilimtokea ikaja ikaacha.
Dr. Hali hii inaweza ijawa inasababishwa na nini?

Je kuna tiba yake?
Habari ndugu John 2030
Pale uliposema anakua kama anakaukiwa shingoni, sijakuelewa sawa sawa Unamaanisha shingo inakauka kwa maana ya kushindwa hata kugusisha kidovu kifuani au kugeuza shingo?
 
Nimeambiwa nina spine stenosis. Je, ugonjwa huu unapona ? Kingine.. Je, nikifanyiwa upasuaji wa spinal cord ni salama kwa hapa Tz au risk kubwa zaidi tofauti na nchi za nje?
Habari bwana Devile
Kabla sijaendelea ningependa unieleze dalili ulizonazo!
 
Habari Mali ya mtu:
Ndugu sababu ziko nyingi sana kutegemea na chanzo chake.

Ndugu.mimba kutunga nje ya kizazi, kitaalam hujulikana kama. Ectopic pregnancy .
Hii mimba hua Mara nyingi inajitungisha nje kabisa ya mfuko wa kizazi.
Yani badala ya kukaa ndani ya nyumba ya uzazi(Uterus)yenyewe huenda kukaa kwenye mirija (Fallopian tub). Ambayo mirija hii kazi yake si hiyo. Kazi ya msingi ya mirija hii ni kusafirisha mayai, kutoka katika sehemu yanapozalishwa(Overy), hadi kwenye nyumba ya uzazi ( uterus).

Mara baada ya utungisho misuli inayozunguka mirija ya fallopian ikishirikiana na vinyweleo vilivyoko ndani ya mirija hii, husukuma kiini tete au yai lililorutubishwa, na kulipeleka kwenye Uterus.

Kiini tete au Yai lililorutubishwa lifikapo kwenye Uterus hujipachika.

MIMBA KUTUNGA NJE YA MFUKO WA UZAZI.

Mimba kutunga nje ya nyumba ya uzazi au ectopic pregnancy.
Ni tatizo ambalo limetokea kuwaathiri Wanawake mbalimbali. Kwa kawaida isipokua Mara chache sana, mimba hizi hua hazikui na kua mtoto kamili.
Aidha mimba hizi ni hatari kwa afya ya mama mjamzito kwa kua Mara nyingi husababisha Mama kupoteza damu nyingi kwa kupasuka mrija na pengine kusababisha kifo.

SABABU
Sababu na chanzo halisi cha tatizo hili hakijulikani. Ingawa kuna mambo kadhaa huwa yanahusishwa kusababisha.
Magonjwa ya maambukizi katika mfumo wa uzazi hasa Yale ya uvimbe.
Sababu nyingine ni matumizi ya vitanzi vya kuzuia mimba hii ni kwa baadhi ya wanawake na kuoteana kwa tishu za kwenye nyumba ya uzazi.
Pia uvutaji wa Sigara hua unahusishwa na tatizo hili au kama mwanamke alishawahi kufanyiwa upasuaji wa maeneo ya tumbo.uliohusu mirija ya fallopian. na kusababisha Mrija husika kusinyaa.

Magonjwa ya kingono kama vile kaswende au Yale magonjwa ya ngozi ndani ya uzazi na mirija kua na umbo lisilo la kawaida na kuvimba.
Utoaji mimba, kwa kutumia dawa ama njia yoyote ile kwani tendo hilo hufanya kuharibu miundo mbinu ya mfumo wote wa uzazi na kusababisha isiwe katika hali ya kawaida.
Ni hayotu kwa uchache naamini utakua umeelimika ndugu.
Sawa mkuu je mwanaume hachangii hii shida?
 
Mkuu kuna rafiki yangu anaumwa kiuno katumia dawa zote za hospital haponi tu tatizo litakua nini sasa
 
Mdogo wangu anakohoa sana usiku Siku mbili hajalala sababu ya kukohoa pia analalamika kupumua kwa shida sana na kifua kumuuma na kubana
 
mimi ninashida nimekaa kwenye sehemu moshi wa gar ulikua unavuja kwa muda mrefu wa safari sasa nimelala nikjikuta naamka usiku baada ya kusikia maumivu kwenye fundo la koo panauma je nitumie dawa dani
 
Habari bwana mawese nimejaribu:
kuhusisha tatizo lako kwa mambo mbalimbali naona inakua ngumu kupata majibu ya moja kwa moja, zaidi ya kukueleza mambo haya yafuatayo.
Kwakua hupati Homa na tatizo lenyewe ni la mda mrefu ni kwamba tatizo hilo liko nje ya uti wa mgongo na nimehusisha na vifupa spines hivi hapa LO1 vertebra kwenye Lumbar spine ni kifupa mwiba cha tano kutoka chini.
Hapo katika kifupa hiki kuna kona kubwa ambayo imekimbilia nyuma zaidi. Ambapo ukisema unyooke vizuri kifupa mwiba hicho kinagusana na LO2 vertebra ambacho ni kifupa mwiba cha nne kutoka chini.

kwa hivyo hapo kuna kua hakuna space zinazoachiana zaidi ya kusagana.
Na vikisagana maumivu yanaanzia hapo, na kusambaa kwenye eneo lote la uti wa mgongo.

Ushauri wangu kwako, mkeo huyo ulienae kwa uzito alionao ndio atakua dawa kwako.
Kila siku muda wa kulala pamoja na asubuhi kabla ya kwenda kazini
Lalia tumbo kisha mkeo awe akikukalia mgongoni katikati. Maeneo ya usawa wa mbavu. Pale juu sio bondeni kuelekea kiunoni.

Na awe akikukalia akitazama miguuni kwako.na akae kwa kujiachia, huku akinesa nesa kama kakalia kiti chenye springi.
Afanye hivyo kama dakika 20 kila siku na wakati huo uwe ukitumia dawa hii yenye mchanganyiko wa dawa mbili.
Glucosamine sulfate 500mg
And chondroitin 400mg
Dawa hii tumia 1x1 kwa siku,kwa muda wa wiki 2

Pia Zingatia haya.
1 Unapokutana na mkeo kimwili, hakikisha awe juu yako na asikae akanyooka, atapokua juu yako halafu akulalie kifua chote.
2 Hakikisha usiinue kifua kumfuata aliko, kua na style hiyo hadi wote mmalize haja za miili yenu.
Kufanya hivyo ni kwa ajili ya kujaribu kuipunguza ile kona iliopo kwenye kifupa mwiba cha tano(LO1 vertebra).
2. Usijaribu kukutana na mkeo kimwili ukiwa upo juu yae. Kufanya hivyo kutaruhusu ile kona iendelee kuwepo. Na kusababisha kusagana kati ya LO1 vertebra na LO2 vertebra.

Mr. Mawese nadhani utakua umeelewa. Asante
Asnte sana mkuu
 
Doctor habari yako naomba kuuliza hivi inakuwaje mtu kama una vidonda vya tumbo unatokewa na vidonda hadi kwenye koo kuna uhusiano gani yani naomba nielekeze, maana Mimi na vidonda vya tumbo ila nmetokewa na vidonda kwenye tezi huku ndani ya koo na kwa nje ya shiko nimevimba kiuvimbe kidogo sasa nimeenda hospital wameniambia eti ni vidonda vya tumbo vimesababisha kwa kwel sikuelewa uhusiano wa vidonda vya tumbo na kuvimba tezi na vidonda kooni.
 
Tatizo ni nini mwili wangu kuwa na vipele vidogovido kifuani ila aviumi wala avina maji vipo tu
 
Thanks dear!. Will be waiting
Habari Cutel
Pole sana kwa kusubiri Sikua nimekusahau ila nilikua na majukumu mengi ya kikazi. Lakini usijali nimerudi.
Dadaangu kutokana na maswali yote niliokuuliza na majibu uliokua ikijibu

Tatizo yako nimehusisha na kushindwa kutoka kwa ute ijulikanao kama Anticoagulants ute hii hua inakuja na kemikali ambayo hufanya kukinga kuta ya Uterus usiharibike wakati wa kuhedhi.

Kemikali itokanayo na ute hii hufanya tukio la kuifanya damu isigande na iwe nyepesi na isikae sehemu yoyote kwenye kizazi yako.
Kitendo hicho hufanya Uterus kuachwa safi na salama baada ya kuhedhi.
Kama unableed pasipokuvuruga utaratibu wa cycle basi shida iko hapa,, ute hii kama inakua hakuna, hata ile kemikali pia itakua hakuna.
Hivyo hapo damu itakua haidhibitiwi na matokeo ni kufanya damu yako kutoka ikiwa heavy kama ilivyo wewe na kwa muda ndefu.
Hali hiyo pia hufanya kukuachia mabaki ya damu maeneo yote ya mapitio(fallopian tube) pamoja na Uterus.
Kitendo hii ya kubaki baki damu, husababisha maumivu wakati wa kuhedhi. Pamoja na layer of uterus(tando) kuharibika.
Ambavyo layer hii inapo haribika hupelekea shepu au umbo la Uterus kua si ya kawida Pia hupelekea ile tishu kubaki bila kinga.
Ambavyo tishu hii ya Uterus ikiondokewa ile layer hua ni rahisi sana kuathiriwa na kazi za endocrine gland zinazohusika na utoaji wa hormones za estrogen na Progesteron zinazochavusha overy.
Hormone hizi zinapokuja katika majukumu yake kama kutakua hakuna layer hii kwa muda ndefu husababisha kuta za kizazi kuanza kumea vivimbe.
Vivimbe hivyo ni kama Intracavitary, ambacho hua kikimea kwenye kuta ya juu ya uterus, na kwa bahati mbaya kadiri unavyoendelea kukua hua ndivyo inavyoteremka chini.Na kuendelea kukua na kua uvimbe mkubwa kama Mama aliemimbika.
Pia intramural hii humea katikati ya tishu laini iliokosa layer na hukaa pembeni ya uterus na hii hua si rahisi kugundulika kwani hua imejificha katikati ya tishu.
Pia Kuna hii Sabmucosal hii Mara nyingi humea pembeni mwa uterus.
Lakini hii ni rahisi kugundulika kwani yenyewe uvimbe hujitokeza kwa juu na kuonyesha kilima.
Lakini kwa wewe vivimbe hivi vyote kwa maelezo niliokuhoji inaonekana huna.hata kimoja
Isipokua uchungu ulionayo ni kutokana na kukosekana kwa ute hii pamoja layer.inayolinda uterus wakati damu ikichirizika.

Pia ziko zivimbe zingine ambazo hazisababishwi na kukosekana kwa anticoaglants, lakini zenyewe hazimei maeneo haya.
Mimi nimekutajia hizo tatu kwakua iko wezekano ya kupatikana nazo mda wowote kutokana na tatizo hilo.

SABABU YAKUKOSEKANA ANTICOAGULANTS.
Sababu ya kupungua au kukosekana kwa ute huu ni.
Dawa za kupanga uzazi Mara nyingi inahusishwa na tatizo hili.
Pia Vipodozi vya kupaka vyenye steroid na baadhi ya dawa za nywele navyo huhusishwa.
Pia kuna sababu za kijenitic, ambazo unaweza kua umerithi hali hiyo.zote hizo ni sababu ambazo zinahusishwa lakini pia kuna maambukizi ya Clamydia na yenyewe pia yapo katika fomu hiyo katika visababishi.

Katika yote hayo iko sababu hii hapa ambayo Wanawake wengi ndio kisababisha kikubwa
Mwanamke Kukaa mda mrefu bila kukutana na mwezi wake. Pia mwanamke kukutana kimwili pasipo kufika kileleni.
Hizi ndizosababu Mara nyingi kwa akina mama wengi.

MATIBABU
Matibabu inategemea kiwango ya tatizo ilipofikia pamoja na visababishi
Lakini tibabu ya msingi kwako ni kuhakikisha kufanya kurudisha anticoagulants.
Na urudishaji wa ute huu ni vizuri zaidi ukatumika mwili wako wenyewe. Pasipo kutumia dawa.

JINSI YA KUFANYA;
Kuhusu hili ningependa uje PM ili nikuelekeze vizuri ikiwa ni pamoja na kukuelekeza dawa za kutumia kwani pia iko haja kutumia aina fulani za antibiotic kwa kua tatizo lishakua la muda mrefu.
Nimatumaini yangu utakua umeelewa vyema Dada cutel
 
Back
Top Bottom