Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

Kuna kipindi hili suala la dawa ya usingizi lilijadiliwa hapa JF. Ufumbuzi ukawekwa hapa jukwaani. Ni hivi, kwa kawaida maji yanafyonza hewa yenye sumu inayopulizwa na kama yataachwa wazi bila kufunikwa yanawezasaidia kuifanya hiyo dawa ishindwe kutoa kusudio lake. Wadau walishauri tukilala tuache ndoo ya maji wazi. Mimi najitahidi sana kutekeleza kufata huo ushauri ili kujilinda. Ingawa sijapata mrejesho wa mtu aliyeacha ndoo ya maji wazi na kuibiwa kwa kupuliziwa dawa ya usingizi, basi yawezekana kuna ukweli na uhalisia katika hilo!
Hakuna ukweli wowote kuwa eti maji yana uwezo wa kuvuta dawa ya usingizi iliyopo kwenye hewa. Hili ukilisema kwenye wasomi wa ukweli watakucheka sana. Hebu toa mfano wowote wa dawa ya usingizi inayovutwa na maji yaliyo kwenye ndoo. Tuambie ni dawa gani tufanye majaribio.
 
Katika panga panga zangu nyumba

hata kama nyumba iwe nzuri kama ikulu au paris ila

ikakosa madirisha ya ku slide (ya kioo) sipangi hiyo nyumba

Tangu wapitishe Tv sehemu ambayo hata mimi sipiti NIMEKOMA.
Madirisha yenye vioo kwa Dar yana karaha zake. Kipindi cha joto kama huna kiyoyozi huwezi kuyafunga yote.
 
Dawa za usingizi nyingi zina chlorine so ikikutana na maji ina dissolve na kutengeneza chloroform,
Hakuna ukweli wowote kuwa eti maji yana uwezo wa kuvuta dawa ya usingizi iliyopo kwenye hewa. Hili ukilisema kwenye wasomi wa ukweli watakucheka sana. Hebu toa mfano wowote wa dawa ya usingizi inayovutwa na maji yaliyo kwenye ndoo. Tuambie ni dawa gani tufanye majaribio.
 
DAWA NI MAJI TU.

Ile spray ikipulizwa kwny chumba chochote chenye maji yaliyo open kwa mfano kwny ndio au karai inafyonzwa yote kwenye maji.

Hata ulaya kuna wakati walikuwa wakiibiwa hivyo.
Huu ni uvumi wa mitaani tangu. Maji hayana uwezo wa kufyonza dawa iliyo kwenye hewa. Tujaribu kuchemsha akili kidogo. Eti maji yako kwenye ndoo halafu mtu anapuliza dawa na yale maji yanakuwa na nguvu ya kuvuta ile dawa isisambae sehemu nyingine lakini ielekee kwenye tu kwenye ndoo yenye maji.
 
Madirisha yenye vioo kwa Dar yana karaha zake. Kipindi cha joto kama huna kiyoyozi huwezi kuyafunga yote.
MKUU KUNA ac ZA chini za kuchomeka kama radio

hadi laki mbili na 50 unapata

ma used naskia ndio hadi 150 unapata

Kwann mtu usijikakamue ununue yako 1

ya kutumika usiku tu? (kwa wale wa hali ya chini kama sisi)
 
ULINZI MZURI TUNAUPATA TUMBATU VISIWANI PEMBA.
UNAAMUA TU, WAKIJA WAKUTE BAHARI, ANASE PALE PALE AU APOTEE KABLA HAJAFIKA HOME.
CCTV IKASOME!! MAMBO YOTE KWA WAPEMBA
 
Dawa ya kupulizia dawa yake ni maji unaweka kwenye jagi au beseni dogo ikipulizwa ndani yote mvuke wa maji mtakuta Kama povu tena walivyo wapuuzi wakisha puliza wanakata au kuongea kwa sauti wanajua washakupiga nusu kaputi wakianza kukata au kuingiza kitu cha kutolea lazima usikie hawataamini wataona kama mzuka na kukimbia mbaya nilikaa mitaa mibovu kipindi fulani wale wahuni waliwaliza watu kwangu wanakuja na makelele yao maji yalinisaidia...nakumbuka ni Sinza hiyo hiyo maeneo ya makabe....
Hebu tueleze hiyo sayansi ya maji yaliyo kwenye beseni dogo yanavyoweza ku-react na dawa iliyopulizwa kwenye chumba ewe mkemia. Tena unasema kwa kujiamini kabisa kuwa dawa ikipulizwa inakutaka na mvuke wa maji. Hivi ukiweke maji ndoo moja kesho yake unakuta yamegeuka kuwa mvuke?
 
MKUU KUNA ac ZA chini za kuchomeka kama radio

hadi laki mbili na 50 unapata

ma used naskia ndio hadi 150 unapata

Kwann mtu usijikakamue ununue yako 1

ya kutumika usiku tu? (kwa wale wa hali ya chini kama sisi)
Asante mkuu. Lakini kwa mazingira ya umeme kukatikakatika nako kuna changamoto zake. Ulinzi wa nyumba ni combination ya measures nyingi anazotakiwa kuchukuwa mtu mmoja mmoja na mtaa kwa ujumla. Ila la air condition nalo ni zuri kwani litaondoa kero nyingine kama joto na mbu hasa ukipuliza dawa na kufunga madirisha vizuri.
 
Dawa za usingizi nyingi zina chlorine so ikikutana na maji ina dissolve na kutengeneza chloroform,
Swali langu ni hili: Maji yanakuwa sehemu moja kwenye chombo kama beseni. Anapopuliza hiyo dawa kuna mvutano gani wa kuivuta na kuipeleka kwenye beseni badala ya kusambaa sehemu zote za chumba?
 
Du nliwahi kuibiwa simu yangu tecno p3 pale dodoma kikuyu..jamaa alitoa lain zangu akaziacha dirishan akasepa na cm..wizi wa madirishan Ni kero jamani..
 
Asante mkuu. Lakini kwa mazingira ya umeme kukatikakatika nako kuna changamoto zake. Ulinzi wa nyumba ni combination ya measures nyingi anazotakiwa kuchukuwa mtu mmoja mmoja na mtaa kwa ujumla. Ila la air condition nalo ni zuri kwani litaondoa kero nyingine kama joto na mbu hasa ukipuliza dawa na kufunga madirisha vizuri.
Baada ya kuibiwa kwenye nyumba niliyokua nikikaa zamani(ile ya madirisha ya nondo)

ilibidi nitengeneze shoti kwenye dirisha langu nilimtafuta fundi wiring akaja akanifyanyia mambo

ikawa usiku nikilala naacha dirisha wazi kabisa nakunja hadi pazia then nawasha ukutani

mbinu ile nilifanikiwa kukuta vitendea kazi vyao vingi sana wakiviacha pale dirishani

kwa kuogopa vichukua wakiamini watapigwa shoti na kweli shoti yake haikua ndogo

Japo kuna siku nilijisahau mwenyewe ikanilamba na wenge langu .

Kwenye hizi nyumba za kupanga ulinzi mtu ujiwekee mwenyewe ukisubiri makubaliano ya pamoja (utajutia siku)
 
Leo imekuwa ni vilio na hamaki kwa raia wa hapa Sinza A, baada ya kuamka asubuhi na kukuta madirisha yao yametobolewa na kukatwa kwa nyavu.

Inasemekana, walipuliza dawa ya usingizi ndipo wakafanya unyama huo. Watu wameibiwa pesa, laptops, simu, vitu vya ndani kibao.

Hapo unapoishi, kuna wizi wowote umefanyika?

Anayejua jinsi ya kujikinga na hiyo sawa, atupe elimu hapa.

Poleni wahanga wote wa wizi huo.

Nawasilisha!


Wale wote walisema ukiweka maji kwenye beseni inasaidia kunyonya sumu naomba kujua kiwango chenu cha elimu.
 
Hata wewe hujatoa suluhisho au niseme suluhisho lako halitekelezeki, asilimia kubwa ya watu wa huko wamepanga kwa hiyo wawe wanatembea na madirisha wakifika kwenye nyumba wanaweka madirisha yao?
mi nimetoa kwa wajenzi a nyumba za kupanga
 
Vipi wewe Mwerevu ,ambaye utajenga kwa mujibu Mawazo yako bila kuzingatia athari za Moto zikitokea atapona mtu kweli ndani ya hiyo Nyumba .
hivi moto ukitokea hata sasa hivi yale madirisha kwani anaweza kutokea mtu?
 
rikiboy,

Acha tu mkuu nilikuwa nina usingizi wa ajabu halafu ikaja mvua ya upepo ikawa inapga dirishani vimatone vinakuja niflash hadi kitandani.

Sasa mimi nikaamka na wenge langu nifunge pazia, kumbe pazia lishaloa lina umeme tayari. Si ndio nikaenda lifata nikunjue, bwana wee (usingizi ulikata wote kwa kilichonikuta).
 
CONTROLA,

Ni kweli kabisa. Ila hili la short ya umeme siwezi kulifanya kabisa. Nimeshashuhudia vifo viwili vya watu wema vilivyosababishwa na aina hii ya ulinzi. Mmoja alikuwa mtoto mdogo anachezea dirisha kumbe aliyeweka alikuwa hajaamka ili azime. Jingine aliondoka akasahau kuzima huku nyuma akaja ndugu yake akashika.
 
Ni kweli kabisa. Ila hili la short ya umeme siwezi kulifanya kabisa. Nimeshashuhudia vifo viwili vya watu wema vilivyosababishwa na aina hii ya ulinzi. Mmoja alikuwa mtoto mdogo anachezea dirisha kumbe aliyeweka alikuwa hajaamka ili azime. Jingine aliondoka akasahau kuzima huku nyuma akaja ndugu yake akashika.
shoti ni muhimu na lazima kwa mitaa korofi kabisa ambayo haipiti siku dirisha halijachanwa

lakini pia yakupasa udhamirie na uamue kweli....
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom