Habari.
Nikweli kumekua Na ongezeko kubwa la tatizo hilo zaidi kwa Wanawake. Na hii nikutokana sana na mambo ya Urembo.
Kwani kuna baadhi ya vipodozi Na dawa za nywele huchochea sana uzalishaji wa Oestrogen mwilini, kuliko kawaida.
Ongezeko hili la uzalishwaji wa oestrogen huchangia kwa kiasi kikubwa sana cha ukuaji wa fibroids
Kemikali hizi zinazoambatanishwa kwenye vipodozi au dawa za nywele hupenya kwenye ngozi kutokana Na matumizi wanayotumia Wanawake kwa lengo la kupendeza.
Kwa ujumla kemikali hizi. Hazimuathiri mtumiaji kwa matumizi Bali hata kwa kuvuta harufutu.
Ukichunguza wamama au wadada wengi hubadiri matumizi ya dawa kua vipodozi.
Kwamfano kuna dawa zilizo katika kundi la steroids kama vile hydrocortisone,Betamethasone,Dexamethasone,Beclometasone,Clobetasol,Prednisolin nk
Kimsingi dawa hizi ni dawa za allergy Na husaidia kupunguza nguvu za kinga za mwili.
Zinapokua katika mfumo wa Cream,Lotion au gelly husaidia kuondoa allergys kwenye ngozi.
Mbali Na kuondoa allergy bali pia huondoa ngozi ngumu Na rough ya nje. (Ngozi ambayo hutusaidia kutukinga Na miale mikali ya jua, kansa, michubuko Na kadhalika.
Dawa hizi kwa kawaida zinatakiwa zitumike kwa dozi maalum.Na kwa muda usiozidi wiki mbili.
Sasa kwa bahati mbaya wamama au wadada wamekua wakibadirisha matumizi ya dawa hizi Na kuzifanya kua vipodozi.
Kwa kawaida dawa hizi hunyonywa Na kuingia mwilini Na husababisha kwenda kuzuia tezi la adenal linalozalisha hormone ya adrenalin lisizalishe hormone hiyo.Na endapo matumizi hayo mabaya yataendelea, hufanya tezi hilo lisinyae Na kufa kabisa.
Matokeo ni mengi mabaya endapo tezi hili litakufa ambayo yanaweza kujitokeza mbali Na hayo ya fibroids niliotaja huko juu. Yakiwepo ya kupungua kinga za mwili, Na kupungua kwa kiwango cha homon ya Oestrogen.Na ikipungua umbo au shepu ya kike huanza kukimbia.
Hapo matokeo ni kuota ndevu Na sauti nzito kama mwanaume. Maziwa ya kifuani hunyauka. Na kuingia katika ukomo wa hedhi kabla ya umri. Na kua Na sura nzito kama mwanaume nk.
Sasa ili ujue upo katika kundi la waathiriwa. Tazama lotion yako ,Cream au gelly walipoandika "COMPOSISION"au INGREDIENTS ukiona kuna hizo dawa nilizozitaja hapo juu basi tambua upo katika hatari. Chukua hatua haraka kwa kuanza kuziacha
Na ukumbuke hutakiwi kuziacha ghafla, anza kuacha taratibu.kwani ukiacha ghafla kutokana Na nilioyaeleza huko juu utapata matatizo makubwa.
Kwani hapo ulipo kama vipodozi hivyo ushatumia muda mrefu basi huenda tezi ya adenal haifanyi kazi.
Hivyo itabidi uziache taratibu ili adrenal aanze kurudia majukumu yake ya kiutendaji kazi.
Kwa upande wa option za matibabu kwa waathirika fibroids, ziko option mbili.kutegemea Na chanzo chake
Ya kwanza ni matumizi ya dawa ikiwa ni pamoja Na kurekebisha mfumo wa homon.
Ya pili ni upasuaji ili kuiondoa fibroids yenyewe lakini pia mfumo wa homon ni lazima uangaliwe. Vinginevyo, baada ya upasuaji fibroids inaweza kurudi
Msweet nimatumaini yangu utakua umenufaika, karibu tena