Mkuu me natatizo la woga sana tena the same time ninahasira hasa pale mpenzi wangu anaponichanganya zile hasira najikuna zimemwangukia mtu hata asiyehusika ila si kwa kupigana hapana ni kwakumfanyia kiburi au kumtolea maneno mabaya na hali hii imenitesa kwa mda mrefu tangu nimebalehe mpaka sasa ninatazamia kuoa. Nilijaribu kuulizia wakaniambia kuwa tatizo linatokana na kutofanya mapenzi kwa mda mrefu. Me kwa upande wangu sijui kama ni tabia ya asili au nilakisaikolojia
Habari bwana kiti chema
Na pole kwa tatizo hilo. Ni kwamba tatizo hilo linaweza kua na sababu mbili.
1 ni kwamba huenda mfumo wa kemikali yaani neurotransimitters.huko sawa.
Kazi ya kemikali hizi ni kupitisha taarifa mbali mbali za ujumbe, kutoka seli moja ya neva mpaka kwenye seli nyingine.
Iwapo kemikali hizi zikawa na kiwango kisicho sahihi(kupungua ama kuongezeka)
Taarifa hazitoweza kusafirishwa katika seli za Neva na hatimae taarifa hizo hazitoweza kufika kabisa kwa ubongo. ama kufika nusu ama kufika zaidi ya taarifa halisi. Au kwa lugha rahisi taarifa Zinakua zikifika kwa ubongo Zinakua za ubongo.
Hali hiyo ambayo Mara nyingi husababisha utendaji kazi wa ubongo ukawa ni wa uongo uongo.
Yani hapo na maanisha mhusika anakua akipewa taarifa na ubongo zisizo sahihi.
KIVIPI NA INAKUAJE
Ni kwamba kama macho ya mhusika yataona kitu cha kufurahisha kawaida.
Ubongo utamualifu mhusika kua anacho kiona ni cha kufurahisha kupita kiasi. Hivyo mtu hapo mtamuona anafurahi ama kucheka sana kwa jambo ambalo ni la kawaida kabisa na pengine jambo lenyewe lilikua si la kumfanya scheme, Bali lilikua ni la kumfanya atabasamu.
Ama macho yanaweza yakaona kitu cha kuudhi kiasi.
Lakini taarifa itayoenda kwa ubongo itakua tofauti, hivyo ubongo utalazimika kutoa taarifa kwa mhusika, taarifa ya uongo.
Kwamba kilichoonekana ni cha kuidhi sana. Hivyo hapo mhusika mtamuona amekasirika sana tena kupita kiasi kwa jambo ambalo hakutakiwa akasirike kiasi hicho.
Hapo ndipo mnashuudia Mtu ana mchoma kisu mwenzie kwa jambo ambalo wangezungumza na likaisha..
Ama masikio yanaweza yakasikia sauti ambayo sio ya kutisha lakini taarifa itafika kwa ubongo tofauti
Na hapo ubongo utalazimika kutoa taarifa kwa mhusika, kua kilichosikika ni hatari sana, na sio hatari ya siku moja ni ya maishani.
Hapo ndipo mtamuona mhusika anaogopa sana tena kwa jambo ambalo sio la kutisha nk.
2 Ni kwamba Nasaba (genetics).
Hapo kama familia ina matatizo haya ya hofu ilio pitiliza. Uko uwezekano hali hiyo ya hofu iliopitiliza kuendelea kadiri ya vizazi na vizazi.
Ndugu kitichema hali hiyo sio nzuri kwanza nikushauri nenda hospitali ukakutane na daktari wa Afya akili.umweleze. tatizo lako. Na uchunguzi wa kina juu ya afya ya akili utafanyika.