Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

Karibia mtaa mzima Sinza A tumeibiwa

Hata kwa wazungu kuna wezi wadokozi, muhimu ni kuwa na security sytems zinazotoa alerts. Unaweza ukafunga motion detectors n.k

Lakini bora mnakutana na hao wadokozi tu hawana madhara. Miaka ya zamani kidogo, kulikuwana majambazi na sio wezi. Wale majambazi wanaokuja na vyuma/mawe fatuma wanafunga mtaa, wanakuja na mgari mkubwa na kukomba kila kitu hadi viporo vya misosi.
 
Dawa za usingizi nyingi zina chlorine so ikikutana na maji ina dissolve na kutengeneza chloroform,
Duh kwahio maji yataongeza nguvu ya dawa uliyopuliziwa na wezi! Maanake chloroform ni dawa ya usingizi. Nakumbuka nilipokuwa shule tulipasua vyura tumiwa tumewalaza kwa chloroform
 
Walio like hapa wote ni watoto wenzako wanaoenda chuo mwaka wa kwanza , sasa wizi umetokea sinza wewe unashusha gazeti ili tujue
1. Mzee wako ananyumba nyingi
2.Alikua muwindaji wa kujitegemea
3.Alikua anamiliki bunduki
4.alikua anashabaha sana
Nakushauri jipige kifuani mara 3 sema mimi ni mjinga sana tena mpumbavu ee Mwenyezi Mungu nisaidie
Kwa akili yako solution umeona kulala na maji kila siku chumbani si ndio. Punga kabisa wewe
SINZA INGEFANYWA SEHEMU YA MASHOGA,MADADA POA,KAMARI,BAA ETC NA SIO MAKAZI YA WATU,IWE MODERN UWANJA WA FISI 🥴 🥴 🥴
Hivi kufanya mjadala bila lugha zisizo na staha ni ngumu sana?
 
Du nliwahi kuibiwa simu yangu tecno p3 pale dodoma kikuyu..jamaa alitoa lain zangu akaziacha dirishan akasepa na cm..wizi wa madirishan Ni kero jamani..
Mwizi mwenye kujitambua
 
Na mkilala usiku muwe mnaweka ule wimbo wa 'Sijalala mwanangu utauwawa bureeeeeeeeeee'
Inaweza saidia kidogo'.
 
Hakuna ukweli wowote kuwa eti maji yana uwezo wa kuvuta dawa ya usingizi iliyopo kwenye hewa. Hili ukilisema kwenye wasomi wa ukweli watakucheka sana. Hebu toa mfano wowote wa dawa ya usingizi inayovutwa na maji yaliyo kwenye ndoo. Tuambie ni dawa gani tufanye majaribio.
Ningalikujibu vizuri kisayansi lakini kwa vile kuna dhihaka imetalamaki na unataka ligi naomba niishie hapo. Samahani
 
Leo imekuwa ni vilio na hamaki kwa raia wa hapa Sinza A, baada ya kuamka asubuhi na kukuta madirisha yao yametobolewa na kukatwa kwa nyavu.

Inasemekana, walipuliza dawa ya usingizi ndipo wakafanya unyama huo. Watu wameibiwa pesa, laptops, simu, vitu vya ndani kibao.

Hapo unapoishi, kuna wizi wowote umefanyika?

Anayejua jinsi ya kujikinga na hiyo sawa, atupe elimu hapa.

Poleni wahanga wote wa wizi huo.

Nawasilisha!
KINGINE ANGALIENI VIKAO MNAVYOKAA KWA AJILI YA ULINZI ULIZANENI KAMAN TUNATOA SADAKA NA ZAKA KAMILI KWA MUNGU

UKISOMA ISAYA UKIMWIBIA MUNGU ATATIA HATA NZIGE NA .MADUMADU KUKUTAFUNA MADUMADU NDIOO HAOO WALIOWAPITIAA

PILI MKUMBUKE HAO JAMAA WENGINE WAKIWNDA KUPIGA KAZI WANAOMBA KABISA MOLA AWALINDE AWAEPUSHE NA MADHARA

SSASA KAMA MNAKAA NYUMBA KUBWA MNAAMKA SALAAMA MNAACHA HATA KUSEMA AHSANTE MUNGU LEOO TUMEAMKA WAZIMA LAZIMA WENZENU WASIKIWE MAOMBI

JIFUNZENI KUSALI NA KUOMBA ASBH NA USIKU
 
!NAJUA MAJAMBAZII WANAFWATILIA SANA HII THREAD KAMA ILE YA 2016
MKIPATA MDA SOMENI MPATE MREJESHO WA SWALI HIILIII
Screenshot_20191028-144324.png
Screenshot_20191028-144313.png
Screenshot_20191028-150123.png
Screenshot_20191028-150018.png
Screenshot_20191028-150222.png
Screenshot_20191028-150154.png
Screenshot_20191028-150313.png
Screenshot_20191028-150229.png
Screenshot_20191028-150452.png
Screenshot_20191028-150346.png
 
Ningalikujibu vizuri kisayansi lakini kwa vile kuna dhihaka imetalamaki na unataka ligi naomba niishie hapo. Samahani
Nina uhakika wa asilimia mia kuwa huna jibu lolote. Tena unasema eti kisayansi? Hapo ndipo umenoa kabisa. Bora ungesema kimuzimu. Mimi siyo mtu wa kumeza kila kitu ninacholetewa mazee. Elimu yangu niliyoipata inatosha kunifanya niweze kujenga logic ya jambo kama hilo. Eti ndoo ya maji ndiyo itasaidia dawa ya usingizi inayonyunyiziwa isifanye kazi. Wadanganyeni wasioenda shule.
 
Duh unatufundisha kukojolea kwenye beseni usiku tukiamka? Acha tabiya ya kishamba ya kukojowa kwenye makopo!! Unalala na maji chumbani kwenye beseni Wewe samaki?
Wewe ni mtanzania kweli? Toa mbinu mbadala. Inawezekana hata nondo ufaham zinafananaje.
 
Leo imekuwa ni vilio na hamaki kwa raia wa hapa Sinza A, baada ya kuamka asubuhi na kukuta madirisha yao yametobolewa na kukatwa kwa nyavu.

Inasemekana, walipuliza dawa ya usingizi ndipo wakafanya unyama huo. Watu wameibiwa pesa, laptops, simu, vitu vya ndani kibao.

Hapo unapoishi, kuna wizi wowote umefanyika?

Anayejua jinsi ya kujikinga na hiyo sawa, atupe elimu hapa.

Poleni wahanga wote wa wizi huo.

Nawasilisha!
Poleeeeee MKUUU NAONA UPEPO WA KISULISULI UMEWAPITIA ....AURUDI TENA HUOOO
 
Mimi nilicho mfanyia mwizi moja hatokuja kunisahau mpaka siku ya kufa kwake.
Sijui kama yupo hai au amekufa.
kwanza nilikata fekeo nusu kipisi, nikalinoa barabara upande moja. Sio mafekeo yote utaweza kuyafanya hivi, kuna mafekeo muhimu.
Baada ya huyu mwizi kninyima raha, nilimfanyia kazi, mpango maalumu.
Siku ya siku mchana kweupe nilishusha mzigo subufer.
uzuri mwizi wangu nilikwisha mjua, nikajua tu huyu lazima aje aniibie.
Nilicho fanya sasa, chumba changu kilikuwa na kibaraza japo ni nadra sana uswazi kupata chumba cha namna hiyo.
usiku nilitengeneza kitanda juu ya kibaraza, kwa njee. nilipanga mbao furesh na kigodoro kidogo kama cha shule bording nikawa nalala juu.
mlangoni niliweka machuma, vipisi vya spring ya magari. juu ya mlango nilitegesha vichuma ambavyo kitendo cha mlango tu kufunguliw vinadondoka vinapiga machuma ya chini. Machuma ya chini niliyajemgea cement ili mlango ukifunguliwa tu nistuke nikiwa nimelala juu ya dari. pia niliona nikiyaegesha tu mwizi anaweza kuchukua akanidhuru katika mapambano.
Nililinda siku bila mafanikio,
Siku ya siku ikawadia, siku ya nne usiku nilifunga mlango wangu kwa njee, mimi nikapanda juu kitandani kwangu. Nilipanga mbao zangu kwa ustadi mkubwa. Kwa njee nikafunga kufuli la solex ambayo huwa wanayafungua kama kwao. Kuhamanisha ndani hana mtu.
Mida ya saa tisa usiku nikamuona mtu kaja pale mlangoni ananyata. kwa sababu nilikuwa nipo on duty sikuwa nimelala.
Nilicho fanya nilikuwa nasoma mazingira, huyu yupo peke yake au, nikajiridhisha yupo peke yake.
Nilimuacha afungue mlango, ile kufungua tu vyuma viligongana. akashikwa na uwoga akarudi nyuma faster. mimi nipo kwa juu namcheki tu.
Nilishuka darini kininja nikawa nyuma yake. Nikawaza faster huyu nikimsulubu hapa itakuwa msala. Nikampa upenyo anikimbie nikala naye sahani moja. Kona ya kwanza, ya pili, tukawa tunaenda kimya kimya. Karibu na bonde nilimchapa moja takatifu mgongoni alidondoka palepale, hakika nilimchimba sana, nilimwachia fekeo palepale. Nikatafuta njia nyingine nikarudi. Ukweli that time, unikimbie labla uniache hatua 20
Mimi usiku huo huo nilimpigia dereva wa town ice, nikahama kimya kimya. Niliacha tu ujumbe kwa mwenye nyumba kupitia kwa jirani apangishe tu, nimevunja mkatabaa.
Mpaka naondoka, sii jirani wala dereva wa town ice amejua chochote. Mizigo yangu yote nikaipeleka maskani home, mimi nikaenda zangu mozambique coz nilikuwa nipo nampango huo.
Sikurudi, sikutaka kujua kama mwizi wangu yupo hai au kisha tangulia.
Ukweli mwizi wangu alinitesa sana. Kupigwa tochi usoni ilikuwa sehemu ya maisha yangu. Aliniibia smart phone ambayo nilinunua kwa kujibana mnoo.
 
Macho Mdiliko nazungumzia ukiweka maji kwenye beseni ile dawa wanayopuliza utakuta povu kwenye beseni au ndoo mimi nimefanya hivyo nina uhakika nayo na unaambiwa na wahuni tuu bhana fanya hivi sasa wewe kama unataka mambo ya kitaalamu tafuta wataalamu watakueleza...
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom